Saturday, June 23, 2018

_*NEVER AGAIN*_👇🏽

🍂 _Never again will I say *"I CAN'T"* because I can do all things through Christ Jesus._
📖 *Philippians 4:13*

🍂 _Never again will I say *"I DON'T HAVE"* because my God shall supply all my needs according to His riches._
📖 *Philippians 4:19*                                

🍂 _Never again will I say *"I AM AFRAID"* because God has not given me a spirit of cowardice but a spirit of power._
📖 *2 Timothy 1:7*

🍂 _Never again will I say *"I LACK FAITH"* because God has given to every man a measure of faith._
📖 *Romans 12:3*                                                                        

🍂 _Never again will I say *"I AM WEAK"* because the Lord is the strength of my life._
📖 *Psalm 27:1*                  

🍂 _Never again will I say *"SATAN IS POWERFUL"* because greater is the God that is in me than the evil in the world._
📖 *1 John 4:4*                

🍂 _Never again will I say *"I AM DEFEATED"* because we are more than conquerors through Christ Jesus._
📖 *Romans 8:37*                

🍂 _Never again will I say *"I LACK WISDOM"* because Christ has become for us the wisdom of God._
📖 *1Corinthians 1:30*    

🍂 _Never again will I say *"I AM SICK"* because through His stripes we are healed._
📖 *Isaiah 53:5*                  

🍂 _Never again will I say *"I AM BURDENED"* because I cast all my burdens upon Jesus who cares for me._
📖 *1 Peter 5:7*            

🍂 _Never again will I say *"I AM IN BONDAGE"* because where the spirit of the Lord is there is freedom._
📖 *2Corithians 3:17*        

🍂 _Never again will I say *"I AM CONDEMNED"* because there is no condemnation for those who are in Christ Jesus._
📖 *Romans 8:1*

*May God bless you Today Tomorrow and Always*

Saturday, June 16, 2018

DALILI ZA KUJIJUA KAMA UNA JINI MAHABA.
NA:MAJOR PROPHET DERICDADY
EMAIL:dericglory@gmail.com
0712412170 au 0679008354

1. Kuota unafanya MAPENZI na MTU unayomjua au usiyemjua kwa sura tofauti.
2. Kuota unafanya mapenzi na mnyama.
3. Kuota unanyonyesha au kujifungua mtoto.
4. Kutokudumu kwnye mahusiano kama ndoa au mchumba.
5. Kuwa na hasira za haraka.
6. Kukwama kwa mipango yako.
7. Kupoteza pesa au vitu vya thamani, unaweza ukaweka pesa kwenye walet au mahali salama kabisa kisha ukakuta zimepungua.
8. Kutokuwa na hamu ya mapenz kwa wanawake na wanaume kutokuwa na nguvu za kiume.
9. Kuota umefunga ndoa.
10. Maumivu ya kichwa,mgongo,kiuno na tumbo haswa chini ya kitovu.
11. Kuvulugika siku au kuharibika kwa mimba au kutoshika mimba kabisa.
12. Kuumwa U.T.I isiyoisha inayojirudia.
13. Kutokupenda kabisa mahusiano.
14. Matiti kujaa au kutoa maziwa na hauko mjamzito au unanyonyesha.

UKIJIJUA UNADALILI HIZI JUA JINI MAHABA AU ANZURA ANAKAA NDANI YAKO.MAANA WADADA WENGI HAWAOLEWI KWA SABABU HII,AMA KUVURUGA NDOA.PIGA NAMBA ZILE KWA MSAADA WA MAOMBEZI YA HARAKA.

  UBARIKIWE NA YESU.

Thursday, June 7, 2018

WHERE TO FIND HELP IN THE BIBLE

*SALVATION*
_____________
Acts 16:31
Acts 4:12
Revelation 7:10
Psalm 27:1
Isaiah 12:2
Philipians 2:12
Romans 10:9
Titus       3:5
1 John 3:14
Ephesians 1:7



*FORNICATION*
_______________
Colosians 3:5
1Thesalonians 4:3-4
1 Corinthians 16:13-18
Revelation 22:15



*LAZINESS*
___________
Proverbs 6:6-10
Proverbs  13:4
Proverbs  20:13
Proverbs   10:4
Proverbs  20:4



*HOW TO PRAY*
_______________
Matthew 6:5-6
Mark 11:24
Job 8:5
Isaiah 51:1-4
1 Samuel 1:12-13
John 15:7



*TEMPTATION*
_______________
James 1:2
2 peter 2:9
Matthew 4:3
1 Corinthians 10:13
Ephisians 6:13
Hebrews 2:18
Genesis 3:6



*IDOLATRY*
____________
Exodus 20:1-3
1 Corinthians 10:14
Leviticus 19:31
Deutronomy 27:15



*THE LOVE OF MONEY*
________________________
1 Timothy 6:6-10
Hebrews 13:5
Leviticus 19:35
Hezekial 18:13
Proverbs 20:17



*BAD COMPANY*
_________________
1 Corinthians 15:33
1 Corinthians 5:9
 2 Corinthians 6:14-16
Exodus 23:1-2



*HUMILITY*
___________
James 4:10
Matthew 18:10
Luke 14:10
1 Peter 5:5-10



*MIND YOUR DRESSING*
_________________________
1 Peter 3:3-5
Deutronomy 22:5
1 Timothy 2:9-10
Isaiah  3:16-17
1 Corinthians 6:19-20



*MARRIAGE*
____________
Genesis 2:24
Romans  7:2
1 Timothy 3:12
Mark     10:9
Proverbs 18:22
Hebrews  13:4-6
Ephesians 5:22-31
1 Peter:3:7-8



*JESUS'S SECOND COMING*
____________________________
Luke 12:40
James 5:8-9
1 John 2:28
2 Corinthians 7:1
John 14:3
Revelation 3:11
Revelation 22:12
Revelation 16:15
Matthew 24:30
Matthew 16:27
Mark 8:38
1 John 3:23



*FAITH*
________
Ephesians 2:8-9
Ephesians 6:16
Luke  17:5
1 peter 1:7
Romans 10:7
Galatians 5:6
Hebrews 11:1
James 1:3-6



*REPENTANCE*
________________
Proverbs 28:13
Proverbs 1:23
2 Chronicles 30:6
Ezekiel 18:31
Acts 17:30
Luke 18:13-14
Luke 13:3
Joel 2:12
Acts 2:38
Zephaniah 2:3


Dericglory@gmail.com
0712412170

Monday, June 4, 2018


 JIFUNZE KOZI HII YA UCHUNGAJI.
MASOMO HAYA YOTE UKIMALIZA UMEPIGA HATUA KUBWA KATIKA UTUMISHI.



SOMO LA 1
MUNGU


1.1  Uwepo wa Mungu

“Mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kuwa yeye yupo  na
kwamba huwapa dhawabu wale  wamtafutao” ( Ebr 11:6). Lengo la
masomo haya ni kuwasaidia wale wanomwendea Mungu, wakiisha
mwamini “Kwamba yupo”; kwa sababu hii hatutajitia  kwenye
ushahidi usiothibitisha  imani ya kuwa Mungu hayuko.katika
kupima muundo wa miili yetu (Zab 139:14)  Ushahidi wa kielelezo
katika ua, Kukazia macho juu kwenye anga pana wakati wa usiku
kukiwa wazi  bila mawingu, haya na mengine yasiyohesabika,
Mawazo ya kangaliifu juu ya maisha,  hakika yanafanya imani ya
kutosadiki kuwa Mungu hayupo iwe ni ya kushangaza. Kusadiki
kuwa Mungu hayuko  hakika inahitajika imani zaidi  kuliko
kuamini yupo,pasipokuwepo Mungu mpangilio haupo, Kusudi au
kutoa maelezo ya asili  ya Ulimwenguni  basi hii itafikiriwa katika
maisha ya mtu asiyeamini kuwa Mungu yupo. Tukikumbuka hili,
siyo ajabu kuwa watu wengi  wanakiri kwa kiwango fulani  cha
kumwamini kuwa Mungu yupo hata katika jamii ambayo vitu vya
mwili  ni Mungu  anayeshinda maisha ya  watu.
   11


Lakini ipo tofauti pana kati ya kuwa na fikra isiyodhahiri ya
kwamba ipo nguvu ya juu, na hasa kweli kuwa na uhakika kwa kile
ambacho Mungu anampa mtu anayemtumikia kwa Uaminifu.
Waebrania 11:6  jambo hili tunasoma;

 “Yatupasa tuamini kuwa (Mungu )yupo na
 Kwamba huwapa thawabu  wale wamtafutao kwa bidii”

Maelezo mengi ya biblia ni historia ya watu wa  Mungu
Israeli; mara kwa mara neno limetolewa kwamba kukubali kwao
kuwa Mungu yupo hakukulingana  na imani zao kwa ahadi
zake.Waliambiwa na mkubwa kiongozi wao Musa'Kwa hiyo
ujue…….Ukaweke moyoni mwako, ya kuwa BWANA ndiye
Mungu  katika mbingu juu, na katika nchi chini,  hapana mwingine.
Basi, zishike sheria zake,  na amri zake  (Kum. 4:39:40).
Neno hili hili limetolewa  - ufahamu wetu katikati yetu ya
kuwa  Mungu yupo hakumaanishi kwamba tunakubalika mbele za
Mungu bila kufikiri.Ikiwa bila mchezo  tunakubali kwamba kwa
kweli tunaye  Muumba,'Kwa sababu hiyo tuzishike sheria na amri
zake’ Ni shabaha ya  mfululizo huu wa masomo kuelezea  amri hizi
jinsi zilivyo na namna ya kuzishika. Tunapochungunza maandiko
kwa kufanya hivi, tutakuta kwamba imani yetu kuwa Mungu  yupo
inatiwa nguvu.

‘Imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la
Mungu’ (Rum 10:17). Vile vile,(Isaya 43:9-12) yaonyesha namna
ya kufahamu unabii wa  Mungu kuhusu wakati ujao - Unabii
unatufanya tujue'kuwa mimi ndiye’ (Isa. 43:13)- yaani  hilo jina la
Mungu, 'Mimi niko ambaye NIKO’ kwa ukamilifu ni kweli (Kut.
3:14.)  Mtume Paulo alifika kwenye mji unaoitwa Beroya, eneo hili
kwa sasa liko kaskazini mwa Uyunani ( Ugiriki) kama kawaida,
12

akahubiri injili (Habari njema) ya Mungu; lakini badala ya watu
kusikia neno la Paulo alilokuwa anasema, tunasoma kwamba, “
Walilipokea kwa kusikia neno (la Mungu, sio la Paulo) kwa
uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone
kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo. Basi watu wengi miongoni
mwao wakaamini  ( mdo 17:11,12)

Imani yao ilikuja kwa kuwa mioyo yao ilikuwa wazi, sawa
sawa (‘ Kila siku’)  na kwa utaratibu wa (‘mambo hayo’)
waliyachunguza katika Biblia, Basi  kupata imani ya kweli haikuwa
Mungu aliwafanya wawe nayo ghafla kwa aina fulani ya upasuaji
wa moyo wa kiroho,  pasipo kujihusisha na neno la Mungu. Ni jinsi
gani basi watu wa Ulimwengu  wanaweza kufuata kwa moyo
pigano juu ya  maovu  la Bill Graham au  uamsho wa mikutano ya
wapentekoste kisha wanahama  tena  kama'Waamini’ ? Ni muda
gani wameendelea katika masuala haya  wakiwa wanachunguza
maandiko kila siku ?  Kwa kweli kukosekana huku kwa imani
ambayo msingi wake upo kwenye Biblia bila shaka kunaonyesha
utupu wa'Waongofu’  hawa na kujikuta  baadae kwa wanayopata
Wakristo,  na ni kwa sababu gani wengi wanaondoka  kutoka
kwenye Ushirika  wa Madhehebu ya wa-Injilisti.
 
Masomo haya  lengo lake ni kukupa mjengo wa  utaratibu
wako mwenyewe  kuchunguza maandiko, ili kwamba nawe pia
uweze  basi kuamini muunganiko kati ya kusikia  Injili ya kweli na
kuwa na imani  ya kweli mara  nyingi kumejitokeza wazi  katika
taarifa ya kuhubiri injili.

• “Wakorintho wengi waliposikia waliamini wakabatizwa”
(mdo 18:8)
• Watu wasikie neno la Injili, waamini ( mdo 15:7)
• Ndivyo tuhubirivyo, na ndivyo mlivyoamini'(1 Kor. 15:11)
   13

• ‘Mbegu’  Kwenye mfano wa mpanzi  ni neno la Mungu
(Luka 8:11) wakati katika huo wa mti wa haradali  ni imani ( Luka
17:6) kwa kuona kwamba imani huja  kutokana na kupokea'Neno
kwa imani’ ( Rum 10:8) “Maneno ya imani,  na mafundisho
mazuri” ( 1Tim 4:6), katika moyo ambao upo  wazi kumwamini
Mungu  na neno lake  (Gal 2:2, Ebr 4:2)

• Mtume Yohana anaisema taarifa  iliyoandikwa ya maisha
ya Bwana  kuwa anasema' kweli ( Yaani ukweli) ili nanyi mpate
kusadiki’ ( Yohana 19:35).Basi neno la Mungu  limeitwa
‘Kweli’(Yoh:17:17) ili mpate  kuamini.

1.2 Nafsi yake Mungu

Ni mwenye enzi, Mungu aliyeandikwa katika Biblia  na
kwamba ni kweli, mtu wa kugusika, naye yupo katika umbo.
Vilevile ni mafunzo ya kwanza  ya Ukristo  kuwa Yesu ni mwana
wa Mungu. Ikiwa Mungu hana umbo , basi  haiwezekani yeye
kuwa na mwana  ambaye alikuwa ni 'Chapa ya nafsi yake' (Ebr 1:3)
Tena  inakuwa vigumu kuendeleza  maisha ya uhusiano wake na
mungu  ikiwa Mungu  ni wazo lililo kwenye akili zetu,
Mkusanyiko wa roho  mahali popote juu katika  anga lisilo na kitu.
Ni huzuni  kusikia kwamba dini za watu wengi  zina wazo lisilo la
kweli  lisilotambulika kuhusu Mungu. Yeye akiwa mkubwa mno
kuliko sisi,  inaeleweka ya kwamba imani  ya watu wengi imeweka
kikwazo kwenye ahadi  dhahiri  kuwa mwishowe tutamwona
Mungu. Israeli  walikosa imani ya kumwona Mungu  alivyo  (Yoh.
5:37) ni dhahiri ana umbo halisi, Imani hii huja kutokana na
kumjua Mungu kwa kuamini neno lake

14

 Heri walio safi wa moyo, Maana watamwona Mungu (Math
5:8)
Na watumwa wake (Mungu) watamtumikia, nao watamwona
uso wake, na jina   lake(Jina la Mungu ) litakuwa katika vipaji vya
nyuso zao (Uf 22:3-4)

Tumaini hili la ajabu kama kweli tunaliamini litaonyesha
matokeo ya matendo  kwenye maisha yetu:

• Tafuteni kwa  bidii kuwa na amani  na watu wote  na huo
utakatifu, ambao hakuna mtu atakaye mwona  Bwana asipokuwa
nao (Ebr 12:14)
• Tusiape, kwa kuwa  aapaye kwa mbingu,  Huapa kwa kiti
cha  Mungu na kwa yeye  na kwa yeye aketiye juu yake  ( Math
23:22) hii itakuwa haina maana ikiwa Mungu  sio mtu mwenye
mwili.
• Tutamwona kama alivyo (akidhihirika katika kristo ) na kila
mwenye matumaini  haya katika yeye  hujitakasa, kama yeye
alivyo mtakatifu (1 Yoh 3:2,3)

Katika maisha yetu haya kumfahamu Mungu wetu wa
mbinguni,  hakujakamilika sana. Tunaweza kutazama mbele,
kupitia giza linalotatanisha la maisha haya hadi mwisho wa
kukutana naye. Kumwona kwa macho yetu hapana shaka kutakuwa
sawa na kumfahamu kwa akili  zaidi. Kutoka vina vya masumbufu
ya mwanadamu. Ayubu aliweza kufurahia  uhusiano wake wote na
Mungu  ambao utimilifu wake  atauona mwisho wa siku.

Na  baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi (Yaani katika
mauti),Lakini pasipokuwana mwili wangu  (Yaani pasipo mwili
unaoharibika ) nitamwona Mungu;Nami nitamwona mimi nafsi
yangu,na macho yangu yatamtazama, wala si mwingine (Ayubu
   15

19:26,27). Mtume Paulo aliyatazamia maisha mengine  yasiyo
machungu  yasiyo na msukosuko: “Maana wakati wa sasa tunaona
kwa kioo kwa jinsi  ya fumbo; Wakati ule tutaona uso kwa  uso” (
1Kor 13:12)

USHAHIDI WA  AGANO  LA  KALE
Ahadi hizi  zilizo katika Agano Jipya  zimejengwa juu kwenye
ushahidi wa mambo yake makubwa  ya  Agano la kale, Kuwa ni
Mungu aliye na mwili. Ushahidi hauwezi kukaza zaidi  lakini ni
mwanzo wa kukubali  hali ya Mungu kama tunataka kuwa  na
ufahamu wa kweli  yoyote  kuhusu dini ambayo msingi wake  upo
kwenye Biblia. Agano la Kale lina mazungumuzo ya Mungu kuwa
ni mtu na mtu uhusiano wa mtu na mtu pamoja  Mungu, ambao
Agano la Kale na Jipya linausema  ni wa pekee kwa  tumaini la
Ukristo  wa kweli. Yafuatayo ni majadiliano ya nguvu  kwa ajili
yake, Mungu aliye na mwili.

“Mungu akasema, Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura
yetu” (Mwa. 1:26) Hivyo mtu amefanywa kwa mfano  na sura ya
Mungu, Kama ilivyodhihirika kupitia Malaika. Yakobo 3:9
anasema … Wanadamu waliofanywa kwa mfano  wa Mungu.
Maneno haya hayatumiki kutaja  mfano wa akili ya mwanadamu,
kwa kuwa hali ya fikra zetu  zipo mbali kabisa toka zake Mungu na
katika njia nyingi  kwa kikubwa  zimepingana na haki
yake.”Maana  mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si
njia zangu, asema Bwana. Kwa maana kama vile mbingu  zilivyo
juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu  zi juu sana  kuliko njia
zenu, na mawazo yangu  kuliko mawazo yenu” ( Isa 55:8 - 9 ).
Kwa hiyo mfano na sura, tunavyoshirikiana naye Mungu, inabidi
uwe ni mfano wa mwili- Lakini yeye hana wa dhambi.
 
16

Popote Malaika  walipoonekana duniani wamesemwa kuwa
wana umbo la watu, kwa mfano, Abrahamu aliwakaribisha malaika
bila kujua, akizania kuwa walikuwa watu wa kawaida. Sisi jinsi
tulivyoumbwa kwa mfano wa Mungu kwa kweli maana yake ni
kwamba tunaweza kufahamu  jambo lingine kuhusu mtu halisi,
ndivyo tulivyo, lakini tunafanana. Basi,  Mungu tunaye mshabihi
siyo mtu mwingine asiyedhahiri ambaye hatuwezi kumfikiria.

“Wao wenyewe Malaika wanafanana na Mungu. Hivyo
Mungu aliweza kumsema Musa, “Kwake nitanena mdomo kwa
mdomo, maana wazi wazi wala si kwa mafumbo. Na umbo la
Bwana yeye ataliona” (Hesabu 12:8) Haya yalikuwa yanamtaja
Musa, akifunzwa na Malaika  aliye kuwa na jina la Bwana (Kut.
23:20:21) Ikiwa Malaika alikuwa na umbo la Bwana, Inaonyesha
kuwa Mungu amefanana na Malaika  Yaani - Kimwili  ana umbo la
Mwanadamu. “BWANA alisema na Musa uso kwa uso  kama vile
mtu asemavyo na rafiki yake. (Kut. 33:11: Kum. 34:10 ). Bwana
alijidhihirisha katika Malaika wake, ambaye uso na kinywa
alifanana na Bwana mwenyewe.

 “Kwa maana yeye anatujua umbo letu,  (Zab. 103:14).Ana
tutaka yeye,  tumfikirie kuwa ni mtu, Baba ambaye tunaweza
kuunganishwa naye.Huyu ataelezwa kwa ushahidi mwingi  wa
mikono ya Mungu, Viganja,Macho  n.k. Ikiwa Mungu alikuwa ni
furushi la Nafsi mahali fulani katika mbingu, ambazo inabidi ziwe
Mungu, ni wazo letu kama tukitaka utu wake;  basi ushahidi huu
unatupotosha kukuza  kusudi lolote.

 “Maelezo ya sehemu ya makao ya Mungu, Wazi wazi
yanaonyesha kwamba “Mungu” ana mahali pake; “Mungu yuko
Mbinguni”( Mhubiri 5:2);Maana ametazama toka patakatifu pake
pa juu, toka mbinguni BWANA ameiangalia nchi (Zab 102:19,20);
   17

“Usikie huko mbinguni, Makao yako” (1Fal. 8:39). Lakini kwa
kupambanua zaidi kuliko hivi tunasoma kwamba Mungu ana “Kiti
cha Enzi” (2 Nya. 9:8, Zab 11:4; Isa. 6:1,66:1).Lugha kama hii ni
ngumu  kuitumia nafsi isiyo wazi  kabisa, inayokaa katika milki ya
Kimbingu. Mungu amesemwa kuwa “Ameshuka kuja chini”
wakati mwenyewe anapojidhihirisha. Hapa panadokeza  makao ya
Mungu yaliyo mbinguni. Inakuwa vigumu kueleza wazo  la
udhihirisho wa Mungu  bila kukubali hali ya umbo la Mungu. Isaya
45 ina ushahidi tele wa Mungu  kujihusisha kwake  katika mambo
ya watu  wake: “Mimi ni BWANA, wala hapana mwingine …..,
mimi ni  BWANA anayetenda haya yote …., Mimi, BWANA
nimeiumba Ole  wake ashindanaye na Muumba wake … Mimi,
naam, mikono yangu mimi,  imezitanda mbingu …, niangalieni
mimi mkaokolewe, enyi ncha zote  za  dunia. mstari hasa kweli huu
wa mwisho  unaonyesha uwepo wake Mungu - Anawataka watu
wamwangalie yeye, Kuwaza uwepo wake  halisi pamoja na jicho la
imani.

Mungu amejifunua  kwetu akiwa ni mwenye kusamehe
anayesema, maneno kwa watu. Hata hivyo msamaha  na usemi
unaweza  tu kutoka kwa mtu: ni matendo ya akili, Hivyo Daudi
alikuwa ni mtu  aliyeupendeza moyo wa Mungu  (1 Sam 13: 14),
inaonyesha kwamba Mungu ana moyo, unaoweza kunakiliwa kwa
kiwango kidogo na mtu, ingawa mwanadamu wa mwili
haupendezi moyo wa Mungu. Mafungu ya maneno kama  BWANA
akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu  duniani akahuzunika
moyo (Mwa. 6:6), hufunua hisia ya Mungu, mwenye ufahamu
kuliko kuwa kishindo cha roho  ya kuwazika katika hewa. Hapa
tunasaidiwa tukubali  jinsi  kwa kweli tunaweza pande zote mbili
kumpendeza na kutokumpendeza,  Kama mtoto anavyoweza  kwa
baba wa mwili.

18

IKIWA MUNGU SI MTU MMOJA
Kama  Mungu si wa kweli, mmoja mwenye kuwepo, Basi
wazo la kupenda  mambo ya roho ni vigumu  kushikana nayo.
ikiwa Mungu ni mwenye haki kabisa  lakini si mtu mwenye umbo,
basi kwa kweli hatuwezi kuiwazia  haki yake ilivyodhihirika kwa
watu. Pande zote mbili, Ukristo uliokenguka na wayahudi  wana
wazo la kwamba haki ya Mungu  inaingia katika maisha ya watu
kwa njia ya
‘Roho Mtakatifu’  Asiyedhahiri  ambaye kwa namna
isiyoeleweka tunafanywa  mfano kwenye akili ya  Mungu, na
kukubalika kwake. Kwa maneno mengine, mara tukitambua ya kwa
mba yupo  mtu mwenyewe aitwaye Mungu, basi tunaweza
kurekebisha tabia  yetu kufuata atakavyo, Kwa msaada wake
utokao  kwenye ushawishi wa neno lake  na kwa kuleta  sifa
inayoonyesha tabia ya  Mungu katika utu wetu.

Lengo la Mungu ni kujidhihirisha mwenyewe  katika mkutano
wa watu waliotukuzwa. Jina la kumbukumbu yake, YEHOVA
ELOI, linamaanisha hivi ( Atakaye kuwa kwa wenye nguvu ni
tafsiri  iliyo karibu sahihi.)  ikiwa Mungu si mtu mwenye umbo,
basi thawabu ya waaminifu  katika ufalme wa Mungu  ujao duniani
inaonyesha ya kwamba  watakuwa nayo wazi tena dhahiri
wakiwepo  katika mwili, Ingawa hawatakuwa katika udhaifu  wa
mwili wa Mwanadamu tena. Ayubu alitamani' Siku ya mwisho’
atakapofunguliwa na mwili wake ( Ayubu 19:25:27); Abrahamu
itabidi awe mmojawapo  wa wale wengi wa hao  walalao katika
mavumbi ya nchi ambao wataamka…… Kwa uzima wa Milele wa
nchi ya Kanani (Dan. 12:2) hivyo basi  ataweza kupata ahadi ya
urithi wa milele  wa nchi ya kanaani, Sehemu inayoonekana katika
dunia hii
(Mwa. 17:8.)  “ Na wataua wake watashangilia….. waimbe
kwa sauti  kuu  vitandani mwao….. ili  kufanya kisasi juu ya
   19

mataifa  (Zab 132: 16; 149: 5,7) Kushindwa kwa watu wote wa
pande mbili, Wayahudi na watu wa mataifa,

Kutambua mafungu ya maneno kama haya  vyema, kwa
ukubwa wa maneno  yenyewe Kuletwa ahadi za kuonekana kwa
Abrahamu, kumeongoza watu kwenye imani potovu la' Nafsi haifi’
ya kwamba Mwanadamu halisi anakuwepo  hai akifa. Wazo hili
halina msaada wa Biblia kabisa. Mungu  hapatikani na mauti, Mtu
mwenye utukufu, analifanya lengo lake, ili kwamba wanaume na
wanawake waweze kuitwa na kuishi katika ufalme wake  ujao
kwenye dunia hii, Kushiriki sifa, zilizoelezwa katika umbo la
mwili.

Waaminifu  wameahidi wa kwamba watarithi mwili wa
Mungu  (2 Pet. 1:4) Ikiwa Mungu si mtu mmoja, basi hii ina maana
tutaishi  milele kwa roho zisizo na mwili. Lakini hili si fundisho la
Biblia. Tutapewa mwili kama ule wa Yesu. (Flp. 3:21), Nasi
tunajua kwamba tutakuwa na  mwili halisi kwenye ufalme  mwili
utakaokuwa na mikono  macho na masikio  (Zek. 13:6, Isa. 11:3 ),
mafunzo ya Mungu  kuwa ni  Mmoja, kwa sababu  hii yanasimulia
Injili ya Ufalme.

Itakuwa  wazi kwamba  hakutaweza kuwa na wazo la kujua
Ibada,  dini au uhusiano  mmoja na Mungu  mpaka itambulike
kuwa Mungu  ni mtu mmoja, na kwamba kwa mwili sisi ni mfano
wake. Ingawa ni mfano usio kamili sana unahitajika kuukuza
kufuata  mfano wa akili yake, Hivyo basi, tutaweza kupata
utimilifu wa mfano wake unaoonekana katika ufalme wa Mungu.
Maana nyingi zaidi  na faraja tunaweza kupata kutoka  mafunzo ya
maneno ambayo yanamtaja Mungu kuwa ni Baba aliye na upendo,
akiturudi kama Baba afanyavyo kwa mwanae (mfano. Kum. 8:5).
Katika maneno yenyewe  ya mateso ya Kristo  tunasoma
20

kwamba,'Lakini BWANA aliriidhika kumchubua’  (Isa. 53:10
),Ingawa  “Alimlilia Mungu” aliisikia sauti yangu…….. Kilio
changu kikaingia masikioni mwake (Zab.18:6). Ahadi ya Mungu
kwa Daudi kuhusu mzao atakaye kuwa ni mwana wa Mungu
ilitakiwa azaliwe kwa Muujiza kwa Mwanadamu; Ikiwa Mungu
hakuwa ni mtu mmoja, asingekuwa na mwana huyo.

Kumfahamu Mungu kwa usahihi ni ufunguo unaofungua
maneno  mengi mengine ya muhimu katika mafundisho ya Biblia.
Lakini kama uongo mmoja  huongoza kwenye uongo mwingine,
Hivyo dhana potovu juu ya mungu inaficha utaratibu  wa kweli
ambao maandiko yanatoa. Kama umepata kuona  kuwa hii sehemu
inadhibitisha, au hata ikiwa ni ndogo, basi, swali linakuja. Je?
Unamjua Mungu kweli?. Sasa  tutachunguza maandiko ya Biblia
zaidi kuhusu  yeye.

1.3 Jina La Mungu Na Tabia Ya Sifa Yake

Ikiwa Mungu yupo, inafaa kufikiri kuwa atakuwa  amevumbua
njia nyingine ya kutuambia habari zinazo mhusu yeye mwenyewe.
Tunaamini ya kwamba Biblia ni ufunuo wa Mungu kumjulisha
Mwanadamu,  na humo ndani ya kitabu tunaona kudhihirika tabia
ya sifa ya Mungu. Hii ndio sababu Neno la Mungu linasemwa
kuwa ni'Mbegu’ yake (1 Petro 1:23) Kwa kuwa kama likigeuza hali
ya mioyo yetu, kiumbe mpya anaumbwa ndani yetu ambaye ana
sifa za Mungu  (Yakobo. 1:18,  2Kor. 5:17). Kwa hiyo sisi
wenyewe tunapotumia  zaidi neno la Mungu na kuchukua masomo
sisi wenyewe, ndivyo zaidi tutafanana  mfano wa mwana wake (
Rum, 8:29) ambaye kwa tabia ya sifa alikuwa mfano kamili  wa
Mungu (Kol. 1:15).Kwa hii imelala thamani ya kusoma sehemu  za
historia ya Biblia, Zimejaa kadhia ya  masomo jinsi Mungu
   21

alivyojishughulisha na watu pamoja na matifa, Daima  akionyesha
msingi ule ule wa sifa.

Katika Kiebrania jina la mtu mara nyingi  lilileta tabia ya sifa
zao  au  taarifa zinazowahusu. Mifano mingine iliyowazi:

• ‘Yesu’'Mwokozi’  Kwa kuwa atawaokoa watu wake kutoka
dhambi zao’ (Math. 1:21)
• ‘Abrahamu’'Baba wa mkutano mkubwa’  Maana
nimekufanya kuwa baba wa mataifa mengi’(Mwa. 17:5)
• ‘Hawa (Eva)'Uhai’ Kwa kuwa alikuwa mama wa wenye
uhai wote (Mwa. 3:20)
• ‘Simeoni’'Kusikia’ Kwa kuwa bwana amesikia kwamba
nalichukiwa, kwa sababu amenipa mwana  huyu (Mwa. 29: 33).
Katika Yeremia 48:17, kuwajua watu wa Moabu ni sawa sawa
na kufahamu jina la moabu.Mara nyingi zaburi  zinamlinganisha
Mungu mwenyewe na jina lake, neno lake na matendo (Zab. 103:1,
105:1, 106:1,2,12,13.) Kwa sababu hii itegemewe kwamba majina
ya Mungu  na heshima vitatupatia  habari nyingi kuhusu yeye
mwenyewe, kwa kuwa  yapo maelekeo mengi  ya tabia ya sifa  na
kusudi  kwa kweli  ana jina zaidi ya moja.Somo lenye kueleza
jambo moja moja  la jina Mungu  linafaa baada ya Ubatizo;
kufahamu zaidi sifa na tabia ya Mungu  kumeelezwa katika jina
lake, ni jambo lingine ambalo  liendelee wakati wa maisha yetu
yote katika Bwana. Linalofuata sana kwa hilo, mengi ni Utangulizi.

Musa alipotaka aelimishwe kwa undani  kuhusu  Mungu ili
imani yake  iimalike wakati wa kipindi kisicho sahaulika sana  cha
maisha yake. Malaika,'Alitangaza
jina
la BWANA:
BWANA,BWANA Mungu, Mwingi wa huruma, Mwenye fadhili,
Si mwepesi wa hasira, Mwingi wa rehema na kweli, Mwenye
kuwaonea huruma watu elfu elfu, Mwenye kusamehe uovu na
22

makosa na dhambi; Wala si mwenye kumhesabia mtu  mwovu
kuwa hana hatia,’ (Kut. 34:5-7)

Huu ni ushahidi ulio  wazi wa kwamba  majina ya Mungu
yanaweka sifa zake.Tendo la kuwa nazo ni uhakika  kuwa ni mtu
mmoja, si busara  kufikiri ya kwamba  fungu la roho laweza kuwa
na dalili na sifa ya tabia  hizi  ambazo vile vile  zaweza
kuendelezwa  ndani yetu wanadamu.

Mungu amechagua hasa jina moja  ambalo amependa ajulikane
na kukumbukwa na watu wake, ni kwa  ufupi, maelezo mafupi, ya
kusudi lake kwa watu.

Israeli walikuwa watumwa Misri, Walihitajika kukumbushwa
lengo  la Mungu kwao. Musa aliambiwa awaambie  Jina la Mungu,
ili kwamba  hili liwasaidie  kuwaletea kusudi la kuondoka Misri na
kuanza safari kuelekea nchi ya Ahadi (1Kor. 10:1) Nasi pia
tunahitajika  kuelewa mambo ya msingi yahusuyo jina la Mungu
kabla ya kubatizwa na kuanza  safari yetu ya kuelekea Ufalme wa
Mungu. Mungu aliwaambia  Israeli  kuwa Jina lake alikuwa
YAHWEH-YAHU (Zab 89:8 uv); Maana yake“Mimi niko ambaye
NIKO” au limetafsiriwa kwa usahihi zaidi,'Nitakuwa ambaye
Nitakuwa’(Kut 3:13-15) Jina hili, kidogo likapanuka wakati ule:”
Tena  Mungu akamwambia  ( Ikiwa ni nyongeza) Musa, Hivi
ndivyo utawaambia wana wa Israel, BWANA (Yahweh) Mungu
wa Babu zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, Mungu wa
Yakobo, ….Hili ni Jina  langu Milele, la kumbukumbu yangu kwa
vizazi vyote. (Kut. 3:15). Kwa sababu hiyo jina kamili la Mungu ni
“BWANA Mungu”
Zaidi Agano la kale liliandikwa kwa Kiebrania  na tafsiri ya
Kiswahili ni lazima kutukia visivyo sawa sawa  wakati ujapo wa
kutafsiri maneno ya Kiebrania  hasa neno “Mungu”  mengi ya
   23

maelezo moja moja  yakosekana  - Tafsiri yetu ya Kiswahili
imetoka kwenye  Kiingereza. Moja ya maneno yanayotumiwa  na
Kiebrania  limetafsiriwa'Mungu’ ni Elohim (ELOI) maana
yake'Wenye Nguvu’ Kumbukumbu ya jina la Mungu, jina ambalo
anatutaka  tumkumbuke, kwa sababu hiyo.

YAHWEH  ELOHIM  -  YAHU  ELOI
 Maana yake
ATAKAYEDHIHIRIKA KATIKA KUNDI LA WENYE
NGUVU.

Kwa hiyo ni kusudi la Mungu kuidhihirisha tabia ya sifa yake,
Umuhimu wake katika kundi kubwa  la watu. Kwa kulitii neno lake
tunaweza  kukuza sifa zingine za Mungu  ndani yetu wenyewe
sasa, hivyo basi kadri ya busara  sana. Mungu alijifunua
mwenyewe  kwa waamini wa kweli katika maisha haya.lakini jina
lake Mungu ni la Unabii wa wakati ujao  hapo dunia itakapo jaa
watu  watakao kuwa sawa naye, pande mbili kwa tabia na mwili
(2Petr 1:4). Ikiwa tunataka kuungana na lengo la shabaha  ya
Mungu na kuwa kama Mungu bila hata kufa tena, kuishi milele
katika uadilifu  wote uliokamilika, basi yatupasa  sisi wenyewe
tujiunge na jina lake.

Namna ya kufanya hivi ni kubatizwa katika jina, yaani la
Yahweh Elohim (Math. 28:19). Hili linatufanya tuwe watoto
(‘Uzao’) wa Abrahamu (Gal,. 3:27-29) uliohaidiwa kurithi milele
nchi (Mwa. 17:8; Rum. 4:13) Kundi la wenye nguvu  (Elohim Eloi)

ambao unabii wa jina la Mungu  utatimilika. Limeelezwa
zaidi kwa habari katika  somo la  3.4. 
24

1.4  Malaika
Yote ambayo  tumeyapima sana katika somo hili yanaletwa
pamoja kwenye tafakari ya Malaika:

• Viumbe walio na mwili
• Huchukua jina la Mungu
• Wao ni njia ambayo roho wa Mungu  anatenda kazi ya
kutimiza mapenzi yake
• Wanapatana tabia na kusudi lake
• Na kwa hiyo wanamdhihirisha yeye.

Tumetaja kwenye somo la 1.3  ya kwamba moja kati ya
maneno  yanayotumika zaidi katika  Kiebrania lililotafsiriwa
“Mungu” ni' Eloi’ ambalo hasa maana yake ' Wenye nguvu’
hawa,'Wenye nguvu’  ambao huchukua jina la Mungu
wanapotokea wana weza  kuitwa 'Mungu’  kwakushirikiana kwao
pamoja na naye karibu. Hawa viumbe wanaitwa Malaika.

Taarifa ya uumbaji wa ulimwengu katika mwanzo  1
inatuambia ya kwamba Mungu  alitamka amri halisi kuhusu
Uumbaji'Ikiwa hivyo’ walikuwa ni Malaika waliotimiza amri hizo:

“Enyi Malaika zake, mliohodari mtendao neno lake,
mkiisikiliza sauti ya neno lake (Zab. 103:20).

Kwa sababu hii  busara husadiki kuwa tunaposoma 'Mungu’
akiumba ulimwengu, kazi hii kweli ilifanywa na Malaika. (Ayubu
38:4-7) anadokeza vile vile namna hii. Sasa ni wakati mzuri
kuelezea kwa kifupi  matukio ya uumbaji kama yalivyoandikwa
Mwanzo 1:

   25

Siku ya Kwanza‘   Mungu  akasema, Na iwe nuru, Ikawa’
(Mstari  3)

Siku ya Pili
'Mungu  akasema, Na iwe anga katikati ya
maji, likayatenga  maji na maji.Mungu akalifanya anga ,akayatenga
yale maji   yaliyo juu ya anga na yale yaliyo chini ya anga: Ikawa
hivyo’  (Mstari 6,7)

Siku ya Tatu ‘Mungu  akasema, Maji yaliyo chini ya
mbingu na yakusanyike  mahali pamoja, (akifanya Bahari na
Bahari kuu)  ili pakavu paonekane; Ikawa hivyo’ (Mstari wa 9)

Siku ya Nne   ‘Mungu akasema, Na iwe  mianga katika
anga la mbingu… Ikawa hivyo’ (Mstari 14:15)

Siku ya Tano ‘Mungu akasema,  Maji na yajae kwawingi
na kitu kiendacho chenye uhai …. ndege waruke juu ya nchi …..
Mungu akaumba kila kiumbe  chenye uhai (Mstari wa 20:21),
Ikawa hivyo.

Siku ya Sita ‘Mungu akasema, Nchi na izae kiumbe
haikwa jinsi  zake…. Mnyama wa kufugwa,nacho kitaambaacho
…. Ikawa hivyo (Mstari 24)

Siku hiyo hiyo ya sita mtu aliumbwa. Mungu akasema, na
tufanye  mtu  kwa mfano wetu, na kwa sura yetu  (Mwa 1:26).
Tuliwahi kutoa maelezo  juu ya mstari  huu katika somo la 1.2.
Kwa muda uliopo, tunataka kujua hapa ya kwamba.'Mungu’ sio tu
anatajwa Mungumwenyewe katika utu'Na tufanye mtu’ inaonyesha
kuwa Mungu anatajwa  mtu zaidi ya mmojaNeno  la Kiebrania
linalotafsiriwa hapa'Mungu’ ni Elohim (Eloi), Maana yake'Wenye
nguvu’ Ukiwa ni ushahidi unaotaja Malaika. Ukweli ni kwamba
26

Malaika  walituumba sisi kwa mfano wao  maana yake ni kuwa
wana sura ya mwili ule ule kama tulio nao. Kwa sababu hiyo ni wa
kweli, wa kugusika, viumbe wenye mwili, wakishiriki mwili ule
ule kama wa Mungu.

‘Mwili’ Kwa maana  hii unatajwa kwa msingi jinsi mtu
mwingine alivyo kwa sababu ya muundo wa mwili wao. Katika
Biblia ipo “Miili” ya  aina mbili  katika  maana halisi ya neno
haiwezekani kwa wakati huo huo kuwa miili hii ya aina mbili.


 Mwili wa Mungu (‘Mwili wa Uungu’)
 Hauwezi kutenda dhambi (Mkamilifu)  Rum 9:14,6:23;
Zab. 90:2, Math 5:48,Yak 1:13)Haupatikani na Mauti ( 1Timotheo
6:16)
 Una nguvu tele na uweza ( Isaya 40:28)

Huu  ndio mwili wa Mungu na Malaika na ambao alipewa
Yesu  baada ya kufufuliwa (Matendo 13:34; Ufunuo  1:18; Ebr.
1:3) Huu ndio mwili  ambao  tumeahaidiwa kupewa  (Luka
20:35,36; Isa. 40:28,31)

 Mwili wa mwanadamu
Hujaribiwa na kutenda dhambi ( Yak 1:13-15 )kwa nia mbaya
ya asili (Yer 17:9; Marko 7:21-23) Huangamia mautini, Yaani
unapatwa na kifo ( Rum. 5:12,17; 1Kor  15:22)  Una kikomo cha
nguvu, sehemu mbili,  kwa mwili (Isa. 40:30) na kwa akili ( Yer
10:23)

Huu ni mwili ambao watu wote, wema na wabaya, kwa sasa
wanao mwisho  wa mwili huo ni kifo (Rum 6:23). Ulikuwa ni
mwili ambao  Yesu alikuwa nao  wakati wa maisha yake  ya  mwili
   27

unaokufa  hapa duniani (Ebr. 2:14-18,Rum. 8:3 Yoh 2:25, Marko
10:18)

MATENDO YA KUONEKANA  NA  MALAIKA
Malaika wakiwa na mwili wa Uungu, inabidi wawe hawana
dhambi na kwa sababu hiyo hawawezi kufa  kwa kuona kwamba
dhambi  huleta mauti (Rum. 6:23). Inapasa wawe na umbo halisi na
mwili wa kuwepo mauti  “Na yaletwe basi maji kidogo  ukanawe
miguu, mkapumzike chini ya mti huu”(Mwanzo 18:4)

Wawili kati ya hao Malaika wakati ule  walikwenda kwa lutu
katika mji wa Sodoma. Tena, walitambuliwa kuwa ni watu  na lutu
pamoja na watu wa  Sodoma.'Basi,  wale malaika Wawili wakaja
Sodomaa jioni aliowakaribisha wakae kwake usiku. Lakini watu
wa Sodoma wakaja kwenye nyumba yake, wakiuliza kwa namna ya
kutisha,'Wawapi wale watu waliokuja  kwako usiku huu ?’ Lutu
akawasihi,' Watu hawa msiwatende neno’  Taarifa ya maandiko ya
Mungu  pia inawaita ni'Watu’, Wale watu ( Malaika )
wakanyoosha mikono yao, wakamwokoa Lutu,  Basi wale  watu
wakamwambia Lutu … BWANA ametutuma tuuharibu  Sodoma
(Mwanzo 19: 1,5,8,10,12,13).

Ufafanuzi wa  Agano jipya  juu ya matukio haya
yanadhibitisha kwamba Malaika wanafanana na umbile la watu.
“Msisahau kuwafadhili wageni; Maana kwa njia hii wengine (Kwa
mfano Lutu na Abrahamu ) waliwakaribisha Malaika pasipo kujua
(Ebr 13:2)

Yakobo alishindana usiku kucha na mtu mmoja ( Mwa 32:24)
ambaye baadae tumeambiwa kuwa  alikuwa Malaika (Hosea 12:4)

28

Watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe
walikuwepo kwenye  ufufuo (Luka 24:4) na wakati wa kupaa (Mat.
1:10) Yesu, kwa  uhakika hawa walikuwa ni Malaika. Ona
vidokezo vya'Kipimo cha Kibinadamu, maana yake cha Malaika’
(Uf 21:17).

MALAIKA   HAWATENDI    DHAMBI
Malaika wakiwa na mwili wa Uungu, hawawezi  kufa, kwa
sababu dhambi huleta mauti, Basi wao hawawezi  kutenda dhambi.
Maneno ya asili katika lugha ya Kiyunani na Kiebrania
yaliyotafsiriwa'Malaika’  maana yake ni mjumbe;  Malaika ni
wajumbe au watumishi wa Mungu, Watiifu kwake, Kwa hiyo
hawafikiriwi wao kuwa ni wenye dhambi. Kwa hivyo neno la
Kiyunani’Agelos’
lililotafsiriwa'Malaika’

vile vile
limetafsiriwa'Wajumbe’ Wanaposemwa wanadamu kwa mfano
Yohana mbatizaji, (Math 11:10) na  wajumbe wake (Luk. 7:25)
wajumbe wa Yesu (Luk. 9:52) na watu walioupeleleza mji wa
Yeriko (Yak. 2:25). Kwa kweli  inawezekana kwamba'Malaika’
katika maana ya wajumbe  wanadamu wanaweza kutenda dhambi.

Mafungu ya maneno yafuatayo ni wazi kwamba  Malaika wote
( Sio tu baadhi yao) kwa umbile ni watiifu kwa Mungu, na hivyo
hawawezi kutenda dhambi.

‘BWANA  ameweka kiti chake cha Enzi mbinguni Na Ufalme
wake unavitawala vitu  vyote (Yaani  haiwezekani kuwepo uasi juu
ya Mungu mbinguni)Mhimidini BWANA, Enyi  Malaika zake,
Ninyi mlio hodari, mtendao neno lake, Mkisikiliza sauti ya  neno
lake Mhimidini BWANA, enyi majeshi yake Yote;  Ninyi
watumishi wake  mfanyao mapenzi yake (Zab. 103:19-21)

   29

“Msifuni, enyi Malaika wake wote …. Majeshi yake yote (
Zab 148: 2 )  Je ! hao wote si roho (Malaika ) watumikao,
wakitumwa kuwahudumia wale watakaourithi wokovu ? ( Ebra. 1:
13,14 )

Kurudiwa kwa neno'Wote’ linaonyesha ya kwamba Malaika
hawajagawanyika katika makundi mawili, kundi moja zuri na
jingine lenye dhambi. umuhimu wa kufahamu vema  umbile la
malaika ni kwamba  thawabu ya waaminifu ni kushiriki mwili wao.
“Wale  wahesabiwao kuwa wamestahili…. Hawaoi  wala
hawaolewi … wala hawawezi kufa tena. kwa sababu huwa sawa
sawa na Malaika (Luk 20:35, 36).

Hili ni neno la muhimu  kulishika. Malaika hawawezi
kufa'Maana hatwai asili ya Malaika (Kwa kuwa tangu asili
hawajatenda dhambi). Ila atwaa asili ya mzao wa Abrahamu ,sababu

ya dhambi’ (Ebr 2:16) Ikiwa Malaika waweza kufanya
dhambi, Basi wale ambao  watakuwa wamestahili thawabu  ya
Kristo atakapo kuja bado  wataweza kutenda dhambi pia, Na kwa
kuwa dhambi huleta mauti  (Rum 6:23)  kwa sababu hiyo
hawataweza kuwa na uzima wa milele, kama tukiwa na uwezekano
wa kutenda dhambi  ni kufanya ahadi ya Mungu  ya uzima wa
milele  haina maana, kwa kufahamu kuwa thawabu yetu ni
kushiriki  mwili ule wa Malaika.  Ushuhuda wa'Malaika (Luk.
20:35,36) unaonyesha kwamba hakuna aina ya Malaika wema na
wenye dhambi; ipo aina moja ya Malaika tu.

Ikiwa  Malaika waweza kutenda dhambi, Basi Mungu
ameachwa  hana  nguvu  za kutenda  tendo la haki  katika maisha
yetu  na mambo ya ulimwengu, kwa kufahamu kuwa ameeleza
kwamba anafanya matendo yake kwa njia ya Malaika zake( Zab
103:19-21) Wamefanywa kwa'Roho wa Mungu  katika  maana  ya
30

kwamba anatimiza  yote kwa nguvu zake. Akitenda kazi katika
Malaika  (Zab 104:4). Kwamba wanamwasi Mungu  haiwezekani.
Mkristo amwombe  kila siku, Mungu ili ufalme  uje duniani, ili
mapenzi yake yafanyike  kama sasa yanavyofanyika mbinguni
(Math 6:10) Ikiwa Malaika wa Mungu iliwapasa washindane na
Malaika wenye dhambi  huko mbinguni, basi,  kwa utimilifu
mapenzi yake  hayakuweza kufanyika huko,  na kwa sababu hiyo
hali hiyo hiyo itapatikana kwenye ufalme wa Mungu  ujao.
Kutumia maisha ya milele kwenye ulimwengu  ambao utakuwa ni
uwanja wa vita  kati ya dhambi na utii, kwa shida hayo sio
matazamio  ya kutia moyo, lakini hilo, kwa kweli, sio ndiyo suala
lenyewe.

MALAIKA  NA  WATU  WANAOAMINI
Ipo sababu nzuri ya kuamini kuwa kila mwamini wa kweli ana
Malaika pengine mmoja maalumu-wa kuwasaidia katika maisha
yao:-

 ‘Malaika wa BWANA hufanya kituo, akiwazungukia na
kuwaokoa  wamchao’  (Zab 34:7)
Mmojawapo wa wadogo hawa  waniaminio  (Yaani wafuasi
dhaifu- Zek, 13:7  Mat 26:31)…Malaika wao mbinguni siku zote
huutazama uso wa  Baba yangu’ (Mat.
18:6,10)
 Wakristo wa kwanza ni wazi waliamini kwamba Petro
alikuwa na  Malaika mlinzi  (Matendo 12:14,15).
Watu  wa Israeli  walipita katika bahari ya Shamu,
waliongozwa na malaika  kwenye jangwa  kuelekea nchi ya Ahadi.
Kutembea kupitia katika bahari ya shamu maana yake ni Ubatizo
wetu katika maji  (1Kor 10:1), Hivyo nasi  vile vile  ina maana
tusadiki  kuwa baadae tunaongozwa  na kusaidiwa na Malaika
   31

tunaposafiri katika jangwa la maisha  kuel;ekea nchi ya ufalme wa
Mungu.
Ikiwa  Malaika wana weza kuwa waovu  katika maana ya
kuwa wenye dhambi, basi Ahadi hizi za Malaika kuongoza  na
kushawishi katika maisha  yetu zinakuwa laana badala ya Baraka.

• Basi tufahamu ya kuwa Malaika ni Viumbe………
• Wenye  mwili ulio sawa na Mungu na huonekana kwa mwili
• Ambao  hawawezi kutenda dhambi
• Daima hufuata amri za Mungu
• Wao ni njia ambayo Mungu katika Roho  nguvu hunena na
• kutenda kazi (Zab. 104:4)

 LAKINI..?
Makanisa mengi ya'Kikiristo’ yana wazo la kwamba  Malaika
wanaweza kutenda dhambi, na kwamba Malaika wenye dhambi
sasa hivi wapo na  wao  wanahusika na dhambi pamoja na matatizo
yaliyopo hapa Duniani. Tutajadili zaidi vya kutosha juu ya
kutofahamu vema jambo hili  kwenye somo la  6. Kwa sasa
tutatengeneza vipengele vifuatavyo:-

Inawezekana kwamba uumbaji ulikuwepo  uliotutangulia sisi
wa kweli,  yaani huo ulioandikwa katika  Mwanzo 1. Pia inaweza
kusadikika ya kwamba  Malaika waliopo walikuja kuwa na
fahamu  za'Wema na Ubaya’ (Mwa. 3:5) walipo kuwa katika hali
kama hii  tuliyonayo katika maisha haya.

Ya kwamba  viumbe wengine walioishi kwa kipindi kile
walitenda dhambi hatujakatazwa kufikiri;  lakini yote haya ni
mawazo  ambayo mioyo ya watu  hupenda kujishughulisha. Biblia
yatuambia kile ambacho tunakihitaji  kujua kuhusiana na hali
iliyopo,  ambayo ni kwamba hawapo Malaika  watenda dhambi,
Malaika wote ni watiifu kwa Mungu kabisa.
32

Hawawezi kuwepo viumbe wenye dhambi mbinguni, kwa
kufahamu kuwa Mungu'ana macho safi na hawezi  kuangalia
uovu’ (Ab. 1:3) katika maelezo haya,  Zaburi 5:4,5  yatuambia:-

‘Mtu mwovu  hatakaa kwako.  wajivunao hawatasimama
mbele za macho yako’ yaani makao ya mbinguni. Jambo la
kwamba ulikuwepo  Uasi juu ya Mungu mbinguni na Malaika
watenda dhambi  ni wazo linalopingana kabisa  na maneno
yaliyotolewa.
       
 Neno
la kiyunani
lililotafsiriwa'Malaika’ maana
yake'Mjumbe’
linataja
wanadamu,
kama
tulivyoonyeshwa'Wajumbe’  wanadamu hawa wanaweza  kwa
kweli kufanya dhambi.

Ya kwamba upo uovu, viumbe wenye dhambi ambao juu yao
mwelekeo wa maisha yote yasiyofaa  wanaweza kutupiwa lawama
kwa kawaida ni moja ya  Imani zaidi iliyoshikiliwa  katika
Upagani.Kwa njia hiyo hiyo mambo yanayohusu Krismas
yameingia kwenye  kile kinachodhaniwa ni'Ukristo’ Basi, vile vile
Ukristo una fikra hizo za Kipagani

Yapo mafungu ya maneno  ya Bibilia yaliyojaa tele ambayo
yanaweza kutoeleweka kusaidia wazo hili la Malaika wenye
dhambi kwa sasa wapo. Haya yamepimwa katika 'Kumsaka
Shetani’  yanapatikana kwa  wachapishaji - Mafungu haya ya
maneno  hayawezi kuruhusiwa kupingana na mafunzo tele ya
Biblia  kwa kutofautiana na haya yaliyokwisha tolewa.


