JIFUNZE KOZI HII YA UCHUNGAJI.
MASOMO HAYA YOTE UKIMALIZA UMEPIGA HATUA KUBWA KATIKA UTUMISHI.
SOMO LA 1
MUNGU
1.1 Uwepo wa Mungu
“Mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kuwa yeye yupo na
kwamba huwapa dhawabu wale wamtafutao” ( Ebr 11:6). Lengo la
masomo haya ni kuwasaidia wale wanomwendea Mungu, wakiisha
mwamini “Kwamba yupo”; kwa sababu hii hatutajitia kwenye
ushahidi usiothibitisha imani ya kuwa Mungu hayuko.katika
kupima muundo wa miili yetu (Zab 139:14) Ushahidi wa kielelezo
katika ua, Kukazia macho juu kwenye anga pana wakati wa usiku
kukiwa wazi bila mawingu, haya na mengine yasiyohesabika,
Mawazo ya kangaliifu juu ya maisha, hakika yanafanya imani ya
kutosadiki kuwa Mungu hayupo iwe ni ya kushangaza. Kusadiki
kuwa Mungu hayuko hakika inahitajika imani zaidi kuliko
kuamini yupo,pasipokuwepo Mungu mpangilio haupo, Kusudi au
kutoa maelezo ya asili ya Ulimwenguni basi hii itafikiriwa katika
maisha ya mtu asiyeamini kuwa Mungu yupo. Tukikumbuka hili,
siyo ajabu kuwa watu wengi wanakiri kwa kiwango fulani cha
kumwamini kuwa Mungu yupo hata katika jamii ambayo vitu vya
mwili ni Mungu anayeshinda maisha ya watu.
11
Lakini ipo tofauti pana kati ya kuwa na fikra isiyodhahiri ya
kwamba ipo nguvu ya juu, na hasa kweli kuwa na uhakika kwa kile
ambacho Mungu anampa mtu anayemtumikia kwa Uaminifu.
Waebrania 11:6 jambo hili tunasoma;
“Yatupasa tuamini kuwa (Mungu )yupo na
Kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao kwa bidii”
Maelezo mengi ya biblia ni historia ya watu wa Mungu
Israeli; mara kwa mara neno limetolewa kwamba kukubali kwao
kuwa Mungu yupo hakukulingana na imani zao kwa ahadi
zake.Waliambiwa na mkubwa kiongozi wao Musa'Kwa hiyo
ujue…….Ukaweke moyoni mwako, ya kuwa BWANA ndiye
Mungu katika mbingu juu, na katika nchi chini, hapana mwingine.
Basi, zishike sheria zake, na amri zake (Kum. 4:39:40).
Neno hili hili limetolewa - ufahamu wetu katikati yetu ya
kuwa Mungu yupo hakumaanishi kwamba tunakubalika mbele za
Mungu bila kufikiri.Ikiwa bila mchezo tunakubali kwamba kwa
kweli tunaye Muumba,'Kwa sababu hiyo tuzishike sheria na amri
zake’ Ni shabaha ya mfululizo huu wa masomo kuelezea amri hizi
jinsi zilivyo na namna ya kuzishika. Tunapochungunza maandiko
kwa kufanya hivi, tutakuta kwamba imani yetu kuwa Mungu yupo
inatiwa nguvu.
‘Imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la
Mungu’ (Rum 10:17). Vile vile,(Isaya 43:9-12) yaonyesha namna
ya kufahamu unabii wa Mungu kuhusu wakati ujao - Unabii
unatufanya tujue'kuwa mimi ndiye’ (Isa. 43:13)- yaani hilo jina la
Mungu, 'Mimi niko ambaye NIKO’ kwa ukamilifu ni kweli (Kut.
3:14.) Mtume Paulo alifika kwenye mji unaoitwa Beroya, eneo hili
kwa sasa liko kaskazini mwa Uyunani ( Ugiriki) kama kawaida,
12
akahubiri injili (Habari njema) ya Mungu; lakini badala ya watu
kusikia neno la Paulo alilokuwa anasema, tunasoma kwamba, “
Walilipokea kwa kusikia neno (la Mungu, sio la Paulo) kwa
uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone
kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo. Basi watu wengi miongoni
mwao wakaamini ( mdo 17:11,12)
Imani yao ilikuja kwa kuwa mioyo yao ilikuwa wazi, sawa
sawa (‘ Kila siku’) na kwa utaratibu wa (‘mambo hayo’)
waliyachunguza katika Biblia, Basi kupata imani ya kweli haikuwa
Mungu aliwafanya wawe nayo ghafla kwa aina fulani ya upasuaji
wa moyo wa kiroho, pasipo kujihusisha na neno la Mungu. Ni jinsi
gani basi watu wa Ulimwengu wanaweza kufuata kwa moyo
pigano juu ya maovu la Bill Graham au uamsho wa mikutano ya
wapentekoste kisha wanahama tena kama'Waamini’ ? Ni muda
gani wameendelea katika masuala haya wakiwa wanachunguza
maandiko kila siku ? Kwa kweli kukosekana huku kwa imani
ambayo msingi wake upo kwenye Biblia bila shaka kunaonyesha
utupu wa'Waongofu’ hawa na kujikuta baadae kwa wanayopata
Wakristo, na ni kwa sababu gani wengi wanaondoka kutoka
kwenye Ushirika wa Madhehebu ya wa-Injilisti.
Masomo haya lengo lake ni kukupa mjengo wa utaratibu
wako mwenyewe kuchunguza maandiko, ili kwamba nawe pia
uweze basi kuamini muunganiko kati ya kusikia Injili ya kweli na
kuwa na imani ya kweli mara nyingi kumejitokeza wazi katika
taarifa ya kuhubiri injili.
• “Wakorintho wengi waliposikia waliamini wakabatizwa”
(mdo 18:8)
• Watu wasikie neno la Injili, waamini ( mdo 15:7)
• Ndivyo tuhubirivyo, na ndivyo mlivyoamini'(1 Kor. 15:11)
13
• ‘Mbegu’ Kwenye mfano wa mpanzi ni neno la Mungu
(Luka 8:11) wakati katika huo wa mti wa haradali ni imani ( Luka
17:6) kwa kuona kwamba imani huja kutokana na kupokea'Neno
kwa imani’ ( Rum 10:8) “Maneno ya imani, na mafundisho
mazuri” ( 1Tim 4:6), katika moyo ambao upo wazi kumwamini
Mungu na neno lake (Gal 2:2, Ebr 4:2)
• Mtume Yohana anaisema taarifa iliyoandikwa ya maisha
ya Bwana kuwa anasema' kweli ( Yaani ukweli) ili nanyi mpate
kusadiki’ ( Yohana 19:35).Basi neno la Mungu limeitwa
‘Kweli’(Yoh:17:17) ili mpate kuamini.
1.2 Nafsi yake Mungu
Ni mwenye enzi, Mungu aliyeandikwa katika Biblia na
kwamba ni kweli, mtu wa kugusika, naye yupo katika umbo.
Vilevile ni mafunzo ya kwanza ya Ukristo kuwa Yesu ni mwana
wa Mungu. Ikiwa Mungu hana umbo , basi haiwezekani yeye
kuwa na mwana ambaye alikuwa ni 'Chapa ya nafsi yake' (Ebr 1:3)
Tena inakuwa vigumu kuendeleza maisha ya uhusiano wake na
mungu ikiwa Mungu ni wazo lililo kwenye akili zetu,
Mkusanyiko wa roho mahali popote juu katika anga lisilo na kitu.
Ni huzuni kusikia kwamba dini za watu wengi zina wazo lisilo la
kweli lisilotambulika kuhusu Mungu. Yeye akiwa mkubwa mno
kuliko sisi, inaeleweka ya kwamba imani ya watu wengi imeweka
kikwazo kwenye ahadi dhahiri kuwa mwishowe tutamwona
Mungu. Israeli walikosa imani ya kumwona Mungu alivyo (Yoh.
