Wednesday, September 12, 2018

*FAHAMU NGUVU ZAKO ZA KUZALIWA KWA UFUNUO WA ROHO MTAKATIFU*

Kumb 33:1-9, Mwanzo 49:3-7, 1Kor 2:10
Kila mwanadamu aliyeumbwa na Mungu Aliye Hai, ameumbwa na nguvu maalumu kutoka mbinguni, ambayo ni mtaji wake maalumu; kiroho, kijamii na kiuchumi.

Mwanzo 49:3
Reubeni u mzaliwa wangu wa kwanza,nguvu zangu na malimbuko ya uwezo wangu. Umewapita wengine kwa ukuu na nguvu.

*1. MZALIWA WA KWANZA KATIKA FAMILIA YOYOTE*
i. Amebeba nguvu nyingi za familia.
ii. Amebeba Baraka za aina mbalimbali za wadogo zake.
iii. Amebeba nguvu ya upendo ndani ya familia.
iv. Mzaliwa wa kwanza ni lango, Zab 24:7-9, ambapo Baraka zote za familia kutoka mbinguni zinapitia kwake na kuwafikia wadogo zake wote.
v. Amebeba ustawi wa familia kiroho na kimwili.

*2. MTOTO WA PILI KATIKA FAMILIA YOYOTE*
i. Ni m’beba neno la uzima.
ii. Kipawa cha ualimu kinakaa vizuri sana ndani yake.
iii. Amepewa neno la uzima la kusaidia kanisa familia na nchi.

*3. MTOTO WA TATU KATIKA FAMILIA YOYOTE*
i. Ni mtawala katika ulimwengu wa roho na wa mwili.
ii. Ni mtunga sheria popote atakapokuwa anaishi, anasoma au anafanya kazi.
iii. Amepewa mamlaka ya kusimamia jamii, kuiongoza na kuitawala.
iv. Anafaa kuwa mwanasheria au kiongozi popote aendapo.

*4. MTOTO WA NNE KATIKA FAMILIA YOYOTE*
i. Amepewa neema ya kumiliki utajiri wa nchi.
ii. Kama akijitambua na kusimama katika zamu yake, ajue amepewa neema na nguvu ya kuutawala uchumi vizuri sana.
iii. Amepewa nguvu ya kumiliki utajiri wa mbingu na dunia.

*5. MTOTO WA TANO KATIKA FAMILIA YOYOTE*
i. Amepewa neema ya kushinda changamoto.
ii. Amepewa stamina ya kushindana na majaribu kwa asili.
iii. Amepewa neema ya kutumika na upako wa juu sana, kama akiokoka na kujitambua, na kusimama katika zamu yake.

*6. MTOTO WA SITA KATIKA FAMILIA YOYOTE*
Ni mtu wa ujuzi, na talanta. Na Amepewa nguvu ya ubunifu wa pekee.

*7. MTOTO WA SABA KATIKA FAMILIA YOYOTE*
i. Amebeba uheri wa Mungu Mtakatifu.
ii. Yeye ni jubilee, yaani maachilio.
iii. Usithubutu kushindana naye maana hautafanikiwa.
iv. Ukimshitaki hauwezi kufanikiwa.
v. Anafaa kuwa mzee wa kanisa.
vi. Anafaa kuwa hakimu kama ataamua kuichukua taaluma hii.
vii. Ukipata kesi yoyote na akakusindikiza ni lazima utashinda, maana utu wake wa ndani ameumbiwa neema hii.

*8. MTOTO WA NANE KATIKA FAMILIA YOYOTE*
i. Amebeba nguvu ya utumishi.
ii. Amepewa neema ya kusaidia wengi kiuchumi, kiroho na kijamii, kama akijitambua na kusimama katika zamu yake.
iii. Akiokakoka na kuwa mtumishi kanisa lolote, atalisaidia sana kustawi, kwa kuwa ni mtu wa kutegemewa sana.
iv. Amepewa neema ya kuwa nguzo.
v. Ukimtambua katika kanisa lako na kumthamini, na kumtumia vizuri, utafanikiwa sana.

*9. MTOTO WA TISA KATIKA FAMILIA YOYOTE*
i. Ni m’beba karama.
ii. Akipokea kipawa anakitunza sana kwa muda mrefu.
iii. Amepewa nguvu ya umoja.
iv. Ni mtu anaweza kuinganisha jamii, nchi au familia na kuleta mshikamano.
v. Anafaa kuwa mwanasiasa endapo akijitambua na kusimama katika nafasi yake aliyokirimiwa na mungu.

*10. MTOTO WA KUMI KATIKA FAMILIA YOYOTE*
i. Yeye ni msamaha.
ii. Amekirimiwa nguvu ya msamaha.
iii. Amepewa uwezo wa kusuluhisha migogoro kwa ufanisi wa hali ya juu sana.
iv. Anafaa kuwa mzee wa kanisa.

*11. MTOTO WA KUMI NA MOJA KATIKA FAMILIA YOYOTE*
Ni faraja kwa familia.
Kuna wakati anapata tatizo la kukataliwa, lakini ni mvumilivu sana.
Mkikaa naye kwa upendo mtabarikiwa sana.

*JiULIZE WEWE NI MTOTO WA NGAPI NAJEE UNAITENDEA VYEMA NAFASI YAKO?*

Friday, September 7, 2018


*KANUNI KUMI ZA KIBIBLIA USIMAMIZI MZURI WA FEDHA:*
  Na: *PROPHET DERICDADY*
Biblia inatoa mwongozo mzuri wa usimamizi wa fedha ambao tukiufanyia kazi tuta punguza kwa asilimia kubwa matatizo mengi ya kifedha tuliyo nayo.Matatizo mengi ya kifedha tuliyo nayo yanachangiwa sana kwa namna moja au nyingine na usimimamizi mbaya wa fedha zetu,wengi wetu tatizo letu kubwa zaidi ni usimamizi wa fedha kuliko kuzalisha na kupata fedha.


usimamizi mzuri wa fedha utalinda uchumi wako na kuukuza uzalishaji wako,kipato chako.Hata kama unazalisha sana fedha lakini kama una usimamzi mbaya wa fedha  uchumi wako utayumba tu.Matatizo mengi ya kifedha tunakimbilia kuombewa na kukemea,lakini hayo yote bila  kujifunza usimamizi mzuri wa fedha utakuwa hujatatua tatizo katika mzizi.hata ukiombewa kupata mpenyo wa kifedha matatizo ya kifedha yatarudi baada ya muda mfupi kwa kushindwa kuzitendea kazi kanuni za fedha.


*1.       MUNGU NDIYE MMILIKI WA FEDHA ZETU*

Fedha ni Mali ya Bwana,sisi tu wasimamizi tu au mawakili,hivyo tunawajibika na vile tunatumia kila fedha tuliyoaminiwa na Mungu.( Mathayo 25:1-30 ; Zaburi 24:1,)


*2.       TAMBUA FEDHA NI SUALA LA KIROHO.*

Kwa mtu wa Mungu fedha ni suala la kiroho,fedha ina athiri na inagusa maisha yako ya kiroho pia.vile unavyo shughulika na fedha kuna sema zaidi juu ya hali yako ya moyo kuliko ushuhuda wako.vile unavyoshughulika na fedha zako ni kiashirio cha ukomavu wako kiriho.LUKA 16:10-11

Fedha inaweza kuwa mungu wako,fedha ina uwezo zaidi kutuvuta taratibu na kwa ujanja kutoka kwa Mungu kuliko kitu kingine chochote.MATH 6:24,Ina nguvu ya kuwa Bwana wetu.