   33

Tumeacha  Kitambo sehemu ya 1:'Mungu ni roho’
(Yohana 4:24)

Katika somo la pili  tunafafanua  kwa  utaratibu zaidi  jinsi
Roho wa Mungu  alivyo. Tunaweza kutoa maelezo kwa ufupi
sababu zilizoonyeshwa  hapo kwa kusema kwamba  roho wa /ya
Mungu ni nguvu au pumzi yake ambayo kwa hiyo nafsi yake
mwenyewe,  Utu wake na tabia,  vimedhihirika kwa mwanadamu
kwa njia ya matendo yake ambavyo Roho huyo
anatimiza.Hivyo'Mungu ni Roho’ kama katika Yohana 4:24
atafsiriwe vema kwa kuwa Roho yake  ndiyo inafanya utu wake.

Mungu amesemwa kuwa yumo katika vitu vingi, kwa mfano:-

 ‘Mungu wetu ni moto ulao’   (Ebr. 12:29)
 ‘Mungu ni Nuru’

   (1 Yoh. 1:5)
 ‘Mungu ni Pendo

   (1 Yoh.4:8)
 ‘Neno (Kiyunani'Lagos’ - Mpango, Lengo,Kusudi, wazo)
  alikuwa Mungu’  (Yoh 1:1)

Hivyo,'Mungu’ ni sifa yake.  Ni kosa lililo wazi kuleta  sababu
za kupinga kwamba  sifa za upendo wa Mungu ni za kuwazika,
kwa kuwa tunasoma  kwamba 'Mungu ni pendo’  tunaweza
kumwita mtu mwingine  Mwema  wenyewe; lakini hii haina maana
kwamba  haupo bila mwili ni namna ya kuwepo yeye ndiko
kunatudhihirishia wema kwetu.

Roho ikiwa ni nguvu ya Mungu, mara nyingi tunasoma Mungu
akiituma au akiiongoza roho yake  kutimiliza mabo yake kwa
kupatana na mapenzi yake  na tabia ya sifa yake. Hata ameelezewa
kuwa anaumba roho  (Yaani Upepo UV). Kusema kwamba  Mungu
34

na roho yake katika maana safi iliyo halisi ni msemo ule ule kwa
namna nyingine - katika maana inakuwa  Uwepo wa Mungu.

Mifano ya  Mungu  akiiongoza Roho yake ni mingi,
inaonyesha mtengano wa Mungu na Roho yake:-

 ‘Yeye (Mungu)  aliyetia kati yao Roho yake mtakatifu’(Is. 63:11)
 ‘Nitatia Roho yangu  (Mungu)  juu yake  (Yesu )’ ( Math.12:18)
 ‘Baba huwapa  Roho mtakatifu’     (Luk. 11:13)
 ‘Roho akishuka kama  hua  toka Mbinguni’ (Yoh. 1:32)
 ‘Nitawamwagia watu wote Roho yangu’   (Matendo. 2:17).

Kwa kweli ushahidi  juu ya 'Roho wa Mungu’ ni uhakika wa
kutosha  kuwa Roho sio Mungu mwenyewe. Tofauti hizi kati ya
Mungu na Roho ni shida nyingine  ilio kwa wale wanao amini
kuwa Mungu ana  Nafsi'Tatu’ ambazo Mungu amelingana na Yesu
na Roho Mtakatifu. Jambo hili kama lingekuwa la  kweli, na kama
Mungu amedhaniwa kuwa sio mtu, basi halikadharika hata Yesu
naye sio mtu halisi.

Kwa umuhimu sana, Mungu asiye mtu hata sala  kuelekea
kwake inakuwa haina maana, kwenye alama  ambayo sala ni
mazungumuzo kati ya fahamu  zetu  na wazo la Mungu ambalo lipo
katika akili  zetu. Daima tunakumbushwa kwamba  tunamwomba
Mungu ambaye ana Umbo makao yake  yapo  Mbinguni (Mhu. 5:2;
Math. 6:9,5:16, 1Fal. 8:30) na kwamba Yesu sasa yuko  mkono wa
kuume huko ili kutoa maombi yetu mbele zake  (1Pet. 3:21, Ebr.
9:24).

Ikiwa Mungu si mtu binafsi, maneno haya yametolewa  bila
kuwa na maana. Bali, Mungu akieleweka kuwa ni wa kweli, Baba
mwenye upendo, Sala ya kumwomba inakuwa ya kweli, Jambo
   35

lililowazi na dhahiri - hasa  tukizungumza na mtu mwingine
ambaye tunamwamini ana mapenzi sana na anaweza kujibu.

Tumeacha  Kitambo sehemu ya 2:'Matumizi ya jina la
Mungu’

Tumefahamu kwamba Jina la Mungu na hilo la mwanae Yesu
yana maana  ya kina sana. Tunaposema 'Mungu’ tunagusa juu ya
kila mwelekeo  wa kusudi lake la Ajabu la upendo na kweli. Ya
kwamba Jina la Mungu  litumike bure kama upole  usio na maana
au kwa maelezo ya kukasirisha, ni moja ya mambo ambayo mtu
hufanya na kumnena  vibaya zaidi Muumba wake.  Kwa sababu hii
kila mtu anayetaka  kumpendeza Mungu na kumheshimu atafanya
kila jitihada  kutotumia vibaya Jina la Mungu  kirahisi- rahisi.
Katika jamii  ulimwenguni pote kufuru  hii  imekuwa sehemu ya
kawaida kwa Lugha za siku hizi;  Kukatisha ile iliyokuwa ni tabia
ya mazoea haita kuwa kazi rahisi. Sala ya kweli ya kuomba msaada
wa Mungu  hakika itasikika. Wale ambao  wapo ndani ya shughuli
yetu  ya kuwaongoza na kuwavuta,  Mf. Watoto,  pia
watakumbushwa
 hatari ya kukufuru:”Maana BWANA
hatamhesabia kuwa hana hatia alitajaye jina lake bure (Kum. 5:11)

Kwa upande mwingine  wapo wale wanaosisitiza kwamba
tusipotumia maneno ya Kiebrania Yahweh  au Yehova (Njia tofauti
ya kutamka  neno lile lile) Tunapozungumuza kuhusu Mungu,
wakati huo tunakuwa tumepotea sana. Miongoni mwao zaidi ya
hawa ni  Chama cha mlinzi, wanasisitiza kuwa  Mkristo asipojiita
mwenyewe ni'Shahidi wa  Yehova’  Basi hana uhusiano na Mungu.

Kwa kufanya hivi, watu hawa  wanatumia jina  takatifu  la
Mungu na  la ajabu kuchochea aina fulani ya mfumo wa Imani wa
36

kuelimisha kiroho, ambapo wanawadharau  watu wengine tu kwa
matamshi au matumizi ya neno moja. Hii sio kusema kuwa ni
vibaya  kutumia Jina la Mungu; Hasa kweli linafaa kutumika
kwenye Sala zetu wenyewe mara tukibatizwa kwa usahihi katika
Jina lake. Ingawa hivyo, Agano Jipya  halitupatii ishara yoyote
kuwa  hili ni lazima au  inatakiwa na Mungu. Aliongoza kuandika
Agano Jipya hivyo basi liliandikwa kwa Kiyunani (Kigriki)
likitumika neno moja la'Mungu’ -‘theos’  likiwa na maana  “Mtu
mkubwa”.

Hakuna tofauti  iliyofanywa  ndani yake  kati ya'Mungu’ na
'Yahweh’ wala haipo amri yoyote dhahiri  inayohusiana kwa
waamini wakiwa ni jumuiya wajiiteje.Petro anamsema mwamini
kuwa ni “ Mkristo” kuliko kumwita ni'Mtu wa Yehova’  au jambo
lingine kama hili (1 Petro 4:16)  kutilia mkazo zaidi  katika
matumizi ya Jina la 'Yehova’  kunapelekea kupunguza thamani ya
kazi  na  Nafsi ya BWANA'Yesu’  kwa njia hii ambayo  wakristo
wengi wa kiinjili wanatia msukumo zaidi kwenye jina  na kazi ya
Yesu huku wakiacha kuangalia  nafsi ya nguvu zaidi iliyo ya
Mungu.

Majina  mengine ambayo jumuia  ya waaminiao ya wakristo
wa kwanza  waliyojiita wenyewe,  hayatii ndani jina la Yehova:-
 
‘Jamii ya Israeli’ (Ef. 2:12)
‘Mkutano mkuu  na kanisa la wazaliwa wa kwanza’ (Ebr. 12:23)
‘Kanisa lake Mungu’ (Matendo 20:28)
‘Kanisa la Mungu aliye hai, Nguzo na Msingi  wa kweli’ (1
Timotheo 3:15)
‘Nyumba  ya Mungu’ ( 1 Timotheo 3:15)

   37

Tunapopita, ujue kuwa waamini
 hawakujiita
wenyewe'Wakristo’. Neno hili maana yake  lilikuwa la kuvunja
heshima, hawa watu wa Kristo walibezwa na maadui zao.

Tumeacha  Kitambo sehemu ya 3: 'Ufunuo wa Mungu’

Kinachufuata sio rahisi  kukishika chote wakati  tunaposoma
kwanza,lakini umuhimu wa jambo  tunalolizungumzia litakuwa
dhahiri kadri masomo yake yanavyosonga mbele. Tunajumuisha
kwenye maana hii ili  uliache somo hili lote  Msingi wa Biblia
ukisha pimwa wenye ufunuo kuhusu Mungu mwenyewe.

Jina la Mungu laweza kuchukuliwa na yeyote  ambaye
amemchagua kujifunua  au kujidhihirisha yeye mwenyewe. Hivyo
watu na Malaika  sawa sawa  na  Yesu huweza kuchukua jina la
Mungu. Hili ni jambo la muhimu ambalo  linatufunulia mengi ya
Biblia. Hata mwana anaweza kuchukua jina la Baba; ana mambo
mamoja na Baba yake,  anaweza kuwa na jina lile lile la kwanza-
lakini si mmoja na kuwa mtu yeye yule kama Baba.  Kwa njia hiyo
hiyo mwakilishi wa kundi  anaweza kusema kwa niaba ya kundi,
anaweza kumpigia mtu wa kwenye shughuli na kusema, Haloo !
hapa ni  wakulima, Si  Bw. Wakulima,  bali anachukua jina lao kwa
kuwa anafanya kazi kwa niaba yao. Basi hiyo hata kwa Yesu
ilikuwa hivyo.

MALAIKA HUCHUKUA JINA LA MUNGU
Tumeambiwa katika Kutoka 23:20,21 ya kwamba  Mungu
aliwaambia watu wa  Israeli kuwa Malaika atawatangulia mbele
yao;'Jina langu limo ndani yake’, waliambiwa. Jina lake Mungu
ni'Yahweh’. Basi,  Malaika huchukua jina la Yahweh,  na hivi
38

anaweza kuitwa Yahweh, au BWANA  kwa herufi kubwa neno
BWANA linatokana na Yahweh, katika Biblia UV ya Kiswahili ni
sehemu moja tu Zaburi  89:8 utakuta neno
YAHU = YAHWEH. Tumeambiwa  kuwa katika  kutoka
33:20 Mtu hataniona uso akaishi;  lakini katika Kutoka  33:11
tunasoma kwamba “BWANA”(Yahweh) alinena na Musa  uso kwa
uso, kama mtu anaposema na rafiki yake - Yaani  kirafiki. Hakuwa
ni BWANA, Yahweh  mwenyewe alikuwepo,  aliyenena na Musa
uso kwa uso,  Kwa kuwa hakuna mtu anayeweza kumwona Mungu
yeye mwenyewe. Alikuwa ni Malaika  aliyechukua jina la Mungu
ndiye aliye fanya hivyo, na tunasoma  habari  za BWANA  akisema
uso kwa uso na Musa  wakati hasa ni Malaika aliyefanya hivyo
(Mdo. 7:30-33).

Ipo mifano mingine mingi ya maneno' Mungu' na BWANA
ikitaja  Malaika  wakiwa Mungu mwenyewe. Mfano mmoja ulio
wazi ni Mwa. 1: 26 “Mungu (Malaika) akisema, na tufanye mtu
kwa mfano wetu”

WATU  NA  JINA  LA  MUNGU
Moja ya maneno  ambayo yanayosaidia  sana katika kuelezea
yote haya  ni katika Yohana 10:34-36. Hapa Wayahudi walifanya
kosa  ambalo wengi wanaoitwa'Wakristo’ wanafanya leo.
Walidhani kuwa Yesu alikuwa anasema kuwa yeye ni Mungu
mwenyewe. Yesu alisahihisha kwa kusema “Haija andikwa katika
sheria yenu,  nimesema Ninyi ni Mungu ? Ikiwa aliwaita Miungu
….. inakuwaje mimi ….” Mnaniambia ninakufuru, kwa sababu
nalisema,  Mimi ni mwana wa Mungu  ? Yesu kwa kweli alikuwa
anasema 'Katika Agano la Kale watu waliitwa Miungu;  mimi
nasema ni mwana wa Mungu, basi imekuwaje mnaudhika  sana?
   39

Yesu kwa kweli alikuwa ananukuu toka  Zab 82 mahali ambapo
waamuzi wa Israeli  waliitwa'Miungu’.

Kama ilivyoonekana, Jina kamili la Mungu katika Kiebrania ni
'Yahweh Elohim’  likiwa na maana, Nitadhihirika katika kundi la
wenye nguvu. Waamini wa kweli ni wale wengi  wenye nguvu
katika maana ndogo ya maisha  haya  nao watakuwa na nguvu tele
kwenye Ufalme. Kwa mlinganisho huu wote umeonyeshwa kwa
Isa. 64:4 na 1 Kor.2:9.

“Watu  hawakusikia,  wala kufahamu kwa masikio, wala jicho
halikumwona Mungu, ila wewe, atendaye mambo kwa ajili yake
amngojaye” Paulo ananukuu mstari huu katika  1 Kor.2:9-10:
Imeandikwa, Jicho halikuyaona, wala sikio halikuyasikia wala
hayakuingia katika moyo wa mwanadamu, mambo ambayo Mungu
amewaandalia wampendao. Lakini  Mungu ametufunulia sisi kwa
Roho. Fungu la maneno katika Isa. 64:4  linasema hakuna hata
mmoja isipokuwa  Mungu anaweza kufahamu mambo
aliyowaandalia waamini; Lakini 1Kor. 2:10 mstari unasema
kwamba  mambo hayo yamefunuliwa kwetu, hivyo katika maana
sisi ni  “Mungu”: sio Mungu mwenyewe katika utu, bali ufunuo wa
Mungu kwa matokeo kuwa tumebatizwa katika jina lake na kujua
Ukweli.

YESU  NA  JINA  LA  MUNGU
Sio jambo la kushangaza kwamba Yesu,  Ikiwa ni mwana wa
Mungu na ufunuo wake mkuu kwa watu, Pia naye atachukua jina la
Mungu. Aliweza kusema “Nimekuja katika jina la Baba yangu”
(Yoh.5:43). Kwa utii  wake, Yesu alipaa kwenda mbinguni, naye
Mungu akampa jina lipitalo majina - Jina la Yahweh, la Mungu
mwenyewe
40

(Fil. 2:9).basi hii ndiyo sababu tunasoma  Yesu anasema katika
Uf 3:12  “Nami nitaandika juu yake  (Mwamini) Jina la Mungu
wangu……na jina langu mwenyewe, lile jpya”Kumbuka Yesu
alitoa kitabu cha Ufunuo miaka mingi baada ya kupaa  kwenda
mbinguni na akiisha kupewa jina la Mungu,  kama ilivyoelezwa
katika  Wafilipi 2:9.

Hivyo anaweza kuliita jina la Mungu “Jina langu Jipya”; Jina
ambalo hivi karibuni alipewa. Sasa tunaweza kuelewa vema  Isaya
9:6,  mahali ambapo kuhusu yeye tumeambiwa “Jina  lake (Ujue
kuwa) utaitwa, Mshauri wa Ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba
wa milele, ….” Huu ni Unabii wa kwamba Yesu  atachukua majina
yote ya Mungu ya kwamba atakuwa ni ufunuo  wote wa Mungu
kwetu.Na ndivyo kwa maana hii aliitwa  “Emmanueli” maana yake
'Mungu  ni pamoja nasi’ ingawa yeye hakuwa Mungu.

Somo  La Kwanza :  Maswali

1.Ni nini  kitakachotusaidia zaidi  kuamini Mungu ?
a)  Kwenda  Kanisani
b)  Maombi na Kusoma  Biblia
c)  Kuzungumuza na  Wakristo
d)  Kutazama maumbile.

2.  Yapi ya haya yafuatayo ni ufafanuzi  sahihi  zaidi wa
Mungu ?
a)  Ni wazo tu katika mioyo yetu
b)  Kipande cha Roho katika Hewa
c)  Mungu Hayupo
d)  Mtu halisi wa Umbo

   41

3.  Je ? Mungu ni
a)  Ummoja
b)  Utatu
c)  Miungu wengi katika mmoja
d)   Haiwezekani kufafanua kwa njia ya  yoyote

4.  Jina la Mungu' Yahweh  Elohim’  lina maana gani ?
a)  Yeye atakaye  kuwa
b)  Atakayedhihirika katika kundi la wenye nguvu
c)  Mkuu
d)  Nguvu

5.  neno'Malaika lina maana gani ?
a)  Kama mtu
b)  Aliyefunikwa na Mabawa
c)   Mjumbe
d)   Msaidizi

6.  Je ?  Malaika  anaweza  kutenda Dhambi ?

7. Ni kitu gani  kinacho kudhihirishia kuwa Mungu  yupo ?
42

Sunday, June 3, 2018

 
 SOMO:FIMBO YA MCHUNGAJI


Hadithi  za  Mchungaji  kinaelezea  mafunzo  makuu  na  matendo  muhimu  ya  kanisa  kutoka  kwa  Biblia  ambayo  Wakristo
wameamini na kutumia kwa siku zote. Kutumia hadithi kueleza ukweli wa Biblia—badala ya mtindo wa kizamani wa kuchambua— husaidia waumini wapya na viongozi kuelezea na kutumia Neno la Mungu kuwafikia wengine jinsi Bwana wetu Yesu Kristo alivyozoea kufanya.
Ukweli wote wa kimsingi kwenye Biblia hukuwa kutokana na historia ya matukio. Maneno ya uuwisho ya manabii na mitume juu ya matukio haya yanatupa thiolojia ya kimsingi ya Ukristo. Roho Mtakatifu hutumia hizi hadithi za kihistoria kuwaelekeza watu kwenye toba, mabadiliko, na mifano ya huduma za kanisa.
Biblia  inaweka  historia  ya  msingi  wa  imani  yetu  na  mazoea  ya  kanisa.  Vitabu  vya  Warumi  na  Waebrania,  kwa  mfano, viliandikiwa watu ambao walikuwa tayari wanafahamu hadithi za Biblia ambamo mafunzo yazo yalitoka. Katika Agano la Kale hayo matukio ya kihistoria yalihusu Adamu na kuanguka kwake, ahadi ya Mungu kwake Ibrahimu kuyabariki mataifa yote, Ibrahimu kumtoa Isaka dhabihu, Musa na Sheria, Aruni kama Kuhani Mkuu wa kwanza, na ushindi wa Daudi juu wa maadui wapegani. Agano Jipya linahusu matukio kama Kuzaliwa kwa Yesu, maisha, kifo, ufufuo, kupaa, na kushuka kwa Roho Mtakatifu siku ya Pentekote— na mengine zaidi.
JINSI YA KUKITUMIA KITABU HIKI Ikiwa Unawafunza Wachungaji Wapya.
Soma na kujadili hadithi kutoka kwa Biblia na wachungaji wapya unaowafundisha. Ikiwa Biblia haijatafsiriwa kwa lugha yao,
waambie  hizi  hadithi.  Waulize  wawahadithie  watu  wao  hizi  hadithi.  Waulize  wafuate  maagizo  yaliyomo  kwenye  Hadithi  za Mchungaji  za  “Bwana  Hekima”,  na  uepuke  na  makosa  yaliyosemwa  na  “Bwana  Pumbavu.”  Hawa  wahusika,  pamoja  na “Mwanafunzi,” “Msaidizi,” na wengine, si watu wa kweli. Wanaakilisha aina za watu waliotajwa katika Biblia. Wahusika wa Kibiblia waliotajwa kwenye hii Hadithi za Mchungaji, hata hivyo, ni watu wa kweli.
Wanafunzi wote wanaosoma ni sharti wachunge kundi wakati wanasoma. Hili kundi lawezakuwa:
•    Kanisa,
•    Kikundi cha kazi kinachofunza viongozi au kinaanzisha kanisa,
•    Ushirika mdogo ndani ya kanisa kubwa. Mwanzoni, ushirika huu waweza kuwa jamii ya mtu mmoja tu, lakini inakusudiwa kuwa kanisa ndogo.

Ikiwa Wewe ni Mchungaji Mpya
Soma na ujifunze hadithi hizi. Wahadithie waumini wapya pamoja na familia na rafiki zao. Wasihi wafanye yale Bwana Hekima
asemayo, lakini waonye wasifanye yale Bwana Pumbavu asemayo.

Chagua Sura kwenye kitabu hiki ambayo inashughulikia mahitaji yako ya muhimu na nafasi yako.
Hadithi za Mchungaji kina Sehemu tatu. Anza na Sehemu ikufaayo kwa mahitaji yako sasa. Kumwinua Yesu Kristo, tumia Sehemu ya I, Saidia Watu Kumvumbua Kristo.
Kuanza au kufufua mikutano, tumia Sehemu ya II, Jenga Makutano Wanaomtii Yesu.
Kuwafunza wachungaji, tumia Sehemu ya III, Endeleza Huduma za Kimsingi za Kanisa.

Ikiwa Unafunza Kwenye Shule.
Hadithi  za  Mchungaji  hakikuandikwa  kitumike  kama  kitabu  cha  mafunzo  shuleni.  Kiliandikwa  kikusaidie  kuwafunza wachungaji wapya wanaotumika kwa makutano. Ikiwa unakitumia kama kitabu cha kufundisha shuleni, inapasa ufanye juhudi zaidi ili
wanafunzi wasikisome tu kisha wafanye mtihani. Bali, inabidi waanze au wachunge kikundi, kama sehemu ya masomo.
Badala ya kupeana tu mitihani, waulize wanafunzi watoe ripoti kuhusu yale wamefunza na wamefanya na makundi yao, na yenye watu wao wamefanya.
Kunayo mazoezi 85 ndani ya Hadithi za Mchungaji. Kila mojawapo ya hizi inawezakuwa msingi wa mazoezi ya kazi. Sio tu kutoa mafunzo kuhusu nyenzo silizomo kwenye hiki kitabu. Ni lazima uwe na muda na kila mwanafunzi ili umsaidie kupanga kazi ya huduma ya majuma mawili yajayo, na pia usikize ripoti na maswali ya mwanafunzi.

Hadithi Za Mchungaji

Sehemu Ya I

Wasaidie Watu Kumvumbua Kristo

Sura za Sehemu ya I ni Uvumbuzi: Weka alama     kwa yale mazoezi watu wako wamefanya yakukuridhisha. I-1 Uvumbuzi wa 1: Tafuta ukweli na maana ya Maisha (Mungu anatupenda na anataka tumfurahiye milele.)
I-2 Uvumbuzi wa 2: Mrudie Mungu Mmoja (Wacha sanamu au chochote kinachukua nafasi ya Mungu wa Utatu.)
1-3 Uvumbuzi wa 3: Tafuta Msamaha na Maisha ndani ya Yesu (amini kazi yake, kifo na ufufuo wake.)
I-4 Uvumbuzi wa 4: Epuka Nguvu za Uovu na Mauti (Yesu alishinda mauti na mapepo)
I-5 Uvumbuzi wa 4: Pambanua Maswala muhimu maishani (Wacha dhambi, tafuta vitu vilivyo na dhamana ya milele.)
I-6 Uvumbuzi wa 6: Tafuta Uzuri halisi (Watu wasemao ni wema pia wanahitaji musamaha wa Mungu.)
I-7 Uvumbuzi wa 7: Tafuta utele wa Maisha Ndani ya Yesu (Onyesha imani kwa kutii, ukianza na ubatizo.)
I-8 Uvumbuzi wa 8: Kuwa mfuasi wa Yesu (kutana, jua na kumfuata Kristo aliye fufuka.)
Yesu alisema hadithi ya wajenzi wawili. Mmoja alikuwa mwerevu na akajenga nyumba yake kwenye mwamba. Mwingine alikuwa mpumbavu na akajenga nyumba yake kwenye changarawe. Hebu nikujuze kwa mtu aliye kama yule mtu Mwerevu katika hadithi ya Yesu. Anapenda kusikiza na kulitenda Neno la Mungu. Tunamwita Bwana Hekima. Anawasili kwa basi kwenye jamii ya
Mwanafunzi, ambapo anaishi na mkoi wake na kufanya uinjilisti huko.
Bwana Hekima anakuja kuiona karakana mpya ya useremala ya Mwanafunzi.
“Umefanya vyema sana, Mwanafunzi. Hii karakana yako mpya ya useremala ni zuri. Najivunia wewe!”
“Ulinifunza vyema nilipokufanyia kazi mwaka uliopita,” Mwanafunzi akajibu, “Sasa niko na kazi nzuri na ninakushukuru wewe. Lakini nahofia yakuwa mara nyingi sikuwa Mwanafunzi mzuri sana.”
“Ulikataa kusikiza nilipokuambia habari njema kuhusu seremala mwingine aitwaye Yesu.”
Mwanafunzi anakunja uso: “Hiyo hadithi ya dini siku zote inakua ngumu kwangu, Bwana Hekima. Ulitumia maneno magumu.”

“Hapa,  hebu  nikusaidie  kusugua  hiyo  meza,”  Bwana  Hekima  anajitolea.  “Wewe  u  sawa.  Nilijaribu  kupingana  nawe  na kulazimisha mafundisho yangu kwa akili yako. Lakini nimejifunza njia bora zaidi ya kushiriki habari njema. Hadithi ni rahisi kuelewa na kukumbuka. Unaweza zirudia kwa familia na marafiki. Hadithi za Biblia si kama hadithi ambazo binadamu wanabuni ili wawafurahishe marafiki na watoto wao. Hizi ni hadithi za matukio ya kweli na yaliotukia kwenye historia.
Rafikiye Mwanafunzi anawasili. Bwana Pumbavu ni mtu wa mauzo wa kampuni auzaye kila kitu isipokuwa kile unataka. Yeye ni kama  yule  mjenzi  mpumbavu  kwenye  hadithi  ya  Yesu.  Anapenda  kufanya  mambo  apendavyo.  Bwana  Pumbavu  anakatiza.
“Mwanafunzi, huyu mtu anafundisha mambo mageni. Sisi hatuhitaji dini mpya huku. Hatuhitaji kubadili jinsi tunavyoishi. Sasa
nisikize. Niko na sabuni mpya unayopaswa kununua, iliyo na manukato mazuri. Hebu inusie.”
Mwanafunzi hamsikizi Bwana Pumbavu. Anajua rohoni mwake kuwa kuna kitu amekosa maishani mwake. Anataka kujua mengi kuhusu Mungu. Anamsikiza Bwana Hekima kwa makini.

I-1—Uvumbuzi 1


Tafuta Ukweli na Maana ya Maisha
(Mungu anatupenda na anataka tumfurahie milele)

Bwana Hekima anamwambia Mwanafunzi hadithi ya Kijana Mpotovu anayepata msamaha, Luka 15:11-32

Mazoezi
Tafadhali soma hadithi hii katika Luka 15:11-32, au muulize mtu akusomee. Ikiwa hauna Biblia ya lugha yako, muulize mtu
akusomee kutoka kwenye Biblia ya lugha nyingine. Ni muhimu usome au umuulize mtu akusomee vitabu vyote vya Biblia tunavyokuomba usome kwenye kitabu hiki. Kama hutafanya hivyo, haya masomo hayatakuwa na maana. Unaposoma au kusikiza hadithi hii katika Luka 15:11-32 tafuta yale Mwanafunzi alivumbua:
•    Mwana alisababishiaje babake uchungu kwa njia zake za maisha?
•    Mwana alionyeshaje kwamba amesikitikia upumbavu wake?
•    Babake alimpokeaje nyumbani alipowasila akiwa na moyo wa toba?
“Mwanafunzi” Bwana Hekima aeleza, “Sisi zote ni kama yule mwana muuasi. Tumemsahau baba yetu aliye mbinguni. Tumefanya vitu vya upumbavu kwa maisha yetu. Mungu anatusubiri kwa mikono yake miwili ikiwa wazi, tayari kutusamehea na kutukaribisha kwenye karamu, kuwakaribisha wanawe waliopotea nyumbani mwao mwa milele.”
Mwanafunzi anawacha kusugua meza ili azingatie yale Bwana Hekima alisema. Lakini Bwana Pumbavu anachukua furushi lake la sabuni na anaelekea mlangoni. Anadhihaki, “Je wewe wafikria ni kweli Mungu hufanya karamu? Mimi nafikria ana mambo ya maana ya kufanyia muda wake!”
Bwana Hekima anamhakikishia. “Ndio, Yesu alinena juu ya karamu na alisifurahia. Ikiwa tutamwomba kwa Jina la Yesu, Mungu atatusamehe na atutumie Roho Mtakatifu ambaye atatusaidia tuachane na maisha yetu ya kale, na tujiunge na karamu kubwa kuliko zote. Kwa sababu ya kifo na ufufuo wake Yesu, Mungu anasamehe na kutupokea kwa furaha, kama tu watoto waliopotea na wamerudi nyumbani. Alisema kwamba kuwa mbinguni naye ni kama karamu kubwa ya arusi.”

3
Bwana Hekima anamwambia Mwanafunzi kuhusu Uumbaji na Kuanguka kwa Adamu.

Zoezi
Tafadhali tafuta sasa hadithi katika Mwanzo Sura 1-3 kuna majibu ya maswali aulizayo Bwana Hekima:
•    Kwa nini Adamu na Hawa ghafla wakaanza kumwogopa Mungu?
•    Je, Mungu alikuwa akifanya nini wakati aliwapata Adamu na Hawa bustanini?
•    Mungu aliahidi kumfanyia nini adui wa uzao wa binadamu?
•    Ni wapi Mungu aliwapeleka Adamu na Hawa kwa sababu ya kutotii kwao?

“Bwana Hekima anaelezea ni kwa nini anamsaidia Mwanafunzi kumalizia meza mpya. “Mungu kwanza alitembea na kuongea na Adamu na Hawa. Aliwaumba watu ili watembee na kuongea naye kama rafiki. Hakuwaumba wateseke, wala wapotee au wachanganyikiwe. Watu waliumbwa waishi na Mungu, wakifurahia maumbo yake. Mungu alitaka watu wampende kwa hiari yao wenyewe, kwa sababu upendo haulazimishwi. Mungu aliwaruhusu Adamu na Hawa kuchagua njia yao wenyewe.   Walichagua kwenda njia yao wenyewe, ambayo ni njia ya adui wa Mungu Shetani, badala ya kumtii Mungu. Ilibidi awafukuze toka paradisoni mwake.”
“Oh, inahuzunishaje!”
“Historia ya binadamu pia inatuonyesha kuwa mwanadamu sasa   huishi mbali sana na Mungu. Tulipoteza urafiki wetu na Mungu. Ulimwengu umejaa vifo na fujo. Bila Mungu, tunaishi kwa hatari kuu ya kiroho. Mungu aliahidi kumshinda adui wetu Shetani na atume Mshindi wakutuokoa tokana na mauti na uovu. Yesu alilipia uasi wetu kwa kifo chake na akafanikisha sisi kumrudia
Mungu kwa ufufuo wake. Kupitia Yesu, tunaweza kurudi nyumbani kwetu na Mungu.”
Baada ya kujadili hadithi hii, Bwana Hekima anauliza Mwanafunzi, “Je unaona sasa maana ya maisha yetu? Mungu anataka sisi tuishi naye kama rafikize. Je ungependa ujue hadithi zaidi kuhusu Mungu, na uiambia familia yako? Mwanafunzi anakubali na Bwana Hekima anashawishi, “Huu hapa ni mstari wetu sisi kukariri pamoja katika Yohana 1:9. Tutakutana tena juma lijalo!”


Tafadhali kariri Yohana 1:9
Zoezi
Tafuta kwenye Warumi 1:9 ni nini kilipita toka Adamu hadi kwa wazao wake watenda dhambi. Tafuta kwenye Warumi 5:13-21 jinsi Adamu wa kwanza anatofautiana na Adamu wa Mwisho.

I-2—Uvumbuzi 2.


Mrudie Mungu Mmoja
(Wachana na sanamu au chochote kinachochukua nafasi ya Mungu wa Utatu.)

Jumaa lifuatalo Bwana Hekima arejea kwenye karakana ya Mwanafunzi. Anamusaidia Mwanafunzi kumalizia viti kadhaa. Bwana Pumbavu  anawasili  amebeba  vijisanamu  mkononi  na  anamwambia  Mwanafunzi,  “Hizi  ziko  na  uwezo  wakuzuia  maovu  toka nyumbani mwako.” Aeleza. “Nunua moja.”
Bwana Hekima asema, “Naona kama hizi ni sanamu.”
Bwana Pumbavu ajibu, “Oh, hapana! Ni za kurembesha tu nyumba yake na kuzuia maovu.”
“Sanamu huleta tu shida kwenye nyumba,” Bwana Hekima amwambia, “Hakika waweza uza kitu kingine upate riziki.” “Ninakwambia hivi! Mimi hupata pesa nyingi kwa kuuza hizi kuliko mizigo nyingine.”
Mwanafunzi auliza, “Kwa nini hivi vitu ni vibaya hivyo, Bwana Hekima?”
Bwana Hekima anajibu, “Ili kujibu swali lako kuhusu sanamu na kueleza kwa nini ni lazima tumgeukie Mungu mmoja wa kweli na kumwabudu yeye tu, Nitakuelezea kuhusu Eliya na Manabii wa Baali.”

Zoezi
Tafadhali tafuta hadithi katika Wafalme wa Kwanza 18:16-39: yale Mwanafunzi na Bwana Hekima wanapata.
•    Kwa nini maafa yalilijia taifa la Israeli?
•    Ni ushindani gani alioandaa Eliya kati ya Manabii wa Baali na Mungu Mmoja na wa Kweli?
•    Ni jibu gani walilopokea manabii wa Baali, na ni jibu gani alilopokea Eliya?
•    Mungu mmoja na Kweli ni nani?
Bwan Hekima aeleza hadithi: “Watu wengi katika Israeli ya kale walijitengenezea sanamu ili wawe na miungu inayoonekana na ambayo ni yao. Waligeuka na kumwacha Mungu wa kweli, na maafa ikaja katika nchi. Pia sisi hujitengenezea miungu na maafa
hutujia, kwa sababu sisi hugeuka na kumwacha Mungu mmoja na wa Kweli. Ni Mungu wa kweli pekee ndiye anatawala dunia,
mbingu, na juu ya mataifa yote ya ulimwengu. Hawezi kumilikiwa au kufungwa na mipaka ya nchi yoyote. Yeye siku zote atuita tumrudie.”
“Ngoja dakika moja!” Bwana Pumbavu analalamika, “Hiyo yawezakuwa njia ya kweli kwako, lakini si kwangu. Babu zetu waliabudu mizimu ilioambatana na hizi sanamu! Nitafuata njia zao.”
Bwana Hekima ansema, “Hebu nikuambie juu ya Mwanamke Aliyekuwa Kisimani aliyefuata njia za babu zao, lakini hakupata njia ya kweli.”
Hadithi Za Mchungaji

Zoezi
Tafadhali tafuta sasa hii hadithi katika Yohana 4:4-42 yale Bwana Hekima alieleza:
•    Je, Yesu alimpa nini Mwanamke Msamaria kwenye kisima?
•    Nini kilimsadikishia yule mwanamke kwamba Yesu alikuwa nabii wa Mungu?
•    Je, Yesu alisema Yeye ni Nani?
•    Nini kilitendeka mwanamke alipowaelezea watu wake juu ya Yesu?
Bwana Hekima aeleza hadithi hii kwa Mwanafunzi na Bwana Pumbavu anapoendelea kuvitengeneza vile viti. “Wakati mmoja Yesu aliongea na mwanamke kando ya kisima katika nchi ya ugenini. Alijitolea kumpa maji ya kumaliza kiu yake ili asiweze kuhisi kiu tena. Yule mwanamke hakuelewa kwamba Yesu animaanisha maji yaletayo maisha mapya ambayo hatujawahi ona tena. Tunayatafuta, lakini hatuwezi yapata.
Mwanamke alimuuliza Yesu kama yeye alikuwa mkuu kuliko babu zake waliokichimba kile kisima na waliwafunza watu kumwabudu Mungu. Aina hii ya ibada inaturidhisha kuliko kitu kingine chochote. Inatupa njia mpya ya maisha ambayo hatukuwahi jua ingewezekana.”
“Mwanafunzi asema, “Ningependa kujua mengi kuhusu Yesu.” Bwana Hekima amwambia Mwanafunzi, “Nitakusaidia kuchukua
hatua rahisi za utii kwake Mungu. Je, utaongea na Mungu wa Kweli pamoja nami na tumuulize akusamehe kwa kumgeuka?” “Unamaanisha kuomba? Mimi sipotayari.”
“Je, ungependa kusikia hadithi zaidi kama hizi ili uiambie familia? Hebu zote tukariri amri moja toka kwenye Biblia itukumbushayo kumwabudu Mungu Mmjoa wa Kweli. Iko katika Marko 12:29-30.”


Tafadhali soma na kukariri Marko 12:29-30.
Zoezi.
Vile hawa wanaume watatu wanaendelea kunena juu ya Mungu katika karakana ya Mwanafunzi, Bwana Pumbavu auliza, “Kwa nini wewe wasema “Mungu mmoja wa kweli?” Waislamu, Wabudhi na Wahindu huabudu miungu mingine, sivyo?”
“Kuna tu Mungu mmoja wa Kweli. Roho zingine zenye watu wanaita miungu ni viumbe tu alivyoumba Mungu. Wakati mwingine Maandiko Matakatifu huviita ‘malaika.’ Hizi roho chachu wakati mmoja walikuwa malaika. Wakamfuata Ibilisi Shetani, na wakaasi Mungu Mkuu Mtakatifu. Akawafukuza toka kwenye uwepo wake kule mbinguni. Hawampendi Mungu. Kumpenda Mungu ni muhimu kuliko kila kitu. Hatuwezi kumpenda Mungu ikiwa tuna miungu mingine. Wokovu wetu unategemea kuungana na Bwana Yesu, jinsi yeye alivyo mmoja na Mungu Baba.”
“Je, Yesu awezakuwaje mmoja na Mungu Baba?” Bwana Pumbavu auliza,  “Sielewi kabisa.”
“Mungu Mkuu wa Majeshi haitaji sisi kumwelewa. Inatosha tu kujua kwamba amefunuliwa kwenye Maandiko Matakatifu kama
Utatu Mtakatifu. Hawa watatu ni Baba, Mwana na Roho Mtakatifu ndani ya Mungu Mmoja.
“Lakini si ni lazima uongeze hawa watu watatu? Unaongeza mmoja, wawili, watatu halafu unapata miungu watatu.” Bwana
Pumbavu auliza.
“La! Hatuwaongezi. Ingekuwa sahihi zaidi kuwajumulisha ikiwa ungejaribu hii isabati tukufu. Moja jumulisha na moja ni moja. Na ukijumulisha tena na moja bado ni moja. Hii ni kwa sababu Mwana daima atoka kwa Baba. Yesu alieleza katika Yohana 15:26 juu ya Roho Mtakatifu, “Lakini ajapo huyo Msaidizi, nitakayewapelekea kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye
atanishuhudia.”
Bwana Pumbavu ananyanyua sanamu zake na kuondoka.


Tafadhali soma Yohana 15:26 sasa.
Zoezi.


1-3—Uvumbuzi wa 3

Tafuta Msamaha na Maisha ndani ya Kifo na Ufufuo wa Yesu (Amini katika kazi, kifo na ufufuo wake, si katika juhudi za binadamu).

Juma lifuatalo, Bwana Hekima anamtembelea Mwanafunzi katika karakana yake na kumsaidia kupaka rangi dawati jipya. Mwanafunzi asema, “Niliiambia familia yangu hizo hadithi. Walizipenda sana, lakini baba yangu asema kuna walimu wengine wazuri kuliko Yesu.” Bwana Hekima ajibu, “Kuna walimu wengine wazuri lakini hawafanani na Yesu. Hebu nikueleze kuhusu Kukamatwa na Kuteswa kwa Yesu, kutoka Matayo 26:31-56.

Zoezi.
Tafadhali soma Matayo 26:31-36 na upate yale Bwana Hekima anaelezea:
•    Ni maneno gani Yesu aliyatamka ya mwisho alipokuwa anakaribia kufa?
•    Je, Yuda alimsaliti vipi Yesu?
•    Ni wakati gani wafuasi wale wengine walimtoroka Yesu?
•    Ni sababu gani makuhani walitumia kumhukumu Yesu?
Bwana Hekima aeleza wanapoendelea kupaka rangi dawati, “Dhambi zetu zimetutenga na Mungu. Hata hivyo, Mungu aliupenda

5
ulimwengu jinsi hii hata akamtoa mwanawe kuturudisha kwake. Aliuumba ulimwengu lakini ulimwengu haukumtambua. Yohana
3:16; na Yohana 1:10 zinaeleza haya. Hata wafuasi wake mwenyewe walimsaliti na kumtoroka. Makuhani wa hekalu la Mungu walimhukumu kifo, hata kama alikuwa mtu mtakatifu na asiye na hatia. Nasi pia, kama tu watu wa Yesu, tumemkataa kwa kuwa sisi zote tumetenda dhambi kwa Mungu. Hata hivyo, Yesu atupenda jinsi hii, kwamba akachagua kufa kwa ajili yetu.Hakuwa tu Mwalimu wetu bali alituokoa na ghadhabu ya Mungu kutokana na dhambi zetu.”
Bwana Pumbavu anawasili mlangoni pa karakana na kupiga yowe, “Tazameni vitu nilivyoleta leo! Nunua mojawapo ya hivi vifaa vya kupasua mbegu.”
Hawamwangalii. Bwana Hekima aelezea Kifo na Kufufka Kwa Yesu.

Zoezi.
Tafadhali tafuta Luka sura za 23 na 24; yale Bwana Hekima anahadhitia:
•    Nini kilichotendeka muda mfupi tu baada ya Yesu kufa, kuonyesha imuhimu wa kifo chake?
•    Malaika waliwaambia nini wale wanawake waliokuwa wakimtafuta Yesu siku ya tatu baada ya kufa?
•    Wale nanaume waliokuwa wakielekea Emau walifika wapi ndipo wakamtambua Yesu?
•    Maagizo ya Yesu ya mwisho kwa wafuasi wake yalikuwa ni nini?
Bwana Hekima amwambia Mwanafunzi na Bwana Pumbavu, “Siku Yesu alikufa, jua lilitiwa giza mchana kuaanzia saa sita hadi saa tisa, na pasia la hekalu likapasuka. Yesu alizikwa na akabaki mfu hadi siku ya tatu. Mungu mtakatifu wa watakatifu kweli hangeruhusu huyu mtu mzuri na asiye na hatia kubaki mfu.”
“Yesu alikuwa dhaifu!” Bwana Pumbavu ahisi, “Yeye angewazuia hawa watu wasimuue!”
“Ni kweli angewazuia, lakini Yesu alikufa kwa kupenda kwake. Alichukuwa nafasi pahali petu masalabani. Siku ya tatu Mungu kamfufua toka kwa  wafu. Akawatokea wafuasi wake  na wakamgusa  na  wakala  naye.  Walimwabudu,  wakimwita,  ‘Bwana’  na
‘Mungu’ katika Yohana 20:28. Ufufuo wake ulivunja nguvu za mauti. Hakuna mtu mwengine aliyewahi shinda mauti jinsi hiyo.” Bwana Hekima auliza Mwanafunzi, “Je, wewe utamtii Mungu bila matakwa? Je, waona sasa ya kwamba Yesu ni mkuu kuliko
mtu mwengine aliyewahi ishi? Je, utamwomba Mungu akuokoe tokana na mauti na akupe maisha mapya katika nguvu za jina la
Yesu? Hapa kuna mstari juu ya Yesu wakukariri pamoja na familia yako: Yohana 3:16.”
Mwanafunzi anakariri huu mstari kwa haraka. Wakati Bwana Hekima anaondoka, Mwanafunzi anasema, “Naweza iambia familia yangu hizi hadithi sasa. Je, tunaweza kutana tena hivi karibuni tuongee juu ya Yesu?”

Zoezi.
Tafadhali kariri Yohana 3:16, na usaidie familia na marafiki zako kuukariri pia.

I-4—Uvumbuzi wa 4)

Epuka Nguvu za Maovu na Mauti (Yesu alishinda mauti na mapepo)

Juma moja baadaye, Bwana Hekima anamsaidia tena Mwanafunzi kwenye karakana. Bwana Pumbavu awasili akihema. “Habari mbaya! Ndugu yako aishiye kule chini kwenye kingo za mto amefariki kwenye ajali ya basi!”
Mwanafunzi anaachilia rangi na anaketi kimya. Bwana Hekima anaketi kando naye, akimwombea kwa huu wakati mrefu wa kimya. Mwanafunzi anafanya kwikwi, “O, hapana! Kwa nini Mungu anaachilia mabaya kama haya kutendeka? Ni faraja gani nitawapa familia yangu?”

Zoezi
Tafadhali tafuta Yohana 11:17-44; yale Bwana Hekima anaelezea:
•    Je, Yesu alihisi namna gani kuhusu kifo chake Lazaro?
•    Je, Yesu alimwambia Martha nini kitatendeka kwa wale wamwaminio?
•    Nini kilimtendekea Lazaro mfu wakati Yesu alipomwita?
Bwana Hekima aeleza, wanaume hawa watatu wakiwa wameketi kwenye karakana ya Mwanafunzi. “Yesu pia alikuwa na rafiki mzuri sana aliyeaga. Yesu alihuzunika sana. Mungu hapendi kuona watu wanateseka. Yesu alikuja kukosoa haya mambo yote. Alimwambia  Martha  kwamba  Lazaro  atafufuka  tena,  kwa  sababu  Lazaro  animwamini  Yesu.  Yeye  ndiye  ufufuo  na  uzima.
Alimwomba Mungu halafu akamwita Lazaro ndani ya kaburi. Lazaro alitoka akiwa hai.
Bwana Pumbavu auliza, “Lakini ni nguvu gani alizonazo Yesu kupeana uhai sasa?”
“Yesu  alionyesha kila  mtu  kwamba  yu na  nguvu juu ya  mauti.  Alipokufa na  akafufuka  tena siku  ya tatu,  aliwapa  wote wamwaminio maisha mapya. Huu uzima ni wa milele kwa sababu tuna Roho wa Mungu ndani yetu.”
Bwana Hekima anawaambia kuhusu Mtu aliyeteswa na Mapepo, aliyekutana na Yesu.

Zoezi
Tafadhali tafuta Marko 5:1-20 majibu ya haya maswali ambayo Bwana Hekima amuuliza Mwanafunzi:
•    Je, mapepo walisababisha yule mtu kujifanyia nini?
•    Mapepo walimwambia Yesu nini?
•    Je, Yesu alimfanyia huyo mtu nini?
•    Je, Yesu alimwambia yule mtu afanye nini baada ya kumponya?

6
Hadithi Za Mchungaji

Bwana Hekima aeleza, “Yesu ni Mwana wa Mungu. Asili yake ni ile ya Mungu. Wafilipi 2:6 yaeleza hili. Mapepo walisababisha yule mtu kulia na kujikata mwenyewe. Alikuwa na nguvu kiasi kwamba mtu hangeweza kumdhibiti. Yesu alipofika, walimtambua kama mwana wa Mungu. Yule mtu alipiga magoti mbele ya Yesu na mapepo wakamwomba Yesu awatume kwenye nguruwe. Yesu aliwaamuru wamtoke yule mtu na wakamtoka. Yesu akamponya kabisa yule mtu. Halafu akamtuma yule mtu nyumbani aiambiye familia yake yale Mungu amemtendea.”
Bwana Pumbavu anaondoka bila kusema lolote na Bwana Hekima anaendelea, “Yesu alipopaa juu mbinguni, alimtuma Roho wake kuishi ndani ya wale wamwaminio. Roho wa Mungu ana nguvu na anatulinda kutokana na maovu. Anatupa maisha mapya ya milele na matakatifu. Anatusaidia kuwaambia wenzetu habari njema ya Yesu.”


Tafadhali kariri Yohana 11:25
Zoezi.


I-5—Uvumbuzi wa 5


Tambua maswala muhimu Maishani (Geuka toka kwenye dhambi na utafute vitu vyenye dhamana ya milele kuliko vile vinavyo pita)

Bwana Hekina anarudi juma linalofuata kumtembelea Mwanafunzi lakini hampati nyumbani wala kwenye karakana. Mwishowe, anamkuta kwenye kinjia. Mwanafunzi anaomba msamaha, “Bwana Hekima, tangia mazishi ya ndugu yangu nimekuwa na shughuli chungu nzima mpaka nikamsahau Mungu. Labda baada ya mwezi moja au mbili…”
“Najua una shughuli nyingi sana, lakini hupaswi kuajilia mambo ya haya maisha yakufanye usahau maswala yaliyo muhimu zaidi. Hebu nikwambie kuhusu Nuhu na Gharika.”

Zoezi.
Tafadhali tafuta Mwanzo 6:3-14: yale Bwana Hekima anaelezea:
•    Je, Mungu alihisije juu ya yale watu walikuwa wakifanya wakati wa Nuhu?
•    Kwa nini Mungu aliokoa Nuhu na familia yake?
•    Je, Nuhu alifanya nini kumtii Mungu?
Wanatembea ndani ya karakana ya Mwanafunzi na wanaanza kutengeneza mlango. Bwana Hekima aeleza Gharika: “Yesu anasema kwamba watu wa siku za Nuhu waliishi maisha kama kawaida, katika Luka 17:27. Walimsahau Mungu na wakawa waovu na wenye fujo. Mungu alingojea kwa uvumilivu ili watubu, lakini wakampuuza Mungu. Mungu ni mtakatifu. Yeye havumilii dhambi. Dhambi na fujo alizoona wakati wa Nuhu zilimhuzunisha na kumkasirisha. Aliamua kuwaangamiza watu pamoja na ulimwengu.”
“Wote kabisa?” Aliuliza Mwanafunzi.
“Karibu wote. Nuhu tu ndiye alikuwa mtu wa kumsikiza Mungu. Nuhu alimwamini Mungu hata kama hangeweza kumwona. Alitumia miaka mingi kujenga safina kubwa hata kama hakuwa ameona maji kwenye hiyo safina ingeelea. Mungu alimwokoa Nuhu kwa sababu alimwamini na kumtii Yeye. Mungu aliiangamiza dunia kwa gharika, lakini Nuhu pamoja na familia yake waliokolewa
kwa kuwa ndani ya safina.
Bwana Pumbavu anasimama mlangoni, akisikiza. Bwana Hekima aeleza, “Hivi leo sisi tuko kama watu wa wakati wa Nuhu. Tunampuuza Mungu na tumejawa na dhambi na fujo. Dhambi zetu zinatuhuzunisha na kutukasirisha. Tutaangamizwa na mauti ikiwa hatutaingia pahali pa usalama penye Mungu ametutengenezea. Hapo pahali ni kama hiyo safina. Na hapo pahali ni Yesu. Tu salama katika mikono ya Yesu ikiwa tutaamini.”
Bwana Pumbavu anakataa, “Lakini Mwanafunzi hafanyi lolote lililo ovu! Kwa nini basi aitaji pahali salama pa kujificha? Yeye anahitaji tuu pesa! Tazama, kile nimeleta. Ni mashine ya peremende. Weka hiyo sarafu ndani, zungusha hiki kishikio na peremende itatoka. Nunua haya mashine wewe Mwanafunzi, kwa ajili ya ii karakana yako. Watu watakuja hapa kununua peremende nawe
utapata pesa nyingi sana. Pesa ndio jambo la muhimu sana maishani.”
Bwana Hekima anamwambia Bwana Pumbavu, “Ningependa nikwambia hadithi ya Yesu ya Tajiri Mpumbavu.”

Zoezi.
•  Tafadhali tafuta ilani ya Yesu katika Luka 12:13-21 kwa watu watafutao tu utajiri.
Bwana Hekima amuuliza Bwana Pumbavu, ambaye bado yuashikilia mashine yake ya peremende, “Je, unaona kwamba huyu tajiri alikuwa tu afanya bishiara yake ya kawaida? Lakini alichukulia mavuno yake kuwa ya maana zaidi kulika Mungu. Kifo kilimjia wakati alikuwa hatarajii. Hakuwa tayari kufa. Yesu asema kwamba atarejea duniani tena. Watu wengine watakuwa wakifanya biashiara yao ya kawaida kama watu wa siku za Nuhu. Hawatakuwa tayari kwa ajili ya Yesu. Wataangamizwa kama watu waliopatwa na gharika. Lakini walio wa Yesu watapona.”
Bwana Pumbavu anaenda zake akicheka, lakini Mwanafunzi anaitikia: “Napaswa kuwa niliomba nawe kitambo sana. Nahisi nafuu. Nitaambia familia yangu hadithi hizi ili niwasaidie wamkumbuke Mungu. Je, unao mstari mwingine wa Biblia wa kunipa nikariri?”
“Jifunze Warumi 6:23. Twaweza kutana tena hivi karibuni?”
“Ndio. Usiku wa leo. Tafadhali tule chakula cha jioni mwangu nyumbani. Mke wangu Sara angependa kukujua, pia.”

7
Zoezi.
•    Kariri Warumi 6:23, juu ya kipaji kilicho cha maana kuliko vyote ulimwenguni.



I-6—Uvumbuzi wa 6


Tambua Uzuri Halisi (Wanadamu Wasemao Wao ni wema pia Wanahitaji Msamaha wa Mungu)

Baada ya mlo mzuri nyumbani mwa Mwanafunzi, Mwanafunzi anamwambia Bwana Hekima, “Sara alitaka mimi nikuulize swali. Kuna jambo linamsumbua.”
“Kwa fursa yako, Mwanafunzi, ningependa kumsikia Sara mwenyewe aeleze shida yake.”
Sara anaona haya. “Wewe ulisema kwamba Mwanafunzi ahitaji msamaha juu ya vitu fulani. Lakini huyu Mwanafunzi si mtu mbaya. Yeye hufanya majukumu yake kama baba na mme  vyema sana. Pia ni mzuri kwa marafiki zake. Je, si hayo yanatosha mtu kuwa sawa kwa Mungu?”
“Hebu nikueleze juu ya Mtoza Ushuru Fisadi.” Baada ya kuelezea hii hadithi, Bwana Hekima anauliza maswali kuona kama
Mwanafunzi na Mkewe Sara wameelewa.