5:37) ni dhahiri ana umbo halisi, Imani hii huja kutokana na
kumjua Mungu kwa kuamini neno lake
14
Heri walio safi wa moyo, Maana watamwona Mungu (Math
5:8)
Na watumwa wake (Mungu) watamtumikia, nao watamwona
uso wake, na jina lake(Jina la Mungu ) litakuwa katika vipaji vya
nyuso zao (Uf 22:3-4)
Tumaini hili la ajabu kama kweli tunaliamini litaonyesha
matokeo ya matendo kwenye maisha yetu:
• Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote na huo
utakatifu, ambao hakuna mtu atakaye mwona Bwana asipokuwa
nao (Ebr 12:14)
• Tusiape, kwa kuwa aapaye kwa mbingu, Huapa kwa kiti
cha Mungu na kwa yeye na kwa yeye aketiye juu yake ( Math
23:22) hii itakuwa haina maana ikiwa Mungu sio mtu mwenye
mwili.
• Tutamwona kama alivyo (akidhihirika katika kristo ) na kila
mwenye matumaini haya katika yeye hujitakasa, kama yeye
alivyo mtakatifu (1 Yoh 3:2,3)
Katika maisha yetu haya kumfahamu Mungu wetu wa
mbinguni, hakujakamilika sana. Tunaweza kutazama mbele,
kupitia giza linalotatanisha la maisha haya hadi mwisho wa
kukutana naye. Kumwona kwa macho yetu hapana shaka kutakuwa
sawa na kumfahamu kwa akili zaidi. Kutoka vina vya masumbufu
ya mwanadamu. Ayubu aliweza kufurahia uhusiano wake wote na
Mungu ambao utimilifu wake atauona mwisho wa siku.
Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi (Yaani katika
mauti),Lakini pasipokuwana mwili wangu (Yaani pasipo mwili
unaoharibika ) nitamwona Mungu;Nami nitamwona mimi nafsi
yangu,na macho yangu yatamtazama, wala si mwingine (Ayubu
15
19:26,27). Mtume Paulo aliyatazamia maisha mengine yasiyo
machungu yasiyo na msukosuko: “Maana wakati wa sasa tunaona
kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; Wakati ule tutaona uso kwa uso” (
1Kor 13:12)
USHAHIDI WA AGANO LA KALE
Ahadi hizi zilizo katika Agano Jipya zimejengwa juu kwenye
ushahidi wa mambo yake makubwa ya Agano la kale, Kuwa ni
Mungu aliye na mwili. Ushahidi hauwezi kukaza zaidi lakini ni
mwanzo wa kukubali hali ya Mungu kama tunataka kuwa na
ufahamu wa kweli yoyote kuhusu dini ambayo msingi wake upo
kwenye Biblia. Agano la Kale lina mazungumuzo ya Mungu kuwa
ni mtu na mtu uhusiano wa mtu na mtu pamoja Mungu, ambao
Agano la Kale na Jipya linausema ni wa pekee kwa tumaini la
Ukristo wa kweli. Yafuatayo ni majadiliano ya nguvu kwa ajili
yake, Mungu aliye na mwili.
“Mungu akasema, Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura
yetu” (Mwa. 1:26) Hivyo mtu amefanywa kwa mfano na sura ya
Mungu, Kama ilivyodhihirika kupitia Malaika. Yakobo 3:9
anasema … Wanadamu waliofanywa kwa mfano wa Mungu.
Maneno haya hayatumiki kutaja mfano wa akili ya mwanadamu,
kwa kuwa hali ya fikra zetu zipo mbali kabisa toka zake Mungu na
katika njia nyingi kwa kikubwa zimepingana na haki
yake.”Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si
njia zangu, asema Bwana. Kwa maana kama vile mbingu zilivyo
juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia
zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu” ( Isa 55:8 - 9 ).
Kwa hiyo mfano na sura, tunavyoshirikiana naye Mungu, inabidi
uwe ni mfano wa mwili- Lakini yeye hana wa dhambi.
16
Popote Malaika walipoonekana duniani wamesemwa kuwa
wana umbo la watu, kwa mfano, Abrahamu aliwakaribisha malaika
bila kujua, akizania kuwa walikuwa watu wa kawaida. Sisi jinsi
tulivyoumbwa kwa mfano wa Mungu kwa kweli maana yake ni
kwamba tunaweza kufahamu jambo lingine kuhusu mtu halisi,
ndivyo tulivyo, lakini tunafanana. Basi, Mungu tunaye mshabihi
siyo mtu mwingine asiyedhahiri ambaye hatuwezi kumfikiria.
“Wao wenyewe Malaika wanafanana na Mungu. Hivyo
Mungu aliweza kumsema Musa, “Kwake nitanena mdomo kwa
mdomo, maana wazi wazi wala si kwa mafumbo. Na umbo la
Bwana yeye ataliona” (Hesabu 12:8) Haya yalikuwa yanamtaja
Musa, akifunzwa na Malaika aliye kuwa na jina la Bwana (Kut.
23:20:21) Ikiwa Malaika alikuwa na umbo la Bwana, Inaonyesha
kuwa Mungu amefanana na Malaika Yaani - Kimwili ana umbo la
Mwanadamu. “BWANA alisema na Musa uso kwa uso kama vile
mtu asemavyo na rafiki yake. (Kut. 33:11: Kum. 34:10 ). Bwana
alijidhihirisha katika Malaika wake, ambaye uso na kinywa
alifanana na Bwana mwenyewe.
“Kwa maana yeye anatujua umbo letu, (Zab. 103:14).Ana
tutaka yeye, tumfikirie kuwa ni mtu, Baba ambaye tunaweza
kuunganishwa naye.Huyu ataelezwa kwa ushahidi mwingi wa
mikono ya Mungu, Viganja,Macho n.k. Ikiwa Mungu alikuwa ni
furushi la Nafsi mahali fulani katika mbingu, ambazo inabidi ziwe
Mungu, ni wazo letu kama tukitaka utu wake; basi ushahidi huu
unatupotosha kukuza kusudi lolote.
“Maelezo ya sehemu ya makao ya Mungu, Wazi wazi
yanaonyesha kwamba “Mungu” ana mahali pake; “Mungu yuko
Mbinguni”( Mhubiri 5:2);Maana ametazama toka patakatifu pake
pa juu, toka mbinguni BWANA ameiangalia nchi (Zab 102:19,20);
17
“Usikie huko mbinguni, Makao yako” (1Fal. 8:39). Lakini kwa
kupambanua zaidi kuliko hivi tunasoma kwamba Mungu ana “Kiti
cha Enzi” (2 Nya. 9:8, Zab 11:4; Isa. 6:1,66:1).Lugha kama hii ni
ngumu kuitumia nafsi isiyo wazi kabisa, inayokaa katika milki ya
Kimbingu. Mungu amesemwa kuwa “Ameshuka kuja chini”
wakati mwenyewe anapojidhihirisha. Hapa panadokeza makao ya
Mungu yaliyo mbinguni. Inakuwa vigumu kueleza wazo la
udhihirisho wa Mungu bila kukubali hali ya umbo la Mungu. Isaya
45 ina ushahidi tele wa Mungu kujihusisha kwake katika mambo
ya watu wake: “Mimi ni BWANA, wala hapana mwingine …..,
mimi ni BWANA anayetenda haya yote …., Mimi, BWANA
nimeiumba Ole wake ashindanaye na Muumba wake … Mimi,
naam, mikono yangu mimi, imezitanda mbingu …, niangalieni
mimi mkaokolewe, enyi ncha zote za dunia. mstari hasa kweli huu
wa mwisho unaonyesha uwepo wake Mungu - Anawataka watu
wamwangalie yeye, Kuwaza uwepo wake halisi pamoja na jicho la
imani.
Mungu amejifunua kwetu akiwa ni mwenye kusamehe
anayesema, maneno kwa watu. Hata hivyo msamaha na usemi
unaweza tu kutoka kwa mtu: ni matendo ya akili, Hivyo Daudi
alikuwa ni mtu aliyeupendeza moyo wa Mungu (1 Sam 13: 14),
inaonyesha kwamba Mungu ana moyo, unaoweza kunakiliwa kwa
kiwango kidogo na mtu, ingawa mwanadamu wa mwili
haupendezi moyo wa Mungu. Mafungu ya maneno kama BWANA
akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani akahuzunika
moyo (Mwa. 6:6), hufunua hisia ya Mungu, mwenye ufahamu
kuliko kuwa kishindo cha roho ya kuwazika katika hewa. Hapa
tunasaidiwa tukubali jinsi kwa kweli tunaweza pande zote mbili
kumpendeza na kutokumpendeza, Kama mtoto anavyoweza kwa
baba wa mwili.