Katika mifano 38 ya Yesu,16 inahusu fedha,katika agano jipya fedha imezungumzwa zaidi kuliko habari za mbinguni na kuzimu vikiunganishwa pamoja.mara tano zaidi imezungumzwa kuhusu fedha kuliko maombi,kuna mistari zaidi ya 1500 inayohusu maombi na imani,wakati kuna zaidi ya mistari 2000 inayohusu fedha na mali.Aslimia 15% ya Biblia  ni kuhusu fedha.


*3.       TUNZA KUMBUKUMBU ZOTE ZA FEDHA*

Kutunza kumbukumbu ni hatua ya kwanza kukusaidia katika kuandaa bajeti yako ambayo utaishi nayo.tafuta daftari ndogo na anza kuweka kumbukumbu za wapi fedha zako zinakwenda,ni kazi ngumu lakini itakusaidi kwa mipango ya muda mrefu ya kifedha.kiasi gani unatumia kwa mwezi kwa usafiri?simu?chakula?matibabu?chakula n.k ni lazima ujue wapi fedha yako inatoka na wapi fedha yako ina kwenda. Nini nina mililki,nini nina dai,nini nina daiwa,natuamiaje(MITHALI 27:23-24, 23:23,)


*4.       FANYA TATHIMINI  YA MARA KWA MARA YA FEDHA ZAKO:*

ni muhimu kufanya tathimini kwa uaminifu kuhusu uchumi wako,mapato yako,madeni,vitega uchumi vyako n.k. hii itakusadia kufanya marekebisho unayoyahitaji na  kukusaidia kuishi kwa mpango,kama huwezi kutathimini hutaweza kupanga,ukishindwa kupanga,tayari umeshindwa kusimamia fedha yako.(MITHALI 21:5  LUKA 14:28)



*5.       JIWEKEE  MFUMO WA KUPANGA BAJETI NA KUUFUATA:*

Bajeti kirahisi nikuandika  katika karatasi nini unategemea kupata kama mapato na njisi gani unategemea kutumia.panga matumizi yako.Ni mpango wa jinsi gani utatumia rasilimali  fedha ambazo unatarajia kupata ,bajeti inapaswa ijumuishi vyanzo vya mapato  pia mpango wa matumizi wa mapato mf.mpango wa chakula,kodi,zaka,utoaji,akiba n.k(Mithali 21:5, Mithali 21:20)


*6.       JIWEKEE  UTARATIBU WA KUWEKA AJIRA*

Weka Akiba, kwaajili ya dharura,akiba kwaajili malengo maalumu, (Mithali 21:20a ;13:11)

Mithali 6. Tenga kiasi cha kuweka akiba anza na kiasi kidogo kwanza.


*7.       JIFUNZE KUTOA KWA UKARIMU-*

(Mithali 11:24-25).kanuni ya uchumi wa Kimungu ni tofauti,kadiri unavyotoa na sivyo unavyo jilimbikizia ndiyo uchumi wako unastawi.Kumtolea Mungu,kutoa kwaajili ya kuwabariki wengine,kutoa kwaajili ya wahitaji(Mithali 28:27 Mithali 11:25.Mithali 19:17,Mithali 3:9-10),Kutoa  kunafungua Baraka za Mungu katika Maisha yako.


*8.       TUMIA FEDHA YAKO KWA HEKIMA NA RIDHIKA NA ULICHO NACHO:*

Zingatia vipaumbele na umuhimu,Epuka matumizi ya anasa,manunuzi ya bila mpangilio,manunuzi ya papo kwa papo,usifanye matumizi yaliyo nje,yanayozidi kipato chako au uwezo wako wa kifedha.Jifunze kuridhika na kuuepuka tamaa.usifuje fedha kwa matumizi ya ovyo.jifunze kuridhika(Mithali 21:20 ;Waebrania 13:5,Mhubiri 6:9)


*9.       TUNZA VITU NA MALI AMBAVYO UMEVIGHARIMIA FEDHA.*

Vitu,mali ni fedha,usipovitunza utatoa fedha tena kununua. Tunza visiharibike ovyo,vitumike kwa uangalifu ili kuokoa gharama ya matengenezo au kununua upya.


*10.   EPUKA MADENI.*

biblia haijakataza moja kwa moja kuhusu kukopa,ila kwa uwiano wa maandiko Haiti moyo madeni,bali inakatisha tamaa kukopa.inazungumza zaidi madhara ya kukopa.Unapokuwa katika deni unakuwa katika kifungo,Madeni yana haribu uhusiano.usitumie fedha zaidi ya ile unayozalisha utaishia kwenye madeni.weka akiba kidogo kidogo badala ya kukopa.

MITHALI 22:26-27,ZABURI 37:21,MITHALI 22:7


*HITIMISHO:*

Pengine umekuwa unapitia katika kipindi kigumu cha kifedha,uchumi wako umeyumba,kabla ya kuhitaji fedha zaidi unahitaji kuzifanyia kazi kanuni hizi za usimamizi wa fedha.Mungu anakusubiri ujifunze na kuzingita kanuni hizi za fedha ili akufungulie mlango mkubwa zaidi wa kifedha,ni jukumu lako kutii kanuni hizi na hali yako ibadilike au ubaki katika hali uliyo nayo.Mungu akubaliki unapochukua uamuzi wa kusimamia fedha zako kama wakili mwaminifu.MUNGU akubariki sana

*son of Alpha and Omega*
   0712412170
*PROPHET DERICDADY*

Monday, September 3, 2018

*IJUE NGUVU YA MAONO KATIKA MAISHA YAKO*
  *SON OF ALPHA AND AND OMEGA*
  _NA: PROPHET DERICDADY_
*0712412170*

*The man doesn’t make the vision; the vision makes the man*.
– Pastor Yonggi Cho

Maono: Ni ule uwezo wa kuyaona maisha ya baadae kwa wakati uliopo, {mtazamo wa maisha yajayo}; maono humfanya mtu ajizuie kutenda maovu kwa ajili ya kulinda na kuyaponya maisha yake na ya kundi zima kwa ujumla.

Kwani “pasipo maono watu huacha kujizuia”

·       Maono hutofautiana kati ya mtu na mtu kulingana na kitu anachokihitaji maishani na kipo ndani yake wakati huu: Kwa mfano:-

·       Maono ya kiongozi ni tofauti na ya mfanyabiashara, ni tofauti kabisa na msomi katika fani yake.

·       Maono ya mchungaji ni kulitunza kundi lisitawanyike na lipate mahitaji yake.

·       Maono ya mwinjilisti ni watu wengi kuokoka

·       Maono ya Askofu ni kuwa mwangalizi wa kundi zima.

Maono huendana na wito wa mtu, na kama biblia inavyosema kuwa “Mwenende kama inavyoustahili wito wenu mlioitiwa; kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo.” [Efeso 4:1b-2]. Ndivyo mtu anavyotakiwa kuenenda sawa sawa na picha anayoiona mbele yake kila wakati na kila mahali ili aifikie na kuifanikisha katika maisha alisia.