Tafadhali tafuta katika Luka 19:1-10
•    Je, Yesu alitambuaje kuwa Zakayo alitaka kumwona?
•    Je, Yesu alimtendaje huyu mtoza ushuru fisadi?
•    Je, Zakayo alimtenda vipi Yesu?
Zoezi.
•    Yesu hakumhukumu huyu mtu jinsi watu wengine walivyo mhukumu. Je, Zakayo alisema atafanya nini, kwa ajili ya shukrani?
Baada ya hayo, Bwana Hekima aeleza juu ya Zakayo: “Kila wakati Yesu huja kwa wale wamtafutao. Anawabadili nyoyo zao. Kamwe hatuwezi kuwa wema kwa juhudi zetu wenyewe. Watu wengine hufikri ni wazuri lakini wana kiburi hata hawawezi ona dhambi zao wenyewe. Yesu anapokuja maishani mwetu, anatupa wema wake. Kama Zakayo, wewe muonyeshe shukrani kwa vitendo.”
“Bado nashangaa,” Asema Sara. “Je, itakuwaje kuhusu mjomba wangu wa kidini?”
“Kuhani humpa sala ili arudie mara nyingi kwa siku! Je, yeye pia ahitaji kuokolewa na Yesu?”
“Ndiyo. Hatuwezi kumpendeza Mungu kwa kufuata mpangilio wa sheria au kwa kufanya tu majukumu yetu ya kidini. Hebu nikwambia juu ya Kuhani na Mtoza Ushuru.”

Zoezi.
Tafadhali tafuta yale Mwanafunzi na Sara walipata katika Luka 18:9-14.
•    Je, ni watu wapi wenye Yesu alikuwa akiambia hadithi hii ya Mtoza Ushuru fisadi?
•    Ni nia ipi aliokuwa nayo huyu mtu wa kidini kwa Mungu?
•    Je, Mtoza Ushuru alikuwa na nia ipi?
•    Ni mtu yupi alimpendeza Mungu na akawa mzuri kweli?
Bwana  Hekima  anamshukuru  Sara  kwa  mlo  mzuri.  Sara  anajibu,  “Asante,  Bwana  Hekima,  kwa  hiyo  hadithi  ya  Biblia. Nimeelewa vyema zaidi leo. Mungu huwasamehe hata wale wabaya.”
Mwanafunzi anamwambia Bwana Hekima, “Tafadhali elezea jinsi ombi fupi kama hilo linaweza kumfanya huyo mtu awe mwema.”
“Ni Mungu tu anayeweza tufanya kuwa wema kweli. Tunapokuwa waaminifu kwake juu ya dhambi zetu na kuamini kuwa
atatusamehe katika Jina la Yesu, Roho wake hutujia akatufanya wema kweli. Twawezakuwa watu wa kidini sana kama huyu mtu kwenye hadithi hii, lakini hilo pekee halimpendezi Mungu. Toba na imani yetu ndiyo inayompendeza.”
Bwana Hekima anapoondoka, anamwambia Mwanafunzi, “Nafikiri Sara anapokea habari njema ya Kristo. Natumai utamweelezia zaidi. Ukifikiri yu tayari, waweza omba naye kwa msamaha katika jina la Yesu, jinsi nimeomba nawe.”
“Nitamwongelesha usiku huu. Tafadhali rudi asubuhi kama utaweza.”



I-7—Uvumbuzi wa 7

Tafuta Uzima Tele Ndani ya Yesu (Onyesha kwa Imani na Kutii, ukianza na Ubatizo)

Asubuhi iliyofuata Bwana Hekima anarudi nyumbani kwa Mwanafunzi. Punde tu, Bwana Pumbavu anatokea mlangoni akiwa anashikilia vitu kadhaa ving’aavyo, vyenye kupindapinda na vilivyo na manyoya. “Mwanafunzi, nunulia mkeo Sara kofia!”


8
Hadithi Za Mchungaji

Mwanafunzi anacheka. “Tuna jambo la muhimu zaidi kuliko manyoya. Mimi na familia yangu tunamtii Yesu. Natumai wewe pia unafanya hivyo, Bwana Pumbavu.”
“Mimi nimefikiria kuhusu hilo. Ninamfuata kwa njia zangu mwenyewe. Usiwe sugu sana juu ya hii imani, Mwanafunzi. Watu wengine husema eti kile wahitaji kufanya ili uingie mbinguni ni kumwamini Yesu. Hakuna zaidi ya hilo. Nitafanya hivyo.”
“Nilisema pia tutamtii.”
“Huwezi. Anasema uwapende pia adui zako. Hicho ni kichaa!”
Bwana Hekima hakubali. “Hapana. Kuamini ni mwanzo tu. Mungu anataka dhihirisho la imani yako kwa utii tu. Hadithi ya
Mfanyi Kazi wa Kushi itawasaidia kuelewa.


Tafadhali tafuta Matendo ya Mitume 8:26-38.
Zoezi.
•    Towashi alisoma juu ya nani katika Maandiko ya Agano la Kale?
•    Ni mambo gani yenye hayo Maandiko toka Agano la Kale yalitabiri kumhusu Yesu?
•    Towashi alifanya nini kuonyesha kwamba alimwamini Yesu?
Bwana Hekima anaelezea Mwanafunzi, Sara na Bwana Pumbavu, wanapoketi nyumbani mwa Mwanafunzi: “Maandiko aliyoyasoma Mkushi yalikuwa Isaya 53. Yaliandikwa karne nyingi kabla kusaliwa kwa Yesu, lakini yalitabiri yale Yesu atafanya. Yalisema kuwa sisi ni kama kondoo ambao wamepotelea kwenye dhambi na kumwacha Mungu. Twastahili kufa, lakini Yesu alichukuwa dhambi zetu, magonjwa yetu, na mateso yetu, na kifo chetu kwenye mabega yake. Kwa kuwa aliteseka na akafa, tumewekwa huru toka dhambi na mauti.”
Sara analeta kahawa na Bwana Hekima anaendelea kufafanua: “Mkushi aliamini katika yale Yesu alimfanyia. Kuonyesha imani yake, alimwomba Filipo ambatize mara moja hapo barabarani, pale alipoona maji. Ubatizo unaonyesha kwamba Roho Mtakatifu ametuunganisha na Kristo katika kifo chake, jinsi yasemavyo Maandiko katika Wakolosai 2:12, na katika Warumi 6. Maisha yetu ya
dhambi yanakufa pamoja na Yesu. Kwa imani, tunaungana katika ufufuo wake na tunaanza maisha mapya ya milele na takatifu. Roho
wake anakuja kuishi ndani yetu.”
Bwana Pumbavu anakunja uso. “Hiyo ni ajabu! Hatuitaji maji kututakaza! Kwa hiyo tutafanya tafakari refu. Nitawauzia kitabu cha Mhindu mtakatifu cha kutufunza jinsi ya kutafakari. Hiki hapa, kitazame.”


Tafadhali tafuta Wafalme wa Pili 5:1-14
•    Namani alifanya nini kudhihirisha imani yake?
Zoezi.
•    Maji ya mto pekee hayakuosha ukoma wa Namani. Mungu alimwosha. Lakini Mungu alitumiaje maji kumfanya Namani kumwamini?
Bwana Pumbavu anashindwa kuuza kitabu chake na anaondoka nyumbani mwa Mwanafunzi. Bwana Hekima anaelezea Mwanafunzi na Sara: “Mungu anatwambia tubatizwe kwenya maji. Kama kuoshwa kwa Namani na ubatizo wa Mkushi, ubatizo wetu katika maji unadhihirisha imani yetu. Hii ndiyo hatua ya kwanza tunayochukua kuonyesha tunamtii Mungu. Ubatizo unadhihirisha kwamba Mungu ameosha dhambi zetu zote kwa damu ya Yesu kama vile Matendo 22: 16 inatufunulia. Yohana wa Kwanza 1:7 inatuhakikishia utakaso wa Mungu.
Mwanafunzi na Bwana Hekima wanaingia ndani ya karakana wakiongea kuhusu ubatizo.
“Mwanafunzi, Mungu anataka wewe uchukuwe hatua hii ya utii, pamoja na familia yako. Hunabudi kumwelezea Sara na wanao
Jinsi Ubatizo Unatuunganisha na Kristo.” “Nitaongea na Sara. Sijui kama tutayari.”


•         Tafadhali kariri Matendo ya Mitume 2:38.
Zoezi.
•         Tafuta Warumi 6:1-14 ni kwa njia gani ubatizo unatuunganisha na Kristo?
•         Pia Warumi 6:1-14, matukio ya ubatizo yanaonekanaje katika maisha yetu?



I-8—Uvumbuzi wa 8


Kuwa Mfuasi wa Yesu (Kutana, Umjue na Kumfuata Kristo Aliyefufuka).

Siku chache baadaye, Bwana Hekima awasili kwenye karakana ya useremala na anamwambia Mwanafunzi, “Hivi karibuni nitaamia eneo lingine la nchi yetu. Natumai kuacha mkutano wa waumini hapa kwanza. Umekwisha sikia habari njema ya Yesu. Unajua hitaji letu la Mungu mmoja wa Kweli na jinsi alivyomtuma Yesu kutukomboa toka dhambini na mauti. Je, uliweza kuongea na Sara kuhusu kudhihirisha imani yenu kwa njia ya ubatizo?”
“Ndiyo. Sisi zote tunaamini kuwa kifo na ufufuo wa Yesu vimetuletea msamaha na maisha mapya. Lakini nataka kujifunza zaidi juu ya ubatizo.”
“Sikiza, basi Jinsi Paulo alikutana na Yesu.”

9

Tafadhali tafuta Matendo ya Mitume 22: 1-16.
Zoezi.
•    Je, Paulo alikuwa akiwafanya nini Wakristo kabla ya kukutana na Yesu?
•    Ni nani aliye nena na Paulo njiani kuelekea Dameski?
•    Je, Paulo alihitaji nini ili awe mfuasi mtiifu wa Yesu?
Bwana Hekima anafupisha hadhiti ilhali anamsaidia Mwanafunzi kumalizia kutengeneza kiti. “Paulo aliwaweka Wakristo wengi gerezani kabla akutane na Yesu. Alifikiri alikuwa akimtumikia Mungu kwa kujaribu kuwazima Wakristo. Hakuamini kwamba Yesu alifufuka toka wafuni. Alifikiri Wakristo ni waongo. Lakini Yesu aliyefufuka akamnenea Paulo. Paulo alikuwa amepofushwa hadi nabii wa Mungu akaja kumponya. Nabii alimwambia ainuke, abatizwe, na aoshwe dhambi zake, kwa kuliitia Jina la Yesu. Nabii alimwambia Paulo kwamba atakuwa shahidi kwa watu wote kuhusu yale aliyaona na kusikia.”
Bwana Pumbavu anaingia kwenye karakana kwa haraka na anaanza kuongea, lakini anamwona Bwana Hekima na ananyamaza. Anasikiza kwa muda mfupi halafu anasema, “Usiharakishe kuingia kwenye mambo haya, Mwanafunzi. Fikiria kwanza. Usibebwe kwa haraka hivyo na hii dini ya Yesu. Itaingilia maisha yako!”
Bwana Hekima anamwomba Mungu kimya kimya, na halafu anaelezea Yesu Alivyo paa juu Mbinguni.

Zoezi.
Tafadhali tafuta Luka 24:36-53 yale Bwana Hekima anamuuliza Mwanafunzi:
•    Je, Yesu alifanya nini kuwadhihirishia wafuasi wake kwamba hakuwa kizuka?
•    Je, matukio gani ya kihistoria hasa ambayo Yesu anatuamuru tutangaze kama habari njema kwa mataifa yote?
•    Je, ni kitu gani cha ajabu ambacho Yesu aliwaahidi wafuasi wake?
Bwana Hekima anamalizia hadithi huku Mwanafunzi na Bwana Pumbavu wanasikiza kwenye karakana: “Yesu alichukuliwa mbinguni kama mwanadamu. Malaika waliahidi kuwa atarudi tena kwa njia hiyo hiyo (Matendo ya Mitume 1:8-11). Kwa wakati huo, Yesu aliwapa wafuasi wake kazi ya kufanya na akawatumia Roho wake Mtakatifu toka juu kuwajaza nguvu ili wafanye hiyo kazi. Hii
kazi ni yetu leo. Aliahidi kutupa nguvu toka mbinguni za kufanya kazi hii, nguvu ambazo zinatujilia kupitia kwa Roho Mtakatifu
aishiye ndani mwetu. Kazi yetu ni kuwaelezea watu wote kumhusu Yesu, hasa juu ya kifo na ufufuo wake, na kutangaza toba na msamaha wa dhambi.”
Bwana Pumbavu asema, “Basi Yesu amesha fika mbali sana kufikia saa hizi. Mimi naondoka. Ninyi wanaume mmekuwa watu wa kichaa kingi cha kidini.”
Bwana  Hekima  hamsikilizi  huyu  Bwana  Pumbavu  na  anaendelea  kumweleza  Mwanafunzi:  “Siku  moja  Yesu  atarudi  na atawafufua wafuasi wake toka kwa wafu, ili tuishi naye milele alipo. (Yohana 14:3). Mwanafunzi, je, u tayari kuchukua hatua hii
kumkaribia Mungu? Sikiza sauti ya Yesu. Kiri dhambi zako na ubatizwe, ukijiondolea dhambi zako kwa Jina la Yesu. (Matendo ya
Mitume 22:16).”
“Najua ndani ya roho yangu kwamba huu ni ukweli. Mimi na familia yangu tutamtii Kristo. Tutabatizwa. Na tayari nimeanza kuwaambia marafiki zangu juu ya Yesu.”

Zoezi:
Fanya yale ambayo Bwana Hekima anamuuliza Mwanafunzi afanye:
•    Kariri Matayo 28:18-20.
•    Waambie wengine yale umeona na kusikia juu ya Yesu.
•    Msifu Mungu kwa ajili ya siku hiyo atakaporudi na kuwachukua wafuasi wake kwenda Mbinguni nao.

























10


Sehemu II


IMARISHA MAKUTANO WANAOMTII KRISTO
Hadithi Za Mchungaji

Sura katika Sehemu ya II ni Amri za Kimsingi za Kristo. Sahisha     zile zinatumika.
II-1Amri ya Kristo ya 1: Tubu, amini, pokea Roho Mtakatifu (Wokovu).
II-2 Amri ya Kristo ya 2: Batiza waumini wapya (halafu ishi maisha matakatifu ndani ya Yesu yanayoanzishwa na huu ubatizo).
II-3 Amri ya Kristo ya 3: Wafanye Wafuasi wa Yesu (Funza utiifu kwa Yesu na kwa Neno lake.)
II-4 Amri ya Kristo ya 4: Upendo (Mpende Mungu na wanadamu, watumikie maskini, wasamehe adui zako).
II-5 Amri ya Kristo ya 5: Omba (Sifu Mungu, kiri dhambi, ombea wengine, ponya, pigana vita vya kiroho).
II-6 Amri ya Kristo ya 6: Fanya Meza ya Bwana (Sherehekia komunyo, abudu Mungu katika Roho).
II-7 Amri ya Kristo ya 7: Toa (Kuwa Matumishi wema way ale yote atupaye Mungu.) Kusudi la hii Sehemu ni kuwafanya wafuasi wamtiio Yesu kuliko vitu vingine vyote.
Katika Biblia tunapata mchungaji aitwaye Tito. Tazama Tito 1:5 jinsi Mtume Paulo alivyomwacha huyu Mchungaji kwenye kisiwa cha Krete kuwasaidia Wakristo wapya. Paulo alimwambia Tito kukamilisha kazi iliyozalia kwa makutano wapya huko Krete.
Wawezakuwa umekutana na Bwana Hekima katika Sehemu ya 1. Ikiwa bado, hebu nimjuze kwako. Yeye ni mchungaji. Yeye si mtu kweli, lakini ni mfano kama wa Tito katika Biblia.
Katika Sehemu  ya I Bwana Hekima alitoa habari njema kwa  Seremala aiitwaye Mwanafunzi. Alitumia hadithi za Biblia.
Mwnafunzi akatoa hadithi hizo kwa familia yake. Sasa familia ya Mwanafunzi na marafiki kadhaa wamempokea Yesu na wamebatizwa. Bwana Hekima ni kama yule mtu mwerevu katika Biblia aliyejenga nyumba yake kwenye mwamba imara, ambao ni Yesu Kristo. Anatumia hadithi kuwasaidia waumini wapya kukua kama wafuasi watiifu wa Yesu Kristo. Hadithi hizi zinasimulia matukio ya kweli katika historia.
Mwanafunzi anaishi pahali ambapo watu wanawatesa wafuasi wa Yesu. Rafikiye Bwana Pumbavu ni mtu wa mauzo anayejaribu kuuza vitu tofauti tofauti ambavyo hakuna avitakaye. Yeye pia ni kama yule Mpumbavu katika Biblia alieyejenga nyumba yake kwenye changa rawe.
Bwana Pumbavu anawasili kwa karakana ya seremala Mwanafunzi na kumwambia, “Nimesikia wewe umekuwa Mkristo. Nami pia. Watalii watanunua zaidi hivyo vitu vya kumbukumbu toka kwangu nikiwa Mkristo. Hebu tazama hapa. Waweza taka kununua kamoja pia.” Anachukua filimbi ya mwanzi kutoka kwa gunia. “Hii ni filimbi ya ndege. Ukiipuliza ndege wanakuimbia. Nitakufunza jinsi ya kuipuliza.” Anapuliza hiyo filimbi na mbwa watatu wanaanza kubweka.
Mwanafunzi anajibu, “Mimi nafuata Yesu kumtumikia Mungu, si kutafuta pesa. Ninamshuhudia kwa marafiki zangu wote.” Bwana Pumbavu anacheka. “Wewe? Unahitaji kusoma Biblia yote kabla hujaanza kuwafunza wengine kule nje! Kwaheri!”
Baadaye siku hiyo Bwana Hekima anawasili. Alimfunza Mwanafunzi kazi ya useremala na hufurahia kuja kwa karakana ya
useremala ya Mwanafunzi kuongea na kumsaidia kazi.
Bwana  Hekima  anaonya,  “La,  ndugu  yangu  katika  Kristo!  Hatusikizi  tu  na  kusikiza  tu  zaidi  haya  Maneno  ya  Mungu. Tunayatenda kidogo kidogo kwa wakati mmoja. La sivyo hayatatufaa. Hebu nikukumbushe kuhusu Wanjenzi Wawili. Yesu aliwaambia wafuasi wake kuwahusu ili sisi tujue umuhimu wa kutii Maneno yake, tangia mwanzo wa maisha yetu mapya ya Ukristo.”

Zoezi
Tafadhali soma hii hadithi katika Matayo 7:24-29. Ikiwa hauna Biblia kwa lugha yako muulize mtu aliye nayo akwambie hii hadhiti. Unapoisoma hii hadithi, jibu maswali yafuatayo ambayo Bwana Hekima ameandaa kwa ajili ya Mwanafunzi:
•    Ni tofauti gani iliyopo kati ya hawa watu wawili waliosikia maneno ya Yesu?
•    Ni nani ndiye Mwamba na msingi wa kila kilicho chema?
•    Je, tufanye nini ili tujenga maisha na huduma yetu kwenye huu Mwamba?
Mwanafunzi anahisia, “Basi haitoshi tu kusikiza maneno ya Yesu! Tunafaa kujua yale Yesu ametuamuru tufanye, lakini kujua tu haitoshi. Lazima tuweke hizi amri za Kristo kwa matendo.”
Bwana Hekima anatabasamu anapo msaidia Mwanafunzi kumalizia meza. ‘Ndiyo! Anasema katika Yohana 14:13, “Ikiwa
unanipenda,  tii  amri  zangu.’”  TUNASIKIZA  na  KUTENDA,  TUNASIKIZA  na  KUTENDA,  TUNASIKIZA  na  KUTENDA. HATUSIKIZI na KUSIKIZA na KUSIKIZA na labda kufanya baadaye.”
“Nafahamu.”
“Njia ya kujenga kwenye Mwamba Yesu Kristo ni kumtii kwa imani na upendo kama wa mtoto mchanga. Mungu hubariki upendo na utiifu wetu kwa Yesu. Haahidi tu kutubariki kwa sababu tunajua Neno lake. Muda mfupi kabla Yesu kurejea Mbinguni, alitupa amri za kutuongoza maisha yetu yote hapa duniani. Tunazipata hizi amri, ziituazo Mwito Mkuu, katika Matayo 28:18-20. Yesu anatuambia tufanye wafuasi. Anatuambia tuanze kuwabatiza halafu tuwafunze kutii mambo yote aliyotuamuru.
“Tunakuwa  wafuasi  kwa  kutii  amri  zote  za  Yesu.  Tunawafanya  wafuasi  kwa  kuwafunza  wengine  kutii  amri  zake  zote. Kuwafanya wafuasi huanza na kutii kwa upendo. Huo ndio msingi. Kanisa la kweli ni kikundi cha watu waliokusanyika pamoja kumtii Yesu kwa upendo. Kanisa la kwanza duniani lilianza kutii amri zote za Yesu mara moja.”
Wanamsikia mtu akiimba. Nduguye Mwanafunzi, Msaidizi, anaingia kwenye karakana amebeba gitaa. “Je, unaweza tengeza hii, Mwanafunzi? Iliachana hapa. Oh, habari, Bwana Hekima. Nafurahi kukupata! Nimewasikia askari wakisema wewe hufanya mikutano isiyo halali. Umo hatarini. Ni lazima uondoke eneo hili mara moja.”
Bwana Hekima anapiga kite. “Siwezi ondoka sasa. Lazima nisaidie familia na marafiki zako kuwa mkutano dhabiti kwanza, wa

11
wafuasi watiifu wa Yesu. Halafu ndio niondoke kupeleka Injili pahala pengine.”
Msaidizi anasema, “Mimi si mfuasi wa Yesu Kristo, lakini Mwanafunzi aliniambia juu yake na ningependa kujua zaidi. Je, Yesu anawaamuru watu wafanye nini?”
Bwana Hekima aeleza, “Inaanza na imani. Yesu aliamuru vitu vingine vingi. Tunaweza fupisha chini ya amri saba. Hatutii amri hizi ili tupate wokovu. Tunapokuwa wa Yesu, utii unakuwa asilia. Tunamtii kwa kuwa tunampenda na tunamuheshimu. Kutii amri
zake kunaonyesha kuwa uhai wake u ndani yetu.
Mwanafunzi auliza, “Amri zake ni zipi?”
“Hizi ndizo amri saba za Msingi za Kristo kwa mpangilio rahisi kabisa”
•    Tubu, amini na ubadilishwe na Roho Mtakatifu.
•    Batiza waumini.
•    Penda.
•    Mega Mkate (Meza ya Bwana).
•    Omba.
•    Toa.
•    Fanya wafuasi.”
Bwana Hekima aendelea, “Hebu tutazame kwenye Biblia tuone kwa kweli Kanisa ni nini.” Anahadithia Mwanafunzi pamoja na nduguye, Msaidizi, Jinsi Wakristo wa Kwanza Walimtii Yesu.

Zoezi.
Tafadhali tafuta Matendo 2:36-47 yale Bwana Hekima aliwauliza wale wanaume wawili:
•    Je, waumini wapya walibatizwa lini na kuongezwa kwa Kanisa?
•    Walimegea wapi mkate kusherekea Meza ya Bwana?
•    Je, walionyesha kwa vitendo upendo wao kwa wenzao?
•    Je, Bwana alilifanyia nini kanisa jipya na tiifu kulifanya nikue?
Mwanafunzi anasikiza kwa makini. “Sasa naelewa kanisa ni nini! Ni watu wakusanyikao kumtii Yesu. Kanisa la kwanza lilimheshimu Kristo. Walikumbuka aliyofunza na walitii maneno Yake kwa dhati na furaha. Familia yangu inaenda kumheshimu Yesu kama walivyofanya Wakristo wa kwanza.”
”Vyema,” Bwana Hekima anajibu. Kwa nguvu za Roho Mtakatifu, walitii hizi amri saba za msingi za Kristo tokea mwanzo.
Baraka na furaha ya Mungu huja kwa makutano wamtiio Kristo kwa upendo.”


•    Saidia mkutano wako wakariri Yohana 14:15.
Kazi ya Kufanya.
•    Saidia mkutano wako wakariri zile amri za kimsingi saba za Kristo, ambazo zimetajwa hapo juu.
•    Andika wimbo mfupi unaoorodhesha Amri saba za kimsingi za Yesu, ikiwa mtu mwingine hajafanya hivyo. Hii inazifanya rahisi wengine kujifunza. Waulize wengine wakusaidie.
•    Saidia mkutano wako wamtii Mungu kutokana na upendo, si hofu.
•    Uliza kila mtu katika mkutano wako kutii Amri za kimsingi za Yesu mbele ya sheria zote zilizoundwa na binadamu.


II-1—Amri ya Kristo ya 1

Tubu, Amini na Ubadilishwe na Roho Mtakatifu

Juma lilofuata, waumini wapya kadhaa pamoja na wengine wanaomtafuta Mungu wanajikusanyika kwenye nyumba ndogo ya Mwanafunzi. Wameketi kwa njia ya mferingo ili waweze kuonana na kuwa na mawasiliano mazuri. Bwana Hekima anawafunza amri ya Yesu ya kutubu, kuamini na kupokea Roho Mtakatifu.
Bwana Pumbavu anawasili kwenye mkutano na kutangaza, “Mimi ni Mkristo sasa. Ninafikiri ndiyo njia bora zaidi ya kuishi.” “Nitaongea nawe baadaye kuhusu hilo,” Bwana Hekima anasema. “Kwa sasa, hebu sisi zote tupange vile tutawaleta watu wengi
kwa Yesu. Sikuja kuhubiri. Zote tunaenda kuongeleshana juu ya yale Mungu angependa tufanye. Ninataka ninyi nyote muongee kuhusu hilo tafadhali.”
Mwanafunzi anasema, “Nina marafiki kando kando mwa barabara kazikazini mwa hapa. Ninataka kuwaambia juu Yesu.”
Bwana Pumbavu asema, “Natumai tunaweza epuka kuwaudhi wale watu, kwa sababu wakati mwingine wao hununua sanamu zangu ndogo. Tusiwe kila wakati tunawaambia wao ni watenda dhambi. Watakasirika.”
“Napinga,” Bwana Hekima asema. “Wakati mwingine kitu cha upendo sana ambacho twaweza kufanyia watu ni kuwaonya kuwa ni lazima watubu dhambi zao. Tusiogope eti kwa kuwa tutawaudhi. Hebu niwaambie kuhusu Mahubiri ya Ujasiri ya Yohana
Mbatizaji.”

Zoezi
Tafadhali tafuta Matayo 3:4-10 jibu kwa maswali ya Bwana Hekima:
•    Watu wa namna gani aliowabatiza Yohana Mbatizaji—watu waliokuwa wazuri na wakustahili huo ubatizo au wabaya sana wakuihitaji?

12
Hadithi Za Mchungaji

Sara asema, “Kwa vile umetuomba zote tuongee, nitasema yale nimevumbua. Sisi tunaojua kuwa tumekuwa na dhambi nyingi katika maishani mwetu tunashukuru zaidi kwa ajili ya msamaha wa Yesu zaidi ya wale wanaofikiri kuwa wao ni wema.”
Bwana Pumbavu anaanza kujibu lakini Mwanafunzi anauliza, “Tunawaambia watu nini cha kwanza juu ya Mungu?” Bwana Hekima asema, “Hebu niwaambie Kitu Kilicho Cha Muhimu Zaidi Kwenye Ujumbe wa Injili.


Tafadhali tafuta Luka 24:36-53 hivi vitu muhimu.
Zoezi
•    Ni matukio gani mawili makubwa kwenye maisha ya Yesu tunayo waeleza wengine?
•    Je, mtenda dhambi ni lazima afanye nini, kulingana na hii taarifa, ndipo apokee msamaha wa dhambi?
•    Je, uwezo wetu wa kuwaelezea wengine juu ya Yesu unatoka wapi?
Bwana Hekima  anaelezea kikundi  kilicho nyumbani  mwa  Mwanafunzi.  “Tunapowaelezea  wengine juu  ya Yesu, tunaeleza kwamba Yeye ‘Ni Mesaya’ yani Aliyetumwa na Mungu, Kristo, Mpakwa Mafuta wa Mungu. Lipi lingine tunawaambia?”
Mmoja wa waumini wapya anajibu kwa woga, “Mwanafunzi aliniambia niwaambie juu ya kifo na ufufuo wake.”
“Ndio! Na tuwaite kwa toba. Tunawauliza sio tu kufanya uamuzi wa kimawazo, bali kimatendo. Watubu na wathibitishe kwa ubatizo.’
Mwanafunzi anachangia mjadala, “Halafu tuwasaidie waumini wapya watumie nguvu za Mungu ambazo Roho Mtakatifu anatupa kuwaambia wengine juu ya Yesu.”
Bwana Pumbavu anakatiza, “Hatuhitaji kuwafanya watu wahisi vibaya juu ya dhambi zao. Hilo linawaudhi. Hii ndiyo sababu serekali haimtaki Bwana Hekima kuishi hapa. Anawaudhi. Watu wanahitaji tu kukubali kuwa Mungu anawapenda! Hilo la tosha.”
Watu kadhaa wanaanza kubishana juu ya hili. Bwana Hekima anasema, “Sikizeni, tafadhali. Watu wanahitaji kutenda zaidi ya
kukubali tu ujumbe. Hebu niwaeleze jinsi Petero alivyomuakilisha Yesu kwa Wayahudi.”


Tafadhali tafuta Matendo ya Mitume 2:22-38.
•    Petero alisema nini juu ya Yesu?
Zoezi
•    Je, Petero aliwaambia watu wafanye nini ili wapate kuokoka?
Kikundi, kikiwa kimeketi kwa mferingo nyumbani mwa Mwanafunzi, wanajadili hili kwa dakika kadhaa, halafu wanauliza Bwana Hekima ikiwa wako sahihi kwa yale wamesema. Anajibu, “Ndio. Mmejifunza vyema. Hebu sasa tuyafupishe. Mtume Petero alihubiri  ukweli  muhimu  sana wa Habari Njema.  Watu elfu  tatu waliitikia  kwa  toba,  Roho  Mtakatifu  akinena na  mioyo  yao. Walibatizwa siku hiyo kwenye kanisa. Ni sharti tusiwahesabu waumini wapya mpaka waongezwe kwa kanisa kupitia ubatizo, la sivyo tutasababisha machafuko. Sasa, ni kweli gani ambazo mitume waliwafunza wale waliomtafuta Mungu?”
Mwanamme mmoja anajibu, “Yesu ndiye Mwokozi aliyekubaliwa na Mungu pitia miujiza kama Bwana na Mesaya.” Sara anasema, “Kifo chake kinatuletea msamaha.”
Mwingine anaongezea, “Ufufuo wake unatuletea ushindi juu ya mauti na maisha mapya kupitia Roho Mtakatifu wa Mungu.” Bado mwingine anajibu, “Mwito wetu ni toba, imani katika Yesu, ubatizo na kuingia kanisani.”
Mwanafunzi anaafiki, “Nitafuata mfano wa Mtume Petero na kuwaambia jamaa wangu hadithi hiyo ya nguvu ya maisha, kifo na ufufuo wa Yesu.
Nduguye Mwanafunzi aitwaye Msaidizi anasema, “Mimi ninataka kumfuata Yesu. Ninaweza tubu dhambi zangu kwa sababu
Roho wa Mungu ananiwezesha kufanya hivyo.” Anachukua gitaa yake na anaanza kutunga wimbo mpya juu ya msamaha wa ajabu wa
Kristo.
“Ajabu!” Mwanafunzi anashangaa, “Ninafurahi kwa kuwa marafiki na jamaa yangu wanakuja kwa Yesu!”
Siku chache baadaye hiki kikundi kinakutana na Mwanafunzi nyumbani mwake na Bwana Hekima anatangaza, “Sitaweza kuja kuwafunza tena. Ninamuachia Mwanafunzi ushukani. Amekomaa katika Kristo na sasa amehitimu kibiblia kama mzee mchungaji. Mimi ninamuekelea mikono kumtuma kulichunga kundi hili wakati sipo.”
“Usituache!” Sara analia.
“Sina  budi.  Mwanafunzi,  tutakwita  ‘kiongozi  mshikilizi’  mpaka  wakati  utaweza  kuifanya  kazi  hii  bila  uelekezi  wangu. Utambatiza Msaidizi na wale wengine.”
Bwana Pumbavu anapinga, “Ni punde sana! Mkoi wangu alisoma Biblia penye inasema kuwekelea kiongozi mpya mikono ni hivi ghafula!”
Mwanafunzi aeleza, “Je, Mtume Paulo alimaanisha nini kwa neno ‘ghafula’? Tunaangalia mfano wake ili tuelewe. Mimi sijaharakisha kuliko vile mtume Paulo alifanya chini ya mazingira haya, kwa kuwa mkutano wapya bila kiongozi wa aina yeyote, na
chini  ya  mateso  katika  Galatia  katika  kitabu  cha  Matendo  14.  Ninafuata  mfano  wake.  Mwanafunzi,  utawabatiza  watu  wale uliwaongoza kwa Yesu.”

Kazi ya Kufanya.
•    Saidia mkutano wako ufahamu vitu tunavyopaswa kuwaambia watu, Luka 24:46-47
•    Panga kile utafanya kuisaidia jamaa yako, marafiki na majirani kutubu na kumwamini Kristo.
•    Saidia waumini wapya kuelewa kwamba wanapo mgeukia Mungu, wanapokea musamaha wa dhambi na vipaji vya Roho
Mtakatifu.



13
II-2—Amri ya Kristo ya 2


Batizwa
(Halafu ishi maisha matakatifu katika Yesu yanayoaanzishwa na ubatizo)

Kundi linalokutana kwa nyumba ya Mwanafunzi linaongea juu ya ubatizo. Bwana Hekima anasema, “Ni amri ya msingi ya Yesu, katika Matayo 28:18-20. Tafadhali uliza swali lolote.”
Bwana Pumbavu anapingana, “Ni mapema sana kuwabatiza watu hawa! Mkoi wangu anasema kwamba kanisa lao hungoja mpaka waumini wamekomaa kwa kila njia. Kwa hivyo kuweni makini. Je, na mkiwabatiza halafu wengine watoke kanisani? Ngojea hadi muone jinsi matendo yao yalivyo. Halafu mnaweza watuza wale walio wema kwa kuwabatiza.”
Bwana Hekima anapiga kite. “Wewe huelewi maana ya ubatizo. Hatuwezi hairisha utii kwa Kristo. Hili huja kwanza. Ubatizo huanza uchungaji wa waumini wapya walio tubu.”
Msaidizi anasema, “Nataka kubatizwa. Je, ni nini lingine Biblia inasema kuhusu ubatizo?”
Bwana Hekima anajibu, “Mwanafunzi, unajua hadithi ya Yule Askari Aliyetubu. Tafadhali Waambie.”


Tafuta katika Matendo 16:22-34 yale Mwanafunzi alieleza.
•    Kwa nini askari alitaka kujiua?
Zoezi.
•    Je, askari alifanya nini punde tu baada ya Paulo kumwakiki kuwa angeweza kuokoka ili na wengine wamjue Kristo?
•    Je, askari na familia yake walibatizwa lini?
Bwana  Pumbavu  analiambia  lile  kundi  lililokuwa  linajifunza  ubatizo  nyumbani  mwa  Mwanafunzi,  “Hatuwezifanya  jinsi isemavyo Biblia. Siku hizi si kama zamani.”
Mwanafunzi anamukosoa, “Ndio ni kama zamani. Dhambi haijabadilika. Mungu hajabadilika. Ubatizo haujabadilika. Yule askari
Mfilipi aliogopa maana alikuwa ameangamia—alifikiri atauawa kwa kuwa ameshindwa kuwalinda wafungwa. Alikuwa na hofu bila tumaini la wokovu. Alijua amepotea. Jamii yangu wako hali kama hii, pia. Wamekuwa waovu sana, lakini Yesu alikuja kuwaokoa wale wanaokubali kwamba wamepotea na hawana tumaini. Ubatizo ni gharama kwa wale wanahitaji uhakiki wa nguvu wa msamaha.” Bwana Hekima anaongezea, “Ndio, mtume Paulo anaeleza katika Warumi 6:3-8 ya kwamba ubatizo si tu utakazo kwa maji. Katika ubatizo, asilia ya dhambi zetu inasulubishwa na Kristo. Tunainuliwa pamoja na Kristo aliyefufuka kwa maisha mapya. Watu wanapotubu, ubatizo wao unawasaidia kuwahakikishia maisha yao mapya katika Kristo. Tunawaelezea kwamba Roho Mtakatifu anawashukia kama kipaji toka kwa Mungu kuwasaidia waishi maisha ya ushindi. Je, Paulo alijuaje kuwa yule mlinda gereza alikuwa
mwanifu?”
Mwanafunzi anajibu, “Kwa matendo yake yule askari aloinyesha anamwamini Yesu. Mara moja aliita familia yake. Na alimtii Yesu kwa kubatizwa. Hebu tuwahimize waumini wapya waanze kuwafanya wafuasi wa Kristo mara moja, wakianza na familia zao wenyewe, jamaa na marafiki.
Msaidizi asema, “Yule askari alionyesha toba na imani yake kwa kubatizwa mara moja.”
“Ndio,” Bwana Hekima anajibu, “Ubatizo ndiyo kanuni pekee ambayo Yesu alilipa kanisa lake kuhakiki wokovu wetu, ambao ni mabadiliko ambayo Mungu anaanza rohoni mwetu. Mitume walimbatiza mara moja kila mtu aliyemgeukia Kristo. Waliwapokea kwenye kikundi kwa njia hii. Mungu aliwaongeza kwenye kanisa, Mwili wa Kristo, kupitia nguvu za Roho Mtakatifu.”
Bwana Pumbavu anakataa, “Lakini marafiki na jamaa wengine wa Mwanafunzi wanaotaka kubatizwa ni walevi na wezi! Watu watalishutumu kanisa ikiwa mtawakubali kabla hawajathibitisha kuwa wanastahili.”
Mmoja wa wanaume anasema, “Nimeiishi maisha ya dhambi sana. Ninataka kutubu na kumfuata Yesu Kristo. Lakini huenda
Bwana Pumbavu anasema kweli. Nitailetea kanisa sifa mbaya ikiwa nitabatizwa.”
Bwana Hekima anamuhimiza, “Ubatizo ni kwa watu wabaya. Sikiza hadithi ya Mtoza Ushuru Aliyesamehewa.”

Zoezi
•    Tafadhali tafuta Luka 18:9-14 yale Bwana Hekima alimweleza yule mtu aliyekuwa amevunjika moyo.
•    Watu wawili walikuwa wakiomba. Ni yupi aliomba ombi refu zaidi?
•    Ni yupi aliyesikizwa na Mungu?
•    Ni yupi aliyehesabiwa haki mbele za Mungu?
Yule mtu aliyevunjika moyo anahisi yu huru. Na anaanza kutabasamu tena. Bwana Hekima anaelezea kikundi, “Mitume hawakutumia ubatizo kama sherehe za kuhitimu baada ya masomo marefu. Hawakuitumia kuwatuza wale walikuwa wamejithibitisha kuwa wanastahili. Hizi tamaduni za kibinadamu zilikuja tu baadaye kwenye baina ya makanisa. Katika Agano Jipya, watu walikaribishwa kwa kanisa kupitia toba na ubatizo. Halafu walikua kiroho wakisaidiwa na Mwili wa Kristo, yaana waumini wenzao, waliowapenda na kuwatumikia.”
Bwana Pumbavu anamwambia Mwanafunzi, “Wewe huna mamlaka toka kwa Mungu ya kuwabatiza hawa watu.”
“Ndio, anayo.” Bwana Hekima anasema. “Tunapata Mamlaka ya Kuwabatiza Waumini Wapya katika Matayo 28:18-20.)


Tafadhali soma Matayo 28:18-20, sasa tafuta:
Zoezi
•    Kwa mamlaka gani Yesu anatuamurisha kuwafanya wafuasi?

14
Hadithi Za Mchungaji

•    Ni vitu gani viwili tunavyowafanyia watu ili wawe wafuasi wa Kristo?
•    Je, Yesu anaahidi kufanya nini ili kuturahisishia kutii huu Utume Mkuu?
Watu wanaondoka kwa mkutano lakini Bwana Hekima anabakia akimwelezea Mwanafunzi Viwango Vitatu vya Mamlaka kwa kazi tunayofanya kama kanisa. “Mwanafunzi, hapa kuna njia rahisi ya kukumbuka ni wapi mamlaka yetu yanatoka:
•    Kwanza kabisa, na juu ya zote, ni amri za Yesu na Mitume wake.
•    Pili, matendo ya Mitume, ambayo hayakuamuriwa.
•    Tatu, tamaduni zetu za kibinadamu—vitu tunavyo kama mwili wa kanisa kuvifanya, ambavyo havijatajwa katika Agano Jipya.
Mwanafunzi anasema, “Ninaelewa. Tunatii amri za Yesu juu ya zile zingine zote. Hizi amri pamoja na zile za mitume ndicho kiwango cha kwanza cha mamlaka. Hakuna chochote kinawezatuzuia kumtii Yesu  kwa upendo.
“Ndio. Kiwango cha pili kinarejelea matendo ya mitume ambayo hayakuamurishwa. Ni mifano kwetu sisi. Hatuwezi kuzuia vitu wao walifanya. Pia hatuwezi kuwaamuru, kwa maana Yesu mwenyewe hakuwahi. Haya matendo ya kimitume ni: mikutano siku ya
kwanza ya Juma, mikutano nyumbani, ubatizo mara moja, na kuwekea mikono wakati wakuwaombea viongozi wapya.” Mwanafunzi anasema, “Tamaduni za kibinadamu ni kiwango cha tatu cha mamlaka. Je, tamaduni zote ni mbaya?”
“La. Nyingi ya tamaduni ni zuri. Zinatuwezesha kufanya kazi pamoja kwa maelewano. Lakini ikiwa mazoeo yanafuruga amri za
Kristo, hatuna budi kuchagua. Tutafuata tamaduni za kanisa letu ama tutamtii Bwana Yesu Kristo?”


•    Kariri Matayo 20:18-20 pamoja na mkutano wako.
Zoezi
•    Batiza waumini wapya bila kuchelewa kwa sababu ya matakwa yaliyo wekwa na mwanadamu.
•    Waache waumini wapya washiriki kama viungo vya mwili wa kanisa kwa nguvu za Roho Mtakatifu.
•    Wasaidie waumini wapya wapeleke Kristo mara moja kwa familia na marafiki zao.
•    Chunguza tamaduni za mkutano wako kuhakikisha kwamba hakuna chochote kinachochelewesha utiifu kwa amri za Kristo na za mitume.

II-3—Amri ya Kristo ya 3

Fanya Wafuasi

Siku chache baadaye Bwana Hekima anarejea kwa basi na anaingia kwa nyumba ya Mwanafunzi. Sara anamwambia, “Mwanafunzi yuko kwa karakana. Ninafurahi kwa kuwa umekuja. Amevujika moyo.”
“Kwa nini? Nini kimefanyika?”
“Bwana Pumbavu na rafikize wanalalamikia kila mtu. Wanamushtumu Mwanafunzi kwa kufunza dini bila kwanza kwenda chuo cha elimu ya kithiolojia. Wanasema yeye anafunza tu kama mtu wa kawaida, na si kama mwalimu halisi wa dini ama afisa wa kanisa aliyesoma.”
Bwana Hekima anaharakisha kuingia  ndani ya karakana. Wanaongea juu ya yale Bwana Pumbavu na rafikize wanasema.
Mwanafunzi analalamika, “Mimi si msemi mzuri. Sina ufasaha wa lugha.”
“Kundi lako ni dogo sana wewe kuhubiri kwa tamaduni ya jukwaani. Unapaswa kueleza hadithi za Biblia ama usome kitu, na uulize maswali kuhimiza kundi hili dogo kujadili kwa uhuru.”
“Ni hivyo mimi hufanya. Nafanya vile wewe ulinifanyia. Ninasoma au ninasema hadithi, kisha nauliza maswali ili watu wajibu na kujadili. Ninahimiza kila mtu kushiriki. Lakini hilo si ndilo Bwana Pumbavu anataka. Anataka tu kusikiza kama msikizaji tu.”
“Hiyo si sawa kulingana na Yakobo 1:22 na Wakorinto wa Kwanza 14:26. Mistari mingi ya Biblia unatuambia tufundishane,
tukosoane na tuonyane. Hili lina maana kwamba inatupasa tuongeleshane katika mikutano. Ili mikutano mikubwa itimize matakwa ya Mungu kwa kanisa, ni lazima watengeneze makundi madogo madogo yanayoweza kujadili neno la Mungu na kupanga jinsi ya kulitekeleza maishani mwao na kwenye huduma zao. Yesu hatuambii tuwe wafasaha wa lugha. Anataka tufanye wafuasi. Unalenga nia mbaya ikiwa una wasi wasi kuwa wewe si mneni mzuri kwenye hadhara. Ni vyema zaidi kuwa mchungaji mwema. Hebu tuangalie Amri ya Yesu ya Kufanya Wafuasi.”

Zoezi
Tafadhali tafuta Matayo 28:18-20 la muhimu sana ambalo Bwana wetu Yesu Kristo anataka tufanye:
•    Ni nini hasa tufanye ndipo tuwafanye wafuasi?
•    Na wafuasi wanapaswa kufanya nini?
Msaidizi, nduguye Mwanafunzi, anawasili kwenye karakana akiwa na gitaa yake. “Sikiza wimbo wangu mpya, Bwana Hekima. Niliutunga kufunza amri za Kristo.” Anaimba orodha rahisi ya amri saba za msingi za Yesu.
“Vyema sana!” Bwana Hekima anampongeza. “Tafadhali wafundishe makutano wapya wimbo huu.” “Njoo ujiunge nasi,” Mwanafunzi anamwambia Msaidizi, “Tunaongea kuhusu kuwafanya wafuasi.”
Bwana Hekima anaonyesha vyombo vya seremala kwenye meza yake ya kazi na anasema, “Kristo aliwaita watu wa kufanya kazi za kawaida wawe wafuasi wake, si waneni mashuhuri. Hawahitaji wafuasi wake kuketi tu kwenye mikutano ya kanisa na kusikiza
waneni shubavu. Anawaamuru wafuasi wake kufanya vitu vilivyo muhimu katika maisha ya kanisa. Hebu nikwambie juu ya Ahadi za
Yesu kwa Wale Wamfuatao.


15
Zoezi
•    Tafadhali tafuta Luka 5:1-11 vile Yesu alisema tutakuwa ikiwa tutamfuata Yeye.
•    Pia tafuta katika Luka 5:27-32 vitu viwili ambavyo Lawi (ambaye pia aliitwa Matayo) alifanya punde tu baada ya kuanza kumfuata Yesu.
•    Yesu hakuja kuwa rafiki wa watu wema sana. Ni aina gani ya watu ambao alisema alikuja kuokoa?
Msaidizi anasema, “Ninajaribu kuwaambia rafiki zangu juu ya Yesu, lakini mimi ni mwoga. Ninaona vigumu kuongea na watu nisiowajua vyema.”
“Mungu atakusaidia,” Bwana Hekima aeleza. “Hapa, hebu tumsaidie Mwanafunzi kupaka rangi hii kabati ambayo anatengeza.
Tunaweza ongea tukifanya kazi. Yesu aliwaahidi wafuasi wake kuwa watakuwa wavuvi wa watu. Kama Petero, hatuwezi fanya lolote kuwafikia watu bila msaada wa Mungu. Ni kwa nguvu zake tu ndipo tunaweza waita watu kwenye toba na imani. Anatupa nguvu kupitia kipaji chake, Roho Mtakatifu. Tunapokea na kutumia hizi nguvu vyema zaidi tunapo fanya kazi kwa pamoja kwa vikundi vya wawili au zaidi.”
“Hii ndiyo sababu nilipata ukumu kuwaongelesha watu juu ya Bwana,” Msaidizi anajishauri, “Nilijaribu kwa uwezo wangu mwenyewe.”
Bwana   Hekima   anadokeza   kwake   Mwanafunzi,   “Chukua   ndugu   yako   Msaidizi   muwe   mkiambatana   naye   wakati unapowashuhudia watu kuhusu Yesu. Hebu tuwaombee ninyi wawili sasa hivi, ili Roho Mtakatifu awajaze na awape watendakazi-
wenza, vile Yesu aliahidi katika Matayo 9:38.”
Baada ya kuomba, Bwana Hekima aeleza, “Wakati Yesu alimwita Lawi, aliacha kila kitu na kumfuata mara moja, jinsi Petero na wafuasi wengine walivyofanya. Wafuasi wa kweli huacha Yesu kutawala sehemu zote za maisha yao na wanamtii mara moja.”
Wanamsikia mtu mlangoni. Bwana Pumbavu amekuja kwenye karakana na kizimba ambamo mna mjusi. “Hawa hula inzi. Nunua moja. Tazama hapa, nitakuonyesha.” Anaachilia moja kwenye sakafu na inakimbia kupitia mlangoni. Paka anamkamata na kutoroka naye.
Wanaongea juu ya majukumu ya Mwanafunzi kama kiongozi, kufanya wafuasi. Bwana Pumbavu anagonga meza kwa mkono,
akaangusha mkebe wa rangi. Anasema kwa sauti, “Wewe huwezi kuwafanya wafuasi hadi ujifunze thiolojia zaidi. Mkoi wangu anasema mchungaji wake alisoma kwa miaka mingi kabla aanze kufunza mtu yeyote juu ya Mungu. Wewe ni farisayo ikiwa utajaribu kuwaambia watu juu ya Mungu wakati wewe mwenyewe hufahamu lolote!”
“La!” Bwana Hekima anaingilia kwa nguvu, “Ni nini hasa unataka Mwanafunzi akafanye kuthibitisha anaweza kuchunga kundi ambalo Mungu amempa? Atembee juu ya maji? Haweziacha kuwashughulikia watu wengine eti kwa sababu yeye si mwadilifu kwa kila njia! Tunapokuja kwa Kristo sisi huwa tunawapenda wenzetu zaidi.”
“Hebu turejelee mada tuliyokuwa tukiongea juu yake,” Mwanafunzi anaomba. “Tunataka kufanya wafuasi. Kitu cha kwanza Matayo alifanya kama mfuasi wa Yesu ni kuwaita pamoja marafiki zake kwa chakula ili amwakilishe Yesu kwao. Tunawasaidia wafuasi wapya kumwakilisha Yesu kwa jamaa na marafiki zao. Tunawaambia juu ya Yesu, mafundisho yake, miujiza yake, kifo na ufufuo wake. 1 Wakorinto 15:2-5 inafafanua kwamba habari njema ni kwamba Yesu alikufa na akafufuka kutoka kwa wafu, na kwa kufanya hivyo alimletea mwanadamu msamaha na uzima wa milele.”
Msaidizi asema, “Niliwasomea familia yangu hilo usiku uliopita. Walimu wa sheria walimwita Lawi na marafiki zake ‘watenda dhambi’. Petero pia alijiita ‘mtenda dhambi’. Hawa watenda dhambi ndio watu wenye Yesu alikuja kuwaita watubu na kuwafanya wavuvi wa watu. Yesu aliita makundi ya watenda dhambi, kama vile watoza ushuru kwa karamu ya Matayo, katika kanisa lake. Anawabadilisha!”
Bwana Pumbavu anachukua kizimba chake cha mjusi na kuondoka kwenye karakana, mmoja wa mikono yake ukiwa na rangi. Msaidizi anaendelea kujadili kufanya wafuasi. “Katika Matendo 2, mitume hawangeweza kuacha kuongea juu ya Yesu, kifo na ufufuo wake. Kwa nguvu za Roho Mtakatifu, watu wengi walitubu. Mtume Petero aliwaambia wabadili mioyo na wabatizwe kwa msamaha wa dhambi na kupokea kipaji cha Roho Mtakatifu. Elfu tatu walitubu na kubatizwa, na wakaongezwa kwa kanisa siku hiyo!”
Bwana Hekima anaongezea, “Na baada ya ubatizo mitume waliwafunza mara moja kutii amri zote za msingi za Kristo. Inasema katika Matendo 2 kwamba watu walisikia na kutenda mafundisho ya mitume, wakiwa na ushirika uliojaa upendo, wakimega mkate pamoja, kuomba, na kuwasaidia wenye mahitaji. Hivyo ndivyo kanisa la kwanza lilianza!”
Mwanafunzi anahisia, “Kanisa letu pia linaanza kwa kumtii Yesu jinsi tu wale Wakristo wa kwanza walivofanya. Walipendana.
Nasi pia tusaidiane kutii yote yenye Yesu aliamuru. Tutawafanya wafuasi watiifu wa Bwana wetu Yesu Kristo!”
“Vyema,” Bwana Hekima anaitikia kwa furaha. “Amri zingine za Kristo tunazitumia tunapokutana pamoja kwa Meza ya Bwana na kwa ushirika wa upendo. Utii kwa Yesu ndiyo nguzo muhimu ya ibada ya kweli. Tunamtii kwa furaha siku kutwa, tukiomba, tukiwaambia wenzetu juu yake na kuwatumikia maskini.”
Mwanafunzi auliza, “Je, ni vitu gani tunavyopaswa kufanya tukutanapo kama mwili kumwabudu Mungu?”
•    “Nitakuorodheshea sehemu muhimu za Ibada:
•    Kuomba,
•    Kusifu Mungu,
•    Kukiri dhambi na kupokea hakikisho la msamaha,
•    Kusherehekea Meza ya Bwana,
•    Kuwa na ushirika na wenzetu.
•    Kutoa,
•    Kujifunza Neno la Mungu.”
“Je, tunavifanya kwa orodha hiyo?”
“Zifanye kwa orodha inayokubalika kwenu.”

16
Hadithi Za Mchungaji

Msaidizi anasema, “Nafikiri kanisa jipya au kundi dogo la jamaa moja au mbili wanaweza fanya vitu hivi wakutanapo pamoja.” “Mkutanapo nyumbani na kundi dogo,” Bwana Hekima anatahadharisha, “Lazima muwe na wakati halisi wa kuanza na wakati
halisi wa kumaliza ibada. La sivyo, ibada itachanganyishwa na mabo mengine na ishindwe kumuletea Mungu uwepo wake wa ajabu na taadhima.”
“Nimeshatambua hilo tayari,” Mwanafunzi anasema. “Kuanza ibada tunamuuliza kila mtu asimame na turudie Zaburi ya sifa. Kuiimaliza tunasimama kwa sala maalum ya kuwachana na ya kubariki. Kwa jinsi hii watoto watajua ni wakati gani wa kuacha
kucheza na kufanya kelele, na wakati gani wataanza tena ibada ikiwa imemalizika.”
Bwana Hekima asema, “Nilikuonyesha wewe na familia yako jinsi ya kufanya ibada rahisi ya kifamilia. Mumeifanya vyema mpaka wengine kama Msaidizi pamoja na mkewe Recho wamejiunga. Lakini sitakuwa hapa kila wakati. Naweza ondoka wakati wowote. Itakubidi uongoze bila msaada wangu. Mwanafunzi, mpe kila mtu kitu cha kufanya. Kumbuka kumpa  mtu kile kitu anafurahiya kufanya. Italingana na vipaji vyao tofauti tofauti vya kiroho. Halafu wote waweza kushiriki.”