18
IKIWA MUNGU SI MTU MMOJA
Kama Mungu si wa kweli, mmoja mwenye kuwepo, Basi
wazo la kupenda mambo ya roho ni vigumu kushikana nayo.
ikiwa Mungu ni mwenye haki kabisa lakini si mtu mwenye umbo,
basi kwa kweli hatuwezi kuiwazia haki yake ilivyodhihirika kwa
watu. Pande zote mbili, Ukristo uliokenguka na wayahudi wana
wazo la kwamba haki ya Mungu inaingia katika maisha ya watu
kwa njia ya
‘Roho Mtakatifu’ Asiyedhahiri ambaye kwa namna
isiyoeleweka tunafanywa mfano kwenye akili ya Mungu, na
kukubalika kwake. Kwa maneno mengine, mara tukitambua ya kwa
mba yupo mtu mwenyewe aitwaye Mungu, basi tunaweza
kurekebisha tabia yetu kufuata atakavyo, Kwa msaada wake
utokao kwenye ushawishi wa neno lake na kwa kuleta sifa
inayoonyesha tabia ya Mungu katika utu wetu.
Lengo la Mungu ni kujidhihirisha mwenyewe katika mkutano
wa watu waliotukuzwa. Jina la kumbukumbu yake, YEHOVA
ELOI, linamaanisha hivi ( Atakaye kuwa kwa wenye nguvu ni
tafsiri iliyo karibu sahihi.) ikiwa Mungu si mtu mwenye umbo,
basi thawabu ya waaminifu katika ufalme wa Mungu ujao duniani
inaonyesha ya kwamba watakuwa nayo wazi tena dhahiri
wakiwepo katika mwili, Ingawa hawatakuwa katika udhaifu wa
mwili wa Mwanadamu tena. Ayubu alitamani' Siku ya mwisho’
atakapofunguliwa na mwili wake ( Ayubu 19:25:27); Abrahamu
itabidi awe mmojawapo wa wale wengi wa hao walalao katika
mavumbi ya nchi ambao wataamka…… Kwa uzima wa Milele wa
nchi ya Kanani (Dan. 12:2) hivyo basi ataweza kupata ahadi ya
urithi wa milele wa nchi ya kanaani, Sehemu inayoonekana katika
dunia hii
(Mwa. 17:8.) “ Na wataua wake watashangilia….. waimbe
kwa sauti kuu vitandani mwao….. ili kufanya kisasi juu ya
19
mataifa (Zab 132: 16; 149: 5,7) Kushindwa kwa watu wote wa
pande mbili, Wayahudi na watu wa mataifa,
Kutambua mafungu ya maneno kama haya vyema, kwa
ukubwa wa maneno yenyewe Kuletwa ahadi za kuonekana kwa
Abrahamu, kumeongoza watu kwenye imani potovu la' Nafsi haifi’
ya kwamba Mwanadamu halisi anakuwepo hai akifa. Wazo hili
halina msaada wa Biblia kabisa. Mungu hapatikani na mauti, Mtu
mwenye utukufu, analifanya lengo lake, ili kwamba wanaume na
wanawake waweze kuitwa na kuishi katika ufalme wake ujao
kwenye dunia hii, Kushiriki sifa, zilizoelezwa katika umbo la
mwili.
Waaminifu wameahidi wa kwamba watarithi mwili wa
Mungu (2 Pet. 1:4) Ikiwa Mungu si mtu mmoja, basi hii ina maana
tutaishi milele kwa roho zisizo na mwili. Lakini hili si fundisho la
Biblia. Tutapewa mwili kama ule wa Yesu. (Flp. 3:21), Nasi
tunajua kwamba tutakuwa na mwili halisi kwenye ufalme mwili
utakaokuwa na mikono macho na masikio (Zek. 13:6, Isa. 11:3 ),
mafunzo ya Mungu kuwa ni Mmoja, kwa sababu hii yanasimulia
Injili ya Ufalme.
Itakuwa wazi kwamba hakutaweza kuwa na wazo la kujua
Ibada, dini au uhusiano mmoja na Mungu mpaka itambulike
kuwa Mungu ni mtu mmoja, na kwamba kwa mwili sisi ni mfano
wake. Ingawa ni mfano usio kamili sana unahitajika kuukuza
kufuata mfano wa akili yake, Hivyo basi, tutaweza kupata
utimilifu wa mfano wake unaoonekana katika ufalme wa Mungu.
Maana nyingi zaidi na faraja tunaweza kupata kutoka mafunzo ya
maneno ambayo yanamtaja Mungu kuwa ni Baba aliye na upendo,
akiturudi kama Baba afanyavyo kwa mwanae (mfano. Kum. 8:5).
Katika maneno yenyewe ya mateso ya Kristo tunasoma
20
kwamba,'Lakini BWANA aliriidhika kumchubua’ (Isa. 53:10
),Ingawa “Alimlilia Mungu” aliisikia sauti yangu…….. Kilio
changu kikaingia masikioni mwake (Zab.18:6). Ahadi ya Mungu
kwa Daudi kuhusu mzao atakaye kuwa ni mwana wa Mungu
ilitakiwa azaliwe kwa Muujiza kwa Mwanadamu; Ikiwa Mungu
hakuwa ni mtu mmoja, asingekuwa na mwana huyo.
Kumfahamu Mungu kwa usahihi ni ufunguo unaofungua
maneno mengi mengine ya muhimu katika mafundisho ya Biblia.
Lakini kama uongo mmoja huongoza kwenye uongo mwingine,
Hivyo dhana potovu juu ya mungu inaficha utaratibu wa kweli
ambao maandiko yanatoa. Kama umepata kuona kuwa hii sehemu
inadhibitisha, au hata ikiwa ni ndogo, basi, swali linakuja. Je?
Unamjua Mungu kweli?. Sasa tutachunguza maandiko ya Biblia
zaidi kuhusu yeye.
1.3 Jina La Mungu Na Tabia Ya Sifa Yake
Ikiwa Mungu yupo, inafaa kufikiri kuwa atakuwa amevumbua
njia nyingine ya kutuambia habari zinazo mhusu yeye mwenyewe.
Tunaamini ya kwamba Biblia ni ufunuo wa Mungu kumjulisha
Mwanadamu, na humo ndani ya kitabu tunaona kudhihirika tabia
ya sifa ya Mungu. Hii ndio sababu Neno la Mungu linasemwa
kuwa ni'Mbegu’ yake (1 Petro 1:23) Kwa kuwa kama likigeuza hali
ya mioyo yetu, kiumbe mpya anaumbwa ndani yetu ambaye ana
sifa za Mungu (Yakobo. 1:18, 2Kor. 5:17). Kwa hiyo sisi
wenyewe tunapotumia zaidi neno la Mungu na kuchukua masomo
sisi wenyewe, ndivyo zaidi tutafanana mfano wa mwana wake (
Rum, 8:29) ambaye kwa tabia ya sifa alikuwa mfano kamili wa
Mungu (Kol. 1:15).Kwa hii imelala thamani ya kusoma sehemu za
historia ya Biblia, Zimejaa kadhia ya masomo jinsi Mungu
21
alivyojishughulisha na watu pamoja na matifa, Daima akionyesha
msingi ule ule wa sifa.
Katika Kiebrania jina la mtu mara nyingi lilileta tabia ya sifa
zao au taarifa zinazowahusu. Mifano mingine iliyowazi:
• ‘Yesu’'Mwokozi’ Kwa kuwa atawaokoa watu wake kutoka
dhambi zao’ (Math. 1:21)
• ‘Abrahamu’'Baba wa mkutano mkubwa’ Maana
nimekufanya kuwa baba wa mataifa mengi’(Mwa. 17:5)
• ‘Hawa (Eva)'Uhai’ Kwa kuwa alikuwa mama wa wenye
uhai wote (Mwa. 3:20)
• ‘Simeoni’'Kusikia’ Kwa kuwa bwana amesikia kwamba
nalichukiwa, kwa sababu amenipa mwana huyu (Mwa. 29: 33).