“Tena Neno la Bwana likanijia, kusema, Yeremia waona nini? Nikasema, naona ufito wa mlozi. Ndipo BWANA akaniambia, umeona vema, Kwa maana ninaliangalia Neno langu, ili nilitimize. Neno la Bwana likanijia mara ya pili kusema, waona nini?  Nikasema, naona sufuria yenye maji yatokotayo, na mdomo wake unaelekea toka upande wa kaskazini….” [Yeremia 1:11-13]

Vijana wengi sana wamejiharibu nafsi zao kwa tamaa za mwili zipitazo hata kuipoteza ile nguvu ya maono iliyokuwa inatenda kazi kwa namna ya pekee sana ndani yao.

Weka mikakati ya kuyatimiza maono hayo kwa wakati muafaka. Historia imejaa watawala waliokuwa tayari kumwaga damu za watu wengi ili watimize maono yao ya kupanua utawala wao. Mkuu katika hao atakuwa ni yule anayetajwa kama Mnyama katika Ufu 13: 5

Katika mwisho wa historia ya ulimwengu huu inaonekana Mungu atampa mtu huyu ambaye pia anaitwa mpinga Kristo mamlaka juu ya mataifa yote duniani.Maono yake yatakuwa ni kuwa mkuu wa wote. Atafungua mdomo na kumkafiri Mungu mwenyewe. Ndiyo maana anaitwa mpinga Kristo. Anafanya yote kinyume na Kristo. Anapinga yale yote yanaoupendeza moyo wa Mungu. Lakini ni wa mwisho na mwenye nguvu zaidi tu katika mlolongo mrefu wa viongozi katika historia waliopinga mpango wa Mungu. Na Mungu atavunja mamlaka yake baada ya muda mfupi.

*You can’t pocess beyond what you see* (Mwanzo 13:14-18), [Huwezi kumiliki zaidi ya pale unapopaona, “Maana aonavyo mtu nafsini mwake ndivyo alivyo” [Mithali 9:1]. Unapo muuliza mtoto mdogo kuwa anataka kuwa nani maishani, unakua unamfanya akueleze kuwa anaona nini katika maisha yake yajayo; yaani anapicha gani inayomfanya asitulie mpaka ameifikia hiyo picha ya maisha yake yajayo. Ndio maana anasema, nataka kuwa mwalimu, au daktari, au dereva n.k vivyo hivyo Mungu anakuuliza leo hii kuwa unaona nini?  Hatuwezi kujifunza juu ya kufanikiwa katika maono kama hatujui tunaona nini? Na hatujui nguvu iliyomo katika hayo maono.

*IGEUKIE NGUVU YA MAONO*

“Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina Roho yangu juu ya wote wenye mwili; Na wana wenu, waume Kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, Na vijana wenu, wataona maono” [Yoeli 2:28]

·       Wazee wenu wataota ndoto-Ndoto huja kutokana na shughuli nyingi za siku hiyo [Mhubiri5:3a], na wazee wameishi miaka mingi kiasi ambacho shughuli zote walizozifanya katika maisha yao mpaka sasa huwapelekea kuota ndoto, na kazi kubwa ya wazee katika maisha ni kutoa ushauri na kuwashirikisha vijana hekima  na maarifa ambayo wameikusanya kwa miaka mingi na Maono ya wazee ni kufa katika uzee mwema ili wakamwone Mungu, ndio maana mazungumzo yao mengi yanahusu uzima wa milele na namna ya kuilinda imani yao. Wazee wengi wamesha timiza maono yao.

·       Vijana wenu wataona maono-Maono hutokana na mtazamo wamaisha yajayo ambayo mtu anatamani kuyafikia lakini bado hajafanikiwa kuyafikia. Ndio maana ya vijana kuona maono. Mtazamo huu hutegemeana na fikra na utashiwa mtu binafsi na namna anavyo enenda katika kusudi la yeye kuishi hapa duniani. Ndio maana vijana wanatakiwa kuona maono kwa kuwamaono yanahitaji nguvu na mikakati thabiti ya kuitimiza ili kupata kinachohitajika.

Nguvu ya maono ipo ndani ya mmbeba maono mwenyewe, na yeye ndiye anayejua afanye nini ili afikie maono yake, tunaposema “Igeukie nguvu ya maono”tuna maanisha ufanye mambo yako kulingana na kile unacho kitarajia maishani, na hii ina maana sawa na ile ambayo mtume Paulo anaelezea kuwa “Mwenende kama inavyoustahili wito wenu mlioitiwa” [Efeso 4:1b].

Mungu ameweka nguvu (uwezo) ndani ya kila mwanadamu inayo mwezesha kuishi hapa duniani Kwa kupata mahitaji yake ya kila siku. Njia pekee ni kufanya kazi ili kupata chakula na mahitaji mengine na “… ikiwa mtu hataki kufanya kazi, basi, asile chakula” [2 Thesalonike 3:10c]. Unapoigeukia nguvu ya maono unakuwa umechukua hatua ya kuyafanyia kazi malengo yako na ile mikakati uliyojiwekea ili kuyafanikisha maono ya maisha yako.

Nguvu hii haionekani, lakini ipo ndani yako, ni nguvu ya kipekee inayokufanya usome kwa bidii, uwe mkulima hodari, ufanye kazi kwa moyo wote, ni nguvu inayokuwezesha kuzaa na kutunza watoto, ni nguvu ya ajabu inayokufanya ujitambue kuwa umekua mtu mzima na unawajibika kwa nafasi yako kama baba au mama, kama kijana ama mzee; ni nguvu isiyoonekana kwa macho haya ya nyama lakini tunaishi nayo ndani yetu.

Uwezo wa kufikiri, uwezo wa kuwaza, uwezo wa kubaini na kujua mema na mabaya, uwezo huu ndio nguvu yenyewe inayopelekea kufanikiwa katika maisha haya kwa kuyafanikisha maono yako katika uhalisia wake. Igeukie nguvu hii ili uyafanikishe maono yako, tafakari na chukua hatua, kwani hakuna mtu wa kumlaumu katika maisha haya zaidi yako mwenyewe. Nataka ujue kuwa Mungu ametuwekea nguvu hii na ujuzi huu ndani yetu ili kupunguza idadi ya maombi yanayopelekwa mbele zake kila wakati.

Kuna mambo mengine yanahitaji tutumie ujuzi tulionao na sio maombi, sina maana ya kuwa maombi hayana umuhimu lakini nina maana ya kuyajua na kuyatumia maarifa tuliyokirimiwa na Mungu wetu. Mungu anaposema kuwa “watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa” [Hosea 4:6a] ana maana ya kuwa kuna ujuzi ambao tunatakiwa kuwa nao kwa kujifunza ama kwa kukirimiwa na Yeye, ambao tunatakiwa kuutumia ili tuweze kuishi sawasawa na mapenzi yake.

MAONO HUENDANA NA MUDA/WAKATI MAALUM

*If you think you can, you can; and if you think you can’t, you can’t; you are always right.*

Siku zote za maisha yako uwe na ndoto za mafanikio, hii itakufanya siku moja uketi pamoja na wakuu wa nchi. Kubali kupokea Baraka kutoka kwa wengine na uwe mtu wa shukrani.

Tumia muda wako vizuri kupanga mambo ya kimaendeleo. Kumbuka watu waliokabiliana na matatizo makubwa ndio walioweza kufikia mafanikio makubwa kiroho, kiuchumi na kisiasa, kwa kuwa wanazikubali changamoto katika maisha, Leo tutaangalia jinsi ya kutokufuata mawazo ya wale wanaotaka kukurudisha nyuma kimaendeleo.