Kazi ya Kufanya.
•    Omba na mkutano wako kwa sababu ya wale wanaomhitaji Yesu, walio karibu nawe na wale walio mbali, sehemu zilizo telekezwa.
•    Waonyeshe wafuasi wako jinsi ya kumshuhudia Yesu kwa wengine kwa njia ya kirafiki, hasa kwa familia na rafiki zao.
•    Punguza idadi ya mikutano katikati mwa juma, ili uwape wafuasi wako muda wa kuwahubiria marafiki zao.
•    Tekeleza sehemu zote muhimu za ibada wakati wa mkutano mkuu wa juma.
•    Msaidie kila muumini kufanya kitu cha kuwajenga wengine wakati wa mikutano.



II-4—Amri ya Kristo ya 4

Upendo

Mwanafunzi na nduguye Msaidizi wanawatembelea majirani na marafiki zao, wakiwaambia habari njema ya Yesu. Msaidizi anawaimbia. Wanaishi vijiji tofauti tofauti, mwendo mfupi, kwa hivyo siku moja wanatembelea eneo la Mwanafunzi, keshoye la Msaidizi. Jirani wa Msaidizi aitwaye, Mlezi, anamwambia Msaidizi, “Mimi ni mwalimu shuleni, lakini nimekuwa mgojwa na kushindwa kwenda kazini.”
Msaidizi anamwambia juu ya Yesu, lakini Mwanafunzi anazalia kimya. Wanapoondoka nyumbani mwake, Msaidizi anauliza, “Kwa nini ulikua kimya? Tunapaswa kumsaidia kwa njia yoyote. Jamaa yake inateseka.”
“Mimi simpendi Bwana Mlezi,” Mwanafunzi anakubali. “Yeye ni shemejiye Bwana Pumbavu. Mwaka uliopita nilimtengenezea viti lakini hakunilipa. Baadaye nilipouliza malipo tulibishana. Akakasirika na kunirushia kitabu. Yeye ni adui wangu. Sitawahi mtembelea tena.”
Wanarudi kwa nyumba ya Mwanafunzi na kumkuta Bwana Hekima anawasubiri. Msaidizi anamwuliza, “Mwanafunzi hataki
kumsaidia Bwana Mlezi wakati wa mahitaji, kwa sababu wamekosana tangia mwaka jana.”
Bwana Hekima anashauri, “Mwanafunzi, ni lazima utii amri ya Yesu ya Upendo, katika Matayo 22:36-40. Ndiyo amri kuu kuliko zote. Hebu nikueleza yale Yesu alisema kuhusu Msamaria Mwema.”

Zoezi.
Tafadhali tafuta katika Luka 10:25-37 yale Mwanafunzi anavumbua kwamba upendo utendaji unaweza fanya:
•    Je, ni nani tunapaswa kumuonyesha upendo, kando na Mungu?
•    Je, Msamaria alifanya nini kuonyesha upendo wake kwa jirani yake?
•    Je, kutokana na mtazamo wa Mungu, jirani yetu ni nani?
Wanaendelea kuyaongea haya nyumbani mwa Mwanafunzi. Bwana Hekima anashauri, “Mwanafunzi, wale viongozi wa kidini waliompita yule msafiri aliyejeruhiwa walijua wameamurishwa kumpenda jirani yao, lakini hawakusimama wamsaidie. Wasamaria na Wayahudi walikuwa maadui wa jadi. Lakini Msamaria hakuacha kumsaidia yule Muyahudi msafiri aliekuwa amejeruhiwa. Mtu aliye na shida, hata kama ni adui, ni jirani yako kulingana na mtazamo wa Mungu. Anatuhitaji tuwapende wote.”
“Je, ni lazima nimpende Bwana Mlezi?” “Unafikiriaje?”
“Ninabaini hivyo.”
“Mungu ni pendo, na tuliumbwa kuwa kama Yeye. Alituumba sisi kumpenda Yeye na kuwapenda wenzetu jinsi Yeye anavyotupenda. Upendo ni lazima uwe na maana. Kuongea tu juu ya Yesu haitoshi. Watu wanatambua kwamba sisi ni wa Kristo
wakati tunapotafuta njia za kuonyesha maana ya upendo kati yetu. Hatuangalii tu yale Mungu anaweza tufanyia.”
“Je wamaanisha nini ukisema ‘upendo wenye maana’?”
“Upendo una maana tu wakatu tunafanya vile vitu anavyotuamuru Yesu. Ibada yetu na vitendo vyetu vya kikanisa vinatokana na hii amri ya kwanza na kuu. Tunatawalasha upendo wetu kwa majirani wetu kwa kuwatumikia kwa njia za maana, hasa wanapo hitaji msaada.”
Bwana Pumbavu anawasili kwenye mlango wa Mwanafunzi amebeba chupa ya kijani kibichi-cheusi. “Hii ni Dawa ya Kunyosha
Sauti,” anatangaza. “Kunywa kijiko kimoja kila mwezi na utaimba vyema sana, wewe Msaidizi. Bwana Hekima, watu watakusikia

17
ukihubiri toka mbali. Hapa, nitaonyesha mfano kwa huyu paka.” Anajaza kijiko na kukiteremsha. Paka anakinukia, anaguruma na kuuma kidole chake. Bwana Pumbavu anawakemea wenzake, “Si lazima mcheke sana hivyo! Hamna tabia njema.”
Sara anakifunga kidole chake kwa bendeji na anasema, “Yesu anatuamuru tuwapende hata watesi wetu. Je, ulijua hivyo, Bwna
Pumbavu? Nilisoma asubuhi ya leo katika Matayo 5:44.”
“Lakini huwezi kumwacha adui akukasirishe na usifanye lolote! Hata paka wanajua ni lazima uwaume wale unadhani wanaweza kukuumiza! Wafanye kuteseka wafanyapo mabaya ndipo wasirudie tena!”
“Tafadhali!” Bwana Hekima anaingilia, “Hebu niwaambia juu ya Mtumishi aliyekataa Kusamehe.”


Tafadhali tafuta katika Matayo 18:21-35:
•    Ni deni kiasi gani mfalme alifutilia mbali?
Zoezi:
•    Je, mtumishi wa kwanza alimtendaje mtumishi wa pili, masikini zaidi?
•    Je, mfalme alimfanyaje yule mtumishi asiye samehe?
Wanaendelea kuongeo juu ya upendo na msamaha kwenye nyumba ya Mwanafunzi. Bwana Hekima aeleza, “Tunawaonyesha maadui zetu upendo tunapowasamehe. Hivyo ndivyo Yesu alitusamehe. Pia tunawaonyesha upendo waumini wapya kwa kuwakaribisha kwenye familia yetu ya kikanisa. Tunaonyesha wafuasi wetu upendo tunapowasikiza na kuwasaidia kuwa na huduma
za kuzaa matunda.
Baada ya maombi, Mwanafunzi anateta. “Nitamsamehe Mlezi. Lakini ni vigumu kuacha kumchukia. Sara, tafadhali andaa chakula kwa familia yake. Nitawasaidia.”
Anachukuwa kabu kubwa la mikate, mayai na vyakula vingine kumpelekea Mlezi, ambaye anashukuru sana. Mwanafunzi anamwambia, “Unahitaju ajira, lakini huwezi kufanya kazi siku nzima. Njoo kafanye kazi kwenye karakana yangu hadi utakapopata nguvu. Unawezafanya kazi nyepesi kama kuchora michoro na rangi kwenye vyombo vidogo vya mbao ambavyo ninatengeza.
Waweza pumuzika wakati wowote ikiwa unahisi uchovu. Utapata riziki ya kutosha familia yako.”
Mlezi anamtizama Mwanafunzi kwa muda mrefu. “Asante. Nitakuwa hapo asubuhi.”
Majuma kadhaa baadaye anamwambia Mwanafunzi, “Ninaweza funza kikamilifu tena. Sikiza. Juu ya mzozo tuliokuwa nao mwaka jana. Nilikukosea. Tafadhali nisamehe. Nitakulipa hilo deni.” Mlezi anaanza kuhudhuria ibada. Punde anampokea Yesu na kubatizwa.
Kwa ibada ya kuabudu, Bwana Hekima analiambia kikundi, “Mungu amewapa kiongozi mzuri. Mwanafunzi sasa anaongoza
ibada za kuabudu bila kuhitaji msaada wangu. Na anazifanya kibiblia. Ninyi nyote mnashirikishwa. Mnatoa ushuhuda, mnanena maneno ya kuhimizana, mnakariri mistari na kusema hadithi za Biblia. Wengine wanaimba, wengine wanaigiza hadithi za Biblia. Mnajibu maswali aulizayo Mwanafunzi baada ya mtu kusoma maandiko kutoka kwa biblia au hadithi. Haya ndiyo Paulo anatwambia tufanya katika Wakorinto Wa Kwanza Mlango 12 na 14. Yote haya ni kibiblia sana na ni ya afya ya kiroho. Ninyi nyote mnapaswa kumshukuru Mungu kwa kuwapa kiongozi ambaye anaweza kuwaongoza katika njia Biblia inasema.”
Wakati  wengine  wanaondoka  baada  ya  mkutano  kwenye  nyumba  ya  Mwanafunzi,  Bwana  Pumbavu  anamwambia  Bwana Hekima, “Bila shaka umemfanya Mwanafunzi ajivune sana! Lakini mimi sipendi jinsi anavyoongoza. Wale watu wapya kwenye kundi  letu  wanavigugumizi  na  wanatoa  majibu  ya  kiupumbavu  kwa  maswali.  Anawaachilia  wakashiriki  mara  nyingi  sana!
Hawastahili haki hii! Anawapa uhuru mwingi sana! Kikundi hiki kinahitaji kiongozi ambaye ni mkali. Mimi naweza ongoza!”
“Oh, hapana!” Bwana Hekima anapiga kite. “Wewe u mkatili sana na neema ya Mungu! Hebu sikiza hadithi ya Wafanyi Kazi
Wenye Wivu.”


Tafadhali tafuta Matayo 20:1-16:
Zoezi.
•    Je, nia yetu kwa waumini wapya inapaswa kuwaje, hata kama sisi tumemfanyia kazi sana na kuteswa kwa ajili yake ilihali wao bado?
Bwana Pumbavu anatoa maoni kwa Bwana Hekima, “Mimi sielewi mafundisho yako! Eti waumini wapya wapate haki ya kupata neema ya Mungu kama sisi!”
“Tunawapokea kanisani kwa wingi wa neema jinsi Mungu alivyotupokea sisi.”
Mwanafunzi anakaribia na Bwana Hekima anawasihi kuweka nguvu umoja wa mwili wa kanisa. Anawaeleza juu ya Ombi la
Yesu ili tuwe Wamoja na Tupendane.



Tafadhali soma Yohana 17:20-23 kupata:
•    Je, Yesu alimwambia Mungu atufanyie nini?
Zoezi
•    Ni njia gani umoja wetu ni kama umoja kati ya Mungu Baba na Mungu Mwana?
•    Je, Yesu alisema ulimwengu utajuaje kwamba Mungu alimtuma Yesu?
Bwana Hekima anamwambia Bwana Pumbavu, “Ninyi wanaume wawili munahitaji kupatana zaidi. Watu wa Mungu wana umoja katika kanisa lake. Sisi zote tu wamoja katika Yesu Kristo. Kanisa la nyumbani ni kikundi cha watu ambao wameuungana kumtii
Yesu kwa upendo, popote walipo. Mungu anataka tusaidiane na tujengane. Yesu hatuambii tumfuate kila mmoja kwa njia yake
mwenyewe. Tunaenenda pamoja.”
“Je, unamaanisha nini ukisema tu wamoja katika Kristo?” Mwanafunzi auliza.


18
Hadithi Za Mchungaji

“Roho Mtakatifu anatuunganisha katika Mwili wa Kristo kwa njia ambayo wanadamu hawawezi kuelewa kwa akili ya kawaida. Yesu alisema katika Yohana 17 kwamba tu Wamoja katika Yeye jinsi Yeye aliye mmoja na Mungu Baba.”
“Mimi sielewi hayo,” Bwana Pumbavu analalamika. “Mimi siamini chochote ambacho sielewi.”
“Hakuna  mwanadamu  aelewaye  kwa  ukamilify  siri  ya  maumbile  ya  Mungu  na  maisha  yetu  mapya  matakatifu  ambayo yamefichwa katika Kristo, kama Wakolosai 3:1-7 inavyotufunulia. Yeye anapendelea utii wetu. Tunaweza jifunza mafundisho mengi ambayo ni mazuri. Lakini ni bora zaidi kumutii Kristo. Jambo jema zaidi ni kutenda yote. Jifunze na utii. Hilo linajenga mkutano, Mwili wa Kristo!”
“Kwa nini unakiita hiki kikundi Mwili wa Kristo?” Mwanafunzi auliza.
“Kanisa la Agano Jipya ni Mwili wa Kristo—si dini wala jengo. Tunamaanisha watu wa Mungu, wale wanaokusanyika kumwabudu na kumtumikia. Tunajifunza kama viungo vya huu mwili kuonyesha upendo wetu kwa Mungu mmoja wa Kweli kwa
matendo na kwa kupendana sisi kwa sisi.”
“Kwa nini upendo ni wa muhimu sana?” Bwana Pumbavu auliza.
“Ni kwa sababu hii ndiyo nia takatifu kwa yote tutendayo. Mwanafunzi, je unakumbuka Yesu alisema nini kuhusu hili?”
“Ndiyo. Alikubaliana na amri ya kale kutoka Kumbukumbu Ya Torati 6:4-5, “Sikia, O Israeli, Bwana Mungu, Bwana ni mmoja. Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na nafsi yako yote na kwa akili zako zote na kwa nguvu zako zote.”
“Kumpenda Mungu ni vigumu tusipoaamini kwamba Yeye ni Mmoja,” Anakariri Bwana Hekima.
“Waumini katika Agano Jipya walikusanyika pamoja kumutii Yesu Kristo kwa upendo. Matendo 2 inaonyesha kwamba baada ya wao kutubu na kubatizwa, waliyatekeleza wafundisho ya mitume katika maisha yao. Walitekeleza ushirika wa upendo, wakatoa kwa roho safi, wakasherehekea Meza ya Bwana na kuomba kwa nguvu. Kanisa la kwanza lilianza na huu muungano, utii wa upendo kwa
Bwana wetu Yesu Kristo. Upendo wa kweli uliozaliwa na Mungu unazaa utii wa furaha; hiki ndicho kiini cha imani yetu.”

Kazi ya Kufanya.
•    Omba ili mkutano wako wawe na mizizi na msingi ndani ya upendo.
•    Saidia Mkutano wakariri Amri ya Yesu ya kupenda, katika Luka 10:27.
•    Panga mkutano wako watumikie watu walio na mahitaji ya kimwili au kiroho.
•    Panga shughuli kama mwili ambao utajenga umoja baina yenu na mikutano wengine.


II-5—Amri ya Kristo ya 5

Omba

Siku chache baadaye, Bwana Hekima anaongea na dreva wa lori kwenye soko juu ya Kristo wakati Mlezi anamkimbilia na kumnong’onezea, “Askari wanapanga kukukamata! Niliwasikia wawili wao wakisema hivyo. Serikali haipendezwi na jinsi unavyoongea hadharani juu ya Yesu Kristo! Njoo!”
Wanaingia haraka kwenye karakana ya Mwanafunzi. Baada ya wao kuomba na Mwanafunzi, Bwana Hekima anakariri, “Sijui ni kwa muda gani nitaendelea kukutembelea. Kabla nienda, nataka kuhakikisha kuwa maombi ni asilia ya maisha yako, na sio tu wakati hatari imetokea. Yesu anatwambia tuombe katika Yohana 16:24, ili furaha yetu ikamilike. Hebu  nikwambie juu ya Ombi la Maana
sana La Yesu wakati alikuwa anatarajia kifo.”


Tafadhali soma Matayo 26:36-46 sasa ili upate:
•    Yesu aliomba wapi?
•    Yesu alimwomba nani?
Zoezi
•    Yesu aliomba akiwa ameketi vipi wakati huu, kuonyesha kuugua kwa maombi yake?
•    Je, shauku kuu ya Yesu kwenye maombi yake ilikuwa nini, ambayo ilimwongoza kuachilia ombi lake la kwanza?
Bwana Hekima anawaelezea Mwanafunzi na Mlezi wakiwa ndani ya karakana ya useremala, “Yesu alizidi kumusihi Baba hadi alipokuwa tayari kukabiliana na kifo. Hakutaka kufa msalabani, bali alitaka zaidi kumtii Mungu Baba yake. Alikuwa na imani kuwa Baba atajibu, hata kama angesema ‘la’ hilo ndilo lingekuwa jibu bora. Nasi vile twapaswa kujifunza kuomba kwa bidii, tukimwamini
Mungu badala ya kudai tu mahitaji yetu.”
“Niliomba kwamba usituache,” Mlezi anasema.”

“Mungu anaweza kunihitaji nibaki. Kama Yesu, wacha tumwombe Baba kupitia kwa nguvu za Roho Mtakatifu, atuonyeshe mapenzi yake, yawayo yale. Je, unakumbuka yale niliwafunza juu ya maombi juma lililopita?”
“Ndiyo,”  Mwanafunzi  anajibu.  “Tunaomba  kwa  Jina  la  Yesu  ambaye  ndiye  njia  pekee  ya  kumfikia  Mungu.  Kifo  chake msalabani kimefanya iwezekane sisi kuingia moja kwa moja katika uwepo wa Baba kuomba kwa ujasiri kile tunahitaji, kama vile Waebrania 4:16 inatufunulia. Utenda dhambi wetu hauzuii maombi yetu kumufikia Mungu tena. Yesu ni muombezi wetu.”
Mlezi anaongeza, “Maandiko pia yanatuambia tusiwaombe waliokufa, katika Kumbukumbu la Torati 18:11. Nilifanya hivyo
kabla nimjue Kristo. Nilifikiri kuwa roho ya mmoja wa mababu zangu aliniambia nisimulipe Mwanafunzi deni la viti alivyonitengezea mwaka jana. Yesu ameniweka mimi na familia yangu huru kutoka kwa hofu ya hao mapepo! Sasa tunajua kwamba Yeye ana

19
mamulaka zaidi ya mapepo.”
Bwana Hekima anajibu, “Ni lazima tuelekeze maombi yetu kwa Mungu pekee. Na ni lazima tuombe kwa Jina la Yesu, mbaye
Mungu Baba amepea mamlaka yote mbinguni na duniani, jinsi Matayo 28:18 inatufunulia.”
Mlezi anauliza Bwana Hekima, “Je, kuna njia moja ya kuomba iliyo ya nguvu zaidi ya njia zingine? Ikiwa nitarudia ombi moja mara nyingi au niseme kwa sauti kuu, je Mungu atanijibu haraka? Bwana Pumbavu aliniambia kwamba Mungu anasikia maombi yetu tu ikiwa tututaomba jinsi kanisa la mkoi wake huomba.”
“Tuna uhuru wa kuomba kwa njia tofauti tofauti jinsi tuonavyo katika Maandiko. Mungu hajali kama tunasimama, keti, piga magoti au lala chini, piga kelele, omba kimya kimya, pekee yako au na wengine. Mungu anataka sisi tuombe toka ndani ya moyo bila kuchanganyikiwa. Alitahadharisha kuomba kwa maneno mengi au maombi marefu ya kurudia rudia ili tuwapendeze watu, katika Matayo 6. Kabla achiachilie wamshike, Yesu alilala chini kifudifudi  kuonyesha hitaji lake kubwa na kuchiachilia kwa Baba. Wengine kwenye Biblia waliketi, simama, piga magoti, au waliinua mikono. Watu waliomba kwa njia mbali mbali. Waliongea, imba, piga yowe, omba pamoja kama kikundi, na waliomba kimya kimya. Maombi yetu yana nguvu, si kwa sababu ya kuketi kwetu, bali ni kwa sababu tu waaminifu mbele za Mungu na tunamtolea Mungu roho zetu, tukiamini kwa udhabiti kwamba Yeye anasikia.”
Mwanafunzi anaongezea, “Wakati mwingine Yesu alienda mbali kuwa pekee yake ili amwombe Babake. Sisi pia tunaomba pekee yetu kila siku kuufanya dhabiti uhusiano wetu na Baba yetu wa Mbinguni. Yesu pia aliomba hadharani, pia sisi, tunawezaomba kwa sauti pamoja na ndugu na dada zetu katika Kristo.”
Bwana Hekima anasema, “Hebu niwaambie juu ya hadithi ambayo Yesu anatufundisha Kuomba. Anatupa sababu kadhaa za
kuomba, ambazo ni muhimu kuliko hali zetu.”

Zoezi.
Tafadhali soma hili ombi, ambalo wengine huita “Sala Ya Bwana”, katika Matayo 6:1-13. Tafuta yatoayo hizi sababu za kuomba kila siku:
•    Kumsifu Mungu
•    Kupanua Ufalme wa Mungu
•    Kuitisha mahitaji yetu
•    Kuomba msamaha
•    Kuitisha ulinzi dhiti ya muovu.
Bwana  Pumbavu  amekuwa  akisikiliza  pale  mlangoni  mwa  karakana,  na  anaingia.  “Nimekuwa  nikimwomba  Mungu  anipe nyumba kubwa na sijafanikiwa. Mungu hujibu tu maombi wakati anajisikia kufanya hivyo. Yeye hufanya vile anafanya kwa vile yeye ni Mungu, na hatuna uwezo wowote wa kumulazimisha.”
“Mungu hutujibu,” Bwana Hekima anaelezea. “Lakini anajibu maombi yetu kulingana na utii wetu, jinsi Yohana wa Kwanza
3:21, 22 inaelezea. Dhambi nne huzuia maombi yetu: kutosamehe, uchoyo, kukosa imani, na kukosa kuwapenda wenzetu. Ni lazima tukiri hizi dhambi. Tukifanya hivyo, Mungu ni mwaminifu na mwenye haki hata kutusamehe na kubadili mioyo yetu, kama vile Yohana wa Kwanza 1:8-10 inatuahidi.”
Jioni hiyo Mwanafunzi anawakusanya waumini nyumbani mwake kumwomba Mungu amulinde Bwana Hekima dhiti ya askari. Kama kanisa la Agano Jipya katika Matendo 4:29-31, wanaomba kwa bidii. Wanamuuliza Mungu awaruhusu wapeleke habari njema ya Yesu kwa watu.

Kazi ya Kufanya
•    Saidia Kundi lako kukariri Sala ya Bwana katika Matayo 6:9-13.
•    Wasaidie baba kuwaagiza watu wa familia zao kuomba kila siku, faraghani na pia kama familia. Wakati bora zaidi wa kuomba faraghani ni asubuhi mapema.
•    Uliza kila mtu kwa familia kutafuta wakati fulani wa maombi ya kifamilia kila siku.
•    Wajuze makutano wakati Mungu anapojibu maombi, ili kuwatia wengine moyo.
•    Waonyeshe wafuasi wako jinsi ya kuomba kwa uaminifu toka ndani ya moyo bila ya kujaribu kuwapendeza watu na maneno makuu au marudio yasiyo na maana.


II-6—Amri ya Kristo ya 6

Mega Mkate

Asubuhi moja Mwanafunzi anamwendea Bwana Hekima nyumbani kwa mkoi wake mapema, akiogopa kuwa askari wanaweza kuwa wamemshika Bwana Hekima. Lakini bado yupo huko. “Tafadhali njoo nyumbani kwangu,” Mwanafunzi anamwomba. “Wakija kukukamata, mkoi wako atatuonya na tutakuficha. Njoo sasa. Waumini wanakusubiri utuongoze kwenye Meza ya Bwana.”
Bwana Hekima anajibu, “Nitakuja, lakini wewe ni lazima uongoze ibada zote tangia sasa na kuendelea. Nimekufundisha jinsi ya kufanya hivyo.”
Mwanafunzi anaongoza mjadala nyumbani mwake, ambao Bwana Hekima alimsaidia kuandaa. Kikundi kinaongea juu ya amri za Bwana Wetu ya Kumega Mkate na kushiriki kwenye siri ya Mwili Wake. Mwanafunzi anaonyesha meza kwa kikombe na mkate. “Bwana Hekima alituonyesha jinsi ya kusherehekea Meza ya Bwana vile tu alijifunza kwenye Maandiko. Hebu tuongee juu ya Kwa
Nini Tusherehekee Meza ya Bwana.”

20
Hadithi Za Mchungaji


Zoezi
•    Tafadhali tafuta Matayo 26:26-27 yale Yesu alisema mkate na kikombe vinamaanisha.
•    Tafuta katika Luka 22:1-22 sababu mabayo Yesu alitupa ya kusherehekea Meza ya Bwana.
•    Tafuta katika 1Wakorinto 11:23-34
•    Kwa nini hatuwezi kula Meza ya Bwana pamoja na chakula cha kawaida?
•    Ni nani anastahili kushiriki Meza ya Bwana?
Mwanafunzi anaendelea kuelezea kundi lake, katika nyumba yake, “Yesu anatuambia kwamba huu mkate ni Mwili wake na kikombe hiki ni Agano jipya ambalo Mungu amefanya kwa damu yake. Kupitia hii sherehe tunatambua kuwa Bwana yu karibu nasi. Agano jipya kati ya Mungu nasi linatuwezesha kumukaribia Mungu kupitia kwa Yesu. Kupitia kwa Yesu, tuna maisha mapya,
matakatifu na ya milele kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Unasoma haya katika Matendo 2:38 na Waebrania 9:15. Kwa kula Meza ya
Bwana, tunaifanya imani yetu dhabiti katika neema ya Mungu.” Mlezi anauliza, “Kwa nini unaliita agano jipya?”
Mwanafunzi anasita ili Bwana Hekima ajibu. “Kabla Yesu afe na kufufuka toka wafu, Mungu alikubali sadaka ya damu ya wanyama ndipo asamehe dhambi za wanadamu. Hilo ndilo lilikuwa agano la kale, lililofanywa na Waisraeli wakiongozwa na Musa. Badala  ya  sheria  zilizoleta  kifo  ikiwa  ungezivunja,  Mungu  sasa  anatupa  Roho  wake  Mtakatifu  kuifanya  mioyo  yetu  upya  na
kutuongoza. Hatuko tena chini ya sheria ya Agano la Kale. Warumi sura 1-8 inaeleza haya.”
Mwanafunzi anasema, “Tunasherehekea Meza ya Bwana kumkumbuka Yesu Kristo na kuonyesha imani yetu katika sadaka ya kifo chake hadi arudi tena. Si lazima tuelewe siri ya haya yanayotendeka.”
“Hilo ni kweli,” Bwana Hekima anaafiki. “Tunasherehekea hii Meza ya Bwana mara kwa mara ili tupokee baraka toka kwa
Bwana kwa sababu ya utii wetu. Mkutano ambao unasahau Meza ya Bwana haumtukuzi Kristo. Meza ya Bwana inaonyesha umoja wetu kama mwili wa Bwana na umoja wetu na Kristo kama Kichwa chetu. Sasa Mwanafunzi atatulisha hii Meza.”
Bwana Hekima anamuuliza Mwanafunzi, “Je, unakumbuka ni nini Meza ya Bwana inaturuhusu kushiriki?”
Mwanafunzi anafikiri kwa dakika moja, halafu anakumbuka, “Wakorinto wa Kwanza 10:16-17 inatuambia kwamba kushiriki mkate na kikombe ni kushiriki mwili na damu ya Bwana wetu. Hatuelewi hili vyema sana. Kwa hivyo tunanukuu Maandiko tunaposhiriki Meza ya Bwana, na kumwamini atende kazi mioyoni mwetu. Kazi yake ya miujiza iko ndani yetu, si ndani ya vipande visivyo na uhai vya mkate. Tunasema vile Yesu alisema, “Chukua na ule; huu ndio mwili wangu. Kunywa, hii ndiyo damu yangu ya Agano Jipya, jinsi isemavyo Matayo 26:26-28.”
Baada ya ibada ya Komunyo, Bwana Pumbavu anasema kwa sauti, “Meza ya Bwana ni sherehe takatifu. Mkoi wangu aliniambia kwamba unahitaji mchungaji aliye hitimu na vyeti na masomo ya thiolojia kuwalisha watu. Na ukiifanya mara nyingi, watu hawataiheshimu.”
Bwana Hekima anakataa. “Kanisa la Agano Jipya lilimega mkate pamoja siku ya kwanza ya juma manyumbani mwao, jinsi Matendo 20:7 inavyotufunulia. Hata kama Mungu hajatuamuru kumega mkate kila juma, mitume walitupa mfano. Hili linaongeza nidhamu na ibada katika makutano wapya. Kundi lolote la waumini, liwe dogo au jipya kiasi gani, lazima lihimizwe kufanya Meza ya Bwana. Bwana hakusema tutii na kungoja hadi tuwe na mchungaji aliyesoma sana! Matakwa ya kibinadamu yanayozuia utii kwa amri za Yesu hufanya madhara makubwa sana.”
Bwana Pumbavu analalamika, “Mkewe Msaidizi Recho alipigana na mke wangu wiki mbili zilizopita. Kwa hivyo tusile Meza ya
Bwana hadi hili lisahaulike. Recho asiruhusiwe kula hadi baada ya miezi sita. Mkoi wangu aliniambia haya.”
“Bwana Pumbavu, wewe umesahau kwamba Meza ya Bwana ni kusherehekea upendo wetu kwa Kristo na kwetu sisi wenyewe. Tunaifanya kwa sababu tunamtii Kristo. Hatuwezi wakataza watu wote eti kwa sababu mtu mmoja katika mwili ametenda dhambi. Kama ni hivyo, hakuna mtu ataweza kushiriki! Na hatuitumii kama kiboko cha kuwaadhibu watu ambao wamekosea, kwa kuwatenga kwa muda mrefu. Wagalatia 6:1 inatufunza kwamba muumini aliyekosea akitubu, tunamrejesha mara moja. Hivyo ndivyo tulifanya. Ndio, dhambi zetu hudhaifisha ushirika wetu na Mungu, na, wakati ukiendelea kusonga, na washirika wenzetu pia. Lakini tunapokiri na kugeuka na kuacha dhambi, Mungu huurejesha ushirika wetu. Kama vile 1Yahana 1:9 inaahidi, Ikiwa tutakiri dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki na atatusamehe dhambi zetu na kututakasa na udhalimu wote. Mkewe Msaidizi Recho aliomba msamaha kwa mkeo. Kwa hivyo tulimkaribisha tena kwa Meza ya Bwana.”
Bwana Pumbavu analalamika, “Ninyi mnaweza msamehe, lakini mimi siwezi!”
Bwana Hekima anaingilia kwa dhati, “Mwili wakanisa haushiriki udaku na husuda bali unawasaidia watu kupata njia ya kurejea kwa Mungu. Ikiwa Recho amekiri dhambi zake kwa Mungu, Mungu amemsamehe. Ni lazima mkutano wamsamehe pia. Hebu tuangalie Hatua Tunaweza Chukua Kwa Waumini Waendao Kando ili kuwarejesha, na la kufanya na wale wasiotubu.”

Zoezi
•    Tafuta Matayo 18:15-17 hatua zakufuata kumrejesha muumini anayehitaji adabu.
Baada ya kusherehekea Komunyo katika nyumba ya Mwanafunzi, Bwana Hekima analiambia kundi, “Ni lazima tuagane sasa. Ni lazima niwaache. Huenda Mungu atanirejesha siku moja.” Machozi yanalenga kwa macho ya watu. Wengine wanalia.
Mwanafunzi anasema, “Bwana Hekima amependa kikundi hiki na ametufundisha kutii amri za Yesu ili tuwe kikundi chenye nguvu  yeye akisha ondoka. Alihakikisha kwamba tuko na kila  kitu tulichohitaju  ili tukue na kuanza mikutano wengine. Zote
tunakushukuru, ndugu.”
“Ngoja,” Bwana Hekima anasema, “Nilisahau kitu. Kuna kitu kingine tunahitaji kufanya.” Anasoma Matakwa ya Kiongozi.

Zoezi

21
Tafadhali sasa tafuta katika Tito 1:1-9 matakwa ya kuwa mchungaji kiongozi.
Bwana Hekima anaambia kikundi, “Kundi halijakamilika bila uongozi wa uungu. Nimechunguza maisha ya Mwanafunzi kama Mkristo kwa miezi michache sasa. Anatimiza matakwa ya Kibiblia ya Kiongozi. Ndungu yake Msaidizi pia ametimiza matakwa haya. Nitawawekelea mikono ninyi wawili sasa, ndio mpokee upako wa Mungu wa kutekeleza majukumu yenu kwa kikundi hiki.”
Bwana Pumbavu analalamika, “Si sawa wewe, Bwana Hekima, kuwaamuru viongozi wetu hivi. Wewe ni mgeni. Wewe si wa kijiji hiki na wewe si mmoja wa kundi hili. Mkoi wangu anasema kwamba maasikofu toka nje hawapaswi kuwachagua viongozi kanisani. Kanisa lapaswa kuchagua viongozi wake lenyewe, kama kanisa la Antiokia lilivyofanya.”
Mkoi wako  alisahau  kitu,” Bwana  Hekima  anajibu.  “Kanisa  la Antiokia  lingeweza  taja viongozi,  jinsi  lilivyofanya katika Matendo 13:1-3, kwa sababu lilikuwa kanisa lenye limekomaa na wafanyikazi wengi waliokomaa. Lakini katika Krete makundi wote walikuwa wote wapya na hakukuwa na wafanyikazi wenye ujuzi. Kwa hivyo Paulo akamwambia Tito, mfanyikazi mwenye ujuzi toka nje, kuwataja na kuwaandaa viongozi wapya, katika Tito 1:5. Kwa hivyo Tito alifanywa ovasia wa makutano wapya, jinsi vile mimi nimekuwa nikifanyia kikundi chenu.”
Kwa Mwanafunzi na Msaidizi Bwana Hekima anasema, “Ninyi wawili ni wachungaji viongozi kwa hili kundi jipya. Mwachunge kwa imani, lakini mna Biblia yakuwaongoza na Roho Mtakatifu wa kuwapa nguvu. Mwanafunzi, utaendelea kumfundisha Msaidizi, jinsi nilivyokufundisha. Msaidizi, lazima uwafundishe wengine na uanze makutano wapya. Nitawaandikia ninyi wawili barua na kujaribu kuwatembelea panapowezekana.”
“Tunatumaini itakuwa hivyo.” Mwanafunzi anasema.
“Je, ninyi wawili mko tayari kuliongoza mkutano kwa uaminifu? Je, mtawafundisha kutii amri za Yesu juu ya zote? Je, mtawatumikia watu hawa kwa unyenyekevu na kuwasaidia waumini wapate nafasi za kutumikia mkutano, jinsi 1Petero 5:1-4 inavyo hitaji?
Mwanafunzi na nduguye wanaahidi mbele ya kikundi, “Tutawalea watu wa Mungu kwa uwezo wa Mungu.”
Bwana Hekima anauliza kikundi, “Je, mnaahidi kwa msaada wa Mungu, mtawaombea hawa viongozi na kuwatii wanapofundisha
Neno la Mungu, na kushirikiana katika huduma watakazo wahami kufanya?” Wote wanasema, “Amina!” isipokuwa Bwana Pumbavu.
Bwana Hekima anawawekelea mikono Mwanafunzi na Msaidizi na anaombea upako wa Roho Mtakatifu kama wachungaji, vile
Tito aliwafanyia wachungaji viongozi wa Krete.
Kikundi kinapiga magoti kuomba. Wengine wanalia. Mwanafunzi anajua kwamba sasa yeye na nduguye wana uwezo wa Roho
Mtakatifu kuwaongoza kundi la Mungu.

Kazi ya Kufanya.
•    Kariri Matayo 26:26-28 ili uweze kuongea maneno haya ya Kristo mnapo sherehekea Meza ya Bwana.
•    Fanya Meza ya Bwana mara kwa mara kwa wote wanaokuja kwa mioyo ya toba.
•    Peana maagizo na mamlaka ya kufanya Meza ya Bwana kwa makutano wapya.


II-7—Amri ya Kristo ya 7

Toa

Waumini wanaondoka nyumbani mwa Mwanafunzi baada ya kumuaga Bwana Hekima. Anabaki akiomba na Mwanafunzi. Mtu anabisha mlango. Askari anasema, “Bwana Hekima, nimekuja kukwambia kuwa ni lazima uondoke eneo la utawala wetu mara moja. Ninakufanyia kibali kukuajilia uende bila kukushika, kwa sababu wewe u mtu mzuri. Ondoka sasa au nikutie mbaroni.”
Sara anaujaza mfuko chakula, kumsaidia Bwana Hekima njiani. Anasema, “Wewe ni mkarimu. Ninashukuru. Mwanafunzi, ni lazima uwafunze wengine pia watii Amri ya Yesu ya kutoa, kama vile Luka 6:38 inavyosema. Waeleze kuwa wamepokea kila kitu chenye wangehitaji ili wamfuate Kristo na kurithi uzima wa milele. Jinsi vile Mungu amewapa, lazima wapeane kwa ukarimu kwa wengine.”
“Wengine wao ni maskini sana na hawana fedha.”
“Wanaweza toa bidhaa aina nyingine kusaidia walio na mahitaji na kutumikia mkutano. Mwanafunzi, tumikia wengine vile mimi nimekutumikia  wewe.  Usiwe  kama  viongozi  wa  ulimwengu  wanaopenda  kuwanyanyaza  wanao  waongoza.  Usiwe  na  pupa  ya mamlaka. Yasambaze kwa wachungaji viongozi wapya katika makutano wapya. Tafuta nafasi ya kuwaambia wengine habari njema ya Yesu Kristo.”
“Nitafanya hivyo,” Mwanafunzi anamwakikishia.
“Nitakupa hii kama zawadi.” Bwana Hekima anampa Biblia.
“Tafadhali tuambie hadithi nyingine ya Biblia kabla uondoke. Basi haiji mpaka baada ya lisaa lingine moja.” “Hebu tusome juu ya Mjane Mkarimu.”


Tafadhali tafuta sasa katika Luka 21:1-4:
Zoezi.
•    Je, mjane alipeana kiasi gani cha jumula ya vyote alivyokuwa navyo?
•    Je, Mungu alipima ukubwa wa toleo lake, kulinganisha na matoleo ya matajiri?



22
Hadithi Za Mchungaji

Bwana Hekima anaeleza, “Ona jinsi yule mjane alitoa yote aliyokuwa anahitaji ili aishi, asili mia moja? Ijapokuwa watu wa Agano la Kale waliamurishwa kutoa kwa Mungu asili mia kumi ya vyote waliopata, chini ya Agano Jipya hiyo amri isiwe ndiyo inatumotisia kutoa. Upendo wetu kwa Mungu unatumotisia kutoa vile tunaweza, kama yule mjane. Paulo aliwafunza Wakristo wa Kikorinto kutenga kitu kila juma kwa ajili ya kazi ya Bwana, katika 1 Wakorinto 16:2. Asili mia kumi ya mapato yetu ni mwanzo mzuri.
Mwanafunzi anakubali.
“Mungu anaahidi kuwabariki wale watoao kwa moyo wa furaha na shukrani, katika 2 Wakorinto 9:6-7. Kila kitu tulicho nacho hutoka kwa Mungu. Tunatoa kwa furaha kwa sababu tuna shukrani kwake. Ukarimu wetu unaonyesha kwamba tunaamini kwamba Yeye ni Bwana juu ya vyote tulivyo navyo. Inaonyesha imani yetu katika ahadi yake yakutulea na kutubariki.”
Mwanafunzi anasoma hadithi fupi ya mjane tena. “Mungu aliona ndani ya roho za mjane na matajiri. Aliona kwa nini walikuwa wakitoa. Matajiri walitoa kutoka kwa mabaki yao, kutimiza wajibu au kuwapendeza watu. Mjane alitoa sarafu mbili ndogo, lakini Mungu alijua ni toleo la furaha toka kwa upendo. Alizingatia hilo kuliko matoleo ya matajiri.”
Bwana Hekima anamwambia Mwanafunzi njia zenye watu wengine kwenye Biblia walitumia matoleo yao:
•    kuwasaidia wachungaji viongozi na mitume,
•    kuwasaidia wajane, mayatima, na wengine
•    kuwasaidia walio na njaa
•    Kujenga au kukarabati hekalu la Agano la Kale.
Bwana Hekima anawaaga. Bwana Pumbavu anangoja nje ya mlango na anamwambia, “Ingekuwa busara wewe uwaahidi serekali kuwa utatii, ili wakurusu uishi huku. Mbona unadhuru maisha yako? Imani yako ina faida ndogo sana maishani mwako. Wacha kufundisha juu ya Yesu na upate kazi nzuri sana hapa!”
Bwana Hekima anapiga kite. “Bwana Pumbavu, wewe huelewi tumaini letu lililo barikiwa. Yale tunatoa sasa yanahifadhiwa kwa ajili ya tuzo yetu mbinguni. Tunamngoja Yesu arudi, jinsi tu alivyoenda, vile Matendo 1:9-11 inasema. Atakapo rejea, kila kitu kitabadilishwa. Tutapokea tuzo ya kimbinguni. Bwana Pumbavu, tafadhali tafuta Ufunuo 21 Jinsi Hatima Yetu Katika Yesu Ilivyo.” Bwana Pumbavu anasema tu, “Kwa heri” na anaenda zake, lakini Mwanafunzi anasoma yale Maandiko ya ahadi macho yake yaking’aa kwa furaha.


Tafadhali soma Ufunuo 21:1-9 sasa upate:
•    Mungu anaishi na nani kwenye Ufalme mpya?
•    Je, nini kitatendeka kwa machozi na kifo mbinguni?
Zoezi
•    Nini kitatendeka kwa wale wanaokataa kumwamini Mungu na kuacha maisha yao ya dhambi?
Mwanafunzi anafurahia, “Inasema tutaishi pamoja na Mungu na kuwa na watu wake. Tutakuwa wakamilifu, na atatukaribisha vile mume humkaribisha bibi harusi mrembo! Hakutakuwa tena na kilio, mateso, wala kifo. Kila kitu kitakuwa kipya na cha kupendeza! Bwana Hekima, ikiwa sitakuona tena, nitakuona wakati Mungu ataumba mbingu na nchi mpya.”
Bwana Hekima anasema, “Mwanafunzi, tunangojea ufalme wa ajabu. Kwa hivyo, usiwe na wasi wasi kujirundikia utajiri na ushawishi katika maisha haya. Hivyi si ndivyo vitu mhimu, kwa maana haya maisha yanapita kwa haraka. Mungu akikubariki na fedha, zitumie kuwasaidia wadhaifu na kumtumikia Mungu. Uliona mfano wangu. Sikuwa mzigo kwenu. Kumbuka ni heri kutoa kuliko kupokea, vile Mungu anasema katika Matendo 20:34, 35.”
Mwanafunzi na nduguye Msaidizi wanamtizama Bwana Hekima akiondoka kwa basi, machozi yakilengalenga machoni mwao. “Huenda tusimwone tena.’ Mwanafunzi anaomboleza.

Kazi ya Kufanya:
•    Kariri 2 Wakorinto 9:6-7, juu ya kutoa kile tunacho kwa furaha. Halafu wafunze wafuasi wako.
•    Panga na kundi lako kuweka hesabu ya pesa ambazo watu wanatoa kama sadaka na jinsi zinatumika.
•    Mteuwe mweka hazina na mtu mwingine wakuhesabu hizo pesa.
•    Mwagize mweka hazina kamwe asipeane mkopo au alipie vitu havijaidhinishwa na viongozi wa mkutano.
•    Mchungaji hapaswi kufanya uamuzi wa jinsi pesa zinatumika pekee yake, au kujichukulia pesa mwenyewe.
•    Panga na mwili wa kanisa jinsi ya kutumia sadaka. Toa msaada kwanza kwa watu walio na mahitaji ya dharura.















23
SEHEMU YA III
ENDELEZA HUDUMA ZA MSINGI

Sura katika Sehemu III ni Huduma ambazo Agano Jipya linahitaji. Sahisha zile wewe na wafuasi wako mnatimiza kikamilifu. III-1 Huduma ya 1: Peleka Habari Njema kwa wengine na Kubatiza Waumini Wapya.
III-2 Huduma ya 2: Jenga Mwili wa Kristo Kutumia Vipaji vya Roho Mtakatifu kuhudumiana.
III-3 Huduma ya 3: Abudu Mungu na Kusherehekea Meza ya Bwana.
III-4 Huduma ya 4: Soma, Fundisha na Tumia Neno la Mungu.
III-5 Huduma ya 5: Anza Makutano Wapya.
III-6 Huduma ya 6: Fundisha Wachungaji (Wachungaji Viongozi) na Viongozi Wengine.
III-7 Huduma ya 7: Endeleza Ushirika Ndani na Kati ya Makutano.
III-8 Huduma ya 8: Tembelea na Kuwashauri Watu walio na shida za kibinafsi au kifamilia.
III-9 Huduma ya 9: Weka ndoa na Imani ya Familia Nzima Nguvu
III-10 Huduma ya 10: Lea Wagonjwa, Maskini na wanaoteswa.
III-10 Huduma ya 11: Kua Kama Kristo na udumishe Nidhamu Katika Mwili wa Kanisa.
III-12 Huduma 12: Nena na Mungu.
III-13 Huduma 13: Iweni Watumishi Wema wa Nyenzo za Mungu.
III-14 Huduma ya 14: Tuma Mitume

Jinsi ya Kutumia Sehemu ya III
Sehemu ya III inashughulika na huduma kumi na nne za msingi. Hizi ni huduma ambazo Mungu anahitaji mkutano kufanya, katika Agano Jipya. Kama Mwanafunzi katika Hadithi za Mchungaji, amua ni shida gani au mwanya ambao mkutano wako unapitia.
Halafu tumia orodha ya huduma hapa juu kama menyu kwenye mkahawa. Tafuta huduma ambayo itaongeza nguvu mkutano wako
kwa wakati huu. Endeleza huo huduma katika mkutano wako kwa kufundisha hadithi zilizopendekezwa chini ya huo huduma, na matumizi yake. Halafu saidia mkutano wako kuuweka ukweli wa Mungu kwa vitendo.
Kwenye Sehemu ya Kwanza ya hiki kitabu tulikujulisha kwa mwalimu aitwaye Bwana Hekima. Yeye si mtu kweli, lakini ni kama mtume Paulo katika Biblia. Bwana Yesu Kristo alimpa Paulo kazi ya kuanzisha makutano ya waumini kwa mataifa. Paulo alifanya  uinjilisti,  kuanzisha  makutano  na  kuwachagua  viongozi  kati  yao.  Aliwafundisha  wafanyikazi  kama  Tito  na  Timotheo
kuiendeleza hiyo kazi baada yake. Paulo hakuwahi sahau makutano aliyoanzisha, na aliwatumia nyaraka kuwatia moyo na kuwapa
maagizo. Tuna baina ya hizi barua kwenye Biblia. Pia tuna nyaraka alizoziandika kuwafundisha Tito na Timotheo kwenye Biblia.
Akifuata mfano wa Paulo, Bwana Hekima anamfanyia uinjilisti mtu aitwaye Mwanafunzi pamoja na marafiki na familia zake. Bwana Hekima alisaidia Mwanafunzi, ambaye ni seremala, kuwapanga waumini wapya kwa kikundi. Wakaanza kufuata amri za msingi za Kristo na kutenda vitu ambavyo Mungu anatwambia tufanye kwa ibada. Askari waliwachukia viongozi wa kanisa na
kumlazimu Bwana Hekima kuondoka kwenye hilo eneo. Mwanafunzi hakumwona kwa muda mrefu.
Mwanafunzi alijitolea kumfundisha nduguye, Msaidizi, awe kiongozi kwenye mkutano. Msaidizi alijibu, “Siwezi kusoma. Lakini naweza cheza gitaa na kuimba.”
“Hivi karibuni utajifunza kusoma vyema zaidi pitia haya mafundisho. Nitakupokeza yale nilijifunza kwa Bwana Hekima. Yeye ni kama Mtume Paulo. Anaendelea kuwafundisha viongozi wapya hapa, hata kama yuko mbali sana. Anatutumia mafunzo kupitia nyaraka. Tutatumia Biblia na pia mafunzo tunayoyapokea toka kwa Bwana Hekima. Yana hadithi za Kibiblia ambazo zinafundisha
watu ukweli wa Mungu.”
Hadithi za Mchungaji kina hadithi ambazo Bwana Hekima anatumia. Hii Sehemu ya III inatueleza jinsi Mwanafunzi anapokeza yale alijifunza kwa wafuasi wake na kundi lake. Kwa njia hii, Mwanafunzi anasaidia kikundi kuendeleza huduma ambazo zinatiririka kutoka kwa amri saba za msingi za Yesu. Anamfundisha Msaidizi na viongozi wengine. Msaidizi anaanza kundi jipya. Rafiki wa Mwanafunzi, Bwana Pumbavu, ni mtu wa mauzo ambaye anajaribu kuuza vitu ambavyo watu hawataki. Anajiunga na kundi kuona kama atafaidika nalo. Hayuko hapo kwa ajili ya upendo wa Yesu, na anamshusha Mwanafunzi moyo asiwafanye wafuasi wanaomtii Kristo.


III-1—Huduma ya 1

Peleka Habari Njema Kwa Wengine na Kuwabatiza Waumini Wapya

Msaidizi anaimba sifa kama kawaida, anapomsaidia Mwanafunzi kujenga ngazi kwenye karakana ya useremala. Bwana Pumbavu anawasili na kuuliza, “Mwanafunzi, unaweza kunijengea mkokoteni mwepesi wa miguu miwili wakuonyeshea vitu niuzavyo, kama ule uliomtengezea mukuza mboga? Sitaweza kukulipa sasa hivi, lakini nitauza vitu vingi na nitaweza kukulipa kwa urahisi mwezi ujao.” Mwanafunzi anafikiri kwa dakika halafu anamwambia, “Nenda uniletee magurudumu kukuu mbili ya baisikeli na mbao, na nitakutengezea. Lakini bila malipo. Bwana Hekima alituhadharisha kukopa na kukopesha pesa.”




24
Hadithi Za Mchungaji

Bwana Pumbavu anabaki akimsikiza Msaidizi akiongea juu ya mipango yake. “Ninataka kuanzisha mkutano wengine—kanisa binti ya hili linalokutana nyumbani mwako, Mwanafunzi. Watu wachache ninakoishi wanaweza kutembea mwendo huu mrefu kufika hapa kuabudu.”
Mwanafunzi  anajibu,  “Nimekuwa  nikiombea  hili  litendeke.  Nitawauliza  walio  kwenye  huu  mkutano wetu wanaoishi  huko waende nawe. Ninafikiri kadhaa watakubali.”
“Hapana!” Bwana Pumbavu analalamika, “Hilo litadhaifisha kanisa letu hapa!”
Mwanafunzi anamkosoa, “Bwana Hekima alisema kwamba njia pekee kufikia eneo hili na Habari Njema ya Kristo ni kuanzisha makutano wengi, moja katika kila jamii. Mkutano katika eneo letu usiwe ndio kikundi dogo. Makundi mengi yatafanya kazi kwa karibu na pamoja. Kwa njia hii tutafikia maelefu kwa ajili ya Yesu. Injili itazidi kuenea kama msabibu mkubwa kwa eneo hili lote.”
Bwana Pumbavu anaondoka na Msaidizi anasema, “Niliwaomba waumini wanaoishi karibu nami kunisaidia kufanya uinjilisti. Walisema kwamba hawajui. Wanaogopa. Je, ni jinsi gani ninawezawasaidia washinde uoga wao?”
Mwanafunzi anakumbuka somo ambalo Bwana Hekima alimwachia, kuhusu jinsi ya kupambana na woga. Anasema, “Bwana
Hekima aliniachia masomo yako na wengine tunaowafundisha kuwa viongozi. Moja wapo ya haya masomo ni juu ya watu wangapi kwenye Biblia walimshuhudia Mungu kwa wengine kwa imani na ujasiri. Itakusaidia kuwaeleza wasaidizi wako jinsi ya kuiweka imani yao kwa mazoezi kwa hiyo hiyo. Watapata ugumu wakiongea juu ya Yesu. Hadithi ya Daudi na Goliathi inatoa mfano wa ujasiri.


Tafuta 1 Samweli 17:1-15 jinsi ya kulishinda jitu la uwoga:
Zoezi.
•    Je, kazi nzuri ya Daudi kama mchungaji ilimtayarishaje kupigana na mtu hatari sana?
•    Kwa nini Daudi alikuwa na uhakika atalishinda lile jitu, hata bila silaha za askari?
Mwanafunzi anaeleza huku anatengeneza ngazi, “Wakati Daudi alipokuwa akichunga kondoo, alijifunza kumtumainia Mungu katika hali za hatari. Alitumia muda kumwabudu Mungu na kusoma Neno Lake. Hili lilimtayarisha kumkabili Goliathi bila uwoga. Watu wengi katika Biblia walikuwa washahidi wa Mungu. Sasa, sikia hadithi sawia ya Wanaume Watatu Kwenye Moto.”


Tafuta Danieli 3:
•    Kwa nini waliweza kukabiliana na hatari bila uwoga?
•    Kwa nini mfalme aliamini kwa ukuu wa Mungu?
Zoezi.
Kuhimiza uinjilisti, Msaidizi anaandika wimbo juu ya kuwa mjasiri kama Daudi. Wimbo unaguza mioyo yao na uwoga si kizuizi tena. Siku iliyofuata Msaidizi anamtembelea Mwanafunzi kwenye karakana yake kumuuliza, “Je, Biblia inatupa mifano ya kufanya uinjilisti bora zaidi? Tunahitaji msaada.”
Mwanafunzi anawacha kukata mbao na kudokeza, “Soma Kornelio na Mkutano wa Kwanza wa Mataifa. Utapata miongozo mitatu kwa uinjilisti.”
Mwanafunzi anaeleza Mwongozo wa Kwanza wa Uinjilisti: Jiandae.