Katika Yeremia 48:17, kuwajua watu wa Moabu ni sawa sawa
na kufahamu jina la moabu.Mara nyingi zaburi zinamlinganisha
Mungu mwenyewe na jina lake, neno lake na matendo (Zab. 103:1,
105:1, 106:1,2,12,13.) Kwa sababu hii itegemewe kwamba majina
ya Mungu na heshima vitatupatia habari nyingi kuhusu yeye
mwenyewe, kwa kuwa yapo maelekeo mengi ya tabia ya sifa na
kusudi kwa kweli ana jina zaidi ya moja.Somo lenye kueleza
jambo moja moja la jina Mungu linafaa baada ya Ubatizo;
kufahamu zaidi sifa na tabia ya Mungu kumeelezwa katika jina
lake, ni jambo lingine ambalo liendelee wakati wa maisha yetu
yote katika Bwana. Linalofuata sana kwa hilo, mengi ni Utangulizi.
Musa alipotaka aelimishwe kwa undani kuhusu Mungu ili
imani yake iimalike wakati wa kipindi kisicho sahaulika sana cha
maisha yake. Malaika,'Alitangaza
jina
la BWANA:
BWANA,BWANA Mungu, Mwingi wa huruma, Mwenye fadhili,
Si mwepesi wa hasira, Mwingi wa rehema na kweli, Mwenye
kuwaonea huruma watu elfu elfu, Mwenye kusamehe uovu na
22
makosa na dhambi; Wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu
kuwa hana hatia,’ (Kut. 34:5-7)
Huu ni ushahidi ulio wazi wa kwamba majina ya Mungu
yanaweka sifa zake.Tendo la kuwa nazo ni uhakika kuwa ni mtu
mmoja, si busara kufikiri ya kwamba fungu la roho laweza kuwa
na dalili na sifa ya tabia hizi ambazo vile vile zaweza
kuendelezwa ndani yetu wanadamu.
Mungu amechagua hasa jina moja ambalo amependa ajulikane
na kukumbukwa na watu wake, ni kwa ufupi, maelezo mafupi, ya
kusudi lake kwa watu.
Israeli walikuwa watumwa Misri, Walihitajika kukumbushwa
lengo la Mungu kwao. Musa aliambiwa awaambie Jina la Mungu,
ili kwamba hili liwasaidie kuwaletea kusudi la kuondoka Misri na
kuanza safari kuelekea nchi ya Ahadi (1Kor. 10:1) Nasi pia
tunahitajika kuelewa mambo ya msingi yahusuyo jina la Mungu
kabla ya kubatizwa na kuanza safari yetu ya kuelekea Ufalme wa
Mungu. Mungu aliwaambia Israeli kuwa Jina lake alikuwa
YAHWEH-YAHU (Zab 89:8 uv); Maana yake“Mimi niko ambaye
NIKO” au limetafsiriwa kwa usahihi zaidi,'Nitakuwa ambaye
Nitakuwa’(Kut 3:13-15) Jina hili, kidogo likapanuka wakati ule:”
Tena Mungu akamwambia ( Ikiwa ni nyongeza) Musa, Hivi
ndivyo utawaambia wana wa Israel, BWANA (Yahweh) Mungu
wa Babu zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, Mungu wa
Yakobo, ….Hili ni Jina langu Milele, la kumbukumbu yangu kwa
vizazi vyote. (Kut. 3:15). Kwa sababu hiyo jina kamili la Mungu ni
“BWANA Mungu”
Zaidi Agano la kale liliandikwa kwa Kiebrania na tafsiri ya
Kiswahili ni lazima kutukia visivyo sawa sawa wakati ujapo wa
kutafsiri maneno ya Kiebrania hasa neno “Mungu” mengi ya
23
maelezo moja moja yakosekana - Tafsiri yetu ya Kiswahili
imetoka kwenye Kiingereza. Moja ya maneno yanayotumiwa na
Kiebrania limetafsiriwa'Mungu’ ni Elohim (ELOI) maana
yake'Wenye Nguvu’ Kumbukumbu ya jina la Mungu, jina ambalo
anatutaka tumkumbuke, kwa sababu hiyo.
YAHWEH ELOHIM - YAHU ELOI
Maana yake
ATAKAYEDHIHIRIKA KATIKA KUNDI LA WENYE
NGUVU.
Kwa hiyo ni kusudi la Mungu kuidhihirisha tabia ya sifa yake,
Umuhimu wake katika kundi kubwa la watu. Kwa kulitii neno lake
tunaweza kukuza sifa zingine za Mungu ndani yetu wenyewe
sasa, hivyo basi kadri ya busara sana. Mungu alijifunua
mwenyewe kwa waamini wa kweli katika maisha haya.lakini jina
lake Mungu ni la Unabii wa wakati ujao hapo dunia itakapo jaa
watu watakao kuwa sawa naye, pande mbili kwa tabia na mwili
(2Petr 1:4). Ikiwa tunataka kuungana na lengo la shabaha ya
Mungu na kuwa kama Mungu bila hata kufa tena, kuishi milele
katika uadilifu wote uliokamilika, basi yatupasa sisi wenyewe
tujiunge na jina lake.
Namna ya kufanya hivi ni kubatizwa katika jina, yaani la
Yahweh Elohim (Math. 28:19). Hili linatufanya tuwe watoto
(‘Uzao’) wa Abrahamu (Gal,. 3:27-29) uliohaidiwa kurithi milele
nchi (Mwa. 17:8; Rum. 4:13) Kundi la wenye nguvu (Elohim Eloi)
ambao unabii wa jina la Mungu utatimilika. Limeelezwa
zaidi kwa habari katika somo la 3.4.
24
1.4 Malaika
Yote ambayo tumeyapima sana katika somo hili yanaletwa
pamoja kwenye tafakari ya Malaika:
• Viumbe walio na mwili
• Huchukua jina la Mungu
• Wao ni njia ambayo roho wa Mungu anatenda kazi ya
kutimiza mapenzi yake
• Wanapatana tabia na kusudi lake
• Na kwa hiyo wanamdhihirisha yeye.
Tumetaja kwenye somo la 1.3 ya kwamba moja kati ya
maneno yanayotumika zaidi katika Kiebrania lililotafsiriwa
“Mungu” ni' Eloi’ ambalo hasa maana yake ' Wenye nguvu’
hawa,'Wenye nguvu’ ambao huchukua jina la Mungu
wanapotokea wana weza kuitwa 'Mungu’ kwakushirikiana kwao
pamoja na naye karibu. Hawa viumbe wanaitwa Malaika.
Taarifa ya uumbaji wa ulimwengu katika mwanzo 1
inatuambia ya kwamba Mungu alitamka amri halisi kuhusu
Uumbaji'Ikiwa hivyo’ walikuwa ni Malaika waliotimiza amri hizo:
“Enyi Malaika zake, mliohodari mtendao neno lake,
mkiisikiliza sauti ya neno lake (Zab. 103:20).
Kwa sababu hii busara husadiki kuwa tunaposoma 'Mungu’
akiumba ulimwengu, kazi hii kweli ilifanywa na Malaika. (Ayubu
38:4-7) anadokeza vile vile namna hii. Sasa ni wakati mzuri
kuelezea kwa kifupi matukio ya uumbaji kama yalivyoandikwa
Mwanzo 1:
25
Siku ya Kwanza‘ Mungu akasema, Na iwe nuru, Ikawa’
(Mstari 3)
Siku ya Pili
'Mungu akasema, Na iwe anga katikati ya
maji, likayatenga maji na maji.Mungu akalifanya anga ,akayatenga
yale maji yaliyo juu ya anga na yale yaliyo chini ya anga: Ikawa
hivyo’ (Mstari 6,7)
Siku ya Tatu ‘Mungu akasema, Maji yaliyo chini ya
mbingu na yakusanyike mahali pamoja, (akifanya Bahari na
Bahari kuu) ili pakavu paonekane; Ikawa hivyo’ (Mstari wa 9)
Siku ya Nne ‘Mungu akasema, Na iwe mianga katika
anga la mbingu… Ikawa hivyo’ (Mstari 14:15)
Siku ya Tano ‘Mungu akasema, Maji na yajae kwawingi
na kitu kiendacho chenye uhai …. ndege waruke juu ya nchi …..