Miongoni mwa jamii tunazoishi, huwa kuna baadhi ya watu ambao hufurahia wenzao wanaposhindwa kutimiza malengo waliojiwekea, Ama huwa na tabia ya kuwakatisha tamaa wanaopenda kujikwamua kutoka katika hatua moja na kuelekea hatua nyingine.
Watu hao mara zote huwakatisha tamaa wenzao kwa jambo fulani, kwa kuwaambia kuwa, wasijaribu kulifanya kwa kuwa hawatafanikiwa. Kumbe watu hao, ilitakiwa kuwatia moyo wale wanaotaka kujikwamua kiuchumi kwa kuwaambia kuwa, wajaribu kufanya jambo walilolikusudia.

“Mawazo ya watu kama hao wasiopenda mafanikio ya wengine mara zote ni sumu ya maendeleo”. Hivyo unapokutana na watu kama hao, unachotakiwa kukifanya, ni kujiwekea mazingira ya kujikinga pale wanapokujia na kutaka kukulisha sumu hiyo.
Lakini kwa upande mwingine, wewe unayependa kupiga hatua kimaisha, unaweza kuyapokea mawazo ya wale wanaowakatisha tamaa wenzao, kama ni njia mojawapo ya kukutoa hapo ulipo na kupiga hatua zaidi.

Kamwe usiruhusu watu hao wasiopenda maendeleo yako kukukatisha tamaa kiasi cha kuharibu ratiba na mipango yako ya kimaendeleo uliyojiwekea. Kwa kuwa, watu wa namna hiyo wapo kila mahali, na kazi yao ni kuharibu mipango mizuri ya maendeleo ya wengine.
Huweza kutumia wengine kuyabeza mafanikio yako, kukucheka, na pengine huweza kukukopa baadhi ya bidhaa zako na kukuletea usumbufu katika malipo, ili mradi wewe uchukie na kuamua kuacha kufanya biashara uliyoianza.

Hizo ni changamoto zilizopo katika maisha yetu ya kila siku cha msingi, ni kusonga mbele na kufanya kile ulichokusudia bila kuangalia wengine wanasemaje juu yako ya kukurudisha nyuma. Wapinzani wa maendeleo ya wengine wapo kila mahali. Wengi wao ni wavivu hivyo wanashindwa kukabiliana na ugumu wa maisha, hupenda kuwakatisha tamaa wengine ambao wamekuwa wakikabiliana na changamoto mbalimbali katika kufikia mafanikio wanayoyataka.
Usifanye makosa katika malengo yako.Kwa kuwa hata katika eneo lako la kazi, iwe ni ofisini ama kwenye biashara wapo wanaokukatisha tamaa ya kuendelea na mipango yako.


Kwa kuwa, katika hali halisi tumetofautiana kifikra na kimaendeleo.Miongoni mwetu wapo wale wenye mipango ya kupenda kupiga hatua kila wakati za kimaisha, na wapo wale ambaohupenda kuangalia wengine wanafanya nini na kuwabeza. Katika hilo, usikate tamaa. Piga hatua zaidi katika kufanikisha malengo yako kwa kuwa na mkakati wa kujiwekea kanuni ya kutafuta ushauri kutoka kwa watu wenye mafanikio zaidi yako. Ukijijengea tabia ya kuuliza maswali pale unaposhindwa, ni sawa na kutibu ugonjwa wa kansa unaokusumbua.

Vile vile ujue kuwa, katika maisha mafanikio yako pia yanategemea msaada wa kimawazo kutoka kwa wengine. Huwezi ukawa na mipango yako mwenyewe na mawazo yako mwenyewe ukafanikiwa bila kuomba ushauri kwa wengine walio mbali zaidi yako kimaendeleo, wale unaoweza kuonana nao na kuongea nao bila matatizo.

Changamoto za mafanikio ni kufanya kazi kwa bidii ili kuleta mafanikio. Bila kufanya kazi kwa bidii ni vigumu kupata mafanikio katika maisha. Njia mojawapo ya kufikia mafanikio hayo ni kuainisha malengo yako unayotaka kuyafikia.


*UPANGAJI MALENGO YAKO*

Jinsi unavyoweza kupanga malengo makubwa katika maisha yako. Watu wengi hushindwa kufikia malengo makubwa kwa kuwa, mara zote hujikatisha tamaa kuwa hawawezi kufanya jambo kubwa la kimaendeleo, kabla ya kujaribu kulifanya. Tabia ya baadhi ya watu hao wanaokuwa na malengo madogo katika mazingira wanayoishi, ina maanisha eneo hilo hakuna ushindani wa kimaendeleo,ama wao wenyewe hawana jitihada za dhati za kupiga hatua zaidi mbele

Lakini ikumbukwe kuwa, katika kutafuta mafanikio hayo ili uwe na maisha bora, usimwangalie mtu jinsi alivyo, kwamba ana urefu gani, ana pesa kiasi gani, digrii aliyonayo ama kuangalia historia ya maisha yake, bali hupimwa kwa uwezo wa kufikiri kwake. Watu wengi wanaofikiria kuwa na malengo makubwa ya mafanikio, katika maisha yao ni kutokana na matarajio waliyonayo.

Inakupasa kila mara ujitahidi kupanua mawazo yako na kubuni mbinu mpya za kukutoka hapo ulipo na kukuweka katika hatua nyingine nzuri zaidi kimaendeleo. Hivyo utambue kuwa, unapotaka kufanya mambo makubwa inakupasa ujijue wewe ni nani na una thamani gani.Kwa maelezo mengine usijishushe hadhi yako kwa kuona kuwa huwezi kufanya mambo makubwa ya kimaendeleo ambayo yatakutoa hapo ulipo na kukuweka katika hatua nyingine nzuri zaidi.

MFANO

Tuangalie mfano wa kijana mmoja aliyeshindwa kupiga hatua mbele baada ya kujishusha hadhi yake na kujiona hawezi.Kijana huyo, aliona tangazo la kazi katika gazeti. Kazi aliyokuwa anapenda kuifanya na pia ameisomea. Lakini hakufanya jitihada za dhati za kuomba nafasi ile, kwa kuwa alijiona hawezi kuipata hata kama angeomba. Aliona kuliko ajitaabishe ni heri aache kuomba nafasi hiyo. Mfano huo si mzuri kwa mtu anayetaka kupiga hatua kimaisha.

Usijishushe hadhi yako ama usikatishwe tamaa kwa hali yoyote ile. Ni vema kujaribu kile unachokipenda na unachokihitaji katika maisha yako, kuliko kuacha kujaribu kwa kuogopa kuwa hautafanikiwa. Kwani matokeo huja baadaye, hata utakaposhindwa, utakuwa na nguvu ya kujaribu tena sehemu nyingine. Wengi wetu, tumekuwa tukijikatisha tamaa katika shughuli mbalimbali tuzifanyazo ama tunazotaka kuzifanya.

Yawezekana umeanzisha biashara kwa lengo la kukuinua kiuchumi, lakini matokeo yake, biashara hiyo haiendi kama vile ulivyotarajia. Jambo la msingi, inakupasa kukaa chini na kujitathmini, kuangalia ni sehemu gani unayokosea. Ama kuangalia, kama una washindani wengi katika eneo hilo, ili uweze kufanya vizuri zaidi yao, kwa kuweka kjvitu vingi tofauti na kuboresha eneo la biashara yako.