Tafuta katika Matendo 10:1-33 yale Msaidizi anavumbua:
Zoezi.
•    Je, Petero alikuwa akifanya nini wakati wale wanaume walikuwa wakisafiri Yopa kumtafuta?
•    Je, Mungu alimwonyeshaje Petero kwamba alipaswa kuwaendea wengine na kukubali njia zao tofauti, badala ya kuwangoja wawe kama yeye?
•    Nani aliyeenda pamoja na Petero na maaskari kule Kaisaria?
•    Nani, kando na Kornelio, mbao Paulo aliwapata wakimngoja huko Kaisaria?
•    Je, Petero alionyeshaje heshima kwa Kornelio kabla hajaanza ujumbe wake wa uinjilisti?
Msaidizi anachukuwa kikwaruso na anamsaidia Mwanafunzi kumaliza kutengeneza meza.
Wanajadili jinsi Petero alivyojiandaa kwa uinjilisti. Mwanafunzi anaeleza, “Alifanya hivyo kwa vitu vifuatavyo:
1)Kuomba.
2) Kusikiza Mwongozo wa Mungu.
•    Wakati wa maombi ya Petero, Mungu alimwonyesha kwamba akubali kila mtu. Badala ya kuwangojea watu wawe kama sisi, tunawapelekea habari njema kwanza.
3) Kuunda kikundi cha utenda kazi.
•    Petero aliwachukuwa wengine akaenda nao badala ya kwenda peke yake.
4) Tafuta wale wanataka kusikia Neno la Mungu kuliko kuendea uma.
•    Alipoingia Kaisaria, Petero alipata marafiki wa Kornelio na jamaa zake nyumbani mwake, wakingoja kusikia Injili.
5. Kuonyesha heshima kwa mtafuta, familia na marafiki zake.
•    Petero aliwaonyesha heshima kwa kuwauliza kwa nini walimuita na kuwasikiza kabla hajaanza kunena. Wakati watu wanaitikia kama Kornelio, tunapaswa kuwasaidia wapeleke habari njema kwa marafiki na familia zao.
Mwanafunzi anaeleza Msaidizi Mwongozo wa Pili wa Uinjilisti: Shuhudia Kristo Jinsi Mitume Walivyofanya, wakifanya kazi kazi pamoja kwenye karakana. “Tunamshuhudia Kristo, jale tumepitia, nay ale ametutendea sisi zote. Umejifunza kusoma vyema zaidi sasa. Tafadhali tazama Matendo ya Mitume 10, mistari 34-43 kupata hili.”

25

Tafuta ujumbe wa Petero katika Matendo 10:34-43
•    Je, ni ushuhuda gani Petero alitoa kumhusu mwenyewe?
Zoezi
•    Vitu gani vitatu vya muhimu ambavyo Petero alisema juu ya Yesu?
•    Je, Yesu aliwaamuru Wafuasi wake wafanye kutokana na ufufuo wake?
Mwanafunzi anaeleza, “Kama Petero, ujumbe wetu wapaswa kueleza kwa maneno mepesi, jinsi Mungu ametubadilisha na kututuma tuwaambie wengine juu Yake. Inatupasa tufafanue uzuri wa Yesu na Nguvu, Kifo na Ufufuo wake. Tunapaswa kuahidi msamaha wa dhambi katika Jina la Yesu.
Mwanafunzi anamwelezea Msaidizi Mwongozo wa Tatu wa Uinjilisti: Wahakikishie Waumini wapya kwa Kuthibitisha
Kukubalika kwao kwa Mungu na kwa Watu wa Mungu.


Tafuta kile kilichotendeka katika Matendo 10:44-48:
Zoezi.
•    Je, ni tukio gani kubwa baada ya ufufuo wa Yesu ambalo Petero alishuhudia, wakati Roho Mtakatifu alishuka ndani ya mioyo ya watu?
•    Je, Petero alifanya nini punde tu baada ya kuthibitisha kazi ya Roho Mtakatifu?
Wanapoendelea kufanya kazi pamoja karakanani, Mwanafunzi anaelezea nduguye Msaidizi, “Petero aliaamuru kikundi kibatizwe punde tu baada ya wao kuamini ujumbe wa Mungu. Alijua kwamba wamekwisha tubu dhambi zao na wamesamehewa, kwa sababu Roho Mtakatifu aliwashukia. Hakungojea kitu kingine bali alithibitisha kazi ya Roho Mtakatifu na ubatizo. Petero alifuata amri ya Yesu ya kuwafanya wafuasi katika Matayo 28:18-20. Alimwambia Kornelio na marafiki zake jinsi ya kupata msamaha wa dhambi katika Yesu. Walipoitikia, aliwabatiza wote mara moja. Tunapaswa kufuata mfano wa Petero, utii mara moja kwa Yesu.”
Msaidizi anaitikia, “Si ajabu tumekuwa wazembe! Kwanza kabisa tuliwaalika tu watu kuhudhuria mikutano yetu, badala ya sisi kuwaendea watu. Tunapaswa kusaidia kila mtu, hasa waumini wapya, kuongea na marafiki na familia zao.”
Mwanafunzi anakumbuka, “Bwana Pumbavu alimwalika mmoja wa wale wahubiri kutoka lile kanisa la mkoi wake kufanya mikutano ya uinjilisti. Alitumia maneno makubwa na ujumbe usioeleweka kwamba watu hawakuelewa. Aliwaomba watu kumtolea sadaka kubwa!”
“Hebu tufanye uinjilisti kama vile Petero alifanya,” Msaidizi anadokeza, “Nitamwomba Mlezi usiku wa leo ikiwa tunaweza
tembelea rafikize pamoja naye tuwaongeleshe juu ya Yesu. Nilisoma katika kijitabu cha masomo ambacho Bwana Hekima aliacha kwamba watu wengine watatukataa. Yesu anasema katika Matayo 10:14 kwamba ikiwa mtu hasikizi, tunamwendea mtu mwengine. Ninataka kupeleka habari njema kwa maeneo mengine kadhaa pia, ambapo jamaa zetu wanaishi. Utanisaidia?”
Mwanafunzi anajibu, Ndio. “Bwana Hekima aliniambia nikufundishe wewe na wengine kuwa viongozi wa makutano wengi na kupeleka Kristo kwa eneo hili lote. Ninahitaji kuwatembelea watu unaofanyia uinjilisti, ili nione kazi yako na nikufundishe jinsi Bwana Hekima alivyonitembelea na kunifundisha mimi. Bwana Hekima alisema tuwe wajasiri kwa Nguvu za Mungu, sio zetu wenyewe.”

Zoezi.
Tafuta kutoka Matendo 6:54 pitia 7:60 jinsi Stefano alivyoleta utukufu kwa Mungu hata kama ujumbe wake ulikataliwa.
Mkewe Mwanafunzi Sara anasikia mlio wa kengele nje ya nyumba. Bwana Pumbavu anasukuma mkokoteni wake, ambao umeufisha kengele kuwaita watu wanunue bidhaa zake. Anamwambia, “Tazama hii mishumaa mirembo. Mwanafunzi yuko?”
Anajibu, “Anafanya kazi.”
Bwana Pumbavu anachukua mshumaa na anasema, “Tazama, una kemikali kwenye nta ifanyayo moto uwake kwa rangi tofauti tofauti. Ni rembo. Hapa hivyi, nitaakisha moja.” Anajisukuma hadi nyumbani na kuakisha mshumaa. Unawaka manjano, halafu nyekundu, halafu samawati, halafu unalipuka kwa kelele na kujaza nyumba kwa moshi wa kusababisha kikohozi.
Msichana jirani, Dibora, anapiga yowe, “Moto!” na anakuja akikimbia kusaidia.
Wanapoacha kukohoa, Dibora anasema kwa furaha, “Nahisi amani na uhakiki tangia Bwana Mwanafunzi anibatize. Yesu yu nami wakati wote.”
“Eti nini?” Bwana Pumbavu anapiga kelele. “Unawezaje batizwa haraka hivyo?” Kwa Sara analalamika, “Huyu ana mototo nje ya ndoa na hata hajui babake ni nani?
Dibora analia kwa kwikwi, “Nimewacha hayo maisha ya dhambi!” Anaanza kuondoka lakini Sara anamshika mkono na kumkalisha kitini.
Bwana Pumbavu anapiga yowe akielekea mlangoni, “Wewe humjui vile namjua. Utaona. Mwanafunzi atasikitika kwamba alimbatiza.” Dibora anatoa ulimi na kumfanyia uso wa kejeli anapoondoka.

Kutii Amri ya Kristo ya Kubatiza
Sara yu tayari kumfariji Dibora. Anakumbuka Hadithi ya Mwanamke aliyekaribia Kuwawa Kwa Kupigwa Mawe ambayo
Mwanafunzi alisema wakati wa maombi.


Tafuta Yohana 8:1-11
Zoezi
•    Kwa nini Mafarisayo walimleta yule mwanamke kwa Yesu?
•    Je, Amri ya Musa ya Agano la Kale iliamuru watu wawafanyeje watu kama hawa?

26
Hadithi Za Mchungaji

•    Je, Mafarisayo walimtendaje huyu mtenda dhambi aliyestahili kifo?
•    Yesu alimtendaje?
•    Nani aliye na haki, tangia Yesu aje, ya kuwahukumu wenye dhambi?
Sara anamwakikishia Diborah, “Rafiki yangu mdogo, je wanadamu wanawezaje kukuhukumu wakati Mungu amekusamehe? Anakupenda! Bwana Pumbavu ametenda kama Farisayo katika hii hadithi. Hawakumjali huyu mwanamke. Walimleta tu kwa Yesu ili wamjaribu. Walimwaibisha mwanamke kwa kumfanya asimame mbele ya umati. Yesu hakumhukumu, ingawa alikuwa mkamilifu na angemtupia mawe. Alimwokoa toka mauti. Amekuokoa toka mauti pia.
“Unaona kabla Yesu aje, Mungu alimpa Musa amri zake zilizowaongoza watu jinsi ya kuishi. Sheria hiyo ilisema usiabudu sanamu, usiue, usidanganye, wala usisini. Tunaipata sheria katika Agano la Kale. Hii Sheria iliwaonyesha watu kwamba Mungu ni mtakatifu na hastahimili dhambi. Watu waliovunja hii sheria walipaswa kuwawa. Yesu ndiye mtu pekee aliyetimiza sheria kikamilifu.
Alipokufa, alimaliza nguvu ya sheria ya kutuhukumu kifo.
“Tulikubatiza wewe kwa sababu ulimwomba Mungu msamaha katika Jina la Yesu, alikuokoa toka mauti na akakupa maisha mapya. Alikupa karama ya Roho Mtakatifu. Tulithibitisha imani yako na ahadi ya Mungu kwa ubatizo. Ulikufa pamoja na Yesu kwa sheria na kwa dhambi zako. Halafu ukafufuka naye katika maisha mapya. Kumbuka msamaha kamili wa Yesu na usitende dhambi tena.”
Mwanafunzi anarudi nyumbani. Sara anamwelezea kile Bwana Pumbavu alimwambia Dibora. Mwanafunzi anamwakikishia, “Jinsi tu walivyo wengi wa watu wajinga, Bwana Pumbavu, anafikiri ni lazima uwe mkamilifu ndipo ubatizwe. Hatungekuwa na mtu yeyote anabatizwa isipokuwa waongo wasemao tu wao ni wakamilifu. Waumini wapya wampokeao Yesu wakiwa watu wazima huwa watoto wapya machoni pa Mungu. Wao hufanya makosa mengi katika utoto wao wa kiroho. Wanahitaji upendo wetu, malezi yetu na kukubalika kwa ubatizo.”

Ubatizo wa Yesu.
Dibora  anawacha  kulia.  Anasema,  “Ninahofu  kuwa  nitatumbukia  dhambini  tena!  Mimi  ni  dhaifu  sana  siwezi  kumtumikia
Mungu.” Sara anamwelezea hadithi ya Ubatizo wa Yesu katika Matayo 3.


Tafuta Matayo Sura 3:
Zoezi
•    Je, Yesu alibatizwa kwa sababu yeye ni mtenda dhambi au alikuwa upande wa watenda dhambi?
Tafuta Matayo 2:
•    Je, ni vitu gani vitatu ambavyo shetani alijaribu Yesu ili avifanye?
Je, shetani alimwahidi Yesu nini ikiwa angemwabudu? (Kumbuka Sura zote mbili za Matayo 3 na 4):
•    Je, Yesu alibatizwa kabla au baada ya kuwaita wafuasi wake na kuanza huduma yake?
Dibora anashangaa, “Yesu hakuwa mwenye dhambi! Alionyesha kila mtu kwamba hakuja kuwahukumu wenye dhambi kama yule mwanamke msinzi kama mimi. Sasa ninafahamu. Hakuwa kama Bwana Pumbavu. Yesu alikuja kuwa upande wetu. Hiyo ndiyo maana ya Ubatizo wa Yesu. Alibatizwa halafu akaanza kazi yake kama mjumbe wa Mungu. Labda nami pia naweza anza kumtumikia Mungu sasa kwa kuwa nimebatizwa, kama vile Yesu alifanya!”
“Ndio, hilo ni kweli kabisa!” Sara anakubali, “Sikiza hadithi ya Wafanyikazi Waliofika Wakiwa Wamechelewa. Utaona jinsi
Mungu hutupa kazi za kufanya punde.”


Tafuta Matayo 20:1-16
Zoezi.
•    Je, mwenye shamba alimwambia mfanyikazi afanye nini, bila kujali ni saa ngapi ya siku?
•    Kwa nini wafanyikazi wa kwanza waliwaonea wivu wale wa mwisho?

Kazi ya Kufanya
•    Tumia hadithi zilizotajwa katika sehemu hii kuwatia moyo watu wako kuwapelekea habari njema familia na marafiki zao.
•    Wasaidie watu wako waandae ushuhuda mwepesi juu ya yale Yesu amewatendea, na waelezee kwa njia nyepesi kuhusu maisha, kifo na ufufuo wa Yesu.
•    Wabatize wote wanaokuja kwa Yesu kwa msamaha wa dhambi punde iwezekanavyo, kuthibitisha toba yao. Wakaribishe katika maisha ya mkutano.
•    Fuata tu matakwa ya Agano Jipya ya Ubatizo. Ni watu wabaya ndio wanaokiri dhambi zao na kutumainia Yesu awasamehe na kuwabadili.
•    Panga mkutano ili Wakristo waliokomaa wawasaidie wale wapya kuelezea familia na marafiki wao kuhusu Yesu.


III-2—Huduma ya 2


Jenga Mwili wa Kristo Ukitumia Karama za Kiroho Kutumikiana



27
Dibora anaongea na Mwanafunzi na mkewe Sara  nyumbani mwao. Anacheka kwa furaha na kusema, “Ninaona maana ya neema! Ninapokea msamaha na ukarimu sawa kama kila muumini kwenye hili kundi la Mungu! Bwana Yesu Kristo ataniruhusu nimtumikie bila kuchelewa! Ninataka kumwonyesha shukrani zangu kwa kumtumikia kwa moyo wangu wote.” Anauchukua mkono wa Sara, “Ninaweza kuanza sasa hivi! Je, ninaweza kukusaidia kazi ya nyumbani ili uwe na wakati wa kutosha  kuandaa hadithi zako za Biblia za watoto?”
Mwanafunzi anaeleza, “Hili linashangaza! Sikujua ni punde hivyo Wakristo wapya wanaweza kumtumikia Mungu. Bwana Hekima aliniambia kuwa kunazo njia nyingi ambazo waumini wapya wanaweza kuwatumikia wengine katika mkutano na jamii. Roho Mtakatifu anampa kazi kila mmoja katika mkutano.”
Dibora anasema, “Tafadhali eleza hili. Je, Roho Mtakatifu anatoaje kazi kwa kila mshirika?”
Mwanafunzi anampa somo la Biblia mbalo liliachwa na Bwana Hekima. Anasoma, “Roho Mtakatifu anafanya angaa vitu vitano katika maisha yetu: kwanza, Roho Mtakatifu anatufanya upya, kama vile Yohana 3:1-8 inatufunulia. Tunazaliwa mara ya pili kwa Roho Mtakatifu. Hata kama miili yetu imekufa katika dhambi, roho zetu zi hai katika Kristo.
Pili, Roho Mtakatifu anatuweka muhuri. Paulo aliandika katika Waefeso 1:12-13 kwamba Roho Mtakatifu ni kama muhuri uliowekwa juu yetu, kutuakikishia ahadi ya Mungu kutuokoa.
Tatu, Roho Mtakatifu anatubatiza kwenye Mwili wa Kristo, jinsi 1 Wakorinto 12:12-13 inatufunulia. Anatufanya tutake kumuishia
Mungu. Nne, Roho Mtakatifu anampa kila mmoja wetu kipawa cha kiroho, kama vile Warumi 12 na 1 Wakorinto 12 inatufunulia. Anampa kila mmoja wetu nguvu za kumfanyia Kristo kazi. Hivi vipawa si kwa manufaa yetu sisi wenyewe, bali ni vya kujenga na kusimamisha mkutano wote. Viongozi wazuri wanamsaidia kila mtu katika mkutano kutumia kipawa chake kutumikia mkutano wote. Tano, anazalisha tunda ndani yetu, Wagalatia 5:22-23. Hata kama Mungu anatusamehe kabisa tunapomjia na tunataka kufanya ya kumpendeza Yeye, Warumi 7 inasema bado tunahitaji kupigana vita ndani mwetu. Yule mtu mpya ndani mwetu anataka kufanya yale yaliyo haki, lakini wakati mwingine, yule mtu wa kale ambaye bado anaishi ndani ya mwili wetu wa kidunia anatusukuma katika dhambi. Hadi tutakapo kufa, tutajitahidi kumfuata Mungu. Roho Mtakatifu anatupa mamlaka na anaongeza nguvu dhamana yake ndani mwetu. Watu wengine hukomaa haraka kiroho lakini wengine huchukua miaka mingi. Tunapomwitikia Mungu kwa imani, tunajifunza kuwa zaidi na zaidi kama Yesu. Tunatazamia wakati ambao tutafufuliwa kwa utukufu na maisha yasiyo na dhambi.”
Dibora anaandika masomo ya Biblia ili adurusu baadaye. Sara anaongezea, “Mungu amekupa vipawa vya kiroho uwatumikie wengine. Kwa mfano, Mwanafunzi ana kipawa cha utawala kama Nehemia. Mimi ni mwalimu kama Ezra. Msaidizi ni mchungaji kama viongozi wa Kiefeso. Anasaidia kuwachunga watu katika mkutano. Wengine katika mkutano ni wafanyikazi wanaotumika kwa karibu sana kama Prisila na Akwila. Hebu nikusomee mifano ya vipawa vya kiroho kwenye Biblia na jinsi watu walivitumia. Tunatumia mifano hii kumhimiza kila mtu apate kazi yake kwenye mkutano.” Sara anasoma orodha ambayo Bwana Hekima aliwaachia, kuwafundisha wengine.

Zoezi. Ukitumia vipawa vya kiroho vilivyotajwa katika Warumi 12:3-8
Ifuatayo ni orodha ya vipawa vya kiroho ambavyo Sara anamwonyesha Dibora. Ikiwa unaweza, weka alama ile kazi Mungu
amekubariki na kipawa chake ili iwe rahisi kuifanya:
   Kutumika kama Samweli katika 1 Samweli 1:20-28
   Unabii kama Yohana Mbatizaji katika Yohana 1:20-28
   Kutoa kama Barnaba katika Matendo 4:36-37
   Kufundisha kama Ezra na Nehemia katika Nehemia 8
   Kuhimiza kama Paulo alivyowafanyia viongozi Waefeso katika Matendo 20:17-38
  Kuongoza kama Musa katika Kutoka 18:13-26 au Nehemia Sura 2-3
   Kuonyesha Huruma kama Daudi katika 1 Samweli 24.

Vipaji vya nyongeza kutoka 1 Wakorinto 12:4-11
   Ongea maneno ya hekima kama Suleimani katika 1 Wafalme 3:5-28
   Ongea kwa akili kama Yakobo aliyedhahatarisha juu ya hatari za ulimi usiodhibitiwa, katika Yakobo 3.
   Kuwa na imani kubwa kama Abrahamu alipoona nyota na kuamini ahadi ya Mungu, katika Mwanzo 15:1-6, au yule mwenye ukoma na akida katika Matayo 8:1-13.
   Kuponya kama Yesu katika Marko 2:1-12 au Petero katika Matendo 3:1-16.
   Kufanya miujiza kama Eliya katika 1 Wafalme 18:16-46.
   Kupambanua maroho kama alivyofanya Paulo katika Matendo 13:6-12.
   Kuongea katika ndimi kama nyumba ya Kornelio katika Matendo 10:44-48.
   Kutafsiri ndimi kama vile Wakorinto waliamurishwa 1 Wakorinto 14:26-28.

Vipaji zaidi kutoka Waefeso 4:11-16
   Enda kwa waliotelekezwa kama Mtume Paulo na Barnaba katika Matendo Sura 13-14
   Tangaza Habari Njema ya Kristo kama mwinjilisti Filipo katika Matendo 8:26-40.
   Mchungaji kama viongozi wa Efeso walivyoagizwa katika Matendo 20:28-34.

Baada ya kupitia hii orodha, Dibora anamsaidia Sara kazi ya nyumbani. Asubuhi iliyofuata Sara anamtembelea Dibora na anamsikiza akimwelezea nduguye kila kitu ambacho alijifunza usiki uliopita, akikumbuka vipaji vya kiroho na mifano ya watu walivyovitumia Kwenye Biblia.

28
Hadithi Za Mchungaji

Dibora anamwambia Sara, “Nilisoma somo lote ulilonipa.”
Wanaongea juu ya vipaji vya kiroho ambavyo Mungu amewapa watu kanisani mwao. Sara anasema, “Nafikiri Bwanangu Mwanafunzi yu na kipaji sawa na Nehemia Mjenzi. Wayahudi walikuwa wamemwacha Mungu. Huyu kiongozi aliwapanga watu wake kuimaliza kazi amabayo wengine walikuwa wamesema haiwezekani. Alikuwa amewaacha washindwe na maadui zao. Jiji lao Yerusalemu, liliharibiwa na wao wakachukuliwa mateka kwa nchi ya kigeni. Baadaye walirudi nyumbani jinsi Mungu alivyoahidi, lakini hawakuujenga ukuta wa Yerusalemu. Ukuta ulikuwa umeanguka kwa karne moja. Nehemia alisikia juu ya haya na akaenda kusaidia. Alikuwa kiongozi wa kweli.”
Dibora anauliza, “Ni vipaji gani vya kiroho nilivyo navyo mimi?”
Sara anajibu, “Ni punde sana kusema kweli, lakini inaonekana unawezakuwa na kipaji cha Samweli cha kuwatumikia wengine. Samweli alichunga hekalu la Mungu kwa hiari. Kama yeye, ulikuwa wa haraka kunisaidia. Na pia inaonekana unaweza kuwa na
kipawa cha kufundisha kama Ezra. Ulimfunza ndugu yako vyema sana. Itakuwa furaha kuu kuona vile Mungu ataendelea kukuza
vipaji vyako vya kutumika.”
Baadaye siku hiyo, Mwanafunzi anarudi nyumbani akiwa na nduguye Msaidizi. Mkewe Sara anawaambia juu ya mjadala waliokuwa nao na Dibora juu ya vipaji vya kiroho. “Nilimwambia uko na kipaji cha uongozi kama Nehemia.”
Mwanafunzi anajibu, “Natumai ni hivyo. Msaidizi, hebu  turudie somo  ambalo  Bwana Hekima  alituachia juu  ya Nehemia kuvumbua dhamana ya kiongozi mzuri.”

Zoezi.
Soma kitabu cha Nehemia upate vitu vifuatavyo (Hili ni zoezi refu, lakini lina dhamana ya kufanywa)
•    Je, Nehemia alihisije juu ya shida za watu wake?
•    Nehemia aliomba nini, juu ya dhambi zake na za watu wake? Tafuta katika Nehemia Sura ya 2:
•    Mungu alifanya nini juu ya ombi la Nehemia akiwa bado anamtumikia mfalme?
•    Nehemia alifanya nini Yerusalemu kabla hajaongea na mtu yeyote kuhusu mpango wake?
•    Nehemaia alifanya nini ndio watu wakaanza kuujenga ukuta?
Tafuta katika Nehemia Sura ya 3:
•    Nehemia aliwapangaje wafanyikazi?
Tafuta Nehemia Sura ya 4:
•    Je, wafanyikazi walipata upinzani upi?
•    Je, Nehemia aliwapangaje hawa watu ndipo wakaushinda upinzani?
•    Je, ni mfano gani mbao Nehemia aliwaonyesha watu wafuate?
Tafuta Nehemia 6:15-17:
•    Kwa njia ngapi ambazo watu waliujenga ukuta?
•    Je, mataifa jirani walisikiaje wakati waliona jinsi Mungu amebariki watu wake?
Tafuta Nehemia 8:1-6 na 9:3
•    Je, nini ambacho viongozi waliwasomea watu, ambacho kilileta ufufuo mkubwa na baraka za Mungu?
Sara anawaletea wanaume kahawa na Msaidizi anamwambia mwalimu wake, Mwanafunzi, “Nimependezwa sana kwamba watu waliujenga ukuta mrefu kwa siku hamsini na mbili pekee baada ya ukuta huo kukaa katika hali ya kuharibika kwa miaka mingi sana. Ninatumainia kuwa kiongozi dhabiti kama Nehemia. Alijali sana shida katika mkutano na jamii yake.”
“Ndio,” Mwanafunzi anajibu, “Nehemia alipoombea mkutano wake na viongozi wa nchi yake, aliombea msamaha wake na wao. Alimwomba Mungu kwa mipango ya hekima ya kuwatumikia watu kwa upendo. Alilinenea kundi lake kwa uaminifu juu ya shida alizoziona na kwa makini, walipanga kukabiliana nazo.” Anamwuliza mkewe Sara kujiunga nao kwa maombi, “Bwana, ninahitaji msaada wako. Ninataka kufuata mfano wa Nehemia kuwapuzia watu wetu wazidi kufanya kazi hata wakiona upinzani. Tunataka kila mtu atumie kipaji chake cha kiroho kuwatumikia wengine.”
Msaidizi anasema, “Nitatunga wimbo juu ya Nehemia, kuwapuzia viongozi wenzangu kufuata mfano wake.”

Kazi ya Kufanya
•    Tumia orodha ya vipaji vya kiroho na mifano ya Kibiblia iliyopo juu kumsaidia kila mtu katika mkutano wako, wakiwemo
Wakristo wapya na watoto, kutumia vipaji vyao vya kiroho kulijenga kanisa.
•    Ongoza kwa unyenyekevu, kama Nehemia, ukikiri dhambi zako mwenyewe kwa Mungu kwanza na kumwomba akupe mipango ya hekima unapowapuzia na kuwapanga mkutano kumfanyia Mungu mambo makuu.











29
III-3—Huduma ya 3

Abudu Mungu na Kusherehekea Meza ya Bwana

Mwanafunzi anafunza nyumbani mwake wakati Bwana Pumbavu na wengine katika mkutano wanaanza kulala. Anawaona vijana wawili wakila kitu wakati wa Meza ya Bwana. Watoto wanatazama huku na huko bila utulivu. Mkewe Sara anamwambia baadaye, “Niliwasikia wengine wakiongea na hawakuwa wakiniona. Walibishana juu ya ni nani watakaye mfuata, Bwana Hekima, Msaidizi ama  wewe.  Mmoja  alimwambia  Bwana Pumbavu.  Mwanarika  alimwambia  mwenzake,  “Hii  inachosha.  Mwanafunzi  kila  mara anafanya kila kitu, na kila siku ni yale yale tu. Ni ibada ya kawaida tu tuifanyayo bila kufikiria. Ndiyo sababu nilibeba kitu cha kula!”
Mwanafunzi anamwandikia Bwana Hekima kumwelezea yale yanaendelea. Bwana Hekima anamtumia Mwanafunzi ujumbe huu kuwasomea makutano, “Ndugu zangu na dada zangu. Ni lazima niwaambie kitu kimoja Paulo aliwaambia Wakorinto katika 1
Wakorinto 11:17-34. Inaonekana wengine wenu wanafanya madhara makubwa wakati mkutanapo. Wengine wenu mnakula wakati wa
ibada ya Komunyo, mbele ya wenzenu walio na njaa. Je, hamna manyumba za kulia na kunywea? Tunatenda dhambi wakati tunasherehekea meza ya Bwana kwa mzaha. Je, mmesahau kuwa Mungu yupo hapo wakati mnaabudu kama mkutano?”


Tafuta 1 Wakorinto 11:17-34:
Zoezi.
•    Je, maneno yapi aliyasema Yesu wakati aliumega mkate usiku alisalitiwa?
•    Je, ni nani tunamtenda dhambi tunapokosa kuheshimu Mwili wa Kristo wakati wa Meza ya Bwana?
•    Je, ni nini tunaangalia sana kabla hatujala Meza ya Bwana ili tusije tukajiletea hukumu juu yetu?
Barua ya Bwana Hekima inaendelea, “Kabla niondoke, niliwafundisha jinsi ya kuabudu. Nilifundisha kwamba Mungu yu nanyi wakati mnakutana pamoja. Tunamwabudu Mungu kwa kila kitu tufanyacho.”
Mwanafunzi anasema, “Ninakumbuka mafundisho ya Bwana Hekima. Tunaabudu kwa maombi na sifa zetu, kwa kufunza Neno, katika Meza ya Bwana kwa kukiri dhambi zetu kwa Mungu, kwa kutoa, na kwa ushirika wetu. Hatufanyi mambo hayo kujitumbuiza.
Mungu anatupa uhuru wa kufanya mambo haya kwa njia mbali mbali. Paulo aliwaambia Waefeso waimbe nyimbo za rohoni na zaburi na nyimbo za kiroho. Nyimbo zaweza kuwa zaburi, maneno yetu wenyewe au nyimbo zilizoandikwa na wengine. Ni za kutoa
ushuhuda wa kazi kubwa ya Mungu na kumshukuru. Pia ni za kutukuza ukuu wa Mungu na kumwabudu Yeye.”
Msaidizi anaongezea, “Bwana Hekima pia alitufunza jinsi katika Agano la Kale watu wa Mungu walimwabudu kwa njia za maalum wakati wa sherehe. Sherehe za Pasaka zilidumu siku saba kukiwa na sadaka maalum na makusanyiko maalum siku ya kwanza na ya mwisho. Suleimani alipojenga hekalu la Mungu, umati ulikuja Yerusalemu kusherehekea. Walikula pamoja na waliishi kwa vibanda. Walisimama kuwasikiliza wana muziki wakiimba na kucheza tarumpeta na vyombo vingine vya muziki. Mfalme Suleimani aliomba ombi maalum kwa ajili yao, akisimama halafu akipiga magoti. Maombi yetu ni kama manukato yanukiayo vizuri kwenye uwepo wa Mungu.”
Mwanafunzi anasoma tena kutoka kwenye hiyo barua, “Hapa kuna vitu ambavyo viongozi wenu wanaweza kufanya ili ibada yenu kwa Mungu iwe nzuri zaidi kama manukato mbele Yake:
•    Omba kwa kujiandaa.
•    Waulize watu kabla ya ibada wakusaidie kwa vipindi mbali mbali vya kuabudu.
•    Msaidie kila mmoja apange sehemu yake kwa makini kabla ya ibada.
•    Panga ili kila mtu, wakiwemo watoto, kushiriki kwa njia mbalimbali.
•    Fanya sherehe kusherehekea matukio maalum, kama Kuzaliwa kwa Yesu, Kifo na Ufufuo wake.
Wanajadili mambo haya kwa dakika chache, halafu Mwanafunzi anaendelea kusoma barua: “Jinsi vile mwandishi wa Waebrania anavyosema, ‘Zamani Mungu alinena na babu zetu kupitia kwa manabii. Lakini katika siku hizi za mwisho, amenena kupitia kwa Mwanaye Yesu, anaonyesha utukufu wa Mungu, na kila kitu kinachomhusu Yesu kinaonyesha utukufu wa Mungu kikamilifu. Baada yake kufa ili atutakase toka dhambini, aliketi mahali pa heshima kwa mkono wa kuume wa Mungu mbinguni. Tunapomwabudu Mungu, tunamheshimu Yesu kwa kuomba kwa Jina lake, kufunza Neno lake na kutangaza kifo chake wakati wa Meza ya Bwana. Tunashughulikia hoja za Mwili wake, mkutano, kwa kutoa na ushirika.”
Kadhaa wanasema, “Ameni!” na Mwanafunzi anamalizia hiyo barua.
Tunapokutana kumwabudu Mungu pamoja na kula Meza ya Bwana, tunashiriki mwili na damu ya Kristo. Mnatangaza kifo Chake. Mnaingia katika uwepo wa Mungu wenyewe. Kama hamtambui hili, mnaudharau mwili na damu ya Kristo. Agano la Kale linatuonyesha jinsi damu iliyomwagika ya Kristo ilivyo ya muhimu.”
Mwanafunzi anasema, “Msaidizi, tafadhali tuambie hadithi ya Pasaka ambayo tulisoma pamoja, jinsi ya kuingia kwenye uwepo wa Mungu.”

Zoezi.
Tafuta katika Kutoka 12:21-42 jinsi Mungu alivyowaachilia watu wake toka utumwani Misri:
•    Nani alieyekufa usiku wa manane?
•    Nini kiliwaokoa Waisraeli wasipoteze wazaliwa wao wa kwanza?
•    Nini kilifanyika baada ya wazaliwa wa kwanza wa Wamisri kufa, kuwaweka mateka Waisraeli huru?
•    Waisraeli walikuwa wakumbukeje kwa uzao zote huu ukombozi mkuu toka utumwani?


30
Hadithi Za Mchungaji

Baada ya mkutano, Mwanafunzi na nduguye Msaidizi wanadurusu masomo ya Biblia ambayo Bwana Hekima aliwaorodheshia, juu ya madhabahu na ibada katika Agano la Kale. Mwanafunzi anamwuliza Msaidizi, “Tafadhali funza haya juma lijalo.”
Wakati Msaidizi anapofunza kila mtu anatega sikio kwa makini. Anaimba wimbo aliotunga kwa ajili ya ibada juu ya damu ya kondoo wa Pasaka ambayo imepakwa pande mbili za kila mlango. Anaelezea, “Katika Agano la Kale, Wayahudi waliompenda Mungu walisherehekea Pasaka kila mwaka. Walikumbuka jinsi Mungu alitumia damu na vifo vya wazaliwa wa kwanza kuwaweka
huru. Huo ulikuwa mfano kutuonyesha sisi jinsi Mwana wa Mungu atatukomboa toka utumwa wa dhambi kwa damu yake. Hili
linaelezewa katika Nakala ya Duniani ya Madhabahu ya Mbinguni katika Waebrania.”


Soma Waebrania 9:1-26 kupata yale Msaidizi alifundisha:
Zoezi.
•    Ni vitu gani vilivyokuwa kwenye sehemu ya kwanza ya nje ya madhabahu?
•    Vitu gani vilikuwa sehemu ya ndani na takatifu zaidi ya madhabahu?
•    Kuhani mkuu alifanya nini mara moja kwa mwaka kufunika dhambi zake na zile za watu wake?
•        Mwana wa Mungu alitunyakuliaje wokovu wa milele? “Msaidizi anawauliza watu, “Je, mna maswali?”
Mmoja anauliza, “Je, ilikuwaje kuabudu katika Agano la Kale?”
“Bwana  Hekima  alieleza  hili.  Nyakati  za  kale,  watu  walichukuwa  mwana kondoo  au  ng’ombe  dume  wakienda  kuabudu. Waliwekelea mikono yao juu yake kukiri dhambi zao; kuhani alikata koo ya yule mnyama. Ilikuwa kazi chafu. Damu hiyo ya sadaka ilitabiri kifo cha Yesu, ambaye damu yake alitakasa mara moja na milele, dhambi za ulimwengu mzima. Mwanafunzi, waweza
nisaidia kueleza hili?”
Mwanafunzi  anaongezea,  “Pahali  Patakatifu  pa  Hekalu  kinara  cha  taa,  meza  na  mkate  mtakatifu.  Nyuma  ya  pasia  katika Patakatifu pa Patakatifu kulikuweko na uvumba na Sanduku la Agano. Kuhani Mkuu aliingia mara moja mwakani na damu kufunika dhambi zake. Kristo alipokufa, hilo pasia lilipasuka wazi, na Yesu akaingia uwepo wa Mungu kama Kuhani wetu Mkuu. Damu yake inatuondelea dhambi na kutuokoa mara moja na daima. Sasa tu huru kuingia kwenye uwepo wa Mungu, Patakatifu pa Patakatifu, na tunatoa maombi yetu kama uvumba Kwake. Tu kwenye uwepo wa Kristo tunapomega mkate mtakatifu kwenye Meza ya Bwana. Yu nasi tunapokunywa kikombe cha agano jipya ndani ya damu yake. Aliahidi kuwa wawili au watatu wakusanyikapo kwa Jina lake, Yupo kati yao.”
Mlezi anasema, “Ninaelewa sasa kwamba sikuwa nimetambua mwili wa Kristo wakati tulikula Meza ya Bwana. Nilikuwa nimesahau kwamba tunaingia kwenye uwepo wa Mungu tunapoabudu pamoja. Nafikiri sisi zote tunahitaji kurekebisha nia yetu ya kuabudu.”
Mwanafunzi anatoa maoni, “Paulo pia anafafanua wazi wazi katika 1 Wakorinto sura 12-14 kwamba kiongozi mmoja asifanye
kila kitu. Wengi wanaotaka wanapaswa kuchukua nafasi zao katika ibada. Toka sasa na kwendelea, nitashiriki majukumu yangu ya uongozi na wengine. Nitawasaidia nyote mnaotaka kushiriki zaidi kufanya hivyo. Tutakua zaidi na mkutano watapata viongozi wapya wanaoweza anza makutano wapya.”
Mwanafunzi anamgeukia Msaidizi, “Nahitaji msaada wako. Tafadhali nisaidie siku za usoni kuandaa watu wetu vizuri zaidi kwa ajili ya Meza ya Bwana. Na ninahitaji msaada wenu nyote, kurekebisha sehemu tofauti tofauti za ibada yetu na huduma zetu zingine. Tutamheshimu Kristo kwa kuendeleza hizi huduma. Msaidizi, nataka wewe utusaidie kwa muziki.” Mwanafunzi anawapa kazi watu wengine pia, ili kuanzia hapo na kwendelea, asiwe tu yeye ndiye wakuongoza ibada.
Baada ya ibada Mwanafunzi anamwambia Msaidizi, “Nitafuata haya maagizo kwa mikutano yetu. Ninatambua sasa kwamba nilikuwa  mzembe.  Jinsi  Paulo  alivyosema  katika  1  Wakorinto  11,  Mungu  aliwaadhibu  vikali  sana  Wakorinto  walioshindwa kuheshimu Mwili wa Kristo wakati wa kusherehekea Meza ya Bwana. Walikosa kukumbuka sadaka ya uchungu aliyoitoa Yesu. Walikosa kuona kuwa wakati tunapokutana pamoja sisi ni Mwili wa Kristo. Mungu anaichukulia siri hii kwa uzito. Ndivyo impasavyo kila muumini katika mkutano wetu. Ndio sababu Paulo alituonya tusifanye Meza ya Bwana iwe kama chakula cha kawaida, kwa maana watu wana tabia ya kupenda chakula zaidi ya kushiriki mwili na damu ya Kristo, jinsi 1 Wakorinto 10:16-17 inavyosema.”

Kazi ya Kufanya
•    Waulize walio na vipawa vya muziki na vipaji vya kufundisha au kutoa maneno ya hekima kushiriki kwa kuongoza sehemu tofauti tofauti ya ibada.
•    Wahimize watu kuonyesha upendo wao kwa Mungu kwa njia na ubunifu mpya. Wahimize wale walio na vipawa vya muziki kutunga nyimbo za sifa kwa Mungu, kutumia mtindo wa muziki wa kwao.
•    Tumia hadithi katika sehemu hii kufunza kwanza Mungu yuko pamoja nasi tunapokusanyika kumwabudu.
•    Panga ili kila mtu ashiriki kwa ibada kwa njia zote, kando na kuimba, wakiwemo watoto.
•    Wasaidie watu wanaoongoza sehemu mbalimbali za ibada kujiandaa mapema.


III-4—Huduma ya 4

Soma, Fundisha na Tumia Neno la Mungu

Mwanafunzi anamtembelea nduguye Msaidizi, anayeishi kilomita chache kutoka nyumbani kwa Mwanafunzi, kumshauri na

31
kuona vile kazi yake inaendelea. Mlezi, mwalimu wa shuleni, anaishi karibu na Msaidizi na anahudhuria kipindi cha ushauri. Mwanzoni aliudhuria mkutano wa Mwanafunzi lakini sasa anakutana na kundi jipya la Msaidizi, karibu na kwenye anaishi.
Baada ya maombi, Msaidizi anaelezea mipango yake. “Mwanafunzi, umenihimiza kuanza mkutano wapya hapa na wafuasi wa Kristo. Ninahitaji usaidizi wako. Nimechanganyikiwa juu ya sheria tofauti tofuati ambazo watu wananiambia ni lazima mkutano wapya wafuate.”
Mlezi  anaongeza,  “Mimi  pia  nimechanganyikiwa.  Shemeji  yangu  Bwana  Pumbavu  anataka  kuja  kuliongoza  hili  kundi  jipya.
Anasisitiza kuwa Msaidizi ni mchanga sana na ni lazima atumie miaka kadhaa kwenye chuo cha Biblia kabla aweze kuwa mchungaji. Anasema mtume Paulo alisomea Biblia kwenye chuo cha biblia katika Yerusalem. Amemwambia karibu kila mtu kwenye kundi letu. Wengine pia wanasema ni lazima tufanye mambo kwa njia tofauti. Wengine wanataka tutumie mishumaa katika ibada zetu. Kila mtu anataka kuuambia mkutano wetu wapya kitu cha kufanya!”
Mwanafunzi anawahakikishia, “Mtiini tu Yesu juu ya wengine wote. Huo ndio msingi wa mkutano wapya. Iwapo hautaweka mamlaka yake kwa amri za Kristo, Shetani ataingilia na kujaza hiyo nafasi, na kila wakati utakuwa na huku kuchanganyikiwa. Kumbuka viwango vitatu vya mamlaka:
•    Kwanza fanya yale Kristo na Mitume wake waliamuru, mbele ya yote.
•    Pili, una uhuru wakufanya vitu vingine ambavyo mitume walifanya lakini hawakuamuru, lakini usilazimu makutano wote kuvifanya kwa sababu ni Mungu tu anayeweza tengeza sheria kwa kanisa nzima duniani.
•        Tatu, angalia desturi yoyote ya kibinadamu kuhakikisha kwamba unajenga mkutano wako wapya na hauzui utii kwa Yesu.” Mlezi anauliza, “Gani kwa hivi viwango vitatu vya mamlaka kinalingana na kuhudhuria masomo kwenye chuo cha biblia?” Mwanafunzi anarudisha hilo swali, “Wewe unafikiriaje?”
Mlezi anatulia kwa muda mfupi, halafu anatoa sababu, “Kristo hakuwahi tuamuru tuhitimu kutoka katika chuo cha masomo. Mitume hawakuwatuma wachungaji waliowateuwa kwa mafundisho kwenye shule kando na mwili wa kanisa. Kwa hivyo hili liko kwa kiwango cha tatu cha mamlaka, yaani tamaduni za binadamu, kiwango cha chini zaidi.”
“Sawa. Hili halimaanishi mafundisho ya chuoni ni mabaya, lakini ni lazima hatuwezi kuyalazimisha mahala pa njia ambazo
Biblia inatufunulia tutumie. Una uhuru wa kuchagua njia ambayo imfaayo ninyi hapa. Chuo cha kielimu kando na makanisa kina faida zake chini ya hali fulani, kwenye makanisa yenye nguvu na kuna wachungaji wakutosha waliosoma. Lakini hakiwezi kuendeleza msukumo mpya kama huu wetu.”
Mlezi anauliza, “Kwa ipi kati ya hivi viwango vitatu vya mamlaka tunawapa wanafunzi wapya viongozi kama vile Paulo alifanya?”
Mwanafunzi anajibu, “Bwana wetu Yesu Kristo na mitume waliwashauri wanafunzi wao, lakini hawakuamuru hili. Kwa hivyo kuwashauri viongozi wapya ni kiwango cha pili, tendo la kiutume la chaguo. Ninapendelea kumfundisha Msaidizi kwa njia ile Bwana
Hekima amekuwa akinifundisha mimi. Tunajaribu kufanya kwa njia ambayo Yesu na Paulo waliwafundisha  viongozi wapya. Bwana
Hekima alisema kwamba anamwiiga mtume Paulo, ambaye aliwafundisha wachungaji wapya wengi. Mmoja wa hawa wachungaji wapya ambao Paulo alikwenda naye akimfunza alikuwa mtu mchanga kwa umri lakini amekomaa kiroho aitwaye Timotheo. Baadaye, wakati Paulo alikuwa akisafiri kuanzisha makutano wapya kwenye nchi zingine—au kuketi gerezani Roma—aliandika nyaraka kwa Timotheo kumhimiza na kuelezea jinsi ya kuwa mchungaji mwema. Alimwambia awafundishe wengine ambao wangewafundisha wengine, kwa msururu wa athiria ya uzalishaji.”


“Naona kile unamaanisha na msururu wa uzalishaji,” Mlezi anasema. “Bwana Hekima alimfundisha Mwanafunzi na wengine. Mwanafunzi anakufundisha wewe, Msaidizi. Wewe unafundisha viongozi wengine sisi tunapofanyakazi kwenye makutano wapya. Nataka unionyeshe jinsi ya kutumia Biblia kama Bwana Hekima unavyofanya. Halafu sisi zote tutafuata mfano wa mtume Paulo.’
“Vyema,” Mwanafunzi anasema, “Msaidizi, unaweza msaidia Mlezi kutafuta Kile Paulo Alimwandikia Timotheo Juu ya
Kutumia Biblia?”



32
Hadithi Za Mchungaji

Zoezi.
Tafuta 2 Timotheo 3:10 pitia 4:5 kile Msaidizi alimsaidia Mlezi kuvumbua:
•    Ni majukumu yapi Paulo alimpa yule mchungaji mchanga Timotheo?
•    Je, tunajuaje kwamba tunawezaiamini Biblia kama Neno la Mungu?
•    Kwa njia gani tunaweza tumia Biblia kuwasaidia wengine?
•    Kwa njia zipi Paulo alimfunza Timotheo kwa matendo na kwa maneno yake?
•    Ni nini Mungu alitupa, ili tuweze kuwafunza wengine kwa uhakika juu ya wokovu kwa imani katika Yesu?
Wakati Mwanafunzi anasikiza, Msaidizi anamwelezea Mlezi, “Paulo alimwambia Timotheo kutumia Maandiko kufundisha, kukemea, kukosoa, na kufundisha kuishi sawa.  Mwanafunzi alinifunza kuwa Maandiko yanapuliziwa na Mungu. Yanabeba mamlaka ya Mungu na yanafunza ukweli wake. Tunapotii Maandiko katika kila kitu yatufundishacho, tunamtii Mungu. Roho Mtakatifu
anatuongoza tunaposoma na kutii Biblia. Anatusaidia kuwa wafuasi watiifu wa Kristo.”
Msaidizi anamwangalia Mwanafunzi, anayesema, “Unafunza sawa, jinsi vile Bwana Hekima alinifundisha mimi nami nikakufundisha wewe. Endelea tafadhali.”
“Paulo alimfundisha Timotheo si tu kwa Neno la Mungu, bali pia kwa mfano. Wanaume hawa wawili walikuwa na uhusiano thabiti. Timotheo aliona njia Paulo alioishi, imani yake na mateso yake. Paulo alimwambia Timotheo aige maneno na matendo yake. Hakukosea kutimiza kila mpango wa kazi ya Mungu maishani mwake. Yesu na Paulo waliteswa kwa sababu ya utii wao kwa  Neno la
Mungu. Shetani alimpinga Yesu kwa kila njia iwezekanayo.”
Mlezi anauliza, “Shetani alimpingaje Yesu?”
Mwanafunzi anamwuuliza Msaidizi kueleza hilo. Msaidizi anasema, “Hebu turudie Majaribu Makubwa ya Yesu toka Kwa
Shetani.”


Tafuta Matayo 4:1-11:
•    Je, ni kwa njia gani tatu ambazo Shetani alimjaribu Yesu?
Zoezi.
•    Je, Yesu alinukuu nini, kumjibu Shetani baada ya kila jaribio? Ni nani alikuja kumtumikia Yesu baada ya majaribio?
Msaidizi  anaeleza,  “Shetani  alitaka  Yesu awache  kumtumaini  Mungu  na  Neno  lake.  Yesu  alijibu  majaribu  ya  Shetani  na Maandiko kila wakati. Yesu alitii Neno la Mungu kuliko afuate maneno ya Shetani. Kukabili majaribu ni ngumu. Yesu alishinda jaribu lake gumu kwa kufuata Neno la Mungu kwa uaminifu. Halafu malaika wakaja kumhudumia.”

Jinsi ya Kusoma Maandiko
Mlezi anamwambia Msaidizi, “Unaita Biblia Neno la Mungu. Unamaanishaje ukisema hivyo?”
Msaidizi anaelezea yale Mwanafunzi amemfundisha. “Biblia ni mkusanyiko wa vitabu 66 vilivoandikwa na watu chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu. Hivi vitabu vinahuzisha sheria za kale, historia, ushairi, unabii, maisha ya Yesu, na nyaraka kwa makutano wapya. Maudhui ya Biblia nzima ni Yesu Kristo. Yohana 3:16 inafupisha ujumbe wa Biblia: ‘Mungu aliupenda ulimwengu jinsi hii hata akamtoa mwanawe pekee ili kila mtu amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele.”
“Nilifikiri Biblia ni vitabu viwili, Agano la Kale na Agano Jipya.”
“Biblia imegawanyishwa katika sehemu mbili,” Msaidizi anaelezea aliyojifunza juma lililopita toka kwa Mwanafunzi. “Agano la Kale linajishughulisha na mwaafaka wa Mungu na Israeli ya kale kuwabariki ikiwa watatii sheria zake na kuwaadhibu ikiwa watakosa kutii. Yesu alipokufa, alitimiza kikamilifu sheria ya zamani na akatuweka huru toka sheria yake ya mauti. Sasa hatufuati sheria za Agano la Kale, kama vile kupigwa mawe ikiwa utafanya kazi siku ya saba, Jumamosi. Agano Jipya linajishughulisha na mwaafaka mpya wa Mungu na wanadamu, kutuokoa kupitia imani katika Yesu Kristo. Linatufundisha kumtumikia Yesu kwa upendo. Tunasoma Agano la Kale kwa makini kwa sababu linatoa mifano ya nguvu ya tabia za Mungu na kazi ya Kristo, kwa njia iliyo rahisi kuelewa.”
“Agano Jipya linatueleza jinsi ya kuwa wafuasi wa Yesu Kristo. Inahusisha:
Injili inaelezea maisha, kifo na ufufuo wa Yesu Kristo. Vinalinganishwa na vitabu vya sheria, vitabu vitano vya kwanza vya Agano la
Kale,
Matendo ya Mitume kinatuelezea jinsi mitume walianza makutano katika nguvu za Roho Mtakatifu baada ya Yesu kupaa mbinguni. Kinalinganishwa na vitabu vya kihistoria vya Agano la Kale ambavyo vinahusiana na safari za waamuzi na wafalme wa Israeli, Nyaraka mbazo mitume na watendakazi-wenza waliandika kusaidia makutano wapya na waumini vinalinganishwa na maandishi ya kishairi ya Agano la Kale kama kitabu cha Methali na Zaburi.
Kitabu cha Ufunuo chenye kimeandikwa na mtume Yohana kinatabiri yajayo siku za usoni na kinalinganishwa na vitabu vya manabii wa mwisho katika Agano la Kale kama Yoeli, Danieli na Ezekieli.”
Mlezi anauliza, “Ni njia gani bora zaidi ya kujifunza Biblia?”
Msaidizi anamtizama Mwanafunzi lakini tena anamwambia ajibu, “Ni mwanafunzi wako, Msaidizi. Umejifunza vitu hivi. Unapswa kuvifundisha.”
Msaidizi anamwelezea Mlezi, “Unaposoma Biblia, anza kwa maombi. Halafu durusu kitabu cha biblia, au soma kichwa kama
maombi au imani. Unaweza chukua siku nyingi utakavyo hadi umalize. Usilenge mstari mmoja tu kwa sababu unaweza kosa kuielewa. Badala yake, usome pamoja na kifungu chote. Soma yale yanautangulia na yale yanaufuata ule mstari unaojaribu kusoma ili uelewe muktadha wake. Ikiwa hautaelewa hicho kifungu, soma sura. Ikiwa hutaelewa sura hiyo, soma kitabu chote.”
“Je, muktadha ni nini?”


33
“Muktadha ni historia ya wapi na nini kinachoendelea,” Msaidizi anasema, “Yale yamezungumziwa au kuandikwa, na yale yanayofuata. Tunatafuta muktadha kujua nani alisema au aliandika, kwa nani au kwa nini. Je uko kwenye sura inayofafanua maono ya kimafumbo, au uko katika mseto wa kihistoria ambao tunautafsiri kwa maana ya kawaida? Ni Shetani anaongea, au mtu mbaya? Kama ni hivyo, hatuamini wala hatufanyi yale wanasema.”
“Itakuwaje ikiwa unasoma muktadha jinsi unasema lakini bado hauelewi kitu?”
“Usiwafundishe wengine kitu chochote usichokifahamu,” Msaidizi anajibu. “Anza kufundisha kutoka Agano Jipya. Baadaye, soma Biblia nzima. Kusoma Biblia haina faida yoyote ikiwa hatutii yale inafundisha. Mwombe Mungu akusaidie utende yale unajifunza.”
“Unaposoma fungu la Biblia, utalielewa vyema ikiwa utatafuta:
•    Nani aliyekiandika kitabu hiki na kiliandikiwa nani?
•    Lini na wapi matukio kwenye kifungu yalitetendeka?
•    Nani anasema kwa hiki kifungu?
•    Kifungu hiki kinatuandaa kufanya nini?

    Jinsi ya kufundisha Maandiko na Kuwafanya Wafuasi wa Kristo.
Msaidizi anashangaa, “Ninakwenda kutunga wimbo juu ya jinsi ilivyo ajabu na kurotubisha kujifunza Neno la Mungu. Je, wimbo huu utasisitiza nini?”
Mlezi anadokeza, “Unaweza taja kuwa tunapotumia Maandiko katika nguvu za Roho Mtakatifu, anabadili maisha yetu.” Mwanafunzi anaongezea, “Tunaweza imba juu ya Mfalme Mwema Yosia na Ufufuo. Alisoma na kutii Neno la Mungu na akaleta
ufufuo kwa watu wake.”