Mungu akaumba kila kiumbe chenye uhai (Mstari wa 20:21),
Ikawa hivyo.
Siku ya Sita ‘Mungu akasema, Nchi na izae kiumbe
haikwa jinsi zake…. Mnyama wa kufugwa,nacho kitaambaacho
…. Ikawa hivyo (Mstari 24)
Siku hiyo hiyo ya sita mtu aliumbwa. Mungu akasema, na
tufanye mtu kwa mfano wetu, na kwa sura yetu (Mwa 1:26).
Tuliwahi kutoa maelezo juu ya mstari huu katika somo la 1.2.
Kwa muda uliopo, tunataka kujua hapa ya kwamba.'Mungu’ sio tu
anatajwa Mungumwenyewe katika utu'Na tufanye mtu’ inaonyesha
kuwa Mungu anatajwa mtu zaidi ya mmojaNeno la Kiebrania
linalotafsiriwa hapa'Mungu’ ni Elohim (Eloi), Maana yake'Wenye
nguvu’ Ukiwa ni ushahidi unaotaja Malaika. Ukweli ni kwamba
26
Malaika walituumba sisi kwa mfano wao maana yake ni kuwa
wana sura ya mwili ule ule kama tulio nao. Kwa sababu hiyo ni wa
kweli, wa kugusika, viumbe wenye mwili, wakishiriki mwili ule
ule kama wa Mungu.
‘Mwili’ Kwa maana hii unatajwa kwa msingi jinsi mtu
mwingine alivyo kwa sababu ya muundo wa mwili wao. Katika
Biblia ipo “Miili” ya aina mbili katika maana halisi ya neno
haiwezekani kwa wakati huo huo kuwa miili hii ya aina mbili.
Mwili wa Mungu (‘Mwili wa Uungu’)
Hauwezi kutenda dhambi (Mkamilifu) Rum 9:14,6:23;
Zab. 90:2, Math 5:48,Yak 1:13)Haupatikani na Mauti ( 1Timotheo
6:16)
Una nguvu tele na uweza ( Isaya 40:28)
Huu ndio mwili wa Mungu na Malaika na ambao alipewa
Yesu baada ya kufufuliwa (Matendo 13:34; Ufunuo 1:18; Ebr.
1:3) Huu ndio mwili ambao tumeahaidiwa kupewa (Luka
20:35,36; Isa. 40:28,31)
Mwili wa mwanadamu
Hujaribiwa na kutenda dhambi ( Yak 1:13-15 )kwa nia mbaya
ya asili (Yer 17:9; Marko 7:21-23) Huangamia mautini, Yaani
unapatwa na kifo ( Rum. 5:12,17; 1Kor 15:22) Una kikomo cha
nguvu, sehemu mbili, kwa mwili (Isa. 40:30) na kwa akili ( Yer
10:23)
Huu ni mwili ambao watu wote, wema na wabaya, kwa sasa
wanao mwisho wa mwili huo ni kifo (Rum 6:23). Ulikuwa ni
mwili ambao Yesu alikuwa nao wakati wa maisha yake ya mwili
27
unaokufa hapa duniani (Ebr. 2:14-18,Rum. 8:3 Yoh 2:25, Marko
10:18)
MATENDO YA KUONEKANA NA MALAIKA
Malaika wakiwa na mwili wa Uungu, inabidi wawe hawana
dhambi na kwa sababu hiyo hawawezi kufa kwa kuona kwamba
dhambi huleta mauti (Rum. 6:23). Inapasa wawe na umbo halisi na
mwili wa kuwepo mauti “Na yaletwe basi maji kidogo ukanawe
miguu, mkapumzike chini ya mti huu”(Mwanzo 18:4)
Wawili kati ya hao Malaika wakati ule walikwenda kwa lutu
katika mji wa Sodoma. Tena, walitambuliwa kuwa ni watu na lutu
pamoja na watu wa Sodoma.'Basi, wale malaika Wawili wakaja
Sodomaa jioni aliowakaribisha wakae kwake usiku. Lakini watu
wa Sodoma wakaja kwenye nyumba yake, wakiuliza kwa namna ya
kutisha,'Wawapi wale watu waliokuja kwako usiku huu ?’ Lutu
akawasihi,' Watu hawa msiwatende neno’ Taarifa ya maandiko ya
Mungu pia inawaita ni'Watu’, Wale watu ( Malaika )
wakanyoosha mikono yao, wakamwokoa Lutu, Basi wale watu
wakamwambia Lutu … BWANA ametutuma tuuharibu Sodoma
(Mwanzo 19: 1,5,8,10,12,13).
Ufafanuzi wa Agano jipya juu ya matukio haya
yanadhibitisha kwamba Malaika wanafanana na umbile la watu.
“Msisahau kuwafadhili wageni; Maana kwa njia hii wengine (Kwa
mfano Lutu na Abrahamu ) waliwakaribisha Malaika pasipo kujua
(Ebr 13:2)
Yakobo alishindana usiku kucha na mtu mmoja ( Mwa 32:24)
ambaye baadae tumeambiwa kuwa alikuwa Malaika (Hosea 12:4)
28
Watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe
walikuwepo kwenye ufufuo (Luka 24:4) na wakati wa kupaa (Mat.
1:10) Yesu, kwa uhakika hawa walikuwa ni Malaika. Ona
vidokezo vya'Kipimo cha Kibinadamu, maana yake cha Malaika’
(Uf 21:17).
MALAIKA HAWATENDI DHAMBI
Malaika wakiwa na mwili wa Uungu, hawawezi kufa, kwa
sababu dhambi huleta mauti, Basi wao hawawezi kutenda dhambi.
Maneno ya asili katika lugha ya Kiyunani na Kiebrania
yaliyotafsiriwa'Malaika’ maana yake ni mjumbe; Malaika ni
wajumbe au watumishi wa Mungu, Watiifu kwake, Kwa hiyo
hawafikiriwi wao kuwa ni wenye dhambi. Kwa hivyo neno la
Kiyunani’Agelos’
lililotafsiriwa'Malaika’
vile vile
limetafsiriwa'Wajumbe’ Wanaposemwa wanadamu kwa mfano
Yohana mbatizaji, (Math 11:10) na wajumbe wake (Luk. 7:25)
wajumbe wa Yesu (Luk. 9:52) na watu walioupeleleza mji wa
Yeriko (Yak. 2:25). Kwa kweli inawezekana kwamba'Malaika’
katika maana ya wajumbe wanadamu wanaweza kutenda dhambi.
Mafungu ya maneno yafuatayo ni wazi kwamba Malaika wote
( Sio tu baadhi yao) kwa umbile ni watiifu kwa Mungu, na hivyo
hawawezi kutenda dhambi.
‘BWANA ameweka kiti chake cha Enzi mbinguni Na Ufalme
wake unavitawala vitu vyote (Yaani haiwezekani kuwepo uasi juu
ya Mungu mbinguni)Mhimidini BWANA, Enyi Malaika zake,
Ninyi mlio hodari, mtendao neno lake, Mkisikiliza sauti ya neno
lake Mhimidini BWANA, enyi majeshi yake Yote; Ninyi
watumishi wake mfanyao mapenzi yake (Zab. 103:19-21)
29
“Msifuni, enyi Malaika wake wote …. Majeshi yake yote (
Zab 148: 2 ) Je ! hao wote si roho (Malaika ) watumikao,
wakitumwa kuwahudumia wale watakaourithi wokovu ? ( Ebra. 1:
13,14 )
Kurudiwa kwa neno'Wote’ linaonyesha ya kwamba Malaika
hawajagawanyika katika makundi mawili, kundi moja zuri na
jingine lenye dhambi. umuhimu wa kufahamu vema umbile la
malaika ni kwamba thawabu ya waaminifu ni kushiriki mwili wao.
“Wale wahesabiwao kuwa wamestahili…. Hawaoi wala
hawaolewi … wala hawawezi kufa tena. kwa sababu huwa sawa
sawa na Malaika (Luk 20:35, 36).