*UBUNIFU-CREATIVITY*

Kuwa mbunifu katika biashara yako kutakupa wateja wengi, na utafanikiwa zaidi. Cha msingi usikate tamaa katika kufikia malengo unayoyakusudia. Kutokana na hali ya kujikatisha tamaa, miongoni mwa watu wengi, wanasaikolojia mbalimbali wamekuwa wakishauri ni vema, watu wajijue vile walivyo ili waweze kujirekebisha pale penye upungufu na kusonga mbele kimaisha.
-Hali ya kujikatisha tamaa ni mbaya sana, ni sawa na ugonjwa usiopona katika mwili wako. Ili kuutibu ugonjwa huo, inakupasa ujielewe wewe ni nani, na una upungufu gani, pamoja na kukubali mabadiliko.

Tatizo kubwa lililopo kwa watu wengi, hawajui kuwa, wao wana uwezo mkubwa tofauti na wanavyojifikiria.Hivyo ni vema kuweka mawazo yako kwenye kipimo halisi, uyachuje na kuchukua yale yaliyo na thamani. Penda kufikiri mambo makubwa. Usijishushe hadhi yako kwa kujiwekea au kufikiri malengo madogo. Anza sasa kuwaza mambo makubwa ili uwe mtu mwenye ndoto njema ya maendeleo.

Kutokana na hali hiyo ya watu kujikatisha tamaa, wale ambao wamewahi kufanya biashara na kufilisika, wengi wao wamekuwa wakisema kuwa hawatarudia tena kufanya biashara hiyo.
Lakini kumbe, haikuwapasa kukata tamaa, bali kujipa moyo, na kuelewa kuwa pamoja na hali hiyo ya kushindwa inawapasa kujaribu tena. Kamwe usikate tamaa katika jambo lolote unaloliwaza ama kulifanya. Kwa kuwa, upo msemo mmoja unaosema, penye nia pana njia.

*MAFANIKIO HUTOKANA NA IMANI YAKO*

Ili kuwa mtu wa mafanikio ni vema kutumia mbinu ya ufikiri kwa ubunifu kile unachotaka kukifanya. Ni vizuri kuwa na imani, unaweza kufanya jambo lako na likafanikiwa, kwani unapoamini litafanikiwa, akili yako itazidi kutafuta njia ya kulifanikisha zaidi.

Kuamini kuwa unaweza kufanya jambo kubwa, kunafungua njia ya mafanikio. Kamwe usiseme ama kufikiri kuwa huwezi kufanya jambo fulani katika maisha yako, badala yake, jaribu kufanya kile unachofikiri kuwa huwezi. Usiruhusu mambo ya mila na desturi ama utamaduni uliouzoea kutawala akili yako. Kuwa mtu wa kupokea mambo na mawazo mapya kila wakati, kisha uyafanyie kazi.

Kila wakati jaribu njia mpya katika kufanikisha mambo yako, pamoja na kuwa mfuatiliaji wa shughuli zako unazozifanya. Iulize nafsi yako, inakupasa kufanya nini ili kuweza kufanya vizuri zaidi? Wakati unajiuliza swali hilo, unakuwa tayari umeshapata jibu, cha msingi ni kulifanyia kazi jibu hilo ulilolipata bila kuchelewa. Pia jiulize ni kwa vipi unaweza kufanya vizuri zaidi?

Pia ni vema ukawa na mazoea ya kusikiliza na kuuliza kwa wengine,kuhusu mambo unayotaka kuyafanya kwani utapata mawazo mengi usiyoyajua kutoka kwa wengine.
Yapanue mawazo yako, kwa kujichanganya na watu mbalimbali wakiwamo wenye ujuzi wanaoweza kukupa mawazo na njia mpya za kufanya mambo. Moja ya kanuni ya mtu anayependa au mwenye mafanikio ni kuwa na muonekano mzuri mbele ya jamii, kuanzia anavyozungumza hadi mavazi yake.

Unaweza usikubaliane nami, lakini ukweli ni kuwa, kama wewe ni mfanyabiashara wa nguo, jinsi unavyokuwa mtanashati mbele za watu, ndivyo watakavyopenda kuja katika duka lako na kununua bidhaa zako hizo. Lakini, kama utakuwa haujijali kwa upande wa mavazi, halafu ukawa mfanyabiashara wa bidhaa hiyo, utapata wateja wale wasiokujua na wanaokujua wachache.

Utanashati unavutia biashara yako, si tu kwa biashara ya nguo, bali hata katika shughuli zako nyingine unazozifanya, uwe ni mwanasheria, mwalimu ama mpishi wa chakula, vile unavyoonekana ndivyo unavyozidi kuimarisha biashara yako. Kumbuka watu wanakutathmini kutokana na muonekana ulio nao. Hebu tuangalie mfano huu kuwa, mtu anafanya biashara ya nyanya, anazipanga mafungu mafungu na kuziuza. Mwingine anafanya biashara hiyo hiyo, na kuziweka nyanya zile katika mfuko wenye kuonyesha bidhaa iliyopo ndani yake na kufunga vizuri.

Biashara hizo zikiwa katika eneo moja, watu wengi watanunua zile zilizofungwa vizuri kwenye mfuko wakiamini kuwa ni salama zaidi. Mfano huo ni sawa na muonekana ama utanashati wako kwa watu katika shughuli yoyote ile unayoifanya. Uvaaji mzuri na wa heshima kwenye jamii, unakufanya uheshimike na kuaminika kuwa unaweza kufanya mambo makubwa unayoyapanga.

Ni vizuri kuboresha mawazo yako kila siku, kama watu maarufu wanavyokuwa.
Kuboresha mawazo, kufikiri na utendaji wako kutakuletea mafanikio katika mipango yako yote.
Hivyo ni vema, kula vizuri ili uweze kufikiri vizuri katika mambo unayoyafanya.
Endapo hautakula mlo kamili, akili yako haitakuwa na uwezo wa kufikiri vizuri, utabakia kuwa mtu wa kushindwa. Kama mtu anakula vizuri, anajilinda na magonjwa mbalimbali, mwili wake unakuwa na afya pamoja na akili yake kuwaza mambo makubwa.

*Akili yako huwezi kuilisha chakula unachokula, bali chakula chake ni mazingira yanayokuzunguka.* Mtu yeyote anayetembea katika nchi ama mikoa mbalimbali, huwa na mazingira ya tofauti, kila anapokwenda hujifunza kitu kitakachomsaidia. Mazingira ya eneo ulilopo yanaifanya akili yako ifikiri zaidi ufanye kitu gani cha mafanikio katika eneo hilo ulilopo kitachokupatia maendeleo.Ukubwa wa jinsi unavyowaza, malengo yako, mazingira yako au vile unavyoonekana, ni kutokana na mazingira uliyopo.