Tafuta 2 Mambo Ya Nyakati 34:1-13:
•    Ni nia ipi Mfalme Yosia alikua nayo kwa Mungu?
•    Ni vitu gani Yosia alifanya kumtafuta Mungu? Tafuta katika 2 Mambo ya Nyakati 14-21:
Zoezi.
•          Kwa nini Mfalme Yosia alishtuka, na kwa nini alitubu moyoni kwa yale alitenda?
Tafuta 2 Mambo Ya Nyakati 34:22-33:
•    Toba ya Mfalme Yosia na kutii kwake Neno la Mungu vilisababisha nini?
Mlezi anamwambia Mwanafunzi, wanapoongea nyumbani Mwa Msaidizi, “Ninataka kuhubiri Neno la Mungu kama wewe. Je, unaweza nieleza namna ya kuandaa ujumbe mzuri?”
Mwanafunzi anamwelezea Mlezi na Msaidizi yale Bwana Hekima amemfunza, “Unapojiandaa kuhubiri, fanya hizi hatua za msingi. Panga, Soma, Fafanua, na Tekeleza.”
•    Panga Ujumbe wako: Omba mwongozo wa Mungu. Fikiria ni ukweli gani hasa mkutano wako unahitaji kusikia. Je, kuna huduma yeyote inayohitaji kuinuliwa? Ni sehemu gani ya Biblia itainua upendo wa mkutano wako kwa huduma ya Kristo?
•    Soma Maandiko: Tafuta kwenye Biblia inafunza chenye watu wako wanahitaji. Tafuta kitabu cha Biblia au fungu fupi, au lengo. Lengo ni mada, kichwa kinachoshughulika na ukweli unaopanga kufundisha. Waweza soma kichwa au kitabu kimoja kwa majuma kadhaa kabla hujakifundisha. Andika vipengee muhimu unavyopata. Tafuta njia ya vitendo vya kweli ya kutekeleza haya mafundisho maishani mwenu.
•    Fafanua Neno la Mungu: Tanguliza ujumbe wako na mfano au swali linalowakilisha kusudi lako kwa wazi. Fafanua vile vipengee muhimu ulivyoandika uliposoma kifungu. Toa mifano au hadithi toka kwa Maandiko au maishani mwako kuwasaidia watu watekeleze mafundisho maishani mwao.
•    Tekeleza Neno la Mungu: Waambie watu jinsi hiki kifungu kinatekelezwa moja kwa moja maishani mwao. Kutamatisha, wahimize kutekeleza mara moja yale wameyasikia.”
Msaidizi anauliza Mwanafunzi, “Utahubiria kundi letu jipya usiku wa leo?”
Mwanafunzi anasema, “La, asante. Lakini nitakusaidia kuuandaa ujumbe kwa mkutano juu ya mamlaka ya Maandiko. Hebu tutazame 2 Timotheo 3:16, 17 tena. Unaweza jumuisha hadithi juu ya majaribu ya Yesu na ufufuo wa Mfalme Yosia kama mifano.
Jioni hiyo Msaidizi alihamanika akiwafundisha watu wake ule ujumbe. Anawakumbusha viwango vitatu vya mamlaka kwa yale tunafanya. “Kiwango cha Kwanza ni amri za Agano Jipya. Kiwango cha pili ni matendo ya Agano Jipya mbayo hayakuamurishwa.
Kiwango cha tatu ni tamaduni za kibinadamu.” Anafafanua viwango hiyi vitatu vyema.
Baada ya kumaliza, Msaidizi anaongezea, “Wengine wetu walinitaka niende kwa chuo cha Biblia kwa miaka michache. Naona sasa hii si amri ya Yesu wala tendo la kitume. Ni utamaduni wa kawaida wa kuwafundisha wachungaji. Ninapanga kuendelea kujifunza Neno la Mungu kutoka kwa Mwanafunzi kwa maana ananisaidia kutekeleza Neno la Mungu vizuri sana kwenu, watu wangu. Kila baada ya wiki mbili Mwanafunzi hukutana nami na kunionyesha jinsi ya kutekeleza zaidi na zaidi ya Maandiko kwa maisha ya mkutano.”
Mlezi anaitikia, “Mwanafunzi, tunashukuru kuwa unatusaidia kufuata Neno la Mungu, kwa kumshauri Msaidizi.”

Kazi ya Kufanya
•    Tumia hadithi kwenye sehemu hii kufundisha kundi lako mamlaka ya Maandiko.
•    Saidia mkutano wako kukariri vitabu vya Biblia na aina ya maandiko yaliyomo kwenye kila kitabu, kama vile ushairi, historia, nyaraka au unabii.

34
Hadithi Za Mchungaji

•    Saidia mkutano wako utofautishe viwango vitatu vya mamlaka kwa ajili ya kazi zao.
•    Andaa ujumbe wako kwa kufuata hatua nne za msingi: Panga, Soma, Fafanua na Tekeleza.
•    Wasaidie wengine katika mkutano wako pia waandae jumbe ambazo zinainua upendo na huduma wa Yesu Kristo.

III-5—Huduma ya 5

Anzisha Makutano Wapya

Baada ya ibada kwa nyumba ya Mwanafunzi, Bwana Pumbavu, na wanawake wawili wakisimama naye, wanamwambia Mwanafunzi, “Ni lazima tuongee nawe. Tumeamua kuwa Mwanafunzi wako, Msaidizi asianzishe kanisa lingine. Watu kadhaa wameacha kanisa letu kuhudhuria hilo. Limedhaifisha kanisa letu. Lazima uwaambie watu katika kundi la Msaidizi warudi huku. Wanasababisha mkawanyiko. Msaidizi anapaswa kuwa akifanya kazi na wewe hapa akitutumikia.”
“Ninaelewa shida yako,” Mwanafunzi anajibu, “Lakini ndugu yangu, Msaidizi, anafanya yale Bwana Hekima na mimi tulimwamuru kufanya. Anawatembelea jamii wake wengi wa Mkewe Recho, ambao wanaishi eneo hilo. Wanaitikia Injili. Sitaki waje hapa. Hilo litapunguza ukuaji wa ufalme wa Mungu. Wacha ufalme wa Kristo upanuke kwa kuongeza makutano kote katika taifa
letu.”
“Ninakubali,” mmoja wa wanawake anasema, “lakini ikiwa utaanzisha mkutano wapya ni lazima uchukuwe uongozi. Msaidizi ni muumini mchanga sana hawezi kuongoza.”
Mwanafunzi anasema kwa uvumilivu, “Kundi jipya la Msaidizi hivi karibuni litakuwa kundi kubwa. Si kundi langu bali ni la Kristo. Sina muda wa kuongoza kila kundi jipya tunaloanzisha. Ninafundisha Msaidizi ili aweze kuliongoza hilo kundi na afundishe wachungaji wengine. Roho Mtakatifu atamwongoza Msaidizi vile tu ametuongoza.” Anauliza, “Je, unataka kusikia Jinsi Paulo
Alianza Makutano?” Mmoja wa wale wanawake anasema ndio na wanaume wachache wanakusanyika kusikiza na Mwanafunzi
anawakaribisha kuketi chini tena.


Tafuta Matendo Sura 13 na 14:
Zoezi.
•    Jinsi waumini wa Antiokia waliwachagua Paulo na Barnaba na kuwatenga waanzishe makutano wapya.
•    Jinsi kundi la kazi lilipeleka Injili huko Pisidia, katika Antiokia na Listra?
•    Kile walifanya Wayahudi walipowafurusha toka miji mingine.
•    Kile Paulo na Barnaba walifanya njiani kupitia kanda kwenye watu walipokea imani pitia ujumbe wao?
•    Kile walifanya waliporejea kwa mkutano wao Antiokia?
Mwanafunzi aelezea kundi dogo lililokusanyika kusikia yale aliyokuwa akimwambia Bwana Pumbavu. “Wakati mkutano waliabudu na kufunga, walitambua kuwa Mungu alikuwa amewatenga Paulo na Barnaba kwa kazi maalum. Viongozi waliwawekea mikono na kuwatuma kama kikosi. Popote walikwenda, walipokelewa vyema na watu kuwahubiria juu ya Yesu. Walishuhudia jinsi
Yesu, mpakwa mafuta ambaye Mungu alikuwa ameahidi, aliwawa lakini akafufuka tena na wengi wakamwona. Waliwaombea
wagonjwa na wengine wakapona. Kule Listra, waliwakataza watu wasiwaabudu kama miungu na wakawaamuru kuacha sanamu zao na kumrudia Mungu mmoja wa kweli.
“Mataifa waliitikia na wengi wakaamini, lakini Wayahudi wengi waliukataa ujumbe huu. Walipofurushwa, Paulo na Barnaba walipanguza vumbi ya miguu yao na wakaenda kwingine. Wakati wakirejea pitia miji hii hii, Paulo na Barnaba waliwateuwa viongozi kuongoza mkutano na wakawakabidhi kwa Bwana kwa njia ya Maombi na kufunga. Halafu wakarejea nyumbani kutoa ripoti kwa
mkutano uliowatuma. Hili ndilo mkutano wetu pia unafanya, kuanza na Msaidizi na kundi lake jipya.” Bwana Pumbavu anapiga kite
kama farasi mwenye hasira na anawaongoza wale wanawake wawili kuondoka.


Kuanzisha Makutano Wapya
Mwanafunzi anaenda tena kumtembelea Msaidizi kumshauri na kumhimiza. Anamwambia, “Msaidizi, jamii ya Recho iliitikia habari njema haraka, kama mataifa wengi katika kitabu cha Matendo. Je, umewauliza wote kutubu, kuamini katika Yesu na kubatizwa
kwa Jina lake?”
“Ndio. Nifanye nini tena?”
“Waonyeshe jinsi ya kuabudu Mungu kwa sehemu za msingi za ibada ambazo ulijifunza kwetu kwenye mkutano mama. Chukua Mlezi akusaidie kuwachunga. Usisahau vitu vya msingi. Wafunze kuomba, kujifunza Neno la Mungu, kukiri dhambi zao na kupokea uhakiki wa msamaha, sherehekea Meza ya Bwana, peana na kupokea ushirika. Wacha kila mmoja ashiriki kwa njia moja au nyingine.
Wafundishe kutii amri saba za msingi za Kristo kupita zingine zote. Je, unasikumbuka?”
“Ninaziimba,” Msaidizi anajibu. “Sitawahi sahau.” Anaimba wimbo unaoziorodhesha, tubu na uamini, ubatizwe, upende, ule
Meza ya Bwana, uombe, utoe, na ufanye wafuasi. “Roho Mtakatifu wa Mungu anatusaidia kufanya haya yote.”
“Vyema,” Mwanafunzi anasema. “Wakati kundi linakutana mara kwa mara, chagua viongozi wengine wazuri na uwawekee mikono na maombi. Unaweza funga, pia, jinsi mitume walifanya, isipokuwa hawakuamurisha hilo. Ni vizuri kuwa na zaidi ya kiongozi mmoja, jinsi tu Paulo kwenye makutano wapya aliyoanzisha. Hawa viongozi wanaweza kuwa washikilizi. Hivyo, unawateua kwa muda tu, kuona vile watafanya kazi. Inachukuwa muda kuona mtu yupi Mungu ametunikia wajibu huu. Wasaidie viongozi watekeleze amri saba za msingi mara moja. Wapokeze yale unajifunza toka kwangu. Nitakusaidia unihitajipo.”

35
Mwanafunzi anamtembelea Msaidizi wiki mbili baadaye. Msaidizi anaripoti, “Nilizingatia yale ulinifundisha. Nilitembelea jamii wengi wa Recho. Halafu nikawachukua tukatembelea marafiki zao. Wengi walimpokea Kristo. Kila mtu kwenye mkutano wangu wapya anatekeleza yale ulinifundisha niwafundishe.”
Wiki chache baadaye Mwanafunzi anamtembelea tena Msaidizi. Msaidizi anaripoti, “Tulianza kundi lingine jipya. Linakutana nyumbani mwa baba mkwe wangu. Niliwawekelea mikono wajomba wawili wa Recho kuwatuma kama wachungaji viongozi wa muda.”
“Ninafurahi kuona Roho Mtakatifu akifanya kazi hapa! Sasa tuna mkutano mjukuu. Nimekuwa nikisoma kitabu cha Matendo. Hebu nikwambie juu ya Jinsi Kanisa La Kwanza Lilianza, ili uweze kufunza mambo haya kwa wale wajomba wawili wa Recho unapoendelea kuwafundisha.


Tafuta katika Matendo 1:
Zoezi.
•    Je, ni wapi Yesu aliwaambia wafuasi wake kupeleka habari njema, kabla apae mbinguni?
•    Nguvu zao zilitoka wapi? Tafuta Matendo 2:
•    Je, nini kilitendeka Roho Mtakatifu alipowashukia wafuasi?
•    Je, Petero aliwaambia nini umati juu ya Yesu?
•    Ni vitu gani walivyotenda wale watu waliotubu vilivyosababisha kuzaliwa kwa mkutano wa kwanza?
Mwanafunzi anamwelezea Msaidizi, nyumbani mwa Msaidizi, “Yesu aliamuru wafuasi wake kupeleka habari njema kwa kila mtu, kuanzia na wale walio karibu sana nasi. Aliahidi nguvu toka Mbinguni, Roho Mtakatifu. Akashuka siku ya Pentekote na kuwajaza wafuasi. Wengine wanaita hili ubatizo wa Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu aliwajaza nguvu. Hafanyi hili tu kutupa hisia au ujuzi wa kibinafsi. Anafanya hivyo kutuwezesha kumtumikia Mungu na kumshuhudia Kristo kwa nguvu na mamlaka. Mitume walishuhudia kwa habari njema kwa umati wa watu kwa lugha yao wenyewe, kile mitume hawakuwa wamewahijifunza. Petero alitangaza kwamba Yesu alithibitisha kwa miujiza mingi ya kwamba Alikuwa Mteule wa Mungu. Baada ya Yesu kufa ili atuokoe toka dhambini na akazikwa, Alifufuka tena.”
“Nakumbuka,” Msaidizi anasema, “Watu elefu tatu walimsikiza Petero na wakatubu dhambi zao. Mitume waliwabatiza na kuwakaribisha kanisani siku hiyo. Wale waumini wapya walikusanyika kila siku kuabudu nyumbani na uwanjani mwa hekalu la Kiyahudi. Punde walianza kutekeleza amri saba za msingi za Kristo, na kanisa la kwanza lilianza Yerusalemu. Walipendana sana.”

Kutii Amri ya Kristo ya Kupenda na Kutoleana Mmoja kwa Mwingine kwa njia ya Kimatendo.
Mungu anaubariki mkutano wa Msaidizi na unakua kwa njia ya kawaida kwa vile watu wanawaeleza rafiki na jamaa zao juu ya
Yesu. Msaidizi anakuja kwa karakana ya useremala ya Mwanafunzi kumwambia, “Mkutano wangu umekua mkubwa sana na watu hawafurahii ushirika na kutumikiana jinsi walivyofanya hapo mbeleni. Wanakuja na kusikiza tu. Hawatambuani tena, na hawatoshei kwenye nyumba yangu. Upendo wetu kwa kila mmoja umeanza kupoa kwa sababu kundi limekua kubwa. Watu hawajuani. Hawaongeleshani. Si tena familia moja kubwa ya watu wapendanao. Hawafanyi uinjilisti jinsi walikuwa wakifanya walipokuwa kundi dogo. Je, tutadumishiaje ushuhuda wa Yesu na ushirika wetu?
Mwanafunzi anajibu, “Hii ni shida ya kawaida. Mkutano una kazi mbili za muhimu, kuwaleta watu kwa Kristo na kuwajenga wawe wafuasi watiifu wa Kristo. Unahitaji kuwapanga mkutano kwa makundi madogo kuzifanya hizi kazi vyema. Hapa kuna orodha ya mapendekezo ya Jinsi ya Kuunda Makundi Madogo ya viongozi wapya wa makundi mapya, ambao watakutana na
familia chache nyumbani.” Anaandika:
Epuka mikutano nyumbani mwa kiongozi ikiwezekana. Watu wanawezafikiri hilo kundi ni lake, na tunawavuta watu wengi kwa Kristo kwa kukutana nyumbani mwa wengine.
Kiongozi hapaswi kushughulikia pesa ya sadaka ya kikundi. Teuwa mtu. Wacha kiongozi awe huru kuchunga kikundi. Usilihubirie tu hili kundi dogo bali soma Biblia pamoja nao. Uliza maswali kuhusu fungu mnalosoma. Wacha kila mtu aongee juu
yake. Himiza kila mtu ashiriki kwa ibada na kwa mafunzo, kulingana na vipaji vyao. Husisha familia nzima katika shughuli hizi.
Usiwaruhusu wageni kulifunza kundi. Wewe na viongozi wengine ni lazima mchunguze maisha yao na mafundisho yao kwanza.
Tafuta watu wakufundisha kama viongozi wapya wakukusaidia kwa kikundi. Pokeza kila kitu umejifunza kwao. Wahimize kuanza makundi yao punde. Hii inadumisha kukua kwa msukumo wa Kristo.

Miezi miwili baadaye kwenye karakana ya useremala ya Mwanafunzi, Msaidizi anashuhudia yale wamekuwa wakifanya. “Wale viongozi wapya wengine nami tunafuata wasia wako. Tulipanga makundi madogo yakutane kwa nyumba kote kwenye eneo hili. Makundi wengine wanatembelea wasioamini. Wengine wanalenga maombi au kwa kuwatuma wafanyikazi kwenye maeneo mapya ya mbali. Wengi wao wanawalea wenye mahitaji katika jamii. Wote wanatafuta njia za kutumia vipaji vyao vya kiroho kuinua mkutano na makundi mapya madogo. Ninakutana mara kwa mara na wachungaji viongozi wote wapya wa makundi madogo, kuomba, kusikiza ripoti zao, kushughulika na shida zao na kuwahimiza.”
“Ajabu!”
“Kundi moja linatembelea jamaa wanaoishi mbali sana. Viongozi nami tunapanga haya makundi kama makutano wapya. Wote wanakutana mara moja kwa mwezi kwa ibada ya pamoja na kusherehekea. Wakati ujao tafadhali kuja.”
Mwanafunzi anadhahadharisha, “Unapaswa kuwa makini sana iwapo wanakutana wote kama kundi moja kubwa. Hiyo ndiyo sababu serekali ilimlazimu Bwana Hekima kuondoka hapa. Mateso kila mara hufuata ukuaji wa kanisa la Kristo.”


36
Hadithi Za Mchungaji

Mdsaidizi anajibu, “Mungu atatuma wengine wao kama mashahidi wa Kristo sehemu za mbali, jinsi tu alivyomfanyia Bwana Hekima. Hili litachukua muda, fedha na bidii, lakini ninataka mkutano wetu ushiriki katika sehemu  muhimu ya kazi ambayo umenifunza.”
“Vyema sana!” Mwanafunzi anakubali. “Mungu anataka kila watu, kundi na tamaduni duniani kusikia habari njema ya Yesu
Kristo. Anafurahia katika neema ya Mungu ifikayo pande zote za dunia.”

Kazi ya Kufanya
•    Mwombe Mungu asaidie mkutano wako utambue wale wanaweza anza mkutano wapya na kuwatakasa kwa maombi, kufunga, na kuwawekea mikono.
•    Tambua kundi lolote la waumini wapya waliobatizwa ambalo linakutana kwa ibada na kumtii Yesu Kristo kama mkutano wapya na uwachagulie viongozi wa nyumbani wapya.
•    Ikiwa hawa viongozi wapya ni wapya kwa imani, wachague tu kama wachungaji viongozi wa muda, hadi watakapo thibitishwa.
•    Wakuze hawa viongozi wapya toka kule nyuma. Waweza kuwa wachungaji viongozi wa muda kwa miezi michache au mwaka au zaidi, hadi iwe wazi ni yupi Mungu amempa kipaji hiki.
•    Wafunze hawa viongozi wapya kutii amri zote za Kristo kwanza na juu ya zote. Waonyeshe jinsi ya kubatiza, kusherehekea
Meza ya Bwana na kutekeleza sehemu za ibada.
•    Waruhusu hawa viongozi wapya watumike hivyo tu iwapo wanakutana na kiongozi aliye na ujuzi anayesimamia kazi yao na kuwakuza.
•    Ikiwa mkutano wako ni mkubwa sana kwamba wakutanapo mtu akiongea hawezi kusikika, na ndipo iwe familia ya upendo kwenye kila mmoja anatumikia wengine, unda makundi madogo madogo. Weka haya makundi yakiwa madogo ili kila mtu aweze kushiriki na kutumikiana mmoja kwa mwingine kwa njia ya vitendo.



III-6—Huduma ya 6

Fundisha Wachungaji Viongozi na Viongozi Wengine.

Msaidizi anakuja kuongea na Mwanafunzi siku moja nyumbani mwake lakini Mwanafunzi anasema, “Nina shughuli nyingi sana siwezi kukutana nawe leo. Samahani.”
Msaidizi anauliza Sara shida iko wapi. Sara anasema, “Sijui. Kuna kitu kimemshusha moyo. Na hataki kukisema.”
Msaidizi anaondoka, akiwa na huzuni. Anamwandikia ujumbe Bwana Hekima, “Nina wasi wasi juu ya Mwanafunzi. Anaonekana kupoteza shauku ya kazi. Kuna kitu si sawa.”
Siku chache baadaye Bwana Hekima anawasili, safari yake ya kwanza baada ya muda. Anampata Msaidizi na wanaenda kuongea na Mwanafunzi. Wanampata Mwanafunzi nyumbani kweke lakini hataki kuongea. Wanaanza kuondoka lakini Sara anawaomba
wakae. “Bwana Hekima,” Anasema, “Oh, ninafurahi umekuja! Nafikiri najua ni nini kibaya. Mkutano sasa umekua mkubwa sana kwamba  Mwanafunzi  amekuwa  na  shughuli  nyingi  sana  hadi  akachoka.  Hana  muda  wa  familia  yake.  Makutano  wengine
anaowatumikia  wanamsaidia  kifedha,  ili  kwamba  haitaji  kufanya  kwa  karakana  yake,  lakini  bado  amelemewa  na  majukumu.
Anakasirika na kila mtu bila sababu yoyote, hata waumini wapya.”
Bwana Hekima na Msaidizi wanamuuliza Mwanafunzi kuomba. Hataki kuomba nao. Wanaketi kimya kwa muda mrefu. Mwishowe, Mwanafunzi anaongea kwa upole. “Nimechoka sana! Nina mengi ya kufanya. Ni lazima wewe Bwana Hekima urejelee uongozi hapa tena. Askari hawajakuwa wakitusumbua. Ni salama.”
Bwana Hekima anakataa. “Una shida kama Musa alikuwa nayo. Alijifanyia kazi zote. Alishindwa kutelekeza majukumu ya uchungaji kwa wengine. Umefanya kazi njema kutelekeza kwa Msaidizi na mikutano wapya, lakini umeshindwa na mkutano wako mwenyewe. Siwezi rudi huku kukusaidia kuchunga watu wako. Ikiwa nitajaribu kuchunga kila kundi ambalo ninasaidia kuanzisha, nitazuia kazi ya Roho Mtakatifu! Nitajichosha na sitawasaidia watu wanaonihitaji.”
Mwanafunzi anaketi kimya akisikiza. Bwana Hekima anaendelea, “Yesu alituamuru kufanya wafuasi na kuwafunza kutii kila kitu alichotuamuru.  Aliwapokeza  wafuasi  kila  kitu  walichohitaji  kufanya  huduma  na  kuanza  makutano  wapya.  Wakati  mwingine aliwatuma wawili wawili, kuhubiri akiwa angali pamoja nao. Alisema watafanya makubwa kuliko yale alifanya baada yake kuondoka.
Walimtii na kupokeza viongozi wapya kila kitu walicho pokea toka kwake. Mungu alibariki utii wao wa upendo.”
“Lakini mimi sina nguvu kama zao.”
“Mungu hukupa nguvu unazohitaji. Sasa ni lazima ufanye yale Yesu alifanya. Wapokeze wengine kwa huduma kila kitu wanachohitaji kufanya huduma. Nilikuwekelea mikono na kukupokeza majukumu ya uongozi. Roho wa nguvu anaishi ndani mwako jinsi aishivyo ndani mwangu. Sasa unajipata na kazi nyingi. Hebu tusome pamoja Wasia wa Yethro kwa Viongozi walio na Shughuli Nyingi.”

Zoezi.
Tafuta katika Kutoka Sura 18 yale Baba Mkwe wa Musa Yethro alimwambia:
•    Je, ni nini ambacho Yethro alitambua Musa anakosea kabla ya kumshauri?
•    Je, watu waliokuwa karibu na Musa walikuwa wakifanya nini tangia asubuhi hadi usiku?
•    Je, wasia wa Yethro wa busara kwa Musa ulikuwa ni nini?

37
•    Je, ni watu wa aina gani Yethro alimwambia Musa achague kama viongozi?
•    Je, ni kwa nini Musa hangewatumikia watu vyema akiwa anashiriki uongozi?
Sara analeta chai na Bwana Hekima anawaelezea hii hadithi kwa Mwanafunzi na Msaidizi. “Musa alikuwa kiongozi mkuu. Aliwatoa watu wa Mungu toka utumwani Misri. Biblia pia inasema alikuwa mtu mnyenyekevu sana. Aliwatumikia watu wake kwa moyo wake wote, lakini hangeweza watumikia vyema akiwa pekee yake. Yethro aliona watu wakimsubiri tangia asubuhi hadi jioni
aamue malalamishi yao. Alikuwa anajichosha pamoja na wale watu. Viongozi wabaya hawashiriki majukumu na wengine. Sasa,
Mwanafunzi, tafadhali niambie unachokumbuka toka hadithi hii.”
Mwanafunzi anafikiri kwa dakika. “Yethro alimwambia Musa achague viongozi waliokomaa ambao wangeshiriki mzigo wa majukumu naye. Hawa watu walihitajika kuwa waaminifu, wakomavu kiroho na wenye uwezo. Yethro alimwambia Musa kuhukumu kesi ngumu pekee zenye viongozi wengine walimletea. Alikuwa ashughulike na viongozi wa idadi kubwa, walioshughulika na
viongozi wa idadi ndogo hadi mwishowe ilikuwa kundi dogo la kumi pale walipoweza kutekeleza kikamilifu uchungaji wa watu.”
“Ndio. Wakati Musa alishiriki uongozi kwa njia hii, alipata wakati wa kuomba na kufundisha. Aliwatumikia watu vyema zaidi. Mwanafunzi, kama Musa, unakazi nyingi sana ya kufanya. Kwa vile una uhusiano mwema na viongozi kadhaa wapya, waache washiriki zaidi mzigo wa majukumu, kuwachunga kwa makundi madogo.”
“Lakini viongozi wapya hukosea,” Mwanafunzi analalamika. “Siwezi waruhusu wafanye makosa.”
“Ndio, unaweza, ndugu yangu,” Bwana Hekima anasema, “Nilikuacha ukafanya makosa mengi mara ya kwanza. Yesu aliwaacha wafuasi wake wakafanya makosa. Wachungaji viongozi wako wapya watafanya makosa—huenda yakawa mengi kama yale nilifanye nilipoanza! Huenda yakawa mengi kama ya wafuasi wa Yesu mara ya kwanza.”
Mwanafunzi anacheka. “Nilitoa wasia huu kwa Msaidizi lakini nikasahau kuutekeleza mwenyewe!”
Bwana Hekima anajibu, “Basi, wacha tutafute kwa pamoja Kile Paulo alimfundisha Timotheo juu ya Kuwafundisha Viongozi
wa Kuwafundisha Wengine.”


Tafuta 1Timotheo 2:1-2:
Zoezi.
•    Je, uhusiano wa Paulo na Timotheo ulikuwa wa ndani kiasi gani?
•    Je, Paulo alimwambia Timotheo afanye nini na yale aliyasikia kwa uwepo wa mashahidi wengi?
•    Je, ni miungano mingapi unaweza pata katika huu msururu wa mafundisho? Anza na Paulo na uhesabu wale wengine.
Msaidizi anamwacha Bwana Hekima na Mwanafunzi, “Je, unaona msururu wa ufuasi katika 2 Timotheo 2:2? Paulo alimpenda Timotheo kama mwana. Paulo alimfundisha, Tito na wengine. Alihakikisha kila mkutano wapya walikuwa na kiongozi wao ambao waliweza wafundisha wengine.”
“Naona. Kuna miungano miwili kwenye msururu katika 2 Timotheo 2:2.”
“Ufuasi ni kama pembe tatu na pande tatu.Upande mmoja ni upendo, mwingine ni Neno, na wa tatu ni kazi au kutekeleza Neno. Pande      zote     za     pembe     tatu     ni     lazima     zishikane     au     pembe     itaanguka.     Paulo     alitekeleza     haya     yote matatu    ya   ufuasi.  Aliwapenda  wafuasi  wake,  na  akamwita  Timotheo  mwana. Aliwafundisha Neno la Mungu kwa uaminifu, akiwapokeza kila  alichopokea. Aliwasaidia kutekeleza Neno la Mungu mara moja
katika maisha yao na maishani mwa kundi. Sasa, unapanga kufanya nini Mwanafunzi?”
“Uhusiano wangu na viongozi wapya umedidimia. Ni lazima nitie nguvu uhusiano wangu na wao kwa kuwasikiliza zaidi. Kabla niwafundishe, yale  makundi yao yanahitaji. Nitawaonyesha jinsi ya kupokeza mafundisho yao kwa wengine ambao wanaweza fundisha wengine pia, vile Paulo alisema. Nitakuwa makini kuomba kila wakati, kusikiliza na kupanga pamoja ninapokutana na viongozi, jinsi ulivyonifanyia.” Mwanafunzi anaandika orodha ya vitu vya kufanya atakapokutana na viongozi wapya kuwakuza:

•  Kuomba ili Roho Mtakatifu atuongoze kwa vipindi vya kukuzana.
•  Wazikize wanafunzi wanapotoa ripoti za shughuli za huduma zao.
•  Wasikize wanapofupisha yale wanajifunza toka kwenye Biblia.
•  Panga shughuli mpya kulingana na mahitaji na nafasi wanazoona kwenye makundi yao madogo.
•  Wape masomo mapya ya Biblia kulingana na mahitaji na nafasi.
•  Weka mipango yetu kwa Bwana pitia maombi.

38
Hadithi Za Mchungaji


Bwana Hekima anasema, “Wakati kiongozi anashindwa kushiriki majukumu ya uongozi na wengine, anakosa unyenyekevu. Anahitaji kuwa mtumishi kiongozi. Yesu alituonyesha watumishi viongozi ni watu aina gani. Alitwambia tuwatumikie watu kwa unyenyekevu bila kujaribu kuwa watu wa maana na nguvu. Soma nami juu ya Mtumishi Kiongozi Aliyeosha Miguu ya Wanafunzi Wake.


Tafuta katika Yohana 13:1-17:
Zoezi.
•    Je, ni jinsi gani Mwana wa Mungu aliwatumikia wafuasi wake kwa unyenyekevu kama mtumwa angelifanya?
•    Ikiwa Bwana wetu na Mwalimu alitumikia wafuasi wake jinsi hii, je tunapaswa kuwatumikia wenzetu kwa nia ipi?
•    Yesu hakutumia tu maneno kuwafundisha wafuasi wake kuwa watumishi viongozi. Alitumia nini kingine?”
“Naona,” Mwanafunzi anamwambia Bwana Hekima, “Yesu alikuwa Mwana wa Mungu na anastahili heshima zote na ibada, lakini aliwatumikia wafuasi wake kwa unyenyekevu. Alichukua kitambaa na kuiosha miguu yao yenye vumbi, jinsi mtumwa angelifanya siku hizo. Mwalimu Mkuu alitufundisha kwa mfano wake mwenyewe. Kwa upendo, tunawaongoza kwa unyenyekevu huo huo. Tunapowafundisha viongozi, hatuwafundishi tu ukweli wa Mungu, bali tunawaonyesha jinsi ya kumtii Mungu kwa mfano wetu wa unyenyekevu.”
Siku iliyofuata Mwanafunzi anawaita viongozi wa mkutano kwenye mkutano na anaeleza, “Ninaenda kuwapa majukumu mengi zaidi. Mtakuwa wachungaji-wenza.”

Mwanafunzi  hakuwa  amemwalika  Bwana  Pumbavu,  lakini  amekuja  na  anaingilia,  “Mwanafunzi,  hakuna  mtu  mwingine amehitimu kutumika kama mchungaji-mwenza. Hawa wanaume hawawezi ongoza watu au makanisa mapya unayosaidia wengine kuanzisha. Ni lazima uwatume kwa chuo cha Biblia kwa miaka mitatu ama minne kabla wahitimu.”
Bwana Hekima hajaondoka bado. Anakataa, “Hilo limejaribiwa lakini ni nadra lifaulu kwa hali kama hii yetu hapa. Hebu tutazame kile mtume Paulo anasema juu ya kuhitimu kwa viongozi. Mwanafunzi, je, unakumbuka Kuhitimu kwa Viongozi ambao
tuliupata katika nyaraka za Paulo kwa Timotheo na Tito?”


Tafuta 1 Timotheo Sura 3 na Tito 1:5-9:
Zoezi.
•    Je, kulingana na Tito 1:5, kwa nini Paulo alimwacha Tito Krete?
•    Je, Tito alihitaji kuwafanyia nini makutano wapya wa Krete?
•    Je, mchungaji kiongozi anapaswa kuwaje? Fafanua mwenendo wake?
•    Mchungaji kiongozi lazima ‘awe anaweza fundisha.’ Kwa nini Mungu anahitaji hili?
Bwana Hekima anaendelea kuwahimiza viongozi wanaokutana nyumbani kwa Mwanafunzi. “Paulo alihakikisha kwamba kila mkutano alio anzisha ulikuwa na viongozi wao. Waliwachunga watu. Walifanya kazi pamoja kama wachungaji-wenza. Paulo hakuona kama kazi yake kwa mkutano wapya imemalizika hadi walipopata viongozi wao wenyewe. Wageni wasioishi kwenye hiyo jamii hawapaswi kuwachunga mkutano. Wakati mwingine Paulo alirudi baadaye kwa mkutano kuwachagua. Alimwacha Tito nyuma kule Krete kuwachagua viongozi huko. Paulo na Tito waliwachagua wanaume toka kwa mkutano wenyewe. Waliwachagua wanaume wanaoheshimiwa na waumini, wasiowaumini, na familia yao. Tabia ya kiongozi ni muhimu tu kama uwezo wake wa kufunza.”

Bwana Pumbavu analalamika, “Hakuna mtu hapa aliyehitimu kuwa kiongozi kwa kanisa kama mkoi wangu.”
Bwana Hekima anajibu, “Makanisa mengine yanaongezea kuhitimu kwa viongozi ambako hakupo kwenye Maandiko, matakwa ambayo Kristo wala Mitume wake hawakuamuru au kutenda. Hizi tamaduni za binadamu zinazuia viongozi wasiwachague viongozi kwa mkutano wapya. Hili linazuia kazi ya Roho Mtakatifu. Iwapo hizi tamaduni zinazuia utii wetu kwa Kristo, ni lazima tuachane nazo.”
Mwanafunzi analiambia kundi, “Bwana Hekima alitupa ushauri huu huu ambao Yethro alimpa Musa. Alisikiza na kutazama kwanza kutambua mahitaji yalikuwa wapi. Hakutoa mashauri hadi alipoona wazi mahitaji na mianya ya huduma. Bwana Hekima hufanya hivyo hivyo siku zote. Anasikiza halafu anatusaidia kupanga shughuli mpya kwa pamoja na anatupa mafungu ya Biblia
kuyasoma ambayo yanalingana na mahitaji. Tutafanya vivyo hivyo. Hebu tuombe tuweke mipango hii kwa Mungu.”
Bwana Hekima anaondoka asubuhi ifuatayo. Mwezi mmoja baadaye, Mwanafunzi anamwandikia, “Nilianza mara moja kuwafundisha wanaume wengine wanne kwa kundi langu kwa bidii ili waweze kuchukua majukumu zaidi. Ninashiriki mzigo wa uongozi  zaidi  kwa  kikamilifu  na  hawa  wachungaji  viongozi.  Tunafanya  yale  Yethro  alimwambia  Musa  afanye.  Sasa  nahisi kupumuzika na ninapata muda wa kutosha na familia yangu. Hawa viongozi wapya sasa wanawafundisha viongozi wapya sana na wanatelekeza majukumu ya uongozi jinsi makundi madogo yanapoongezeka. Wote wanakuta kwamba wana muda wa kutosha na familia zao, na kuomba na kujiandaa kufundisha. Asante sana kutusaidia kutelekeza na kutaja viongozi zaidi. Roho Mtakatifu anawatumia watu zaidi kufanya kazi kubwa.”

Kazi ya Kufanya.
•    Chagua viongozi katika kila mkutano wapya, ukifuata matakwa katika 1 Timotheo 3 na Tito 1:5-9.
•    Wafundishe wanaume wa kutegemewa kuwa wachungaji viongozi, na uwasaidie hivi punde kuwafundisha viongozi wengine wapya.

39
•    Wafunze viongozi wapya kwa maneno yako na kwa mfano wako wawe watumishi viongozi na si wadhibiti wa kiburi.
•    Weka nguvu kwa uhusiano kati yako na viongozi unaowafunza.
•    Kutana mara kwa mara na viongozi unaowafunza. Omba na usikize ripoti zao. Panga masomo mapya na shughuli pamoja.
Enenda nao wanapotembelea watu wao na waache wao waongee.
•    Wacha wale unaowafunza wahubiri wakati unawatembelea, kuonyesha watu wao kwamba unaheshimu uongozi wao na una imani nao. Ni kazi yako kuwaandaa vyema kwa hayo mahubiri. Unahitajika kuwasikiza ili ujue jinsi ya kuwasaidia wawe bora zaidi.

III-7—Huduma ya 7

Endeleza Ushirika Ndani na Kati ya Makutano

Siku  iliyofuata, kundi  la wanaume  kutoka  kwa  mkutano  wa  Mwanafunzi liliwasili  Nyumbani kwake na  Bwana Pumbavu anayetangaza, “Mwanafunzi, tunataka kumsikia yule mhubiri mashuhuri toka kanisa la mkoi wangu sasa. Tunakualika uambatane nasi kwenda kujifunza jinsi ya kuendesha kampeni ya kweli ya Mungu. Kila kitu tunafanya si sawa. Lazima tufanye uinjilisti kama yeye. Anajua kuhubiri! Ninaenda kuanza kundi jipya hapa ambalo linafuata mafundisho ya huyu mtu  mashuhuri! Wengine kanisani wanakubaliana nami. Haya ni mapenzi ya Mungu kwa kanisa letu.”

Tii amri ya Kristo ya Kupendana Mmoja na Mwingine
Mwanafunzi anahisi hasira anapotazama nyuso za hawa wanaume. Anamwabia Sara baada ya wao kuondoka, “Inaonekana hili wazo ambalo Bwana Pumbavu alileta toka kanisa la mkoi wake linaenea mkutanoni mwetu. Tayari limesababisha mgawanyiko
mchungu.”
Wakati uliofuata mkutano unapokutana unabishana mmoja na mwingine. Machafuko yanaenea. Anamtumia Bwana Hekima ujumbe, ambaye anajibu kwa waraka kwa watu wa mkutano wa Mwanafunzi. Mwanafunzi anawasomea:

Ndugu na dada, ninawaomba mfuate mfano wa Paulo katika kitabu cha 1 Wakorinto. Ninawaomba kwa jina la Yesu mwache kubishana ninyi kwa ninyi. Ishi kwa umoja wa kweli ili kusiwe na mgawanyiko katika mkutano. Nawasihi muwe wenye nia moja, muungane kwa mawazo na kusudi. Mlijifunza kutii amri za Yesu kwa imani na upendo kama wa watoto wadogo. Msiwache sasa. Wengine  wenu  wanasema,  ‘Namfuata  Bwana  Hekima,” Wengine  wanasema,  “Namfuata  Mwanafunzi.”  Wengine  wanataka kumfuata mhubiri kutoka kanisa ambalo Bwana Pumbavu huwa anatembelea mkoi wake. Je, Kristo amegawanywa kwa vipande? Je, mimi, Bwana Hekima, nilisulubishwa kwa ajili yenu? Nia hii inatokana na kiburi.
Nilipo kuja kwenu  mara ya kwanza, sikutumia  maneno  makubwa au  mawazo  ya juu. Nilisistiza  Yesu na kifo chake msalabani. Ujumbe wangu na mahubiri yangu yalikuwa ya kawaida, bali Roho Mtakatifu aliyatumia. Hatutumii hekima ya ulimwengu. Kumbuka kwamba si wengi wenu walikuwa werevu au wenye nguvu machoni mwa ulimwengu, lakini Mungu alifanya mambo ya ajabu maishani kwa Nguvu Zake. Mwanafunzi anafuata mfano wangu, na ni lazima mmtii yeye pamoja na wachungaji viongozi, kwa sababu wanawafundisha Neno la Mungu.

Bwana Pumbavu anaanza kuingililia lakini Mwanafunzi anaendelea kusoma.

Je, mlisahau kwamba ninyi nyote pamoja ni hekalu la Mungu na Roho Mtakatifu wa Mungu anaishi ndani mwenu? Msiwe wenye kiburi kumfuata kiongozi mwanadamu. Sisi zote ni watumishi wa Kristo, na anampa kila mtu kazi ya kufanya kanisani mwake. Mtu mmoja napanda mbegu na mwingine anamwagilia maji, bali Mungu anafanya hizi mbegu zikue. Ninyi ni shamba la Mungu na jengo la Mungu, si letu. Huu mgawanyiko kati yenu unatokana na kiburi.

Waraka wa Bwana Hekima unadurusu jinsi Kiburi na Upumbavu Kiliwagawanyisha Watu Wote.


Tafuta katika Mwanzo 11:1-9:
•    Watu walitumainia kwa ukuu wa nani?
Zoezi
•    Je, Mungu alifanya nini kukomesha huu uasi wa kiburi dhiti yake?
Mwanafunzi anajadili waraka wa Bwana Hekima na Mkutano wake, kwenye nyumba yake, “Watu wamegawanyika kwa nchi, lugha na desturi mbalimbali kwa maelefu ya miaka, sasa kwa hekima ya Mungu, anatuleta pamoja kiroho katika Kristo, jinsi yalivyokuwa makusudi yake mwanzoni.”
Mmoja wa viongozi wapya waliochaguliwa anaongezea, “Juzi tulisoma hili kwa kundi letu dogo. Yesu alituombea zote katika Yohana 17. Aliomba, “Baba, wafanye wawe wamoja, jinsi wewe nami tulivyo wamoja. Ombi hili la Yesu limejibiwa kanisani kote ulimwenguni hivi leo, kwa sababu, tu mwili mmoja katika Kristo. Yeye ni kichwa chetu. Huenda tusitende kama tunavyohitajika, lakini hilo halibadili ukweli kwamba Roho Mtakatifu anatuunganisha.” Wanatamatisha mkutano kwa maombi ya umoja wa kiroho katika Kristo.
Siku iliyofuata Mwanafunzi anatembelea mwanafunzi wake Msaidizi na kumwambia, “Kundi linaloongozwa na Bwana Pumbavu limegawanyisha mkutano wetu. Tafadhali njoo unisaidie.” Wanajadili jinsi watu walio na uchi wa mamlaka na utawala kila mara


40
Hadithi Za Mchungaji

manasababisha migawanyiko ya uchungu. Msaidizi anamwambia mwalimu wake, “Nimemaliza tu kusoma katika 1 Wakorinto 13
kwamba hao pia walikuwa na migawanyiko. Nafikiri tunaweza pata msaada katika Sura ya 13, Sura ya Upendo.


Tafuta katika 1 Wakorinto Sura 13:
Zoezi
•    Je, karama zetu zinamanufaa gani ikiwa hatuzitekelezi kwa upendo?
•    Je, ni vitu gani ndivyo upendo?
•    Je, ni vitu gani visivyo upendo?
•    Ni vitu gani upendo hufanya?
•    Ni vitu gani ambavyo upendo haufanyi?
Wanaposafiri kurejea nyumbani kwa Mwanafunzi, Msaidizi anatoa maoni juu ya yale wamesoma, “Ikiwa tutatekeleza vipaji vyetu kwa kiburi badala ya kwa upendo, hivo vipaji ni bure. Mungu anaweka upendo ndani mwetu, kutufanya tujali haja za wengine. Anatupa nguvu za kuwasamehe. Upendo si kile tunahisi, bali ni kile tunafanya. Tunaweza waonyesha watu upendo kwa imani, hata
kama hatuhisi hivyo. Wakati mwingine inachukua muda kwa hisia zetu ziweze kuambatana na uamuzi wetu wa kupenda.”
Mwanafunzi anaomba, “Mungu Mpendwa, nisamehe kwa kuwakasirikia wale wanaogawanyisha, na unipe ujasiri wa kukabiliana nao kwa uthabiti na upendo.”
Siku iliyofuata Mwanafunzi na Msaidizi wanamtembelea Bwana Pumbavu kumsihi awache kusababisha machafuko. Bwana
Pumbavu anabadili mada. Anapayapaya, “Mwanafunzi, watu wako wengine hawawatumikii maskini jinsi ulivyowaamuru. Unawaruhusu  wanakufua  mamlaka  yako!  Itisha  mkutano  na  uwaambie  wakutii  au  waondoke!  Hawa  ndiyo  wanaosababisha machafuko kanisani!”

Jinsi ya Kukabili Utofauti wa Maoni katika Mkutano.
Mwanafunzi anamwambia Bwana Pumbavu, “Hatuzuii machafuko kwa kutumia utaratibu wa nguvu hivyo. Hebu nikwambie hadithi ya ufalme uliogawanyika. Mfalme Daudi alimpenda Mungu kwa moyo wake wote, na Mungu akamwahidi kwamba wazao
wake watatawala kama wafalme milele. Mwanaye Suleimani alimwomba Mungu ampe hekima ya kuongoza Israeli vyema, na
alijenga Hekalu la Mungu Yerusalemu. Mwanawe Suleimani, Rehoboamu, hata hivyo, hakujali Mungu, au watu wa Mungu jinsi babake na babu yake walifanya. Alisikiza mashauri mabaya na akafanya uamuzi kwa Mkutano ambao Uliugawanyisha Ufalme wa Israeli.


Tafuta 1Wafalme 12:1-19:
•    Je, watu walimwuliza Mfalme Rehoboamu afanye nini?
Zoezi.
•    Rehoboamu alikuwa na vikundi viwili vya washauri. Ni gani alilosikiliza?
•    Watu walifanya nini wakati Rehoboamu alikataa kuupunguza mzigo wao?

Bwana  Pumbavu  anawasikiliza  Mwanafunzi  na  Msaidizi  bila  kukatiza,  halafu  anasema,  “Nawashukuru  kunitembelea  na kunielezea haya yote. Nitafikiri juu yake.”
Msaidizi anarudi nyumbani kwake na Mwanafunzi anarejea kwenye karakana yake ya userelemala kuyatafakari haya mambo. Anatambua kuwa wakati mwingine inanufaisha kufanya kazi kwa mikono ilihali unatafakari Neno la Mungu. Anaomba, “Baba, nisaidie nisuluhishe haya machafuko kwa hekima.” Anakumba yale Bwana Hekima alimfundisha juu ya jinsi Mikutano Miwili inasuluhisha Mzozo. Anafikiria juu ya jinsi Paulo na mitume wenzake walikabiliana na shida ambayo ilikuwa imeligawanya kanisa kule Antiokia.

Zoezi.
Tafuta Matendo Sura 15 jinsi viongozi wa makutano wawili walikabili maoni tofauti:
•    Je, viongozi waliruhusu kila mtu aseme upande wake wa mzozo?
•    Je, Petero alionyeshaje heshima kwa Mafarisayo waliozozana  naye?
•    Ni lini Yakobo alipata jibu la mzozo?
•    Je, Mungu aliwasaidia kukubaliana na uamuzi wao? Kama ni hivyo, namna gani?
•    Je, Wakristo Wakiyahudi waliwalazimu mataifa kufuata desturi zao?
•    Paulo na Barnaba walipoanza safari yao ya utume iliyofuata, nini kilisababisha watengane, makundi ya kazi mawili badala ya moja?
Msaidizi anarejea kumsaidia Mwanafunzi kukabiliana na mgawanyiko kwa mkutano uliofuata nyumbani mwake. Mwanafunzi anasema, “Matendo 5 inafunua kwamba watu humtumikia Mungu kwa njia mbalimbali. Umoja katika kanisa la Kristo haumaanishi kuwa kila muumini au kila mukutano una vipaji, maoni au mazoea sambamba. Hatuwalazimu kutufuata. Kuwalazimu kuwa sawa si
umoja. Tunawaamuru tu watu watende amri za Kristo na mitume wake. Kulikuwa na mgawanyiko mkubwa kwenye kanisa la
Antiokia. Wafarisayo walisisitiza amri zile zingine kana kwamba zilikuwa na mamlaka sawa na ya Mungu. Kanisa lilihitaji usaidizi kutoka kanisa lingine.”
Mwanafunzi anasoma sehemu za Matendo 15 na anauliza Msaidizi aeleze. Anaeleza, “Paulo na Barnaba walisafiri toka Antiokia hadi Yerusalemu na wakafanya kazi pamoja wakati wa mkutano huu kuelezea jinsi Mungu alikuwa amewakubali mataifa kanisani bila

41
kuwafanya wafuate desturi za Kiyahudi. Viongozi wakuu Yerusalemu walikuwa Petero na Yakobo. Walisikiza kwa makini watu wakielezea maoni yao, bila kuwakatiza. Halafu, bila kuwalaumu, wakawaonyesha watu Maandiko na kwa nguvu za Roho Mtakatifu Mungu aliwafungua mataifa toka desturi za Kiyahudi. Viongozi walisikiliza kwanza, halafu wakasema kweli kwa upendo. Wafarisayo mwishowe walikubali na kuwa chini ya wengine na wote wakakubali huo uamuzi. Mungu akaponya mgawanyiko.”
Watu kadhaa wanasema, “Amina!”
Msaidizi anaendelea. “Baadaye, hata hivyo, Paulo na Barnaba walizozana kuhusu jinsi ya kufanya huduma. Walishughulikia mzozo wao faraghani, bila udaku au kulaumiana. Kila mmoja aliheshimu maoni ya mwingine na walikubaliana kufanyia mazoezi vipaji vyao vya kiroho kila mtu kivyake. Mungu alibariki kazi ya kila mmoja wao, walipokwenda kila mtu njia yake na vikosi viwili
badala ya kimoja, kuhimiza makutano na kuanza wengine wapya wengi.”

Tofauti kati ya Amri na Utaratibu
Watu wa Mwanafunzi walitaka kufanya haki na kusikiza kwa makini alipokuwa akieleza, “Hebu tuzingatie mizozo hii miwili
katika Matendo 15. Wa kwanza ulikuwa juu ya mamlaka ya amri ya Kristo kwa kanisa. Wa pili ulikuwa ni kuhusu utaratibu wa kutekeleza amri hizi. Paulo na Barnaba walizozana juu ya swala la mpangilio. Kanisa limeungana chini ya mamlaka ya amri za Kristo. Lakini Wakristo wako huru kuchagua utaratibu tofauti tofauti wa kuzitekeleza katika huduma mbalimbali, kulingana na vipaji vyao vya kiroho. Migawanyiko huja wakati tunachanganyisha viwango vya mamlaka kwa kanisa la Kristo. Amri zake ni kiwango cha kwanza; tunazitii wakati wote. Lakini utaratibu wa kuzifanyia mazoezi unaweza tofautiana zaidi.”
Mjadala  unaendelea  kwa  muda  mrefu.  Bwana  Pumbavu  na  wafuasi  wake  hawawasikilizi  wenzao.  Wanazidi  kumsuda Mwanafunzi. Bwana Pumbavu ndiye msemaji wao na anaendelea kusema, “Mwanfunzi ni mtu mzuri. Lakini anakosa elimu na hana shahada toka chuo cha Biblia kinachojulikana. Kwa hivyo hatuwezi kuwa na uhakika kuwa anatufundisha ukweli wote.” Wengine wachache wanaketi kando yake na wanarudia jambo hilo hilo.”
Mwanafunzi anasema, “Hatujaafikiana kikamilifu na kila mtu hapa na ninaona kwamba wengi wenu mnaanza kuchoka. Wale wanataka kuondoka wanaweza fanya hivyo.”
Wanawake na wanarika wanaondoka. Ni mtu mmoja tu, Yakobo, anaendelea kukubaliana na Bwana Pumbavu. Alikuwa akihudhuria kanisa la mkoi wa Pumbavu na hivi majuzi alihamia katika jamii ya Mwanafunzi. Yakobo anasema kwa mara ya tatu,
“Nafikiri tunapaswa kufanya kila kitu sambamba na kanisa ambayo nimekuwa nikihudhuria.”
Mwanafunzi anawaambia wanaume, “Si hisi kama ni sawa kulisha Meza ya Bwana tukiwa kwa mgawanyiko kama huu. Tumeyasikia maoni ya kila mtu. Ninawauliza wachungaji viongozi kufunga na kuomba na kukutana tena ili kumaliza mgawanyiko huu.”
Siku  chache  baadaye  wachungaji  viongozi  wanakutana  na  Bwana  Pumbavu  na  wafuasi  wake.  Wanaomba  na  kuimba. Mwanafunzi anamwomba Pumbavu, “Tafadhali tuambie ni mabadiliko gani hasa unataka kuingiza kwa mkutano, mbali na kuingia mahali pangu kama kiongozi mkuu.”
Bwana Pumbavu anaanza kunena, lakini Yakobo anamkatiza kusema, “Wacha niseme ukweli. Wengi wetu hatutaki yale Bwana Pumbavu anataka. Anataka tumwite mchungaji wa kanisa hili punde tu Mwanafunzi akisha ondelewa, ijapokuwa hata yeye pia haja hitimu kutoka chuo cha masomo cha kiseminari ya thiolojia. Kile sisi tunataka ni kufuata mfumo wa kanisa letu tulilotoka. Tunapenda mtindo wao wa kuabudu. Wana vyombo vikubwa vya kuabudu na kila mara wanakodi ukumbi kufanya mikutano mikubwa ya uinjilisti, na wana waimbaji maarufu na wanamuziki wakulipwa.”
Bwana Pumbavu anaongezea, “Tunakosa huu msisimko hapa. Naamini kwamba makosa yote katika eneo hili nzima ni lazima yafuate mwongozo na utaratibu mmoja, kwa minajili ya umoja.
Viongozi wachungaji wote wanakataa mara moja. Mwanafunzi anaeleza yale amejifunza toka kwa hiyo mizozo miwili katika Matendo 15. Anasema kwa upole, “Ninafurahi kwa kuwa huu mzozo si juu ya amri za Yesu. Huu ni mzozo juu ya njia tofauti tofauti za kufanya huduma. Mhubiri umpendaye anatumia utaratibu tofauti kufanya uinjilisti. Mimi sina kipaji chake. Mkutano wetu si
wakwasi wa kutosha kutumia utaratibu wao. Utaratibu wetu wa uinjilisti unafanya kazi vyema katika jamii yetu. Viongozi wetu na
zaidi ya watu wanapenda kuendelea kutumia utaratibu huu hapa wenye Mungu amekuwa akibariki. Huu utaratibu ni rahisi kwa watu wetu kufuata. Hatuwalaumu watu wa Kanisa la kwanza la Yakobo wanaomfuata mhubiri wao na kutenda mambo kama yeye. Hatuwaulizi wabadilike. Karibu sisi zote tunakubaliana juu ya hili sasa. Hebu tuombane msamaha kwa kulaumiana kwa ajili tu ya kutamani utaratibu tofauti.”
Viongozi wanasema, “Amina.”
Mwanafunzi anaeleza, “Kanisa la kwanza kule Yerusalemu walikutana kila siku kwenye uwanja wa hekalu la Kiyahudi na nyumbani mwao. Kila mara walikula pamoja, walishiriki mali zao na waliwasaidia maskini. Walikuwa kama familia ya upendo. Makutano katika siku za mitume mara kwa mara walituma wageni kwa makutano wale wengine kuwatia moyo. Walisuluhisha tofauti
zao kwa upendo badala ya kulaumiana. Wakati makutano ya mataifa walifuata utaratibu tofauti, waliendelea kuwa na ushirika pamoja
na makutano ya Wayahudi. Waliruhusu kila utamaduni kufuata desturi zao mradi tu waheshimiane na kutii amri za Kristo. Twaweza fanya hivyo hivyo.” Wanafungua Maandiko na kulinganisha tofauti kati ya kanisa la Kiyahudi kule Yerusalemu na mkutano wa Mataifa kule Kaiseria, katika Matendo Sura 2 na 10. Pia wanafikiria  jinsi mkutano wa mataifa kule Galatia ulitofautiana na ule wa mkutano wa Wayahudi.
Bwana Pumbavu  anaondoka, lakini Yakobo  anakiri, “Sikujua  Biblia inaruhusu  tofauti hizi kuweko kwenye makutano. Na sikuwahi pambanua kati ya utaratibu utofautianao na amri za msingi zipatikanazo kote ulimwenguni ambazo hazibadiliki. Kwa hivyo niko tayari kufuata ushauri wa wachungaji viongozi na kumkubali Mwanafunzi kama kiongozi wangu. Utaratibu wake ni tofauti na
ule wa mchungaji wangu wa kwanza, lakini naona sasa kwamba hili si swala la muhimu.”