Hili ni neno la muhimu kulishika. Malaika hawawezi
kufa'Maana hatwai asili ya Malaika (Kwa kuwa tangu asili
hawajatenda dhambi). Ila atwaa asili ya mzao wa Abrahamu ,sababu
ya dhambi’ (Ebr 2:16) Ikiwa Malaika waweza kufanya
dhambi, Basi wale ambao watakuwa wamestahili thawabu ya
Kristo atakapo kuja bado wataweza kutenda dhambi pia, Na kwa
kuwa dhambi huleta mauti (Rum 6:23) kwa sababu hiyo
hawataweza kuwa na uzima wa milele, kama tukiwa na uwezekano
wa kutenda dhambi ni kufanya ahadi ya Mungu ya uzima wa
milele haina maana, kwa kufahamu kuwa thawabu yetu ni
kushiriki mwili ule wa Malaika. Ushuhuda wa'Malaika (Luk.
20:35,36) unaonyesha kwamba hakuna aina ya Malaika wema na
wenye dhambi; ipo aina moja ya Malaika tu.
Ikiwa Malaika waweza kutenda dhambi, Basi Mungu
ameachwa hana nguvu za kutenda tendo la haki katika maisha
yetu na mambo ya ulimwengu, kwa kufahamu kuwa ameeleza
kwamba anafanya matendo yake kwa njia ya Malaika zake( Zab
103:19-21) Wamefanywa kwa'Roho wa Mungu katika maana ya
30
kwamba anatimiza yote kwa nguvu zake. Akitenda kazi katika
Malaika (Zab 104:4). Kwamba wanamwasi Mungu haiwezekani.
Mkristo amwombe kila siku, Mungu ili ufalme uje duniani, ili
mapenzi yake yafanyike kama sasa yanavyofanyika mbinguni
(Math 6:10) Ikiwa Malaika wa Mungu iliwapasa washindane na
Malaika wenye dhambi huko mbinguni, basi, kwa utimilifu
mapenzi yake hayakuweza kufanyika huko, na kwa sababu hiyo
hali hiyo hiyo itapatikana kwenye ufalme wa Mungu ujao.
Kutumia maisha ya milele kwenye ulimwengu ambao utakuwa ni
uwanja wa vita kati ya dhambi na utii, kwa shida hayo sio
matazamio ya kutia moyo, lakini hilo, kwa kweli, sio ndiyo suala
lenyewe.
MALAIKA NA WATU WANAOAMINI
Ipo sababu nzuri ya kuamini kuwa kila mwamini wa kweli ana
Malaika pengine mmoja maalumu-wa kuwasaidia katika maisha
yao:-
‘Malaika wa BWANA hufanya kituo, akiwazungukia na
kuwaokoa wamchao’ (Zab 34:7)
Mmojawapo wa wadogo hawa waniaminio (Yaani wafuasi
dhaifu- Zek, 13:7 Mat 26:31)…Malaika wao mbinguni siku zote
huutazama uso wa Baba yangu’ (Mat.
18:6,10)
Wakristo wa kwanza ni wazi waliamini kwamba Petro
alikuwa na Malaika mlinzi (Matendo 12:14,15).
Watu wa Israeli walipita katika bahari ya Shamu,
waliongozwa na malaika kwenye jangwa kuelekea nchi ya Ahadi.
Kutembea kupitia katika bahari ya shamu maana yake ni Ubatizo
wetu katika maji (1Kor 10:1), Hivyo nasi vile vile ina maana
tusadiki kuwa baadae tunaongozwa na kusaidiwa na Malaika
31
tunaposafiri katika jangwa la maisha kuel;ekea nchi ya ufalme wa
Mungu.
Ikiwa Malaika wana weza kuwa waovu katika maana ya
kuwa wenye dhambi, basi Ahadi hizi za Malaika kuongoza na
kushawishi katika maisha yetu zinakuwa laana badala ya Baraka.
• Basi tufahamu ya kuwa Malaika ni Viumbe………
• Wenye mwili ulio sawa na Mungu na huonekana kwa mwili
• Ambao hawawezi kutenda dhambi
• Daima hufuata amri za Mungu
• Wao ni njia ambayo Mungu katika Roho nguvu hunena na
• kutenda kazi (Zab. 104:4)
LAKINI..?
Makanisa mengi ya'Kikiristo’ yana wazo la kwamba Malaika
wanaweza kutenda dhambi, na kwamba Malaika wenye dhambi
sasa hivi wapo na wao wanahusika na dhambi pamoja na matatizo
yaliyopo hapa Duniani. Tutajadili zaidi vya kutosha juu ya
kutofahamu vema jambo hili kwenye somo la 6. Kwa sasa
tutatengeneza vipengele vifuatavyo:-
Inawezekana kwamba uumbaji ulikuwepo uliotutangulia sisi
wa kweli, yaani huo ulioandikwa katika Mwanzo 1. Pia inaweza
kusadikika ya kwamba Malaika waliopo walikuja kuwa na
fahamu za'Wema na Ubaya’ (Mwa. 3:5) walipo kuwa katika hali
kama hii tuliyonayo katika maisha haya.
Ya kwamba viumbe wengine walioishi kwa kipindi kile
walitenda dhambi hatujakatazwa kufikiri; lakini yote haya ni
mawazo ambayo mioyo ya watu hupenda kujishughulisha. Biblia
yatuambia kile ambacho tunakihitaji kujua kuhusiana na hali
iliyopo, ambayo ni kwamba hawapo Malaika watenda dhambi,
Malaika wote ni watiifu kwa Mungu kabisa.
32
Hawawezi kuwepo viumbe wenye dhambi mbinguni, kwa
kufahamu kuwa Mungu'ana macho safi na hawezi kuangalia
uovu’ (Ab. 1:3) katika maelezo haya, Zaburi 5:4,5 yatuambia:-
‘Mtu mwovu hatakaa kwako. wajivunao hawatasimama
mbele za macho yako’ yaani makao ya mbinguni. Jambo la
kwamba ulikuwepo Uasi juu ya Mungu mbinguni na Malaika
watenda dhambi ni wazo linalopingana kabisa na maneno
yaliyotolewa.
Neno
la kiyunani
lililotafsiriwa'Malaika’ maana
yake'Mjumbe’
linataja
wanadamu,
kama
tulivyoonyeshwa'Wajumbe’ wanadamu hawa wanaweza kwa
kweli kufanya dhambi.
Ya kwamba upo uovu, viumbe wenye dhambi ambao juu yao
mwelekeo wa maisha yote yasiyofaa wanaweza kutupiwa lawama
kwa kawaida ni moja ya Imani zaidi iliyoshikiliwa katika
Upagani.Kwa njia hiyo hiyo mambo yanayohusu Krismas
yameingia kwenye kile kinachodhaniwa ni'Ukristo’ Basi, vile vile
Ukristo una fikra hizo za Kipagani
Yapo mafungu ya maneno ya Bibilia yaliyojaa tele ambayo
yanaweza kutoeleweka kusaidia wazo hili la Malaika wenye
dhambi kwa sasa wapo. Haya yamepimwa katika 'Kumsaka
Shetani’ yanapatikana kwa wachapishaji - Mafungu haya ya
maneno hayawezi kuruhusiwa kupingana na mafunzo tele ya
Biblia kwa kutofautiana na haya yaliyokwisha tolewa.
33
Tumeacha Kitambo sehemu ya 1:'Mungu ni roho’
(Yohana 4:24)
Katika somo la pili tunafafanua kwa utaratibu zaidi jinsi
Roho wa Mungu alivyo. Tunaweza kutoa maelezo kwa ufupi
sababu zilizoonyeshwa hapo kwa kusema kwamba roho wa /ya
Mungu ni nguvu au pumzi yake ambayo kwa hiyo nafsi yake
mwenyewe, Utu wake na tabia, vimedhihirika kwa mwanadamu
kwa njia ya matendo yake ambavyo Roho huyo
anatimiza.Hivyo'Mungu ni Roho’ kama katika Yohana 4:24
atafsiriwe vema kwa kuwa Roho yake ndiyo inafanya utu wake.