Unapokuwa na watu wenye mawazo ya kuchelewa kufanikisha mambo, nawe utakuwa mtu wa kuchelewa kufikia malengo uliyojiwekea. Kwa maana nyingine, kushirikiana na watu wenye mawazo makubwa kunakufanya uwaze mambo makubwa ya maendeleo.
Pia kukaa karibu na watu wenye malengo ama maono ya mafanikio, kunakufanya nawe uwe katika hali hiyo.Kuna msemo usemao  *nionyeshe rafiki zako, namimi nitakuambia wewe ni nani*

_NB: Katika jamii tunayoishi, kumekuwa na watu wenye tabia zilizogawanyika katika makundi matatu._

Kundi la kwanza, ni la watu wale ambao wameona kuwa hawawezi kufanya jambo likafanikiwa kabisa. Wamekuwa na ujuzi na kukubali ujuzi huo katika eneo moja, yaani wameridhika na hali hiyo. Kama, Mungu amekupa ujuzi wako mzuri na ukabahatika kupata kazi sehemu nzuri, pamoja na kufanya kazi ile, utumie ujuzi wako katika maeneo mengine.
Unaweza kufungua ofisi yako na kuanzisha kitu chako mwenyewe huku ukiendelea na kazi yako.

Kamwe usijikatishe tamaa kwa kuona kuwa huwezi kufanya hivyo, kudhani kuwa, wewe umeumbwa kwa ajili ya kufanya kazi za wengine tu. Kuna watu wenye malengo makubwa na waliopanga kuyatimiza lakini kutokana na ushindani uliopo hufika mahali na kushindwa kuendelea na mikakati waliyojiwekea.Tunaweza kusema, wamekata tamaa na kuacha kuyafanyia kazi malengo yao, mwishoni hupoteza mwelekeo kabisa.

Kundi hili, wamejijengea tabia ya hofu, hofu ya kushindwa kutimiza malengo yao, hofu ya ulinzi, hofu katika jamii inayomzunguka na kupoteza kila wanalicho nacho.
Kundi la watu hawa, kamwe hawatafanikiwa kwani wameshajiweka kwenye kundi la kushindwa ingawa lina watu wenye akili, vipaji walivyojaliwa na Mwenyezi Mungu.
Kundi la tatu ni la watu wale ambao hawako tayari kukatishwa tamaa, hawa ni asilimia ndogo sana katika jamii.

Kundi hili pamoja na kukatishwa tamaa, katika mipango yao, wamekuwa wakijitahidi kufanya jitihada mbalimbali ili wajikwamue katika hali hiyo waliyonayo na kuwa katika hatua nyingine.
Mara zote hupumua mafanikio katika maisha yao. Kundi hili pia lina furaha kwa kuwa limeshakamilisha baadhi ya malengo waliyojiwekea. Wamekuwa wakipitia changamoto mbalimbali, lakini wamezishinda, wamekuwa wakiangalia siku mpya ikianza na jambo jipya. Ni ukweli usiopingika kuwa, kila mmoja wetu anapenda kuwa katika kundi la tatu, ambalo kila mwaka wanapata mafanikio, wanaofanya mambo mbalimbali na matokeo yake yanaonekana.


*MATOKEO YA MAONO* (The Impact of Vision)

*Katika maisha kuna nyakati tunapaswa kupanda katika vilele vya milima yetu binafsi ili tuweze kuuona mustakabali wetu (our future) kutokea katika kile kiwango cha juu tulikosimama*         (Dr. John Tibane)

*Mafanikio katika maisha ni safari, ila kuweza kukaa katika safari hii kunahitaji msukumoKatika maisha kunanyakati tunapaswa kupanda katika vilele vya milima yetu binafsi ili tuweze kuuona mustakabali wetu (our future) kutokea katika kile kiwango cha juu tulikosimama.* (Dr John Tibane).

Mafanikio katika maisha ni safari, ila kuweza kukaa katika safari hii kunahitaji msukumo wa ndani  pamoja na ujasiri. Bila vitu hivi muhimu wengi wetu hukata tamaa njiani na kuiahirisha kwa urahisi safari yao kuelekea mafanikio. Ni kwa jinsi unavyoupenda mustakabali wako na ni kwa jinsi unavyoipenda kesho yako ndiko kutakakokupa msukumo wa ndani pamoja na ujasiri. Ili kuweza kuiona kesho yako au mustakabali wako pasipo vizuizi inahitaji msaada wa kimungu (divine assistance) katika hali ya rohoni.

Kati ya siri mojawapo inayoweza kukusaidia ni kuandika katika karatasi nini unachokiona katika kesho yako, je unaona uzuri, furaha, amani, utajiri, mafanikio, au afya? Andikainawezekana kuwa ni kwenye chumba chako cha sala au sehemu unayopenda kuitumia kufikiria au kuwaza kiundani mambo ya maisha yako (meditation space).


Ili sasa kuianza safari yako kuelekea nchi yako ya ahadi, inakupasa kushuka chini kutoka mlimani ulikokuwa na kuja ardhini (In reality). Kumbuka kuwa kilakitu unachokiona huku chini katika ardhi kinaweza kuwa ni tofauti kabisa na vile ulivyoviona ukiwa juu katika kilele cha mlima, sasa unalazimika kuendelea kushika vema yale maono yako ya kweli uliyoyaona ukiwa juu, hata kama uhalisi unaoonekana huku chini ni tofauti. Utaanza kuishi na kutembea katika kuyafikia maono yako ukiwa hapa chini lakini si kama unavyoyaona mambo ukiwa chini bali kama ulivyoyaona ukiwa pale kileleni juu. Hii ndiyo tunayoiita ‘imani’  hakika ya mambo yatarajiwayo na bayana ya yale yasiyo onekana katika uhalisi hapa chini bali kama yalivyoonekana tukiwa kileleni pale juu.


Pasipo maono watu huangamia, maisha ya watu huharibika kabisa, watu huishi kihasara hasara tofauti na walivyo tazamiwa kuishi. Wanakosa uwezo wa kujitawala na kuwa na kiasi, wanakuwa watu wasiotawalika na waharibifu. Maono ya kweli  yanatupa kujiweza, kujitawala wenyewe, kuvumilia na kuwa na matazamio mema. Msukumo wa ndani na ujasiri huzaliwa kutoka katika maono ya kweli.


*Faida za maono .*

1.    
       *1. Maono ya kweli huyatia nguvu maisha yako.*

Maono ya kweli hukupa sababu na maana ya kwanini unaishi. Unatiwa msukumo, unahamasishwa, ni kama vile simu inapokosa chaji inalazimika kuwekwa katika umeme ili iweze kuongeza uwezo wa kufanya kazi. Maono ya kweli ni kama nguvu ya umeme ndani yetu. Maisha yako yanakuwa yaliyojaa, huna muda wa kupoteza kuanza kuongelea watu na kuchunguza maisha ya watu wengine na kamwe hutopata tatizo la kujihisi mpweke usiye na chakufanya.


2.      *2. Maono ya kweli huzikutanisha pamoja nguvu au nishati zilizopo ndani yako.*

Ndani yako una nguvu na nishati mbalimbali kama vile nguvu za kiroho, kimwili, kihisia, kiakili na nyingine nyingi. Nishati hizi ni kama vile miale ya mwanga ambayo inachomoza kutoka kwako. Maono ya kweli yanakuwa kama kioo kinachokuza (magnifying glass) kinachokutanisha miale yote hii katika sehemu moja, na hapa ndipo nguvu zako au nishati zako huweza kutumika katika kiwango cha juu zaidi cha ufanisi na matokeo bora zaidi.