Kazi ya Kufanya

42
Hadithi Za Mchungaji

•    Panga njia za kuongeza nguvu ushirika wa mkutano wako, na kati ya makutano.
•    Unaweza ratibishia ushirika michezo au kujivinjari kwa aina nyingine ili kuleta furaha kwa ushirika wa kikundi au mkutano wote.
•    Ratibisha nyakati za ushirika na makutano wengine, na watumikie wanapohitaji msaada.
•    Wakati mizozo inatishia umoja wa mwili wa kanisa, ratibisha mkutano kuwasikiliza wale wanataka kuongea. Halafu wacha wachungaji viongozi wafikiri juu ya hilo, omba na kupendekeza la kufanya.
•    Usiwatambue watu kuwa wachungaji viongozi ila kwa kweli wawe wanawachunga wengine. Hili linaweza kuwa kama viongozi wa kundi dogo. (1Petero 5:1-4)
•    Wafunze viongozi umuhimu wa kumsikiza kila mtu na kuafikiana kimaombi.
•    Kuwa na uhakika kwamba hatua unayopendekeza inahakikisha mara moja utii kwa amri yoyote  ya Yesu inayohusiana na hiyo hatua, na kwamba sio tu kuwapa mamlaka na uthibiti zaidi juu ya wachache.


III-8—Huduma ya 8

Tembelea na Kushauri.

Mwanafunzi anafuata mfano wa Bwana Hekima wa kutembelea viongozi wapya anaowafundisha mara kwa mara. Nyumbani mwa Msaidizi, anauliza, “Je, mkutano wako unaendeleaje?”
Msaidizi anajibu, “Nina wasi wasi. Familia ya Mlezi wana malaria tena. Amevunjika moyo. Mwanawe pia alivunjika mguu. Mkewe ana huzuni na anakaa akilia na kuangalia tu juu. Je, unaweza waongelesha?”
Wanaitembelea familia ya Mlezi na wanashangazwa kumpata Bwana Pumbavu huko. Anamwambia Mwanafunzi, “Mkewe
Mlezi, Karmeni, ni dadangu. Nilikuja kumwomba shemeji yangu mkopo kwa sababu mauzo yangu yamekwenda chini sana hivi karibuni. Lakini amepoteza kazi yake ya walimu kwa sababu ya ugonjwa wake. Labda unaweza nisaidia.”
Mwanafunzi anamwambia kwa uthabiti, “Nimekwambia mara kadhaa kwamba mimi sitoi mikopo. Mlezi na Karmeni ndio wanaohitaji msaada.”
Bwana Pumbavu anamwambia Mlezi mbele ya mkewe Karmeni, “Mnapata shida hizi kwa kuwa wewe na mkewe mmetenda
dhambi sana. Ninyi hamjaokolewa kweli na Yesu kwa sababu ikiwa mngekuwa Wakristo wa kweli hamngeteseka sana hivi.” Karmeni anakimbia toka mle chumbani akilia kwa sauti kubwa.
“Ninakataa kuyasikiza haya!” Mlezi anapiga mayowe. Anatoka nyumbani. Mwanafunzi na Msaidizi wanamfuata. Anawaambia, “Bwana Pumbavu amevuruga familia yangu sana. Tunaondoka kanisani.”
Msaidizi anajaribu kumpembeleza aendelee kushiriki lakini hakusikiza. Mwanafunzi anarudi nyumbani na kuomba na Sara. Anaharakisha kwenda nyumbani mwa Bwana Pumbavu na kumkemea, “Familia ya dadako Karmeni imeondoka kwa mkutano kwa
sababu wewe umewavunja moyo.”
“Ninafurahia!” Bwana Pumbavu anajibu, “Kanisa li heri bila huyo mtu katili. Karmeni asingemuoa.”
Mwanafunzi anahisi hasira lakini hasemi lolote. Siku ifuatayo anarejea kumtembelea Msaidizi na kumtia moyo. Anachukuwa somo ambalo Bwana Hekima alikuwa ametoa, kushughulikia Wakristo waliovunjika mioyo. Anampata Msaidizi nyumbani mwake anacheza wimbo wa huzuni kwenye gitaa yake. Mwanafunzi anamsomea, “Huduma ya msingi ni kuwatembelea watu wetu na kuwashauri. Hapa kuna njia za kutumika kusaidiana kumtumainia Mungu na kufurahi, hata wakati maisha ni machungu. Roho wa Mungu anaitwa Mshauri. Jifunze kuhusu Nabii aliyevunjika Moyo, kuvumbua jinsi Mungu alimsaidia.”


Tafuta 1 Wafalme 19:1-18
Zoezi.
•    Je, ni kwa nini Eliya alivunjika moyo? Soma Sura ya 18 pia ikiwa unataka kujua hadithi nzima.
•    Ni msaada upi ambao Mungu alituma kwanza, kumsaidia Eliya?
•    Je, ni maneno gani ya kwanza yenye Mungu alimwambia Eliya kwenye pango?
•    Je, Eliya alitambuaje kuwa Mungu alikuwa akiongea naye?
•    Je, Mungu alimwambia Eliya afanye nini, kumtia moyo?
Recho anawaletea chai Mwanafunzi na Msaidizi wakiendelea kujifunza kutoka kwa hilo somo, “Hata manabii wajasiri wa Mungu walivunjika moyo. Mungu alimpa Eliya nguvu za kufanya miujiza mikubwa, lakini malkia Yezebeli akatisha kumuua, akatoroka, akihofu. Alitorokea mbali na mwili wake ukachoka. Alimwacha mtumishi wake nyuma na akaenda pekee yake, ambalo lilikuwa kosa.
Alihitaji rafiki. Alitaka afe. Sehemu ya kuvunjika kwake moyo ilitokana na uchovu wa mwili wake. Mungu akatuma malaika akiwa na
chakula na maji na akamwacha alale hadi mwili wake upate nguvu. Halafu Mungu akamwongelesha. Maneno ya kwanza ya Mungu yalikuwa swali, “Kwa nini uko hapa?” Mungu alimsikiza Eliya kwanza. Mungu alitumia sauti ya upole, tulivu kumnong’onezea Eliya, si dhoruba ya hasira. Mwishowe, Mungu alimpa Eliya sababu ya kuishi. Alimpa Eliya kazi ya kufanya na matumaini mapya katika nguvu zake.”
Wakasoma 1 Wafalme 19 tena. Mwanafunzi anasema, “Tutafuata mfano wa Mshauri Mkuu. Tunapojua kwamba watu wamevunjika moyo, tunawatembelea. Kwanza, tutafute kama kuna sababu ya kimwili inayosababisha shida yao. Je, wamechoka, wana njaa, wagonjwa? Ombea uponyaji na uhudumie hahitaji yao ya kimwili. Halafu uliza maswali upate nini mbaya. Sikiza kwa uvumilivu kwa sababu ya kweli ni kwa nini watu wamevunjika moyo au wanaangaika. Kuwa mpole. Mungu anawanenea watu

43
wanaougua kupitia upendo wetu, bali sio kwa hasira yetu.”
Msaidizi anasema, “Ninahitaji kufanya hili kwa ajili ya Mlezi na familia yake. Ninapaswa kuongea faraghani naye, kama vile
Mungu aliongea na Eliya, kwa sauti ya upole.”
Msaidizi anasoma kutoka kwa funzo, “Usiwahi rudia kwa wengine ripoti mbaya ambazo umesikia, isipokuwa unauhakika kabisa ni za kweli na hasijatiwa chumvi. Epuka udaku. Wape waumini waliovunjika moyo matumaini kwa kuwakumbusha wao ni nani katika Kristo. Waulize waseme maneno ya kutia moyo yaliyomo Waefeso 1:3-14 kwa sauti na wadai hii ahadi ya thamani. Hebu wasome mistari hii ama warudie baada yako. Mara nyingi wana dhambi maishani mwao ambazo hawajakiri kwa Mungu. Wasaidie wakiri dhambi zao. Wasaidie wamsamehe yeyote ambaye amewakosea, hasa watu wa familia yao. Wahakikishie msamaha wa Mungu. Mwishowe, wasaidie wapate njia za kumtumikia Mungu, hata katika hali ngumu.”
Msaidizi analiweka chini somo na kushangaa, “Ndio, nitafanya hivi! Nitapanga huduma ya kutembelea na kushauri katika mkutano wetu. Ninakutana na wafanyikazi wetu usiku wa leo. Tafadhali baki unisaidie, Mwanafunzi!”

Zoezi
Tafuta katika Waefeso 1:3-14 ahadi kadhaa za thamani za kuwatia moyo waumini katika Kristo.
Huo usiku Msaidizi anaelezea wafanyikazi-wenza kwenye mkutano wapya, “Watu wetu wanakabiliwa na shida ambazo tunaweza tu maliza kwa kuwatembelea nyumbani kwao. Wengine wamo kwenye mapambano na watu wengine, kwa kawaida, ni mtu kwenye familia zao. Wengine ni wagonjwa, wakongwe na dhaifu, au hawana ajira. Wengine wanang’ang’ana na ulevi, madawa ya kulevya au shida za ngono. Waumini wengine wapya hawana uhakika na wokovu wao na mahala pao kwa kanisa la Kristo. Wengi wana marafiki na jamaa ambao hawaja mjua Yesu. Hebu tupange ili kila muumini mpya anatembelewa mara kwa mara na mtu mwingine. Tafadhali, Mwanafunzi, tuambie la kufanya.”
Mwanafunzi anashauri kwa hekima, “Wewe ndiwe kiongozi hapa. Unajua la kufanya. Waambie.”
Msaidizi analiambia kundi, “Nendeni wawili wawili. Waume watembelee waume na wake watembelee wake. Epuka udaku. Mabwana na wake zao waweza kuzitemblea familia pamoja. Omba na watu unaotembelea. Tumia hadithi ambazo nimewafundisha, kuwaelezea watu juu ya Yesu na msuluhishe shida zao. Ninyi waumini mliokomaa zaidi, nendeni na waliowachanga kutembelea marafiki zao wasiookoka, na mwasaidie waumini wapya wajifunze haraka yale ya kusema. Kumbuka sisi zote ni wachungaji kama Yesu, Mchungaji wetu Mkuu. Sisi zote tunalea kondoo wake kwa upendo na huruma. Iweni wenye huruma! Msiwakatize watu wakiwa wanakula au wanafanya kazi. Iweni wasafi, wenye heshima na wapole. Waonyesheni Yesu vile alivyo.”
Msaidizi  na  Mwanafunzi  wanaitembelea  familia  ya  Mlezi  ambayo  ilishaondoka kwa  mkutano.  Tena  Msaidizi  anamwuliza
Mwanafunzi aongee na familia ya Mlezi lakini Mwanafunzi anakataa, akisema, “Wewe ndiwe mchungaji wao.” Msaidizi anaiambia familia ya Mlezi jinsi Ayubu aliteseka.
“Marafiki  wa  Ayubu  walijaribu  kumfariji  wakati  alikuwa  mgonjwa,  amefiwa  na  anaugua,  lakini  walimuongezea  tu  shida. Walizidi kumwambia kwamba aliteseka kwa sababu alikuwa mbaya. Ayubu alitaka kumwuliza Mungu kwa nini aliteseka hivyo, kwa
sababu aliwaona watu waovu wakiishi kwa raha. Hebu nikufafanulie Jinsi Walewanaougua Wanaweza Farijika.”


Tafuta Yakobo Sura 1 na 2:
•    Je, Mungu aliijaribuje imani ya Ayubu?
•    Je, Ayubu alielewa kwa nini Mungu alikuwa akimjaribu? Sasa tafuta katika Ayubu Sura ya 38 na 42:
•    Je, Mungu alimjibuje Ayubu?
•    Nini kilimtendekea mwishowe?
Zoezi
Kwenye nyumba ya Mlezi, Msaidizi anamfariji yeye na Karmeni. “Mateso huja kwa ajili ya sababu nyingi. Tunajiletea mateso kwa maana tunafanya vitu vya upumbavu. Mungu pia hutumia mateso kutukosoa, kutusaidia tumkumbuke Yeye, au kutupeleka nyumbani mbinguni. Anaruhusu mateso kutujaribu na kuimarisha imani yetu. Wakati mwingine anatuponya kwa nguvu zake. Wakati mwingine anatuonyesha nguvu zake katika udhaifu wetu, jinsi Paulo aliwaambia kanisa la Korinto.”
Karmeni na watoto wanaenda kulala, lakini Mlezi anataka kujifunza zaidi. Msaidizi anafafanua nia ya Paulo kwa Mateso.”


•    Tafuta katika 2 Wakorinto 1:3-7 chanzo cha faraja yetu:
Zoezi.
•    Tafuta katika 2 Wakorinto 4:7-12 kile maumivu mwilini mwa muumini inaonyesha.
•    Tafuta katika 2 Wakorinto 12:7-10 sababu iliyofanya Mungu aruhusu Paulo kuteseka.
Msaidizi anaendelea kuomba na Mlezi na kumfariji, “Mungu hapendi tuteseke. Yesu alikuja kuchukua mateso yetu kwa mabega yake. Tukimwamini Mungu, ataleta kitu kizuri kutoka kwa mateso yetu, jinsi alivyoleta uzuri kutokana na mateso ya Yesu, Paulo na Ayubu. Sasa hebu nieleze juu ya Mwanamme Kipofu ambaye hakuna Mtu alimwamini.”

Zoezi.
•    Tafuta katika Yohana Sura 9 baina ya mambo mazuri yaliyotendeka kwa sababu ya upofu wa huyo mtu.
•    Tafuta Yakobo 5:13-20 maneno ya wasia kwa watu manaopitia wakati mzuri na mgumu.
•    Tafuta katika Waebrania 12:5-12 sababu maalum kwa nini Mungu anawaadhibu waumini wanaozidi kutenda dhambi.
Wanapoondoka nyumbani mwa Mlezi, Mwanafunzi anamwambia Msaidizi, “Ulishauri vyema. Nilijua utaweza. Ndio sababu nilinyemaza.”


44
Hadithi Za Mchungaji

Siku iliyofuata Msaidizi anamchukuwa mkewe Sara kumtembelea mkewe Mlezi Karmmeni. Recho pia amesoma juu ya kutembelea na kushauri. Anaelezea Karmeni, “Mateso yako hayamaanishi Mungu amekuacha.”
Baadaye wanakutana pamoja kujaribu kutafuta chanzo cha kuvunjika moyo kwao. Mlezi anasema, “Ninajua chanzo. Niliiacha familia yangu ikasahau uaminifu wa Mungu. Hatujakuwa tukiomba kama familia. Hebu tuombe pamoja sasa na tumuulize Mungu alete uzuri toka kwa mateso yetu, jinsi alivyomfanyia Ayubu.”
Washirika wengine toka mkutano wa Msaidizi wanailetea chakula ile familia na wanaendelea kuisaidia kwa siku kadhaa. Imani
ya hiyo familia inapata nguvu na wanarudi kwa mkutano. Punde Mungu anaponya magonjwa yao ya kimwili pia. Mlezi anaanza kuwatembelea wengine na kuwaambia juu ya Yesu na kuwafariji. Anapenda kuelezea wale anasaidia, “Mungu alitumia mambo mabaya kuleta mambo mazuri kwetu.”
Wakati wa ibada Msaidizi anatangaza, “Mkutano unatambua malezi ya huruma ambayo Mlezi na Karmeni wanawapa wengine wengi. Sasa tutawawekea mikono kuwatuma kama mashemasi, kama katika Matendo 6.” Kundi linashangilia.

Kazi ya Kufanya
•    Endeleza huduma ya kutembelea na kushauri wale wana shida. Tafuta watu kwa mkutano wako wanaopenda kushauri wengine.
Wafundishe kuwatia moyo na kuwahimiza, ukitumia hadithi zilizomo kwenye sehemu hii.
•    Orodesha kwamba kila mtu anatembelewa mara kwa mara, hata kama hawana shida.
•    Wafunze waumini wapya kutii amri za msingi za Yesu, ambazo zimeorodheshwa katika Sehemu ya I
•    Enenda na waumini wapya kuwasaidia kutembelea na kuwashuhudia marafiki zao wasiookoka.
•    Toa malezi maalum kwa wazee na wadhaifu, wagonjwa na wenye mahitaji mengine.


III-9—Huduma ya 9.

Weka Ndoa na Imani ya Familia Nzima Nguvu.

Bwana Pumbavu anawasili nyumbani mwa Mwanafunzi na mkokoteni, akionyesha vitu kadhaa vya kuuza. “Tazama hizi,”
anasema, “Aina mpya ya batri ambazo hazitawahi isha moto. Nunua sanduku lote la kumi na mbili kwa taa yako.” Mwanafunzi anauliza, “Ikiwa haziishi moto, kwa nini ninunue nyingi hivyo? Je, umefunikia nini chini ya hiyo nguo?” “Vyombo vyangu binafsi.” Mwanafunzi anaondoa hiyo nguo na anapata sanamu, aina yenye watu huabudu kama miungu.
“Hivi ni mapambo tu ya kupamba nyumba yangu!” Bwana Pumbavu anajitetea.
“Kwa nini basi ukavificha?”
“Nilijua hutakubali! Una akili ndogo! Ikiwa ungekuwa na imani kubwa ungejua kwamba sanamu si kitu na usingeteta juu yake. Nina imani kubwa, kwa hivyo ninaweza uza hizi sanamu bila shida.”
“Sielewi akili yako,” Mwanafunzi anajibu, “Kafiri wanaozinunua huzitumia kwa kuabudu.”
“Wewe hauna imani ya kweli. Hakuna mtu kanisani mwenye imani ya kweli isipokuwa mimi. Watu wako wanafaa kuwa wanaishi maisha mazuri, lakini karibu familia zote zina shida. Waume wanapigana na wake wao na wanawaacha watoto wao. Hawana imani! Mimi naitunza familia yangu vizuri. Mke wangu asipofanya kile nasema, nampiga!”
Mwanafunzi anajibu, “Ni kweli kuwa familia zetu zina shida, na inaonekana yako pia ina shida. Nilimwambia Bwana Hekima kwamba tunahitaji kuweka nguvu imani za familia nzima. Aliniachia somo hili juu ya Abrahamu mtu wa imani. Hebu tulisome. Lakini kwanza, ahidi kuwa hautauza hizi sanamu.”
Bwana Pumbavu ananung’unika, “Vile unasema. Sitauza tena baada ya haya. Sitaki shida na kanisa langu.”
Mwanafunzi anaendelea, “Vyema. Sasa hebu tusome juu ya Abrahamu Mtu wa Imani kuvumbua imani ya kweli ni nini. Mungu alimwahidi Abrahamu kuwa atabariki mataifa yote kupitia mmoja wa wazao wake. Huyo ni Yesu. Abrahamu aliamini ahadi hiyo.”

Zoezi.
Tafuta Mwanzo 21:1-7 nani alifanya iwezekane kwa Mkewe Abrahamu mzee na tasa Sara kupata mototo. Tafuta katika Mwanzo 22:1-18:
•    Je, Mungu aliijaribuje imani ya Abrahamu?
•    Mungu alimwokoaje mototo wa Abrahamu?
•    Ni ahadi gani ambayo Mungu alimpa Abrahamu kwa sababu alimtumainia Yeye?
Bwana Pumbavu anajiegemeza kwenye mkokoteni wake mbele ya nyumba ya Mwanafunzi akiwa kimya kwa muda mchache. Halafu anasema, “Abrahamu alikuwa na imani kuu kuliko vile mtu yeyote anaweza kuwa nayo hivi leo. Yeye na mkewe walifanya hivyo zamani sana. Sisi tunakabiliana na shida tofauti siku hizi.”
Mwanafunzi anajibu, “Mfano wa Abrahamu unatumika hata kwetu leo hii. Mungu alimpa mwana, ambaye kupitia kwake ahadi ya kubariki mataifa yote ingetimia. Hiyo inatuhusu sisi. Aliijaribu imani ya Abrahamu kwa kumwambia amtoe mwanawe sadaka, kwa kumuua madhabahuni. Abrahamu alimtumainia Mungu vya kutosha hadi kumtii, na Mungu akaokoa Isaka kwa kutuma kondoo ya kiume ambayo aliwawa mahali pake. Huu ulikuwa mfano, unabii, wa jinsi Yesu angekufa mahali petu miaka 2,000 baadaye. Kupitia kwa Yesu, ambaye ni uzao wa Abrahamu, Mungu alitimiza hiyo ahadi ya kubariki familia zote za dunia.”
“Hata angenibariki na mauzo kidogo.”
“Juu ya kumpiga mkeo, hilo sio sawa. Mungu aliumba ndoa na aliiumba ikiwa nzuri. Anatupa watoto wetu na anawabariki.

45
Tukiufuata Mwongozo wake wa Familia, tunaishi kwa amani.”


Soma Waefeso 5:21-33 kupata:
•    Kwa nani ndio wake Wakristo wananyenyekea?
Zoezi.
•    Je, bwana Mkristo anapaswa kufanya nini kustahili unyenyekevu wa mkewe?
•    Kwa kiwango gani mme anapaswa kumpenda mkewe?
•    Je, ndoa ya Kikristo ni mfano wa nini? Soma Waefeso 6:1-3 kupata:
•    Jukumu la watoto katika nyumba ya Kikristo ni nini?
•    Jukumu la wazazi ni nini?
Mwanafunzi anamweleza Bwana Pumbavu, wakiwa wamesimama kando ya mkokoteni wake nje ya nyumba ya Mwanafunzi, “Maandiko yanatuambia kwamba mwanaume na mwanamke wanapaswa kuwaacha wazazi wao kuungana kwa ndoa. Ni lazima waaminiane maisha yao yote. Mme lazima ampende mkewe vile anajipenda mwenyewe. Mke lazima amheshimu mmewe na anyenyekee kwake. Mme hatamtawala mkewe kwa maneno ya hasira na vitisho. Badala yake, Paulo anawaambia wanyenyekee kila mmoja kwa mwingine. Ikiwa mme anampenda mkewe na anaitunza familia vyema, mke atamfuata kwa furaha.”
Bwana Pumbavu anakatiza, “Hilo linatumika wakati wote wawili mke na bwana ni Wakristo. Mke wangu si Mkristo. Ni mjinga. Ninapanga kumpa talaka na nioe msichana barubaru Mkristo! Ndipo watoto wangu watakuwa na tabia njema!”
Mwanafunzi anaeleza, “La! Paulo anatwambia katika 1 Wakorinto 7:10-16 kuishi na wenzetu wasioamini ikiwa wanapenda.
Anawaambia waumini ambao hawajaoa kuoa tu wafuasi wenzao wa Kristo. Paulo pia anatwambia jinsi ya kuwafundisha watoto wetu.” Mwanafunzi anaanza kusoma fungu hili lakini Bwana Pumbavu anaondoka.

Jinsi ya Kuwafundisha Watoto Kuwa na Imani Katika Kristo.
Kwa mkutano uliofuata Mwanafunzi anauambia mkutano wake, “Ni lazima tuweke maisha ya familia zetu nguvu. Paulo anawambia  watoto  katika  Waefeso  6:1-4  kuwatii  wazazi  wao  katika  Bwana  ili  wapate  kuishi  maisha  marefu  na  ya  baraka.
Anawaambia wazazi kuwafundisha watoto wao vyema, si kuwakasirisha kwa kuwapa amri ambazo hawawezi kutii kwa urahisi. Wazazi wema huwafunza watoto wao jinsi ya kuzitii. Unawezatumia hadithi toka kwa Biblia kuwafundisha kuomba na kutii mari za
Yesu. Kila familia inapaswa kupanga ibada ya familia kuabudu nyumbani mara kwa mara. Hebu tujifunze juu ya Wana Wazuri na
Wabaya Wa Kuhani Eli.”


Tafuta katika 1 Samweli sura ya 3:
Zoezi.
•    Je, kwa haraka gani Samweli alitii alipofikiri ni Eli alikuwa akimwita?
•    Je, ni nini Eli alishindwa kufanya na wanawe waasi?
Mwanafunzi anaendelea kuelezea mkutano kwenye nyumba yake, “Mungu alimwonya Eli awarekebishe wanawe. Kama Kuhani Mkuu wa Israeli, Eli alikuwa anatoa mfano mbaya kwa taifa nzima. Wanawe walikuwa wakitumia vibaya nafasi na mamlaka yao kwa kuwaibia na kuwatesa watu, lakini Eli hakufanya lolote kuwakataza. Kwa sababu Eli hakuwarekebisha wanawe, waliangamia wote. Wazazi wa Samweli, kwa upande mwingine, walimfundisha Samweli kutii mara moja na kwa furaha. Mungu alimbariki maisha yake yote kwa utiifu wake.”
Mwanafunzi anawauliza watu waongee juu ya yale wanapanga kufanya kuzitia familia zao nguvu. Yakobo, ambaye amekuwa mwaminifu kwa Mwanafunzi na anakua haraka katika Kristo, anaitikia, “Kama wazazi, tuna walinda watoto wetu toka hatari za kiroho  kwa  kuwafundisha  wakiwa  bado  wachanga.  Tunawaelezea  yale  tunataka  wafanye.  Tunawataraji  kutii  kwa  haraka  jinsi Samweli alivyofanya. Wasipotii haraka na kwa furaha, tunawakosoa. Je, ninyi wamama mnakubaliana nami?”
Baada ya muda wa kimya Sara anajibu, “Ninakubali, Yakobo. Watoto wachanga sana hujifunza haraka tunapowarekebisha mara moja na kimwili, jinsi Methali 13:24 inasema. Watoto wakubwa wanapokataa kutii na tunawanyang’anya kitu wanachopenda kwa muda, wanajifunza kututii. Ni lazima tuheshimu watoto wetu na tusiwapigie kelele au kuwatusi. Tusiwasahihishe kwa hasira au tutawajeruhi. Na tunahakikisha wazazi wote wawili wanafundisha sheria sawia.”
Dibora anaongea kwa mara  ya kwanza kwa  mkutano kama huu.  “Inatupasa kuwafundisha watoto wetu kwa mfano  wetu. Tunawafundisha kuepuka ulevi na upendelevu. Tunawaonyesha jinsi ya kuchagua marafiki ambao hawatawaingiza kwa maovu. Tunawaonyesha kuwa na bidii, kufanya kila kitu kwa bidii, kwa njia sawia na ile ungelimfanyia Bwana. Tunawafundisha namna ya
kutumia Neno la Mungu maishani mwao wenyewe.”
“Bora sana!” Mwanafunzi anashangaa. “Hapa kuna hadithi juu ya familia katika Biblia. Ni rahisi kuwafundisha watoto. Ninyi wazazi mnawezafunza watoto wenu ukweli wa thamani toka kwenu. Waambie watoto wenu na kwa watoto wengine ambao wazazi wao si Wakristo.”


Tafuta katika Mwanzo sura 24 jinsi Mungu alimpa Isaka Mke.
Zoezi
Tafuta katika Mwanzo 29:1-30 kile Yakobo alifanya kuthibitisha pendo lake kwa Recho. Tafuta Matendo 7:9-14:
•    Je, Yusufu alifanya nini kuonyesha kwamba aliwasamehe nduguze ambao walimuuza kama mtumwa?”
•    Je, Mungu alitumiaje mateso ya Yusufu kuiokoa familia yao toka janga la njaa?


46
Hadithi Za Mchungaji

Tafuta katika Luka Sura 1 na 2 ni katika familia gani Yesu alizaliwa.
Mwishoni mwa mkutano kwenye nyumba ya Mwanafunzi, Sara anauliza wamama wangojee kidogo. Anawaambia, “Mwanafunzi amenisaidia kuwa mwalimu wa watoto. Anataka kuorodhesha hadithi za watoto na kuwasaidia kuwasilisha moja kwa mkutano kila juma kwa njia ya kuigiza.”
Mwanafunzi anaongezea, “Hebu tuwaulize babazao pia washiriki. Hadithi hizi zina nguvu wakati watu wazima pamoja na watoto wanashiriki.”
Sara anaomba, “Wale baina yenu ambao wangependa kuwafundisha watoto, tafadhali saidia. Tutajiandaa kwa pamoja kila juma. Tunawataka watoto wawe na furaha na heshima wanapojifunza. Ikiwa wanaume wanashiriki pia, hiyo itakuwa hata bora zaidi.
Tunahitaji msaada wako kwa hilo Mwanafunzi.”
Mkewe  Yakobo  anawaambia  watoto  wake,  “Kuanzia  kesho  tutakuwa  tukiomba  pamoja  kama  familia  kila  asubuhi  kabla hamjaenda shuleni.”

Kazi ya Kufanya
•    Saidia familia katika kanisani mwako kufuata mfumo wa mamlaka wa Mungu katika familia.
•    Saidia familia yako kupanga nyakati za kusoma Neno la Mungu, kuimba, na kuomba pamoja.
•    Wafundishe wazazi kuwarekebisha watoto wao kwa upendo.
•    Orodheshea watoto kusikia Hadithi za Biblia, halafu waziigize na kushiriki katika ibada.
•    Waulize watu wazima pia kuigiza hadithi za Biblia wenyewe au pamoja na watoto.


III-10—Huduma ya 10

Lea Wagonjwa, Maskini na Wanaoteswa

Dibora,  jirani  ya  Mwanafunzi,  anawasili  nyumbani  mwake  mapema  asubuhi  kumwambia,  “Mkoi  wangu  Yusufu  yuko korokoroni! Ulimsaidia kuanza mkutano wapya hapa mjini. Huwa wanakutana nyumbani mwake. Serikali mjini mwake wanachukia Ukristo. Ana watoto tisa na wanakufa njaa.”
Mwanafunzi na mkewe Sara wanachukua gunia la mchele na vyakula vingine na kumpelekea mkewe Yusufu, Lisa.
“Yusufu yuko korokoroni,” Lisa anawambia, “Wanaenda kumfikisha mahakamani kumhukumu kwa kufanya mkutano bila idhini. Mwanafunzi, unaweza nisaidia kupata wakili? Sijui jinsi ya kushughulikia hili. Niwie radhi nikiwatengenezea chai.”
Lisa anaenda kwa jikoni ndogo na Sarah anamnong’onezea, “Haya maswala ndio ulisema utatelekezea wengine. Wengi wa watu kwenye mkutano wetu ni maskini. Wengine hawajasoma. Wewe na mimi pekee yetu hatuwezi tunza watoto wote.”
Mwanafunzi anapiga kite, “Unasema ukweli. Tunahitaji kuwauliza watu katika mkutano wetu kushughulikia maswala haya.
Mmoja wa wajane anahitaji kukarabati nyumba yake na huyu mke anahitaji msaada wa kupata wakili wa kumtetea Yusufu.”
Wakati wanarudi, wote wawili Msaidizi na Bwana Pumbavu wanawangojea nyumbani mwa Mwanafunzi. Bwana Pumbavu analalamika, “Mwanafunzi, tafadhali nikopeshe pesa za kutosha kununua kipaza sauti ili nitangaze kile ninauza. Itaongeza mauzo yangu na nitakurudishia mwezi ujao.”
“Nimekukataza kuomba mikopo!”
“Kazi yako kama mchungaji ni kuwatunza maskini na wahitaji. Umetutelekeza!”
“Ninawajali maskini sana,” Mwanafunzi anajibu. “Lakini kitu kibaya chenye mtu anawezakumfanyia mtu mzembe ni kumpa tu pesa. Nitafurahi nikikusaidia upate ajira. Wakati huo utaweza kusaidia kutunza maskini, badala ya kuwa mmoja wao.”
Msaidizi anasema, “Ninawafunza makutano wangu kuwatumikia maskini. Nilianza na fumbo la Kondoo na Mbuzi.


Tafuta katika Matayo 25:31-46:
•    Nani ambaye tunatumikia tunapowatumikia maskini?
Zoezi.
•    Nini kinawatendekea wasioamini baada ya wao kufa ikiwa hawawasaidii maskini?
Wakati Sara anampa chai na Bwana Pumbavu katika nyumba ya Mwanafunzi, Msaidizi anafafanua, “Yesu alisema kwamba maskini, wenye njaa, waombolezao, na wasio na hatia wanaoteseka wanapokea baraka toka kwa Mungu. Tunapowatumikia hawa watu, tunamtumikia Mungu. Tunapowaacha watu hawa, tunamkataa Mungu.”

Jinsi Mungu Hutosheleza Mahitaji ya Watu Wake.
Mwanafunzi anaongeza, “Watu maskini, kama kila mtu mwingine yeyote, wanapaswa kuombea mkate wao wa kila siku na sio tu
kuombaomba. Lakini kuombaomba kuna heshima kuliko kuitisha mkopo ukiwa unajua haunuii kurudisha. Hii ndiyo aina ya ujanja sana ya kuiba. Sisi zote tunapaswa kumtumainia Mungu kututoshelezea mahitaji yetu.”
Bwana Pumbavu analalamika, “Hilo ni rahisi sana wewe kusema ukiwa na chakula mezani mwako.”
Mwanafunzi anasema, “Hebu niwaambie jinsi Mungu alivyotunza watu wake, Waisraeli, katika kitabu cha Kutoka. Walikuwa watumwa Misri kwa miaka mingi. Mungu akawatumia nabii aliyeiitwa Musa. Musa akamwambia Farao (mfalme) wa Misri kwamba anawataka watu wake wawe huru. Wakati farao alikataa, Mungu alituma mapigo kumi mabaya sana kwa nchi ya Misri. Mwishowe, Mungu akatuma malaika wa kifo kuua wazaliwa wakiume wa kwanza wote. Musa akawaonya Waisraeli wachinje mwanakondoo na

47
kupaka damu yake kwa milango yao ili kwamba wakati yule malaika anapita, asiwadhuru. Mwana wa farao akafa. Mwishowe aliwaachilia watu wakaenda. Sura chache za kwanza za Kutoka zinahusu haya. Msaidizi, unaweza malizia hii hadithi?”
“Nitajaribu,” Msaidizi ansema. “Waisraeli walitembea toka Misri hadi bahari ya Shamu, na wakasimama. Hawakuwa na mahali pa kwenda. Farao akabadili nia yake na kutuma jeshi liwarudishe. Mungu akafungua njia kavu katikati mwa Bahari ya Shamu Waisraeli wapitie, na wakati Jeshi la Wamisri lilijaribu kuwafuata, bahari ikawafunika. Halafu Waisraeli wakakaa jangwani miaka
arobaini kabla warudi nchi yao nyumbani. Hawakupata chochote cha kula jangwani, na wakati mwingine hawakupata hata maji, lakini
Mungu aliwapa kila kitu walichohitaji. Halafu Mungu akawapa Mana Ya Kimiujiza.”


Tafuta katika Kutoka 16:11-35:
•    Je, ni jinsi gani Mungu aliwalisha watu wake?
Zoezi
•    Je, zawadi ya mana iliwakomesha watu kulalamika na kutomtii Mungu?
Msaidizi anasema hadithi nyingine, wanapokunywa chai katika nyumba ya Mwanafunzi. “Kwa njia kama hiyo, Yesu anawajali walio na mahitaji. Hebu niwaambie Jinsi Yesu Anatoa Mwili wake Kuliwa.


Tafuta Yohana Sura ya 6:
Zoezi.
•    Katika mistari  2-3, Yesu aliwafanyia nini wagonjwa na wenye njaa?
•    Katika mistari 14-27, ni vitu gani viwili ambavyo watu walitaka Yesu afanye?
•    Kwenye mistari 17-21, jinsi gani Yesu alionyesha kuwa yeye ni Mfalme juu ya maumbile?
•    Kwenye mistari 28-40, ni nani ndiye Mkate toka mbinguni na jinsi gani tunaupokea?
•    Kwenye mistari 41-69, tunafanya nini, ili tupate mkate utupao uzima wa milele?
Msaidizi  anaendelea,  “Yesu  aliponya  watu  wagonjwa.  Wakati  wasikizaji  wake  hawakuwa  na  chakula,  aliwalisha.  Watu walimtaka awe mfalme na awape chakula cha bure kila wakati. Yesu angefanya hivyo kwa urahisi. Yeye ndiye Mfalme wa kweli juu ya vyote. Anatawala hata maumbile. Alituliza dhoruba na akatembea juu ya maji. Yesu alijua kuwa chakula cha kimwili hakinge badili mioyo yao. Bado wangekuwa tu mbali na Mungu. Yesu alitaka wapate chakula kinachoshibisha milele. Hiki chakula ni Yesu mwenyewe. Katika Yohana 6 aliwaambia kwamba iliwabidi wale mwili wake, ndio wapate uzima wa milele. Mungu anamtaka kila mtu amwamini Yesu na apokee uzima wa milele toka kwake. Tunapokuwa sehemu ya kanisa, Mwili wa Kristo, anatupa huu uzima.”
Bwana Pumbavu anajibu, “Hiyo ni hadithi nzuri sana lakini hainiongezei chakula kwenye meza ya familia yangu. Kwa heri!”

Mashemasi Wanaonyesha Upendo wa Kristo.
Baada ya Bwana Pumbavu kuondoka, Msaidizi anamwuliza Mwanafunzi, “Je, ninawashughulikiaje maskini kwenye mkutano wangu na mkutano wageni kabisa, bila ya kutelekeza kazi yangu ya kuongoza na kufundisha mkutano?”
“Unapaswa kuichochea moto karama yako ya kiroho ya kufundisha, bila kutelekeza wenye mahitaji. Viongozi wa kanisa la Yerusalemu walikabiliwa na shida sawia na hii. Wajane wengi walihitaji malezi lakini wao walikuwa na shughuli nyingi wakifundisha habari njema. Hebu niwaambie kuhusu Mashemasi wa Kwanza.”


Tafuta katika Matendo Sura 6 & 7:54-60:
Zoezi.
•    Je, Mitume walihakikishaje kwamba wajane wakigeni hawakutelekezwa?
•    Je, mitume walijuaje ni nani wakuchaguliwa kuwatumikia maskini?
•    Stefano alikuwa mtu wa aina gani, mmoja wa wale saba aliyechaguliwa kuwatumikia wajane?
Mwanafunzi anamwelezea Msaidizi, “Mitume hawangewachilia majukumu yao ya kufundisha na kuongoza kanisa Yerusalemu, ili wawashughulikie maskini. Kwa hivyo wakawauliza watu wawachague wanaume saba wenye sifa nzuri, waliojaa hekima na Roho Mtakatifu. Mitume waliwaombea hawa wanaume na wakawawekelea mikono. Wanaume na wanawake waliowashughulikia maskini kwa njia hii waliitwa mashemasi. Mashemasi ni watumishi wa watu wa Mungu. Stefano, mmoja wa mashemasi, pia aliwahubiria Wayahudi wasioamini katika nguvu za Roho Mtakatifu. Uso wake uling’aa na aliona Yesu ameketi kando ya Baba kule Mbinguni. Walimpiga wawe akafa.”
Msaidizi anajibu, “Ninakumbuka yale ulifunza kuhusu Mashemasi. Paulo alimwambia mwanafunzi wake, Timotheo, kwamba mashemasi ni lazima wawe wazazi wazuri na waume au wake waaminifu. Lazima wawe Wakristo waliokomaa wenye sifa nzuri, si wenye tama ya pesa au wenye upendelevu wa vileo. Wanawake wawili waliowatumikia maskini walikuwa Dorkasi, aliyewashonea nguo maskini, na Lidia, aliyewapa kundi la mitume la Paulo mahali pa kulala.”
Msaidizi anapiga kite. “Ninaelewa sasa jinsi ninaweza kwendelea kuongoza kanisa langu wakati bado ninahakikisha kwamba maskini wanapata msaada. Nitaita mkutano kuwachagua mashemasi wa kuwatumikia, jinsi tu walivyofanya waumini wa kwanza.”
Juma moja baadaye Msaidizi anaripoti kwa Mwanafunzi, “Mkutano wangu ulimchagua Mlezi na mkewe Karmeni kutumika kama mashemasi. Tuliwawekelea mikono na kuomba kwamba Mungu atawafanya werevu kama Stefano wanapowatumikia maskini.”
“Ndio. Na tafadhali soma katika Yakobo kupata Jinsi Wazee Wanashughulika na Wagonjwa.”

Zoezi.
Tafuta sasa katika Yakobo 5:13-17 yale wazee wanawafanyia wagonjwa:



48
Hadithi Za Mchungaji

Kazi ya Kufanya.
•    Orodhesha watu katika mkutano na jamii yako wanaohitaji msaada.
•    Omba na mkutano wako juu ya kuwatumikia hawa watu maskini.
•    Amua watu gani katika mkutano wako wanatimiza matakwa ya ushemasi, kuwatumikia maskini kwa niaba ya kikundi.
•    Chagua mashemasi wanaofuata matakwa ya Paulo kwa maombi na kuwekelea mikono.
Mwanafunzi anamwambia Msaidizi, “Tunaweza saidia watu ambao wanateseka kwa kuwakumbusha kwamba Yesu pia aliteseka. Alikuwa binadamu tu kama sisi zote.”
“Nilifikiri alikuwa Mungu.”
“Ndio ni Mungu. Lakini alipozaliwa na Bikira Maria alichukuwa asilia yetu ya kibinadamu. Alijiondelea utukufu na utakatifu wake kama Mwana Wa Mungu na akawa mwanadamu kamili, akiwa na udhaifu wetu wote. Tofauti pekee ni kuwa hakuwahi tenda dhambi. Wafilipi 2:1-11 inaelezea haya. Waebrania 2:17-18 inaelezea kwamba ilimbidi awe mwanadamu ili atumike kama Kuhani wetu Mkuu na kuteswa ili awasaidie pia wanaoteseka.”


III-11—Huduma ya 11

Kuwa kama Kristo na Dumisha Nidhamu Katika Kundi.

Yakobo  anakuja  nyumbani  mwa  Mwanafunzi  na  kumwambia,  “Ndugu  Mwanafunzi,  nimegundua  kwamba  mmoja  wa wafanyikazi wangu, Safira, ananiibia. Safira ni dada katika Kristo. Nilimwongelesha juu ya hili, lakini akakasirika. Je, niipuuze hii dhambi kuzuia mvutano kwenye kikundi?”
Mwanafunzi anajibu, “La, hatuwezi puuza dhambi katika kundi. Biblia inatwaambia tukabiliane nayo haraka. Hebu nimchukue mke wangu Sara, na tutafuata maagizo ya Kristo ya kumwendea moja kwa moja. Huenda pamoja tukamsaidia Safira kutubu. Tutakwenda kwa upendo na upole, kama Wagalatia 6:1 inasema.”
Wanawasili kwa nyumba ya Safira na kuuliza waongee naye peke yake. Yakobo anamwambia. “Nimekukodi umsaidie mke wangu kupika na kusafisha nyumba. Nilikulipa vyema. Lakini uliiba taulo na vitu vingine toka kwetu.”
Safira anatetemeka kwa woga. Sara anamchukuwa kando na kumwakikishia, “Hatupo hapa kukuaibisha. Tunataka wewe upokee msamaha wa Mungu na baraka zake kikamilifu. Kuna kitu unahitaji uelewe kabla tuongee juu ya yale ulifanya. Yesu alitufundisha kwamba baraka za Mungu zinawajilia wale waishio kama Yesu. Hebu tusome Vianzo vya Furaha pamoja.”


Tafuta katika Matayo 5:1-16 ahadi za Mungu kuhusu baraka:
Zoezi.
•    Kwa njia gani Yesu alielezea watu wanaopokea furaha toka kwa Mungu?
•    Je, tunapaswa kujibu aje wakati watu wanatutesa kwa sababu ya kumfuata Yesu?
•    Tunawezaje kumletea Mungu utukufu pitia matendo yetu?
Sara anaelezea Safira juu ya nidhamu. “Sasa kwa vile sisi ni wa Kristo, Roho wake anatupa shauku na nguvu ya kuwa kama
Kristo. Hatutaki tena kufanya mabaya, lakini utu wetu wa asilia wa dhambi unatusukuma kufanya maovu. Tunang’ang’ana kati ya yale utu wetu wa asilia wa zamani unataka na yale maumbile yetu mapya yanataka. Tunapotumbukia dhambini, Roho Mtakatifu anatusadikishia dhambi na anatuleta kwa toba. Pia anatumia wandugu na dada wengine kutuhimiza kutenda haki, kutuita kwa toba na kutuhakikishia msamaha wa Mungu.”
“Lakini mimi ni mtu mbaya. Mimi si mwema kama wewe.”
“Wewe  ni  mototo  wa  Mungu  na  anakubadilisha,”  Sara  anamhakikishia  Safira.  “Mungu  hutukosoa  kama  mama  mzuri anavyokosoa watoto wake katika upendo. Usahihisho unatuweka mbali na hatari. Bila ya usahihisho kwa upendo, mtoto anaweza cheza na moto au sumu, au akimbie mbele ya gari. Mungu anatuokoa toka kwa hatari kwa kutukosoa. Katika Agano la Kale, manabii waliandika vitabu kumi na saba kuwaonya Israeli kuwacha dhambi. Israeli hawakuyasikiza masahihisho ya Mungu na wakatumbukia kwa hatari mbaya sana ya kiroho na kimwili. Sasa tuna Roho Mtakatifu. Anatusaidia kuishi maisha mapya tuliyo nayo katika Kristo. Wakati Kristo alituamuru kutubu na kubatizwa, alikuwa anatwamuru tuendelee kwenye haya maisha mapya. Hebu nikwambie Njia Roho Mtakatifu anatufanya Watakatifu.”


Tafuta Wagalatia 5:16 pitia 6:3:
Zoezi
•    Vitu gani baya ambavyo tunafanya kwa mazoea wakati hatumjui Kristo?
•    Ni matunda gani tisa ambayo Mungu huzalisha ndani mwetu pitia Roho Mtakatifu?
•    Je, tunafanyia nini utu wetu wa zamani wa asilia wa dhambi kuepuka dhambi za dunia hii?
•    Je, tunasaidiaje kuwarejesha waliotumbukia dhambini?
Wanaume wanamwacha Sara aendelee kuongea na Safira. Anaeleza, “Kama wafuasi wa Yesu, tufanya kutii Yesu kwa upendo mazoea yetu ya kila siku. Hili hutupa raha na huleta baraka za Mungu. Pia linatulinda kutokana na hatari za kiroho. Kila siku tunaomba na kutumia Neno La Mungu maishani mwetu. Tunafuata mfano wa Kristo katika matendo yetu na kufanyia mazoezi tunda la Roho. Tunawatii wale walio na mamlaka juu yetu. Hizi ndizo njia za kufanikisha nidhamu kuepuka hatari ya kiroho. Tunapofanikisha haya mazoea, Roho Mtakatifu anatupa nguvu kushinda dhambi.”

49
“Kwangu huo unaweza kuwa muujiza mkubwa sana.”
“Hauko pekee yako. Sisi zote tumelazimika kusulubisha tamaa zetu za kale kwa njia moja na Mungu hutusaidia kila wakati. Katika Agano Jipya, mtume Paulo anatwambia tuwaonye watu dhiti ya hatari za kiroho na kimwili wanapofanya haya makosa:

Kusababisha ugomvi au machafuko
Uzembe
Au udaku                         Ufisadi au ulevi

Tama au wizi                                                         Mafundisho ya kupotosha

Sara anamwakikishia kwa upole Safira, “Mungu atakuweka huru toka kwa mazoea yako mabaya. Tafadhali mwombe afanye sasa.”
Safira analia kwa muda, halafu anamwomba Mungu amsamehe. Anaenda nyumbani mwa Mwanafunzi na Sara na anamwambia muajiri wake Yakobo, “Tafadhali nisamehe. Nitarejesha vile niliiba toka kwako. Nasikitika sana.”
Wakati wa mkutano uliofuata Safira anakiri kwa mkutano, “Nimekuwa na dhambi maishani mwangu. Nilijaribu kuzificha. Hata kuiba. Lakini lilikiri zote hizi na nikapokea msamaha wa Mungu. Natumai ninyi nyote mwaweza kunisamehe.”
Watu wanajibu kwamba watamsamehe, lakini Bwana Pumbavu anakuja kwa Mwanafunzi baadaye na kulalamika, “Hiyo ni rahisi
sana. Wizi ni dhambi kubwa sana. Lazima apate adhabu kabla tumruhusu arudi kwa mkutano. Lazima angoje athibitishe toba yake.” Mwanafunzi anakataa, “La, Bwana Pumbavu. Sisi hatumhukumu moyo wake. Anahitaji msaada wetu sasa kumfuata Kristo.
Anahitaji nguvu za Mungu kuepuka dhambi. Sara anajitolea kuomba naye kila asubuhi kabla aende kazini, mpaka awe na nguvu na ujasiri. Yesu alitufunza tusihesabu ni mara ngapi tunasamehe. Badala yake, tujitolee kusaidiana kuepuka majaribio. Mungu ametusamehe mengi sana kwamba nasi ni lazima tuwe na hamu ya kusameheana kwa shukrani. Ikiwa hatuwezi kusamehe, tunafunga
mioyo yetu toka kwa msamaha mkuu wa Mungu. Mungu hutuokoa kwa neema, si kwa kitu chochote tunafanya kuthibitisha wema
wetu.”
Bwana Pumbavu anadhihaki, “Tunaweza basi kufanya dhambi vile tunataka, kwa sababu Mungu atatusamehe!” “La!” Mwanafunzi anashangaa, “Wazo kama hilo linaonyesha tu kwamba hatujatubu kweli.”

Kuwakosoa Viongozi Kwenye Mkutano
Bwana Pumbavu anamtembelea Yakobo na kumlaumu Mwanafunzi, “Alikuwa na roho nyepesi sana kwa Safira kwa sababu haka kamwizi kadogo ni mwanamke mwenye sura nzuri.” Yakobo anacheka. Bwana Pumbavu anawaambia watu wengine kadhaa kitu
hicho. Punde lawama inaenea kama surua kati ya waumini.
Kwa  mkutano  uliofuata,  Safira  ameketi,  kwa  furaha  anangoja  kusherehekea  Meza  ya  Bwana  pamoja  na  mkutano.  Bwana
Pumbavu anasimama na kusema, “Lazima tusimamishe hiki kipindi. Huyu mwanamke hastahili kula komunyo. Yeye…”
Mwanafunzi anamkatiza. “Nilisoma na Bwana Hekima yale Biblia inasema juu ya kukabiliana na waumini wanaokosea. Ikiwa tunapigana mmoja na mwingine, lazima tusameheane na kupatana kabla ya kula Meza ya Bwana.”
Bwana Pumbavu anauliza, “Lakini itakuwaje kama ni kiongozi wa kanisa ndiye anafanya hilo kosa?”
Yakobo anajibu, “Viongozi wetu wote wanamajukumu makubwa. Ikiwa wametumbukia dhambini, wanaweza kuwajeruhi watu wengi. Neno la Mungu linafundisha kwamba ikiwa kuna malalamishi juu ya mmoja, lazima tuyazingatie kwa makini sana. Kama haya malalamishi yanatokana na udaku, wivu au kiburi, Biblia inasema yapuuzilie mbali. Ikiwa una ushahidi wa kutosha wa kosa, kabiliana
nalo. Ikiwa kiongozi atatenda dhambi hadharani, ni lazima tumsahihishe mbele ya mkutano wote kama onyo kwa wengine. Wakati
mmoja mtume Petero alianguka kwenye makosa na Paulo akamkosoa hadharani. Viongozi wanahitaji kusahihishwa hadharani wanapowaongoza wengine kwa dhambi. Kama sivyo, makosa yao yatasababisha machafuko makubwa. Si kazi rahisi kuwa kiongozi wa Kristo.”

Zoezi
Tafuta katika hadithi ya Ufarisayo wa Petero katika Wagalatia 2:11-21:
•    Wakati Petero alipokuwa anawaongoza waumini kwenye dhambi, Paulo alimkosoaje?
•    Matendo ya Petero yaliendaje kinyume na habari njema ya neema ya Yesu Kristo?
•    Kwa nini Petero alikuwa akitenda kama mafarisayo?
•    Tunaokolewaje, kwa kufuata sheria kwa makini au kwa imani katika Yesu Kristo?
•    Petero alikubali kukosolewa. Hebu zote tufanye hivyo. Tafuta 2 Samweli 11:1-12:25, hadithi ya Siri ya Daudi:
•    Kwa njia gani tamaa ya Daudi kuficha dhambi yake ilimfanya atende dhambi zaidi?
•    Je, nabii alikosoaje siri ya huyu kiongozi?
•    Mungu alimwonyeshaje Daudi kuwa amesamehewa?
Yakobo anaeleza, “Katika hadithi hizi, viongozi walikosolewa. Mtume Paulo alimkosoa mtume Petero kwa kukataa waumini wengine wa mataifa kutokana na kiburi bandia. Petero alikataa habari njema ya Yesu na matendo yake na akawaongoza watu wengine kwa dhambi hiyo. Ijapokuwa Petero alifundisha kwamba tunaokolewa kwa imani katika Kristo, bado alikuwa anatenda kana kwamba
aliokolewa kwa kutii sheria za Kiyahudi. Ilimbidi Paulo amkosoe mara moja hadharani ili mkutano wote uelewe hilo kosa. Nabii
Nathani pia alimkosoa Mfalme Daudi hadharani ili Waisraeli wote waweze kuuchukulia utakatifu wa Mungu kwa uzito.”
Yakobo anamgeukia Bwana Pumbavu na kuuliza, “Je, una ushahidi kwamba mmoja wa viongozi wetu ametenda dhambi ya uzito ya kustahili kukosolewa na mkutano?”
Bwana Pumbavu anasema, “Oh, sahau hayo mambo yote!” Yakobo anamkemea, “Wewe ndiye uliyesababisha huu udaku.”