Mungu amesemwa kuwa yumo katika vitu vingi, kwa mfano:-
‘Mungu wetu ni moto ulao’ (Ebr. 12:29)
‘Mungu ni Nuru’
(1 Yoh. 1:5)
‘Mungu ni Pendo
(1 Yoh.4:8)
‘Neno (Kiyunani'Lagos’ - Mpango, Lengo,Kusudi, wazo)
alikuwa Mungu’ (Yoh 1:1)
Hivyo,'Mungu’ ni sifa yake. Ni kosa lililo wazi kuleta sababu
za kupinga kwamba sifa za upendo wa Mungu ni za kuwazika,
kwa kuwa tunasoma kwamba 'Mungu ni pendo’ tunaweza
kumwita mtu mwingine Mwema wenyewe; lakini hii haina maana
kwamba haupo bila mwili ni namna ya kuwepo yeye ndiko
kunatudhihirishia wema kwetu.
Roho ikiwa ni nguvu ya Mungu, mara nyingi tunasoma Mungu
akiituma au akiiongoza roho yake kutimiliza mabo yake kwa
kupatana na mapenzi yake na tabia ya sifa yake. Hata ameelezewa
kuwa anaumba roho (Yaani Upepo UV). Kusema kwamba Mungu
34
na roho yake katika maana safi iliyo halisi ni msemo ule ule kwa
namna nyingine - katika maana inakuwa Uwepo wa Mungu.
Mifano ya Mungu akiiongoza Roho yake ni mingi,
inaonyesha mtengano wa Mungu na Roho yake:-
‘Yeye (Mungu) aliyetia kati yao Roho yake mtakatifu’(Is. 63:11)
‘Nitatia Roho yangu (Mungu) juu yake (Yesu )’ ( Math.12:18)
‘Baba huwapa Roho mtakatifu’ (Luk. 11:13)
‘Roho akishuka kama hua toka Mbinguni’ (Yoh. 1:32)
‘Nitawamwagia watu wote Roho yangu’ (Matendo. 2:17).
Kwa kweli ushahidi juu ya 'Roho wa Mungu’ ni uhakika wa
kutosha kuwa Roho sio Mungu mwenyewe. Tofauti hizi kati ya
Mungu na Roho ni shida nyingine ilio kwa wale wanao amini
kuwa Mungu ana Nafsi'Tatu’ ambazo Mungu amelingana na Yesu
na Roho Mtakatifu. Jambo hili kama lingekuwa la kweli, na kama
Mungu amedhaniwa kuwa sio mtu, basi halikadharika hata Yesu
naye sio mtu halisi.
Kwa umuhimu sana, Mungu asiye mtu hata sala kuelekea
kwake inakuwa haina maana, kwenye alama ambayo sala ni
mazungumuzo kati ya fahamu zetu na wazo la Mungu ambalo lipo
katika akili zetu. Daima tunakumbushwa kwamba tunamwomba
Mungu ambaye ana Umbo makao yake yapo Mbinguni (Mhu. 5:2;
Math. 6:9,5:16, 1Fal. 8:30) na kwamba Yesu sasa yuko mkono wa
kuume huko ili kutoa maombi yetu mbele zake (1Pet. 3:21, Ebr.
9:24).
Ikiwa Mungu si mtu binafsi, maneno haya yametolewa bila
kuwa na maana. Bali, Mungu akieleweka kuwa ni wa kweli, Baba
mwenye upendo, Sala ya kumwomba inakuwa ya kweli, Jambo
35
lililowazi na dhahiri - hasa tukizungumza na mtu mwingine
ambaye tunamwamini ana mapenzi sana na anaweza kujibu.
Tumeacha Kitambo sehemu ya 2:'Matumizi ya jina la
Mungu’
Tumefahamu kwamba Jina la Mungu na hilo la mwanae Yesu
yana maana ya kina sana. Tunaposema 'Mungu’ tunagusa juu ya
kila mwelekeo wa kusudi lake la Ajabu la upendo na kweli. Ya
kwamba Jina la Mungu litumike bure kama upole usio na maana
au kwa maelezo ya kukasirisha, ni moja ya mambo ambayo mtu
hufanya na kumnena vibaya zaidi Muumba wake. Kwa sababu hii
kila mtu anayetaka kumpendeza Mungu na kumheshimu atafanya
kila jitihada kutotumia vibaya Jina la Mungu kirahisi- rahisi.
Katika jamii ulimwenguni pote kufuru hii imekuwa sehemu ya
kawaida kwa Lugha za siku hizi; Kukatisha ile iliyokuwa ni tabia
ya mazoea haita kuwa kazi rahisi. Sala ya kweli ya kuomba msaada
wa Mungu hakika itasikika. Wale ambao wapo ndani ya shughuli
yetu ya kuwaongoza na kuwavuta, Mf. Watoto, pia
watakumbushwa
hatari ya kukufuru:”Maana BWANA
hatamhesabia kuwa hana hatia alitajaye jina lake bure (Kum. 5:11)
Kwa upande mwingine wapo wale wanaosisitiza kwamba
tusipotumia maneno ya Kiebrania Yahweh au Yehova (Njia tofauti
ya kutamka neno lile lile) Tunapozungumuza kuhusu Mungu,
wakati huo tunakuwa tumepotea sana. Miongoni mwao zaidi ya
hawa ni Chama cha mlinzi, wanasisitiza kuwa Mkristo asipojiita
mwenyewe ni'Shahidi wa Yehova’ Basi hana uhusiano na Mungu.
Kwa kufanya hivi, watu hawa wanatumia jina takatifu la
Mungu na la ajabu kuchochea aina fulani ya mfumo wa Imani wa
36
kuelimisha kiroho, ambapo wanawadharau watu wengine tu kwa
matamshi au matumizi ya neno moja. Hii sio kusema kuwa ni
vibaya kutumia Jina la Mungu; Hasa kweli linafaa kutumika
kwenye Sala zetu wenyewe mara tukibatizwa kwa usahihi katika
Jina lake. Ingawa hivyo, Agano Jipya halitupatii ishara yoyote
kuwa hili ni lazima au inatakiwa na Mungu. Aliongoza kuandika
Agano Jipya hivyo basi liliandikwa kwa Kiyunani (Kigriki)
likitumika neno moja la'Mungu’ -‘theos’ likiwa na maana “Mtu
mkubwa”.
Hakuna tofauti iliyofanywa ndani yake kati ya'Mungu’ na
'Yahweh’ wala haipo amri yoyote dhahiri inayohusiana kwa
waamini wakiwa ni jumuiya wajiiteje.Petro anamsema mwamini
kuwa ni “ Mkristo” kuliko kumwita ni'Mtu wa Yehova’ au jambo
lingine kama hili (1 Petro 4:16) kutilia mkazo zaidi katika
matumizi ya Jina la 'Yehova’ kunapelekea kupunguza thamani ya
kazi na Nafsi ya BWANA'Yesu’ kwa njia hii ambayo wakristo
wengi wa kiinjili wanatia msukumo zaidi kwenye jina na kazi ya
Yesu huku wakiacha kuangalia nafsi ya nguvu zaidi iliyo ya
Mungu.
Majina mengine ambayo jumuia ya waaminiao ya wakristo
wa kwanza waliyojiita wenyewe, hayatii ndani jina la Yehova:-
‘Jamii ya Israeli’ (Ef. 2:12)
‘Mkutano mkuu na kanisa la wazaliwa wa kwanza’ (Ebr. 12:23)
‘Kanisa lake Mungu’ (Matendo 20:28)
‘Kanisa la Mungu aliye hai, Nguzo na Msingi wa kweli’ (1
Timotheo 3:15)
‘Nyumba ya Mungu’ ( 1 Timotheo 3:15)
37
Tunapopita, ujue kuwa waamini
hawakujiita
wenyewe'Wakristo’. Neno hili maana yake lilikuwa la kuvunja
heshima, hawa watu wa Kristo walibezwa na maadui zao.
Tumeacha Kitambo sehemu ya 3: 'Ufunuo wa Mungu’
Kinachufuata sio rahisi kukishika chote wakati tunaposoma
kwanza,lakini umuhimu wa jambo tunalolizungumzia litakuwa
dhahiri kadri masomo yake yanavyosonga mbele. Tunajumuisha
kwenye maana hii ili uliache somo hili lote Msingi wa Biblia
ukisha pimwa wenye ufunuo kuhusu Mungu mwenyewe.