3.     *3.Maono ya kweli hurekebisha tabia zetu*

Kile ulichoweza kukiona ukiwa pale kileleni mwa mlima wako binafsi kinauwezo wa kubadilisha tabia zako. Kinakufanya ushindwe kufanya kitu chochote cha kipuuzi ambacho kinaweza kuiharibu kesho yako nzuri uliokwisha iona ukiwa pale juu, kinakufanya uwe makini sana katika maamuzi unayoyafanya kila siku. Jinsi unavyo fikiri, jinsi unavyo zungumza na hata kutenda inakuwa kama vile tayari umeshafika kwenye ile nchi ya ahadi uliyoiona ukiwa pale juu. Maisha na mizunguko yako ya kilasiku yanaongozwa na maono yako ya kweli.


4.      *4. Maono ya kweli yanazishinda hofu zako.*

Kwa kawaida kitu chochote unachokiangalia kwa mkazo hupanuka na kuwa kikubwa. Kama utayatilia mkazo  matatizo yako basi yataongezeka na kuonekana makubwa na hatimaye kukuogopesha. Unapoogopeshwa au kutishwa na tatizo fulani unakata tamaa katika kulitafutia ufumbuzi na kuendelea mbele. Watu waliofanikiwa kamwe hawachagui kuyatazama matatizo yao (kama yanavyoonekana wakiwa chini ya mlima) bali huzitazama fursa mbalimbali za mustakabali wao (kama zilivyoonekana wakiwa kileleni). Kwa jinsi utakavyozidi kuyatazama mafanikio, fursa zitapanuka na zitaongezeka na kukushawishi katika kuendelea na safari yako ya mafanikio. Upendo wa kweli kupitia maono ya kweli huziweza hofu zote.


5.      *5. Maono ya kweli yana uwezo  wa kuvuta msaada.*

Maono ya kweli wakati wote yanauwezo wakushawishi kila aina ya msaada uhusianao na maono hayo kuja, kama ni watu, fedha, vibali, na vitendea kazi vingine. Wako watu wanakila kitu lakini wamekosa tu maono, wanasubiri vile walivyo navyo vivutwe kwa sumaku ya maono ya kweli ili viende kutumika kule kuliko sahihi.  Wako watu wamezaliwa ili tu wawe msaada wa maono uliyonayo. Wanasubiri kwa hamu wewe uyaandike maono yako.


Ili kuhesabiwa pamoja na waliofanikiwa inakudidi uweze kuyaangalia mambo katika kiwango cha juu zaidi ili uweze kupata maono ya kweli ambayo yatazaa uwezo wa wewe kuipenda kesho yako.

*son of Alpha and Omega*
*0712412170*
*PROPHET DERICDADY*

Saturday, September 1, 2018

*NJIA ZA KUEPUKA HASIRA.*

1: *Epuka Mabishano*: Mara nyingi hasira hupandishwa na mabishano baina ya mtu na mtu/watu.
Njia kubwa na rahisi ya kuepuka kupandwa na hasira, ni kwa kuepuka kubishana na mtu au watu, hasa wale wanao onekana wagumu kuelewa.
Penda kuepuka kujibizana au kumjibu  mtu kwa ukali.

2: *Penda kujishusha*: Unapogundua umemkwaza mwenzako, na akaanza kuzungumza kwa sauti ya juu na yenye ukali, basi penda kujishusha na kuzungumza kwa utaratibu, au kuomba radhi.
Hii husaidia kumshusha hasira mwenzio, kushuka kwa hasira kwa mwenzio husaidia kushusha yako pia.

3: *Jifunze kuwa na matumizi mazuri ya kinywa*:
Mara nyingi kinachompandisha mtu hasira huwa ni kauli chafu.
Jifunze kuwa na kauli njema itakusaidia kuepuka migogoro ambayo itakufanya upandwe na hasira au umpandishe mwenzio hasira.
Hasa kauli zenye kujaa matusi, kejeli, au dharau hupandisha mtu hasira.
Na sauti yenye ukali, kukoroma, au ukaripiaji, humpandisha mtu hasira.

4: *Penda kudharau watu*:
Dharau tunayo izungumzia hapa sio ile dharau ya kumbinulia mtu mdomo, wala kumshusha na kumpandisha macho.
Hapana, kudharau means "Humpi mtu attention anayoitaka ili kugombana na wewe "

Ukiona mtu anakutusi, analeta kejeli, au hata kuleta shari.
Njia pekee ya kumuepuka ni kwa kumdharau kama mtu asiye na akili, aliyekosa heshima na maadili.
Hivyo hujibizani nae, wala kumpa attention anayoitaka.

5: *Penda kuheshimu upeo wa mtu*:
Binadamu tumetofautiana upeo wetu wa kutafakari, kuelewa, na kujibu jambo, hivyo sio kila wakati mtu atakujibu au kufikiria kama ulivyotaka akuelewe.
Ukiona umemuambia mtu kitu halafu akakujibu hovyo, basi chukulia kama ndipo uwezo wake kufikiri ulipoishia.
Kama unaweza kumrekebisha basi tumia lugha safi, na sauti iliyojaa upole, na umueleweshe kwa hoja zilizo jaa hekima na busara.
Kumjibu hovyo pia huweza kuleta mtafaruku kati yenu.

6: *Jifunze kuishi na watu:*
Binadamu tumetofautiana historia zetu, kuendana na jamii tulizo ishi na aina ya maisha tunayopitia.

Kuna watu ukali, kupenda ugomvi, hasira za karibu, gubu/ulalamishi, ndio tabia zao.
Hata ukizungumza jambo la kawaida huwa wanalikuza.
Hivyo ni vyema kujifunza kuishi na watu wa aina hii, na njia pekee ni kuepuka kujibizana nao.

7: *Penda kusoma mood ya mtu:*
Ukiona mwenzio kapandwa na hasira, usijibizane nae.
Ukiona yuko na uchovu, usipende kumsumbua wala kumlalamikia jambo.
Ukiona yuko na stress, mpe tulizo, usimsumbue wala kumkaripia.
Ukiona yuko na hofu kupindukia, usimtishe kwa lengo la kumcheka, mpe tulizo.
Ukiona ana huzuni aidha amefeli jambo, au amefungwa team yake, au ameondokewa na kitu, au kakikosa, basi ni vyema kumfariji badala ya kumtamkia maneno ya kukera, kuudhi, dharau, au kejeli.
Hii itakusaidia kuepuka kugombana nae.

8: *Penda kuelimisha:* Wengi wetu tunapenda kuwa walalamikaji, ukaripiaji, na ndio tunachukulia kama njia sahihi za kutoa madukuduku yetu.
Tunakosea sana, hapo lazima utamkera mtu.
Njia nzuri ni kujifunza kumuelimisha mwenzio pale anapokosea, kumshauri, na yote yatumie sauti tulivu na kauli nzuri.
Hii itasaidia kuepuka ugomvi, achana na tabia ya kumtukana, kumlaumu, kumkaripia mwenzio.
Hii itampandisha hasira, na itakupandisha hasira wewe pia pindi ukijibiwa hovyo.

Hizo ni njia ya kuepuka wewe kupata hasira, pamoja na kuepuka kumpandisha hasira mwenzio.

*NJIA ZA KUTIBU HASIRA YAKO.*
- Ukiona ushaanza kupandwa na hasira ni vyema kukaa kimya, epuka kujibizana na mtu ili kuepuka ugomvi, au kuepuka asikujibu mambo yatakayo kupandisha hasira zaidi.
Au kama unaweza basi badilisha mada, au kama haiwezekani, endelea kunyamaza ili kuepusha shari.