50
Hadithi Za Mchungaji

Dibora anakiri, “Ninaaibika sasa kwa kuwa nilisikiza udaku, na nikaurudia. Nilimlaumu mchungaji wetu Mwanafunzi, kwa uvumi wa ujinga.”
Yakobo anajibu, “Nafikiri mbwa mwitu mkali, fisi, amejaribu kugawa mkutano wetu kwa kueneza lawama kinyume na kiongozi wetu. Mwanafunzi, tafadhali tusamehe sisi wale tuliosikiza huu uvumi na tukaingia kwenye mtego huo.”
Wanamtukuza Mungu kwa umoja uliorejea, na wanaendelea kwa furaha na Meza ya Bwana. Safira anamwambia Sara baadaye, “Nimeshangazwa na upendo na kukubali kwa mkutano. Sijawahi ona msamaha kama huu kwenye familia yangu. Jinsi neema ya
Mungu ilivyo kuu!”
Mwezi mmjoa baadaye Safira anaripoti kwa Mkutano, “Mkewe Mwanafunzi amekuwa akinisaidia kufanya mazoea ya maombi kila siku na kushinda tabia yangu ya zamani ya wizi. Mungu ameiondoa hiyo tama mbaya toka moyoni mwangu. Hata kuifikiria tu kunanichukiza sasa. Ni furaha kuu kujua kwamba Mungu ameniosha na kunipa moyo safi.”

Kazi Ya Kufanya.
•    Saidia watu waendeleze mazoea ya nidhamu ya kiroho ya maombi kila siku, na kuwasamehe wengine.
•    Tumia hadithi katika sehemu hii kufundisha jinsi ya kukosoa watu kwa upendo.
•    Waelezee watu wako jinsi kukosoa kama huku kunatulinda kinyume na hatari za kimwili na kiroho.
•    Fafanua kwa nini, kwa neema ya Mungu, tunasamehe, kosoa na kurejesha—lakini sio kuadhibu—wale wametenda dhambi.
•    Kosoa kwa upendo wale wanaotenda dhambi. Fuata maagizo katika Matayo 18:15-17, Wagakalatia 6:1 na 1 Timotheo 5:19-20.
•    Wapokee wale wanaotubu na kurejea kwa ushirika na kuwahakikishia neema, utakaso na msamaha wa Mungu.


III-12—Huduma ya 12

Ongea na Mungu

Asubuhi iliyofuata askari anawasili nyumbani kwa Mwanafunzi na kumchukua korokoroni. Hakimu anamwambia, “Nitafanya mashtaka kuamua ikiwa imefanya mikutano bila idhini toka kwa serekali yetu ya mji. Adhabu ya kufanya mikutano ya uharibifu ni kali sana. Hakuna mtu ataruhusiwa kukutembelea isipokuwa mkeo.”
Jioni hiyo Sara anakuja kumtembelea na anamwambia Mwanafunzi, “Haya yametendeka kwa sababu watu wengi wamekuwa wakija kwa Bwana. Sisi zote tumekuwa tukiomba kila siku kwa ajili ya wokovu wa watu waliopotea, na nafasi ya kuwaambia juu ya Kristo. Bwana alijibu maombo yetu. Lakini imevutia walewasiopenda Wakristo.”
Mwanafunzi anaomba, “Bwana, nipe nafasi ya kushiriki habari yako njema na wafungwa wenzangu kwenye jela hii.” Mungu anajibu hili ombi. Baada ya juma moja, wafungwa sita wamekuja kwa Kristo.
Wiki tatu baadaye hakimu anafanya mashitaka. Yusufu, mzee aliyekuwa amekamatwa mapema, amehukumiwa kwa wakati huo pia. Wamemwajiri wakili mmoja, lakini haweki bidii kuwatetea. Mwendesha mashtaka anawaita mashahidi wanaowalaumu waumini kwa kuacha desturi na utamaduni nzuri wa jamii. Bwana Pumbavu pia anatoa ushahidi kinyume na Mwanafunzi. Inaonekana wazi mtu
alimlipa kupeleleza mkutano. Hakimu anatangaza, “Ninyi nyote mtakaa korokoroni hadi nipange kunyongwa kwenu. Hiyo ndiyo
hukumu ya kufanya mikutano ya uharibifu.”
Msaidizi anakutana kisiri na wazee wa mkutano wa Mwanafunzi kwa nyumba ya Yakobo na anawaambia, “Ndugu na dada zangu, mmekasirika na mna hofu. Msife moyo. Bwana Hekima alitufunza toka kwa Neno la Mungu kwamba hatupaswa kuwakasirikia watu wanaotuudhi. Vile Yesu  alisema wakati walimsulubisha, ‘hawajui watendayo.” Mungu  atayatumia haya kwa  wema.  Zidi
kumwombea Msaidizi na Yusufu. Kumbuka, vita vyetu si kinyume ya watu bali kinyume ya nguvu za mapepo wachafu. Fuata mifano
ya wale waliomba katika Biblia, kama Abrahamu, Ester na yule Mjane asiyekoma. Hebu niwaambie juu ya Maombi ya Ujasiri ya
Abrahamu.”


Tafuta katika Mwanzo 18:16-33:
Zoezi
•    Kwa njia gani Abrahamu alizidi kuwaombea watu waovu wa Sodoma?
•    Je, Abrahamu alinyenyekea au alijivuna wakati akiomba?
•    Je, Mungu aliitikiaje huruma na kutokoma kwa Abrahamu?
Msaidizi anawaelezea wazee waliokusanyika nyumbani mwa Yakobo, “Abrahamu aliwaombea watu waovu wa Sodoma. Walikuwa wageni kwake, lakini aliwahurumia. Mungu alijibu sehemu ya maombi yake ya huruma. Abrahamu hakudai kitu chochote
toka kwa Mungu bali aliomba kwa unyenyekevu. Pia sisi tunaombea majiji, nchi na serekali zetu na zile zilizo mbali nasi. Tafadhali
saidia mkutano kuomba jinsi hii wakati Mwanafunzi hayupo.”
“Kumbuka kuombea sio tu ninyi wenyewe na familia zenu, bali pia mkutano wote. Waombee viongozi wenu. Muulize Mungu awaunganishe na awajaze Roho Mtakatifu na Nguvu zake ili mmtumikie. Waombee wenye mahitaji na jela. Omba Mungu atupe zote nafasi zaidi na wafanyikazi zaidi wakuwaendea mpaka watu waliotelekezwa kuwaambia habari njema. Sasa, hebu niwaambie jinsi Mungu Anatumia Msichana Yatima Kuliokoa Taifa.”


Tafuta katika Ester 3:13-5:3 na 7:1-8:
Zoezi

51
•    Ni kwa sababu ya hatari gani kubwa ndio Mordekai alikuwa anaomboleza?
•    Je, Wayahudi walifanya nini kujiandaa kwa mkutano wa Malkia Ester na Mfalme?
•    Je, Malkia Ester alifanya nini kuonyesha upendo wake kwa watu wake na imani yake ya ujasiri?
•    Durusu kwa ufupi kitabu chote cha Ester, kuona jinsi, kwa maombi ya watu wake, aliliokoa taifa.
Msaidizi anaendelea kuwafafanulia wazee katika nyumba ya Yakobo, “Mungu alimwinua Ester kuwa Malkia ili aweze kuwaokoa watu wao toka kwa maangamizi. Yeye na watu wake waliomba na kufunga kwa siku tatu kabla ya yeye kukutana na Mfalme. Alihatarisha maisha yake kumwendea, na kwa imani yake, watu wao waliokolewa. Katika Agano la Kale, Mungu anaonyesha neema
kwa  wale  wanaomkataa.  Yesu  anatwambia  tuwaombee.  Mungu  hufanya  kazi  kupitia  maombi  yetu  kuwaokoa  watu  toka  kwa
maangamizi. Tunapaswa kuwa tunaomba mioyoni mwetu kila wakati. Hatupaswi kuchoka kuomba. Maombi ndio silaha yetu ya maana zaidi kwenye vita vya kiroho. Sasa wacha niwaambie kuhusu Mjane Asiyekoma.”


Tafuta katika Luka 18:1-8:
Zoezi
•    Je, yule mjane aliwezaje kumsihi hakimu mfisadi kumsaidia?
•    Kwa vile Mungu ndiye hakimu wetu, tunapaswa kumwomba bila kukoma? Kwa nini?
•    Je, ni nini Kristo anataka kupata ndani yetu akirudi?
Msaidizi  anamalizia  kufundisha  kwa  maneno  haya,  “Hakimu  mfisadi  alimsaidia  mjane  kwa  sababu  alizidi  kumwomba. Hakukubali chochote kimzuie. Mungu ni hakimu mwema. Atajibu maombi yako ili upate haki. Usikubali chochote kikuzuie kuomba
maombi ya uaminifu. Zingatia walio karibu nawe wakati mnaomba kwa kikundi. Usiwachoshe na maombi marefu, yakurudiarudia
kama  wale  waombao  miungu.  Epuka  lawama  na  udaku.  Kuwakosea  wengine  kunazuia  maombi  yetu.  Kumbuka Adui  anataka kutukatiza na kutufadhaisha. Mara nyingi Yesu alijitenga ili aombe pekee yake usiku. Kama Yesu, chukua muda ukiwa mbali na shughuli za ulimwengu.”
Wakati Msaidizi anatoka nje anapatana na askari watatu wanamngojea. Wanamshika na kumpeleka jela. Anawasihi wamweke kwenye chumba kimoja na Mwanafunzi lakini wanakataa.
Waumini wanafunga na kuomba manyumbani mwao. Wengine wanakutana kwa vijikundi na kumwombea Mwanafunzi na Msaidizi usiku kucha. Bwana Pumbavu anawasili kwa mkutano kwa duka la Yakobo na anasema, “Kama kweli tunataka Mungu ajibu maombi yetu, ni sharti tuombe tukiwa kwa magoti yetu. Si tukiwa tumesimama. Si tukiwa tumeketi. Si tukiwa tumelala chini. Ni kwa
magoti yetu tu. Biblia inasema Mfalme Suleimani aliomba akiwa amepiga magoti na mikono yake imenyoshwa kuelekea mbinguni.
Hiyo ndiyo njia pekee!”
Yakobo anamjibu, “Wewe unamfadhaisha kila mtu kutoka kwa lengo la maombi. Watu wawili wamo korokoroni na wewe unataka tuangazie kukamaa kwa miili yetu! Mungu ana haja zaidi na kukaa kwa mioyo yetu. Katika Biblia wanaongea na Mungu kwa njia mbalimbali. Wakati mwingine wanaomba kimya kimya. Wakati mwingine wanaomba kwa sauti. Wakati mwingine wanaomba wakiwa wamesimama au wamelala chini. Wengine wao wanatumia zaburi toka kwa Biblia au kuimba maombi yao. 2 Wakorinto 3:17 inasema, “Panapo Roho wa Bwana, pana uhuru.”
Bwana Pumbavu anaondoka. Wanaongea juu ya njia za kusaidia mkutano kuomba vyema zaidi. Wote wanakubaliana kuomba kila siku, pekee au na familia zao. Wanawake wawili wakongwe wanaahidi kukusanyika kila asubuhi mapema kuomba pamoja. Yakobo anawauliza waumini kuunda msururu wa maombi. “Wakati mtu anatambua hitaji, anamwambia mwenzake. Huyo mwenzake anamwambia mwenzake, mpaka kila mtu anayeshiriki kwa msururu wa maombi awe anaomba. Kila mtu anaweza kuomba kwa njia mbalimbali kwa wakati mbalimbali.”

Nguvu ya Kuomba Kwa Jina la Yesu.
Siku iliyofuata Yakobo na wazee wanaenda kumwombea Ruthu, mwanamke ambaye ameolelewa hivi karibuni ambaye ni
mgonjwa sana, “Bwanangu Tobiasi alinipiga na nikaanguka. Amekuwa akitumia madawa ya kulevya. Nina uchungu mwingi sana sasa.  Bwana  Pumbavu  pia  anakuja  na  kuanza  kuhubiri,  akitumia  maneno  makubwa.  Anawaambia  wazee,  “Sasa  kwa  kuwa Mwanafunzi yuko korokoroni, ninapaswa kuliongoza kanisa.”
“La, hautaweza!” Yakobo anapinga. “Na wacha kutumia maneno wakubwa kuwavutia hawa watu na nguvu zako za kiroho! Sasa, wacha wazee wafuate maagizo katika Yakobo 5.” Wanamwaga mafuta kidogo kichwani mwa yule mwanamke na kumwombea kwa Jina la Yesu. Wanaomba kwa imani na unyenyekevu, wakitumia maneno mepesi.
“Je, ni makosa yangu?” Ruthu anauliza kwa homa yake, “Je, nimetenda dhambi sana?”
Bwana Pumbavu anaanza kusema ndio lakini Yakobo anamwambia mwanamke, “Ikiwa dhambi fulani zinakutatiza, kiri na umwamini Mungu kwa msamaha.”
Wakiwa wanaomba, bwanake Tobiasi anausukuma na kuufungua mlango. Anawasikia wakiomba kwa Jina la Yesu na analaani. Anampiga Yakobo, lakini katika hali hii, anaanguka na kujeruhi kilimbili chake.
Bwana Pumbavu anapiga mayowe, “Toroka! Hatuwezani na hizi nguvu!” Ruthu, hata hivyo, analia, “Usiende! Nakuomba ubaki.
Mwanafunzi alitufundisha juu nguvu za Yesu juu ya pepo wabaya. Alisema mkemee shetani naye atawakimbia.”
“Ndio,” Yakobo anajibu. “Hiyo ni Yakobo 4:7. Hatutamkimbia shetani bali tutasimama hapa na kumpinga. Tutamlazimisha atuondokee katika jina la Yesu.” Anatoa Hadithi ya Mvulana Aliyeteswa na Mapepo.”


Tafuta katika Marko 9:14-29:
Zoezi.
•    Je, wafuasi walikuwa wakifanya nini wakati Yesu aliwakuta?
•    Kwa nini wafuasi hawangeweza kutoa huyo pepo mchafu?

52
Hadithi Za Mchungaji

•    Je, Yesu alimwomba Baba kufanya nini?
•    Je, Yesu alifanya nini ndio amtoe yule pepo?
Yakobo anaelezea, “Badala ya kuomba, wafuasi wa Yesu walikuwa wakibishana wakati aliwasili! Hawangeweza kutoa yule pepo kwa sababu hawakuwa wakitegemea nguvu za Mungu. Yesu aliwakemea kwa kukosa imani. Alimwambia baba kuamini. Halafu
akaamuru yule pepo kumwachilia yule mvulana na asiwahi rudi tena. Alimponya kabisa yule mvulana. Sasa, hebu tufanye yale Yesu
alifanya, kwa Tobiasi. Njoo, tumwombee!”
Bwana Pumbavu anamlalamikia Yakobo, “Usituambie la kufanya sana hivyo! Wewe ni muumini mpya. Wakati Mwanafunzi hayupo, mimi ninashika ushukani. Mlezi pia amekuwa akiwaongoza watu katika kanisa hili sana.”
Mmoja wa wazee anamkemea Bwana Pumbavu, “Yale usemayo sio sawa. Yakobo ana haki zote za kufanya kazi nasi. Na tunahitaji msaada wa Mlezi pia, hata kama anatoka kwa mkutano mwingine. Katika Agano Jipya, viongozi waliendelea kutumikia
makutano mbalimbali. Walisafiri mara kwa mara kusaidia mkutano wenye mahitaji. Maandiko yanahitaji uhusiano huu kati ya
makutano. Hayapaswi kuwa makundi yaliyojitenga. Mkutano wowote ni sehemu ya mwili mkubwa wa Kristo kwenye eneo hili.” Kwa wengine anasema, “Njoo, hebu tumwekee mikono na kumwombea huyu mtu aliyepakawa.”
Bwana Pumbavu anapiga nduru, “Hapana! Msipinge hayo mapepo! Yatatushambulia!” Wazee hawamsikizi na anakimbia toka mle  chumbani  na  anasimama  akichungulia  pembeni  mwa  mlango. Wazee  wanakemea  pepo  kwa  jina  la  Yesu.  Kwa  saa  moja inayofuata wanamsaidia Tobiasi kukiri dhambi zake kwa Mungu katika Jina La Yesu na anapokea nguvu za Roho Mtakatifu kumlinda
kinyume ya yule mwovu. Mwishowe, Tobiasi anatulia na kuchiachilia kwa Mungu. Anakiri dhambi zake na kumwomba Yesu
amwokoe. Baada ya dakika chache za kimya anashangaa, “Mapepo waovu wameondoka!”
Wanamsifu Bwana. Tobiasi anamwambia Yakobo, “Nina jambo la kukiri kwako. Ninafanya kazi na serikali na niliwashtaki viongozi wenu kwa kufanya matendo ya uharibifu kinyume ya serikali. Bwana Pumbavu alinijulisha kwenye mikutano yenu ya siri ilikuwa ikifanywa. Nilikuwa nikimhonga naye alikuwa akiniambia kila kitu.”
Siku iliyofuata Tobiasi, baada ya kuwekwa huru toka kwa mapepo ya utesi, anawaambia serekali ukweli. Wanamwachilia Mwanafunzi na Msaidizi, ambao wanarejea kwa nyumba ya Mwanafunzi na wanakuta kundi ndogo likiombea kuachiliwa kwao. Wanamsifu Mungu kwa furaha kuu.

Kupambanua Kati ya Aibu ya Kuhisiwa na Hatia ambayo ni ya Kweli Mbele za Mungu.
Baadaye siku hiyo Dibora anawasili nyumbani kwa Mwanafunzi akiwa ana hema. “Nisaidie!” Analia, “Ndugu yangu Samweli anataka kujiua! Njoo uongee naye! Nilimwambia juu ya Yesu lakini hakuweza kunisikiliza.”
Mwanafunzi na Sara wanaharakisha kwenda nyumbani kwa Dibora. Anawaelezea, “Samweli anashikilia wembe, akilia. Dibora anaharakisha na kumnyang’anya ule wembe. Samweli anatoa kwikwi ya kulia, “Nina aibu nyingi sana na sitaki kuishi. Tafadhali
nendeni mbali nami!”
Sara anauliza kwa nini anahuzuni mwingi hivyo. Baada ya kipindi kirefu cha kimya anamwambia, “Mwalimu pumbavu wa chuo alinipa daraja ya kuanguka na siwezi kwendelea. Siwezi kuishi na hii aibu. Nilisoma kwa bidii vile ningeweza, lakini singeweza kukumbuka majibu hayo. Nilisoma kwa bidii kuliko wanafunzi waliopata alama za juu! Nimejiletea mimi na familia yangu aibu.”
Sara anamnong’onezea Mwanafunzi, “Bwana Hekima angefanya nini na Samweli?”
Mwanafunzi anaombea hekima kimya kimya, halafu kwa upole anamwahikikishia Samweli, “Umeaibika lakini hukufanya lolote baya. Mungu hakuhesabii hatia kwa sababu umefeli kwenye chuo. Ulifanya kile ungeweza. Hauhitaji kujiua. Yesu Kristo atakuja kwa moyo wako na kuondoa hiyo aibu.”
“Nisipokufa, lazima nimkabili huyo mwalimu. Ana vyombo vya dhamana vya kutambua kemikali. Nitamwibia hizo. Hataweza kuthibitisha ni mimi niliyeiba!”
“La, la!” Mwanafunzi anasisitiza. “Hilo ni haramu! Lazima uelewe tofauti kati ya aina mbili za aibu. Moja ni hisia tu. Nyingine inatokana na hatia ya ukweli inayostahili adhabu ya Mungu! Kuanguka somo kunaleta tu aina ya kwanza ya aibu, ambayo si ovu.
Lakini kuiba ni dhambi ya kweli. Inaleta hatia na inastahili adhabu ya Mungu!”
“Sielewi tofauti.”
“Hebu nieleze Hadithi ya Biblia juu ya Mfalme Sauli na aina Mbili za Aibu.”

Zoezi
Tafuta 1 Sam. 20:27-34 yale Mwanafunzi alimsaidia Samweli kuvumbua:
•    Tafuta katika mstari wa 30 kwa nini Mfalme Sauli alisema kuwa Yonathani aliiabisha familia yake.
•    Tafuta katika mstari 34 kwa njia gani Sauli alimtendea Daudi aibu.
•    Ni aibu ya mwanamme yupi ilitokana na hatia ya kweli mbele ya Mungu, Sauli au Yonathani?
Mwanafunzi anaelezea Samweli, “Yonathani alihisi aibu lakini hakuwa na hatia mbele ya Mungu. Hakuwa amefanya lolote baya. Babake mwenye vivu na kisasi Mfalme Sauli hakuhisi hatia hata kama alitaka kutenda uhalifu mbovu. Alitaka kumwua mtu asiye na hatia. Alikuwa na moyo wa kiburi na dhambi mbele ya Mungu. Je, unaona tofauti?”
“Ndio! Hii inasaidia! Kushindwa kwa somo kwenye chuo kikuu ilikuwa ni aibu lakini sio uovu. Lakini kutaka kuiba toka kwa mwalimu ni uovu mbele ya Mungu. Nilihisi aibu kwa kile si ovu, lakini sikuhisi aibu kwa dhambi ambayo nina hatia ya kweli. Niliomba usiku uliopita kwamba Mungu anisaidie kumuumiza huyu mwalimu kwa njia moja au nyingine. Sikuwa sawa. Lakini nitakabilianaje na wazazi wangu? Walitumia fedha nyingi sana kunipeleka chuoni.”
“Mungu atakusaidia. Kwanza, kiri dhambi zako kwa Mungu na uulize msamaha. Unajua kuhusu sadaka ya Kristo kwa ajili ya dhambi zetu. Sasa unajua kwa nini unauhitaji. Kukiri dhambi ni sehemu muhimu sana ya maombi. Kutaka kumuibia mwalimu ni dhambi ya kweli na inaleta aibu ya kweli mbele ya Mungu. Ni lazima ukiri hii dhambi.”

53
“Sijui jinsi ya kukiri dhambi kwa Mungu. Sijawahi kufanya hivyo.”
“Kukubali aibu ya kweli, kunasaidia kusahau tofauti kati ya hatia ya kweli mbele ya Mungu na hisia zetu za aibu. Tunahisi aibu wakati mzazi, mwalimu au serekali wanapotukemea hadharani. Tunahisi aibu wakati tunafanya kitu ambacho kinasababisha watu wafikirie sisi ni watu wabaya au familia yetu ni duni. Hisia kama hizi za aibu wakati mwingine hazistahili. Hali huwa zinatufanya tuonekane wabaya wakati hatujafanya chochote kibaya mbele ya Mungu. Sasa, hebu tuombe pamoja tukiri dhambi zako za kweli. Ukitaka, nitasema ombi la kukiri katika jina la Yesu, na unaweza rudia hayo maneno baada yangu.”
Samweli anarudia ombi la msamaha katika Jina la Yesu baada ya Mwanafunzi. Mara tu alipoanza kuongea na Mungu ikawa rahisi  kuendelea  kuomba  na  kukiri  dhambi  zake  kwa  meneno  yake  mwenyewe.  Siku  chache  baadaye  imani  na  toba  yake zinathibitishwa kwa ubatizo.”

Kazi ya Kufanya.
•    Tumia hadithi zilizomo kwenye hii sehemu kufunza mkutano wako kuomba kwa uaminifu, pekee na familia zao.
•    Saidia mkutano wako kuombeana na kuombea wale walio na mahitaji. Wawezahitajika kuwatembelea manyumbani, na kuomba nao na kuwasaidia waanze.
•    Andaa mkutano kuwaombea wagonjwa na wale waliogandamizwa na mapepo wabaya.
•    Wakati wa ibada ongoza mkutano kuombea miji, mataifa na serekali za ulimwengu.
•    Wasaidie watu wanaohisi aibu kukiri hatia yao ya kweli na kuamini katika kifo na ufufuo wa Yesu, kuwaletea msamaha na uzima wa milele.

III-13—Huduma ya 13

Iweni Watumishi wema wa Nyenzo za Mungu

Mlezi na mkewe Karmeni wanakuja kwa nyumba ya Mwanafunzi kumwambia, “Familia toka sehemu zingine za nchi wanahamia huku. Wengi wanaishi kwa vyumba duni vya mashambani, si mbali toka hapa, chini kwa mto. Tunapaswa kuwasaidia.”
Hebu twende tuwaone.” Mwanafunzi anajibu.
Wanatazama vyumba bovu ambavyo watu wanaishi ndani wakati wanasikia kengele ikipigwa. Bwana Pumbavu anausukuma mkokoteni wake kwa haraka sana kuwaelekezea. Anasema, akihema, “Hivi karibuni askari wanaenda kuwafukuzilia mbali hawa watu. Wameketi kwa mali ya uma.”
Mlezi anashangaa, “Ni aibu gani hii! Nitasihi serekali kwa ajili yao.”
“La!” Bwana Pumbavu anakataa, “Wacha hawa watu waende! Wanachukua kazi za wafanyikazi ambao huwa wanaishi hapa. Wana desturi za kigeni. Wanavalia tofauti. Mtasababisha shida kwa serikali iwapo mtawatetea. Hawa sio shida yenu. Ikiwa mnataka kuwasaidia watu maskini, mnaweza kunisaidia. Ninahitaji baiskeli. Halafu nitaweza kuzunguka nikiwakaribisha watu wengi kanisani mwetu!”
Karmeni anapiga kite.
“Tazama hapa, Mwanafunzi.” Bwana Pumbavu anainua chupa ya unga mweupe. “Nunua hii dawa itokayo kwa ndovu. Meza kidogo kwa siku na utakuwa mkubwa.”
Mlezi anasema, “Mjomba wangu alijaribu na akasema kwamba haikupanua hata pua lake! Mwanafunzi, inatupasa tuwasaidie hawa walio maskini hohehahe. Nilisoma kwenye Biblia jinsi Mungu anatwambia tuwasaidie maskini. Haisaidii kuwapa tu pesa.
Tunapaswa kuwasaidia pia kwa njia zingine.” Anasema hadithi ya Dorkasi.


Tafuta katika Matendo 9:36-43:
•    Je, watu walisema nini kumhusu Dorkasi?
•    Je, Dorkasi aliwasaidia akina nani?
Zoezi.
•    Ni kwa hali gani Dorkasi na Petero waliwatumikia wengine?
Mlezi anawaelezea Mwanafunzi na Bwana Pumbavu wanaposimama wakiangalia vile vyumba bovu vya familia ngeni, “Dorkasi aliwasaidia maskini na wajane mbao hawakuwa na mtu mwingine wakuwasaidia. Yeye na Petero waliwatumikia wengine katika jamii kwa unyenyekevu. Wakati Petero aliwasili, aliwatoa watu wote chumbani, akapiga magoti, na akaomba. Mungu akamfufua Dorkasi
toka kwa wafu.”
Karmeni  anaongezea,  “Tuna  nafasi  hapa  ya  kumfanyia  Bwana Yesu  Kristo  mengi  mazuri.  Anatuamuru  tutoe  na  kuwalea maskini.”
“Ndio!”  Mwanafunzi  anajibu.  “Anatwambia  katika  Matayo  25:31-46  kwamba  yale  tunazifanyia  hizi  familia  maskini  kwa upendo, tunamfanyia yeye. Mungu anaahidi malipo mbinguni kwa wale wanowasaidia maskini kwa upendo wa Yesu. 1 Yohana 3:17
inasema kwamba ikiwa tunawapuuza, hatuna upendo wa Mungu mioyoni mwetu. Upendo wetu waonyesha kuwa tu wana wa Mungu.”

Wezi wa Wakati na Pesa.
Mwanafunzi anaendelea, “Mungu anatupa nafasi ya kuwatolea na kuwatumikia wengine. Tunapaswa kutoa wakati wetu na uwezo
wetu kwa ukarimu. Wakati mwingine tunadharau nafasi ya kumtolea Mungu. Tunatumia pesa vibaya. Tunapoteza wakati wetu kwa mazungumzo ya upuzi, ubishi, wasiwasi au shughuli ambazo hazina dhamana. Vitu hivi ni wevi. Vinatuibia wakati na pesa zetu.


54
Hadithi Za Mchungaji

Tunapaswa kupanga jinsi ya kutumia wakati wetu, vipaji vyetu vya kiroho na pesa zetu kwa Mungu. Tunapaswa kutoa kwa maombi na imani ili tutekeleze mipango yetu.
“Sawa!” Mwanafunzi anadhibitisha. “Tusiwe kama mjenzi pumbavu katika Luka 14:28-30. Hangemaliza kujenga kwa sababu alishindwa kupanga kwanza.”
Hawa wageni maskini wanahitaji msaada wetu.” Mlezi anasema, “Biblia inafunua jinsi Mungu aliwabariki wale waliosaidia watu waliokuwa wakitoroka vita, njaa na ugandamizi. Hebu tupange jinsi ya kuwasaidia hawa maskini. Mfano mmoja ni hadithi ya Ruthu
Mjane Mwaminifu.”


Tafuta katika kitabu cha Ruthu:
Zoezi.
•    Katika Sura 1, ni jinsi gani Ruthu alionyesha ujasiri na imani kwa Mungu?
•    Katika sura 2, ni jinsi gani Boazi alionyesha ukarimu kwa mjane mgeni?
•    Katika Sura ya 3, ni jinsi gani wale wajane wawili wanachukua nafasi kusuluhisha shida zao?
•    Katika Suara ya 4, ni jinsi gani Boazi alihatarisha mali yake kusaidia mtu mwengine?
•    Katika Sura ya 4, ni vitu gani vizuri ambavyo Mungu alisababisha kutendeka kwa Ruthu kama matukio ya ukarimu wa Boazi?
Karmeni anashangaa, “Ninaona! Kitabu cha Ruthu kinawafunza matajiri na maskini jinsi ya kutenda. Ruthu hakuwa na mapato na hakuwa na mtu wa kumtetea kwa ugandamizi. Alikuwa maskini hohehahe. Hata hivyo, alibaki mwaminifu kwa Mungu na kwa mamake mkwe. Hakuwa mvivu. Alifanya bidii kuokota nafaka kwenye shamba lake Boazi. Alikuwa jasiri. Alifuata wasia wa Naomi na akachukuwa nafasi kumuuliza Boazi kutetea hazi zake kama mjane Mwisraeli.”
Mwanafunzi anaongezea, “Boazi, kwa upande mwingine, alikuwa kabaila. Angempuuza Ruthu. Badala yake, alikuwa mkarimu kwake. Alimruhusu kukusanya nafaka na akawazuia wafanyikazi wengine wasimdhuru. Alitekeleza wajibu wake kama mwokozi-wa- jamaa hata kwa mjane mgeni, maskini. Kuhatarisha mali yake, alimchukuwa Ruthu kuwa mkewe. Mungu alibariki huu ukarimu. Daudi na Yesu walikuwa wazao wa Ruthu na Boazi. Hadithi ya Ruthu na Boazi inatuonyesha jinsi vile Yesu aliwaokoa waumini wote wawe mwanamwali wake. Yeye ni mkombozi wetu. Anatuokoa kwa mahitaji yetu. Tuwateteapo wenye mahitaji, kama vile Boazi alivyomtetea Ruthu na Naomi, tunamwiga Kristo.”

Majukumu Mawili Makuu ya Mkutano.
Mwanafunzi anaendelea, “Nimesoma jinsi watu wa Kristo wanabadili ulimwengu. Kuna majukumu mawili makuu. Ni kama
miguu miwili itubebayo. Jukumu la kwanza ni kuwafanya wafuasi wa Kristo. Lile lingine ni kuwatumikia watu kwa upendo. Mambo haya yote ya husikitisha ulimwenguni kwetu, kama vile umaskini, mateso na vita, yalikuja kwa sababu ya dhambi. Yanaendelea kwa sababu dhambi inatawala maisha yetu. Tunapotubu na kumjilia Mungu, anavunja ngome ya dhambi na anaanza kuponya madhara ya dhambi ndani mwetu.”
Wanawatizama wanaume wawili wakipigana. Mmoja anamlaumu mwenzake, “Uliiba pombe yangu!” “Inatupasa pia kuwaelezea hawa watu maskini juu ya Yesu,” Karmeni anafiria.
“Tutafanya yote mawili,” Mwanafunzi anasema, “Tutafanya kazi kwa pamoja kama kanisa. Yesu atavunja ngome ya vita, umaskini na ufisadi. Watu wanapomgeukia Mungu, wanampa kila kitu: wakati wao, kazi zao, na familia zao. Hatuishi kwa ajili yetu
tena. Tunakoma kuibiana na kuumizana. Tunaanza kutumikiana kwa upendo. Ikiwa tu maskini, tunabaki waaminifu na kufanya kazi
kwa bidii kama Ruthu. Wale walio kabaila au wenye mamlaka hawapaswi kujitumikia wenyewe. Kama Boazi, wanapaswa kuwatumikia wengine, ili kila mtu atendewe haki na kuishi kwa amani. Hebu tuongee na wale wanaume kabla hawajauana na tutafute jinsi tunaweza wasaidia kusuluhisha shida zao.”
Bwana Pumbavu anasema, “Mimi ninakataa kuwakaribia. Wanaugonjwa.” Anasukuma mkokoteni wake kurudi barabarani.
Siku iliyofuata Mwanafunzi na Mlezi wanakutana na wazee wengine na kupanga kusaidia zile familia ngeni. Wanaombea msaada wa Mungu kwa watu maskini. Wanawatembelea mara kadhaa kwa wiki kuona ni nini wanahitaji zaidi. Wanafanya kazi na wao kwa pamoja kujenga kisima kwa sababu maji ya mto yana vijidudu. Msaidizi anapangia watu wengine kazi na kwenda shule kwa watoto
wao. Karmeni anaelewa lugha yao, ambayo ni tofauti kidogo, na anawafunza wanawake kuongea lugha ya hapo. Anawatafsiria
wanapoongea na madaktari au maafisa wa serikali.
Familia ngeni zinaitikia kwa shukrani. Wanapokea habari njema ya Kristo. Msaidizi na Mlezi wanaanza mkutano na wanawafundisha viongozi kadhaa wa kiume. Msaidizi anawasaidia kuandika nyimbo juu ya imani yao na kuimba kwa mtindo wao wa kipekee wa muziki. Kwa miezi michache wengi wanakuja kwa Kristo kuliko kwa makutano wale wengine wote.

Kazi ya Kufanya
•    Tumia hadithi katika sehemu hii kuwasaidia watu wako kutumikia maskini katika Jina La Yesu.
•    Wasaidie walio na kipaji cha kiroho cha huruma kupanga huduma ya kuwasaidia watu ambao hakuna mtu mwingine anataka kuwasaidia  katika  jamii  yenu.  Hawa  wanaweza  kuwemo  wahamiaji,  wakimbizi,  wajane,  mayatima,  walevi,  wapendelevu madawa ya kulevya, walio korokoroni na wenye shida kubwa za kiuchumi.
•    Tafuta njia za kusaidia wale walio na mahitaji kupata nafasi ya kusuluhisha shida zao.
•    Tafuta haki ya wanaoteswa, hata kama unahatarisha maisha yako.
•    Wacha watu waaminifu pekee wawajibike kwa matoleo ya mkutano na uwasaidie kuweka kumbukumbu nzuri ya haya matoleo.
•    Muagize mweka hazina kutowahi peana mkopo au kupeana pesa bila idhini ya wazee.


55
III-14—Huduma ya 14

Tuma Mitume

Bwana Hekima anamtembelea Mwanafunzi tena, baada ya miezi kadhaa. Mwanafunzi anamwambia Bwana Hekima, “Umetufundisha namna ya kufundisha! Nakushukuru! Umetuonyesha jinsi ya kusikiliza kabla ya kuanza kufundisha, ili tufundishe yale  mkutano  wapya wanahitaji. Ulituonyesha  jinsi  ya  kutumia hadithi,  ili  wanafunzi  wetu  wakumbuke ukweli  wa  Mungu an kuupokeza kwa wengine. Ulituonyesha jinsi ya kuuliza maswali juu ya yale tumefundisha, kutusaidia kufikiria na kuyatumia kwa makutano wetu.
“Mimi nilikufundisha njia ambayo Yesu alitumia.”
Bwana Hekima na Mwanafunzi wanamtembelea nduguye Msaidizi, na wanamkuta Bwana Pumbavu kwa nyumba yake. Anamwambia Bwana Hekima, “Mwanafunzi amenitendea vibaya sana kwa hivyo siku hizi mimi ninahudhuria mkutano ya Msaidizi.”
Bwana Hekima anawaambia, “Ninaenda eneo la nchi ambapo hakuna makanisa, kuanzisha kazi ya Bwana. Ninaunda kikundi cha
kazi, na nilikuja kumwomba Msaidizi kuungana nami. Umeanzisha mkutano na watu toka utamaduni mwingine na umekuza viongozi katika huu utamaduni. Mungu amekupa karama na shauku ya kuanzisha makutano. Wewe ni ‘yule aliyetumwa.’ Hiyo ndiyo maana ya neno ‘mtume’. Tutajifunza lugha mpya na utamaduni mpya.”
“Huwezi mchukuwa Msaidizi!” Bwana Pumbavu anapinga, “Anamajukumu hapa, na kazi nyingi ya kufanya! Kando na hayo, mkutano ni maskini sana hawawezi kumsaidia kama mtume. Baada ya sisi kusimama kama kanisa ndio tunaweza fikiria juu ya kuwatuma mitume.”
Mwanafunzi anakubali. “Hii ni nafasi kwa Msaidizi kupeleka injili kwa watu ambao hawajawahiisikia. Mungu aliahidi Abrahamu kwamba kupitia wazao wake mataifa wote watabarikiwa. Hii ahadi inatimia katika Yesu Kristo, uzao wa Abrahamu. Yesu anasema katika Matayo 24:10 kwamba mwisho wa dunia na hatima ya kuja kwake itatimia baada ya injili kuhubiriwa kwa kila taifa. Hakumaanisha mataifa ya kisiasa, bali makundi ya makabila—watu wa utamaduni mmoja.”
“Ndio!” Bwana Hekima anakubaliana. “Yesu anasema katika Matendo 1:8 kwamba tutakuwa mashahidi wake katika sehemu za karibu na mbali, katika utamaduni wetu na utamaduni mwengine. Amri yake ya mwisho kwetu katika Matayo 28:18-20, ni kuwafanya wafuasi mataifa wote wa ulimwengu. Mungu hubariki makutano ambao wanatii amri zake. Anawapenda watu wote wa ulimwengu na anawataka wamjue kupitia kwa Yesu Kristo, Mwanawe. Hebu nikwambieni juu ya Yona, Mtume Asiye Kubali, ambaye mbeleni alifikria kama Bwana Pumbavu juu ya kufikia tamaduni zingine.”

Mungu atawaokoa Watu toka Mataifa Wote Wa Ulimwengu.
Zoezi.
Tafuta katika kitabu cha Yona:
•    Je, huyu nabii Mwisraeli alifanya nini wakati Mungu alimpa ujumbe wa jiji adui?
•    Je, ni jinsi gani Mungu alihakikisha mapenzi yake yamefaulu, hata wakati yule mtume alikataa kwenda kule alikotumwa?
•    Ni kwa njia gani hadithi hii inaonyesha upendo wa Mungu hata kwa mataifa maovu kabisa ulimwenguni?
“Haya  ni  maongezi  hatari!”  Bwana  Pumbavu  anapiga  kelele,  anapomsikiliza  Bwana  Hekima,  Mwanafunzi  na  Msaidizi, nyumbani mwa Msaidizi. “Hatuhitaju kwenda nchi za mbali kutafuta watu wanaohitaji kutubu toka dhambini!”
Bwana Hekima anaendelea kufafanua, “Yona alikataa kuhubiri kwa taifa adui. Alipanda meli kwenda pande tofauti. Mungu akatuma dhoruba na halafu samaki kumrudisha. Yona alijifunza kwa njia ngumu kwamba ni lazima atende mapenzi ya Mungu.
Mungu  aliwajali  watu  wenye  dhambi  wa  Nineve  vile  tu  alivyowajali  watu  wengine  ulimwenguni.  Wakati  walitubu,  Mungu aliwasamehe jinsi anavyowasamehe wale wanaotubu na kumgeukia. Mungu anatupa upendo kwa watu hata kama wako tofauti nasi.
Anatutuma kuwapelekea habari njema na anatubariki tunapoenda kwa hiari yetu. Ikiwa hatuendi vile anatuamurisha, atawafikia watu
hao kwa njia nyingine, lakini hatutapokea hizi baraka maalum.”
Bwana Hekima anamwambia mkewe Msaidizi Recho, “Mungu amekupa kipaji cha kiroho cha kuwapenda watu na kuwasiliana na watu wa tamaduni zingine. Tafadhali nenda nami. Msaidizi, u maskini, na sitarajii mkutano wako, ambao pia ni maskini, kukulipa mshahara. Wanapaswa kuwasaidia wengine, vile tu wafanyavyo makutano wengine ambao Mungu ameinua eneo hili. Mpango wangu kwako ni kwamba wewe nami twende tufanye kazi kama watendaji wa biashara ambayo imetupa ajira huko. Tutapata riziki jinsi mtume Paulo alivyofanya katika Matendo 18. Marafiki wa Paulo, Prisila na Akwila, walimpa ajira ya kutengeneza mahema. Tuna marafiki Wakristo ambao wako kama Prisila na Akwila. Watatupa ajira kule tunaanzisha makutano.”

Jinsi ya Kupeleka Habari Njema kwa Watu Wa Utamaduni Tofauti.
Recho anasema, “Sijui kufanya kazi na watu wa utamaduni tofauti.”
Bwana Hekima anaeleza, “Tunafanya kwa njia ile Mungu alikuja kwa utamaduni wetu. Fikiria kufanyika mtu kwa Yesu. Mungu alimtuma Yesu kama mtume kutwambia habari njema. Hakuja kama mfalme hata kama alistahili kuabudiwa na kila mtu. Aliwacha pahali pake pa utukufu mbinguni na kuja kama mtoto asiye na uwezo. Alijifunza utamaduni wa Wayahudi kama mvulana mdogo.
Alipofundisha, watu walimsikiza, sio kwa sababu alikuwa mwenye nguvu au mashuhuri. Walimsikiza kwa sababu walijua maneno
yake yalitoka kwa Mungu. Wale ambao hawakupenda yale aliongea walimuua. Kwa sababu ya upendo wake kwetu, alivumilia hivi vitu vyote. Hangetuokoa kwa njia nyingine yoyote.”
“Lakini wanafanyaje hayo?’ Bwana Pumbavu anauliza. “Hawawezikuwa watoto tena na kukua kwa utamaduni mpya!”
Bwana Hekima anaitikia, “Hatuwezi kuwa watoto lakini tunaweza ingia katika utamaduni mwingine kwa njia kama ya kitoto. Tunajinyenyekesha  jinsi  Yesu  alifanya,  na  kujifunza  lugha  na  utamaduni  toka  kwa  wale  watu.  Tunawaachilia  watufundishe.


56
Hadithi Za Mchungaji

Tunajenga uaminifu na uhusiano wa upendo, kama vile Ruthu alivyofanya, alipohamia katika utamaduni mwingine, ule wa Israeli. Alishikana na Waisraeli kwa sababu aliwapenda, kuanza na mama mkwewe, Naomi.”
Msaidizi anaongezea, “Wakati tunawajua watu vyema, tutajua jinsi ya kuwaambia habari njema kwa maneno ambayo wanaelewa. Mtume Paulo alisema katika 1 Wakorinto 9:19-23 kwamba kwa Wayahudi alifanyika Muyahudi, na kwa mataifa wengine alikuwa kama wao. Alifanyika kama wengine kwa jinsi ingewezekana, kuwaleta kwa Kristo. Nafikiria itakuwa raha!”
Bwana Hekima anasema, “Niliwaletea somo. Linaorodhesha namna mitume wanavyoweza iga kufanyika mtu kwa Kristo kama
Paulo alivyofanya:
a). Nenda kaishi kati ya watu; ishi jinsi waishivyo, isipokuwa dhambi. b). Pata Msaidizi, akusaidie ujifunze ile lugha.
c). Chagua sentensi chache za kujifunza kwa lugha yao kila ziku.
d). Nenda matembezi na fanyia mazoezi hizi sentensi na watu hamsini unaoweza kuwapata siku hiyo.
e). Ukisha jua lugha yao vyema, anza kusema hadithi za Biblia juu ya Mungu na Mwanawe Yesu Kristo. f). Angazia wale wanakupokea na kuwapuuza wale wanakupinga hadi wakati mwingine.
g). Ongea na wakuu wa nyumbani. Hii inafanya iwe rahisi kwa jamii nzima kuja kwa Kristo.
Bwana Hekima anaendelea kumfafanulia Msaidizi na Recho, “Wakati watu toka utamaduni mwingine wanakuja kwa Kristo, tunapaswa  kuwa  makini  kuwafundisha  amri  za  Kristo  na  za  mitume  na  sio  utamaduni  wetu  sisi  wenyewe.  Wacha  wenyewe waendeleze  utamaduni  wao  wanapoendelea  kukua.  Ikiwa  tutaingiza  kitu  kingine  kando  na  Biblia  kwao,  tutawachanganyisha. Watafuata utamaduni wetu badala ya Kristo. Nyingi za tamaduni ni nzuri, lakini tukichukuwa desturi moja hadi nyingine, huwa karibu kila wakati, zinasababisha madhara. Tutawaambia tu kuhusu Kristo na kuwabatiza wale wanatubu na kumwomba Mungu msamaha katika Jina la Yesu. Halafu tutawakusanya kama mwili wa kanisa kumwabudu Mungu na kumtumikia kwa upendo.”
“Hebu tuanze punde iwezekanavyo!” Msaidizi anasema kwa furaha, “Punde tu litakapopatikana kundi la waumini waliobatizwa, tutawafundisha sehemu za msingi za ibada—sifa, maombi, toba, kukiri dhambi na Meza ya Bwana, Neno, Kutoa na Ushirika. Nitawafundisha kuimba sifa kwa mtindo wa musiki wa utamaduni wao. Tutawasaidia kutii amri zote za Kristo. Tutawapa vifaa vya kusoma na kutumia Maandiko, jinsi tu ulivyotufanyia sisi, Bwana Hekima. Wale wanaochunga familia zao tutawachagua kama wazee wa makutano wapya.”
Recho anakubali kwa shauku na Bwana Hekima anatamatisha, “Tunapowafundisha wazee wapya tutaondoka. Tutakuwa tukiwatembelea mara kwa mara kushauri viongozi wao, lakini hatutaongoza makutano yao. Mungu atainua viongozi kati yao haraka, jinsi alivyofanya katika Matendo, na tutawafundisha.”

Mitume Wakabiliana na Desturi Mpya.
Bwana Pumbavu anadhihaki, “Hamwezi kuanzisha makanisa hadi muwe na pesa za kuwalipa wachungaji wao na kujenga
kanisa.”
“Tumejadili hili mara nyingi.” Bwana Hekima anajibu. “Wakati pesa hazipo, hatuwachi hilo lisimamishe kazi ya Bwana. Tunaendelea kukutana manyumbani. Lazima kuna zaidi ya makanisa ndogo lakini zilizonawiri za nyumbani ulimwenguni hivi leo, kama ile ilikutana nyumbani mwa Filemoni. Paulo aliwasalimu katika Filemoni 2.
“Huwezi unda makanisa mapya haraka hivyo!” Bwana Pumbavu anaendelea kupingana. Wale watu ni tofauti sana na sisi. Wataingiza desturi zao za kigeni katika makanisa mapya, vile tu wale wageni walioko kule mtoni wamefanya. Wanaimba nyimbo kwa njia tofauti inayoumiza maskio yangu na wanakula vyakula ambavyo siweziguza. Hawatumii sherehe na utaratibu wetu. Watu wa utamaduni mwingine ni lazima wajifunze desturi zetu zote kabla waweze kuwa Wakristo!”
Bwana Hekima anapiga kite ya huzuni, “Ninasikitika kwamba wewe huelewi neema ya Mungu, Bwana Pumbavu. Hatuabudu orodha ya utaratibu na utamaduni. Tunamwabudu Kristo na kumtumikia kwa upendo vile aliamurisha. Hebu turudie hadithi ya Baraza la Kwanza la Kanisa.”


Tafuta katika Matendo Sura ya 15:
Zoezi.
•    Ni yapi ambayo waumini wa Kiyahudi walifundisha ambayo yalipinga neema ya Mungu katika mila za Kiantiokia?
•    Mungu anatuhitaji tufanye nini ili tuokoke?
•    Mungu alionyeshaje kuwa watu wote waweza kuokoka bila kuacha mila zao?
•    Hata kama hawakuwa chini ya Sheria, ni yapi Wakristo mataifa walihitajika kufanya kuepuka kuwaudhi waumini wenzao wa
Kiyahudi waliokuwa bado wanafuata sheria ya Agano la Kale?
•    Je, Baraza liliwahimizaje waumini?
Bwana Pumbavu anaenda zake. Hakuwahi hudhuria mkutano wowote tena.
Bwana Hekima naendelea kumuagiza Msaidizi na Recho kuhusu kazi ya utume. “Kitabu cha Matendo kinanukuu safari tatu za mtume Paulo. Wakati watu wake wenyewe, Wayahudi, walikataa ujumbe wa Paulo juu ya Kristo, aliwaendea Mataifa walioupokea. Waumini wengine wa Kiyahudi walisema kwamba waumini mataifa ni lazima wafuate utamaduni wote wa Wayahudi ili waokolewe. Paulo na Barnaba walipinga hili vikali. Walisema kuwa Mungu haitaji sisi tufuate sheria zozote au utamaduni wowote ndipo tuokoke. Mungu anatuokoa kwa Neema kupitia imani ndani ya Yesu Kristo jinsi tu tulivyo. Hatupaswi kubadili utamaduni wetu.”
Sara anasema, “Bwana Hekima, tutaheshimu kwa furaha utamaduni mwengine kule tutatumika kama watume.”
“Nilijua mtaweza. Mtume Paulo alilikumbusha Baraza la kule Yerusalemu juu ya kuja kwake Kornelio na watu wake. Walikuwa Mataifa, lakini walipomgeukia Mungu, aliwapa vipaji vya Roho Mtakatifu. Hili liliwathibitishia mitume kuwa Mungu amewakubali jinsi walivyo, bila kufuata desturi za Kiyahudi. Petero na wazaidizi wake wa Kiyahudi walifurahia na kuwabatiza siku hiyo. Baraza

57
liliamua kutowawekea Sheria ya Musa ya Agano la Kale. Badala yake, waliwaomba Mataifa wawache kuwaudhi majirani wao Wayahudi. Waumini wote walitiwa moyo, kwa sababu hili lilihifadhi kanisa la Kristo katika umoja. Lilikuwa na umoja, sio kwa sababu kila mtu alifuata utamaduni huo, bali ni kwa sababu wote waliokolewa kwa imani katika Kristo na wangefuata utamaduni mbalimbali kwa uhuru. Je, unakumbuka Maono ya Petero?”


Tafuta katika Sura ya 10:
Zoezi.
•    Ni mara ngapi Mungu alimwambia Petero aamuke, auwe na ale wanyama ambao walikuwa wamekatazwa kwa desturi zao?
•    Haya maono yalimsaidia Petero kukabiliana na desturi nyingine. Mungu alimtaka Petero awatendeje wageni?
•    Je, tunajifunza nini kutokana na maono na matendo ya Petero kuhusu  kukubali utamaduni tofauti?

“Naona,” Msaidizi anasema. “Tunawapa uhuru sawa watu wa desturi zingine ambao mtume Paulo aliwapa kwenye safari zake za utume. Hatutawahitaji kujifunza lugha yetu au kufuata mila zetu au mtindo wetu wa kuimba. Tutawafundisha kumgeukia Mungu anayewasamehe na kuwakubali jinsi walivyo. Atawapa kipawa cha Roho Mtakatifu jinsi alivyotupa tulipomgeukia. Roho Mtakatifu atawaongoza kwenye kweli yote. Atawahukumu kuhusu dhambi. Atawaonyesha ni desturi gani ambazo ni nzuri na gani zinapinga Ukuu wa Bwana Yesu Kristo.”
“Tutawatuma wewe na Recho,” Mwanafunzi anamwambia Msaidizi. “Tutawawekea mikono na kuwatuma na baraka zetu. Tutawaombea kwa uaminifu wakati wa ibada na kwenye makundi yetu madogo. Tutasaidia na vipaji ndogo ndogo vya upendo na kuwatembelea ikiwa tunaweza. Mtakuwa mabalozi wa Mungu kwa hao watu, na sisi tutakuwa wenzenu kwa kazi ya Mungu.
Tafadhali tutumie ripoti mara kwa mara ili tuweze kufurahia kila kitu chenye Bwana anafanya na kuombea msaada wakati kuna shida.
Hata kama makutano wapya mnaoanzisha hawawezi kufanana na hawa mkutano kwa nje, tutakuwa zote mwili mmoja katika Kristo. Anatuunganisha, sio kwa lugha, mila au utamaduni, lakini kwa Roho Mtakatifu ndani mwetu.”
Makutano wote wapya wa eneo hilo wanakutana kisiri usiku mmoja mahali palipotengwa, pasipoonekana na serikali. Wanaomba na kuwawekea mikono kwa Msaidizi na Recho, kuwatuma pamoja na Bwana Hekima na kufanya wafuasi wa Kristo kwa nchi ya
mbali.
Watatu waliotumwa wanasafiri kwa eneo jipya na wanaishi na familia zinazowasaidia kujifunza lugha yao. Wanafanya kazi kwa bidii kupata riziki yao. Wanavifanya vitu walivyojifunza toka kwa hadithi za mitume. Watu wanawaamini, kwa sababu wanafanya kwa bidii na kuonyesha mfano wa Yesu maishani mwao. Msaidizi anatuma ripoti kwa mkutano wake. “Watu wengi wanampokea Kristo. Tulibatiza idadi nzuri leo. Desturi zao ni tofauti sana lakini Mungu anabariki kazi yetu wakati tunaheshimu mila na desturi zao.”
Hiyo ripoti inaleta furaha na kuinua makutano waliowatuma Msaidizi na Recho moyo. Roho wa Mungu anafanya kazi kupitia hao kuzalisha makutano wapya ambapo hapakuwa na yoyote, jinsi tu alivofanya na Bwana Hekima wakati alianza kumfundisha Mwanafunzi kuwa kiongozi wa watu wa Mungu.