Jina la Mungu laweza kuchukuliwa na yeyote ambaye
amemchagua kujifunua au kujidhihirisha yeye mwenyewe. Hivyo
watu na Malaika sawa sawa na Yesu huweza kuchukua jina la
Mungu. Hili ni jambo la muhimu ambalo linatufunulia mengi ya
Biblia. Hata mwana anaweza kuchukua jina la Baba; ana mambo
mamoja na Baba yake, anaweza kuwa na jina lile lile la kwanza-
lakini si mmoja na kuwa mtu yeye yule kama Baba. Kwa njia hiyo
hiyo mwakilishi wa kundi anaweza kusema kwa niaba ya kundi,
anaweza kumpigia mtu wa kwenye shughuli na kusema, Haloo !
hapa ni wakulima, Si Bw. Wakulima, bali anachukua jina lao kwa
kuwa anafanya kazi kwa niaba yao. Basi hiyo hata kwa Yesu
ilikuwa hivyo.
MALAIKA HUCHUKUA JINA LA MUNGU
Tumeambiwa katika Kutoka 23:20,21 ya kwamba Mungu
aliwaambia watu wa Israeli kuwa Malaika atawatangulia mbele
yao;'Jina langu limo ndani yake’, waliambiwa. Jina lake Mungu
ni'Yahweh’. Basi, Malaika huchukua jina la Yahweh, na hivi
38
anaweza kuitwa Yahweh, au BWANA kwa herufi kubwa neno
BWANA linatokana na Yahweh, katika Biblia UV ya Kiswahili ni
sehemu moja tu Zaburi 89:8 utakuta neno
YAHU = YAHWEH. Tumeambiwa kuwa katika kutoka
33:20 Mtu hataniona uso akaishi; lakini katika Kutoka 33:11
tunasoma kwamba “BWANA”(Yahweh) alinena na Musa uso kwa
uso, kama mtu anaposema na rafiki yake - Yaani kirafiki. Hakuwa
ni BWANA, Yahweh mwenyewe alikuwepo, aliyenena na Musa
uso kwa uso, Kwa kuwa hakuna mtu anayeweza kumwona Mungu
yeye mwenyewe. Alikuwa ni Malaika aliyechukua jina la Mungu
ndiye aliye fanya hivyo, na tunasoma habari za BWANA akisema
uso kwa uso na Musa wakati hasa ni Malaika aliyefanya hivyo
(Mdo. 7:30-33).
Ipo mifano mingine mingi ya maneno' Mungu' na BWANA
ikitaja Malaika wakiwa Mungu mwenyewe. Mfano mmoja ulio
wazi ni Mwa. 1: 26 “Mungu (Malaika) akisema, na tufanye mtu
kwa mfano wetu”
WATU NA JINA LA MUNGU
Moja ya maneno ambayo yanayosaidia sana katika kuelezea
yote haya ni katika Yohana 10:34-36. Hapa Wayahudi walifanya
kosa ambalo wengi wanaoitwa'Wakristo’ wanafanya leo.
Walidhani kuwa Yesu alikuwa anasema kuwa yeye ni Mungu
mwenyewe. Yesu alisahihisha kwa kusema “Haija andikwa katika
sheria yenu, nimesema Ninyi ni Mungu ? Ikiwa aliwaita Miungu
….. inakuwaje mimi ….” Mnaniambia ninakufuru, kwa sababu
nalisema, Mimi ni mwana wa Mungu ? Yesu kwa kweli alikuwa
anasema 'Katika Agano la Kale watu waliitwa Miungu; mimi
nasema ni mwana wa Mungu, basi imekuwaje mnaudhika sana?
39
Yesu kwa kweli alikuwa ananukuu toka Zab 82 mahali ambapo
waamuzi wa Israeli waliitwa'Miungu’.
Kama ilivyoonekana, Jina kamili la Mungu katika Kiebrania ni
'Yahweh Elohim’ likiwa na maana, Nitadhihirika katika kundi la
wenye nguvu. Waamini wa kweli ni wale wengi wenye nguvu
katika maana ndogo ya maisha haya nao watakuwa na nguvu tele
kwenye Ufalme. Kwa mlinganisho huu wote umeonyeshwa kwa
Isa. 64:4 na 1 Kor.2:9.
“Watu hawakusikia, wala kufahamu kwa masikio, wala jicho
halikumwona Mungu, ila wewe, atendaye mambo kwa ajili yake
amngojaye” Paulo ananukuu mstari huu katika 1 Kor.2:9-10:
Imeandikwa, Jicho halikuyaona, wala sikio halikuyasikia wala
hayakuingia katika moyo wa mwanadamu, mambo ambayo Mungu
amewaandalia wampendao. Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa
Roho. Fungu la maneno katika Isa. 64:4 linasema hakuna hata
mmoja isipokuwa Mungu anaweza kufahamu mambo
aliyowaandalia waamini; Lakini 1Kor. 2:10 mstari unasema
kwamba mambo hayo yamefunuliwa kwetu, hivyo katika maana
sisi ni “Mungu”: sio Mungu mwenyewe katika utu, bali ufunuo wa
Mungu kwa matokeo kuwa tumebatizwa katika jina lake na kujua
Ukweli.
YESU NA JINA LA MUNGU
Sio jambo la kushangaza kwamba Yesu, Ikiwa ni mwana wa
Mungu na ufunuo wake mkuu kwa watu, Pia naye atachukua jina la
Mungu. Aliweza kusema “Nimekuja katika jina la Baba yangu”
(Yoh.5:43). Kwa utii wake, Yesu alipaa kwenda mbinguni, naye
Mungu akampa jina lipitalo majina - Jina la Yahweh, la Mungu
mwenyewe
40
(Fil. 2:9).basi hii ndiyo sababu tunasoma Yesu anasema katika
Uf 3:12 “Nami nitaandika juu yake (Mwamini) Jina la Mungu
wangu……na jina langu mwenyewe, lile jpya”Kumbuka Yesu
alitoa kitabu cha Ufunuo miaka mingi baada ya kupaa kwenda
mbinguni na akiisha kupewa jina la Mungu, kama ilivyoelezwa
katika Wafilipi 2:9.
Hivyo anaweza kuliita jina la Mungu “Jina langu Jipya”; Jina
ambalo hivi karibuni alipewa. Sasa tunaweza kuelewa vema Isaya
9:6, mahali ambapo kuhusu yeye tumeambiwa “Jina lake (Ujue
kuwa) utaitwa, Mshauri wa Ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba
wa milele, ….” Huu ni Unabii wa kwamba Yesu atachukua majina
yote ya Mungu ya kwamba atakuwa ni ufunuo wote wa Mungu
kwetu.Na ndivyo kwa maana hii aliitwa “Emmanueli” maana yake
'Mungu ni pamoja nasi’ ingawa yeye hakuwa Mungu.
Somo La Kwanza : Maswali
1.Ni nini kitakachotusaidia zaidi kuamini Mungu ?
a) Kwenda Kanisani
b) Maombi na Kusoma Biblia
c) Kuzungumuza na Wakristo
d) Kutazama maumbile.
2. Yapi ya haya yafuatayo ni ufafanuzi sahihi zaidi wa
Mungu ?
a) Ni wazo tu katika mioyo yetu
b) Kipande cha Roho katika Hewa
c) Mungu Hayupo
d) Mtu halisi wa Umbo
41
3. Je ? Mungu ni
a) Ummoja
b) Utatu
c) Miungu wengi katika mmoja
d) Haiwezekani kufafanua kwa njia ya yoyote
4. Jina la Mungu' Yahweh Elohim’ lina maana gani ?
a) Yeye atakaye kuwa
b) Atakayedhihirika katika kundi la wenye nguvu
c) Mkuu
d) Nguvu
5. neno'Malaika lina maana gani ?
a) Kama mtu
b) Aliyefunikwa na Mabawa
c) Mjumbe
d) Msaidizi
6. Je ? Malaika anaweza kutenda Dhambi ?
7. Ni kitu gani kinacho kudhihirishia kuwa Mungu yupo ?
42
No comments:
Post a Comment