- Jifunze jinsi ya kukaa na mtu mwenye gubu, lawama, ukiona kashaanza lawama tu basi shusha sauti yako haraka sana, au nyamaza, au omba udhuru utoke mara moja.

- Mtu anapokuudhi jifunze kubeba maumivu,  vumilia na ujishushe sababu kuendelea kujibu kwa ukali hukufanya uzidi kupandisha hasira.
Hii itakusaidia kipindi uko kwenye sehemu ambayo huwezi kuondoka karibu na aliyekuudhi...mfano: Kwenye daladala.

- Ukiona ushaanza kukasirika basi ondoka mahali penye mabishano.

- Ukipandwa na hasira, epuka kukaa karibu na aliyekuudhi, au kukaa karibu na silaha yeyote.

- Pata glass moja ya maji pindi unapoona hasira zimekupanda.

- Ukijijua una hasira kali zinazoweza leta madhara, ni vyema ukajizuia kufanya maamuzi yoyote.
Na njia sahihi ni wewe kukaa mbali na eneo la tukio.

- Kusali/kuswali husaidia kushusha hasira.

- Kuna nyakati inakuwa ngumu kuzizuia hasira sababu uko katika mazingira ambayo huwezi kuondoka, na huwezi kuvaa earphone ili usimsikilize sababu ni mtu unaye muheshimu.
Hapa ndipo unapotakiwa kujifunza kuwa kuidhibiti hasira huanzia ndani ya nafsi yako mwenyewe.
Nyamaza kimya, msikilize yeye.
Anza kujenga mawazo ya kitu kingine tofauti "Mfano: Dah lile pilau la jana".
Hii itakusaidia kuufanya ubongo wako usitafsiri zile kelele zake zinazopita masikioni mwako.
Na kuufanya ubongo uwe na mawazo tofauti kabisa.

Unadhani hii inafanyaje kazi???
Hebu fikiria, ulishawahi kuwa darasani,  mwalimu anafundisha, lakini mawazo yako mbaali.

Mwisho unastukia kipindi kimeisha na hujui kilichofundishwa.

*MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA.*

- Epuka kubaki na kinyongo au chuki kati yenu, jifunze kusamehe pale hasira zinapoisha.
Na kama ni mtu wa karibu, basi ni vyema mkaya suluhisha au kusameheana bila kuombana msamaha.
Chuki huzalisha madhara mengi zaidi.

- Epuka kununa nuna baada ya hasira kuisha, hii itakusaidia kukuacha huru bila stress za mtu yeyote.
Onyesha tabasamu pale hasira zinapoisha.

NB: Wanaume ni vyema kujifunza kuwa mpenzi wako akikununia baada ya kukorofishana, haimaanishi kuwa ndo hataki kuwa na wewe tena.
Wengine hununa kwa nia ya kutaka kubembelezwa, anahitaji kuiona thamani yake kwako.
.
Hata hivyo, hizi ni njia ambazo wewe utazitumia kuendana na eneo ulilopo, na ukubwa wa tukio.
Mara nyingi ukifatilia wanaopandwa na hasira huwa inatokana na wao kupenda kujibizana na mtu, tena kwa maneno ya kukera, na sauti ya juu.
Hapa lazima utapandwa tu na hasira, na mwenzio atapandwa na hasira.
Mwisho mnapigana.
.
Ukitazama sana watu wanaoudhi wenzao, utagundua ni kwasababu hawajui kusoma mood za wenzao, hawajui kutumia vinywa vyao vizuri ili kuwasilisha jambo.
Wanapenda kulalamika sana na kutumia kauli chafu na sauti kali.
.
Mungu awabariki sana na kuwafanyia wepesi.
Amen.

*Jifunze kuwa kimya HASIRA  inatibika*

*son of Alpha and Omega*
   0712412170

Tuesday, August 28, 2018

_*WEWE NI MGODI WA BARAKA*_

  _Kuna umhimu wa kujua wewe ni wathamani sana kuliko lulu,rubi,ata tanzanite_

  uthamani wako upo katika maamzi yako *if you born poor its not your mistake* kuzaliwa maskin sio kosa lako nikosa na udhembe wa baba yako, *But if you die poor it's your mistake* usikubari kufa maskini kisa umezaliwa familia maskini jijue wewe ni mtu *special* na hakuna mtu wa kufanana na wewe.
  amini inawezekana ukainuka tena kiuchumi usikubali kujiambia haiwezekani *imposible is the word only found in dictionary of foolish*   changamoto za leo zione kama daraja na darasa la mafanikio yako kesho

  *challange give eye of understanding*

   Ukiamini wewe ni wakushindwa utashindwa mpaka mwisho *if you fail to plan you plan to fail* jipe sababu elfu ukijithamini nakuamini nini unafanya kitakupa nguvu ya kufikia mpango wa Mungu kwenye maisha yako *remove failure is an option in your life*

 Hakuna alie wahi kufanikiwa akiwa amestarehe wote walipambana,simama,jiamini,fanya kile ambacho ni bora na kinaweza kukupa nguvu wewe unaweza *just do it*
  *walk with your dream everything is possible under the sun* daudi wa biblia alitembea na ndoto yake na akawa mfalme,yusuph alitembea na ndoto yake akawa waziri mkuu misri.usidharau ndoto yako kwasababu  wewe ni dhaifu huna elimu,umezaliwa hujalelewa na baba,yatima ama huna mfadhiri. *mawazo yako yakujionea huruma ni adui yako wa kwanza wa umaskini* Amini wewe unaweza fanya jambo lolote na ukafikia malengo stahiki  *adui yako wa pili ni mazingira yako* siku, zote uwa yanakuvunja moyo ukitazama uharisia
  *jamaa na ndugu zako,ni adui yako wa 3* ukitaka kuishangaza dunia jikane na simama kama mti mkavu *they know your history but not your future* ukisimama kama shujaa mwenye malengo ndoto,maono utaacha historia yako jiamini *nothing to fear but to fear itself* songa mbele wewe ni mgodi wa baraka.
     waache wachimba madini wakutafute usiku namchana usilale simama utimilize maono yako wewe ni shujaa jiamini.

 *0712412170*
_*SON OF ALPHA & OMEGA*_
 *PROPHET DERICDADY*

Monday, August 27, 2018

SOMO: ZIJUE AINA ZA NDOA MHIMU KUJUA

Katika pita pita zangu nimekutana na maneno haya juu ya aina za ndoa nimeamua nishare nanyi wana jamii.
Angalizo kwa ulie katika aina yoyote tajwa,usijitie hatia ktk hali uliyonayo. Kikubwa mtumainie Mungu upate faraja na amani katika maisha kwa maana yeye ndie msemaji wa mwisho na ikiwa ameruhusu jambo hilo litokee kwako maana yake kwake kuna suluhisho la kudumu.

1⃣ Ndoa ya Uhalamia(Kidnaper Marriages.

Hii ndoa ya watu ambao wamechukuana bila utaratibu maalumu. Mchungaji hafahamu,sheikh au wazazi hawafahamu.

Na wala Hakuna Mahari imetolewa ni ndoa ya uharamia ambao wao tu wawili wanahimizana na kukwapuana kinyemela.
Baadaye watu wengine wanakuja kujua tayari watu wanaishi pamoja.

2⃣ Ndoa ya Ujambazi (Hizi ni ndoa za mtu kulazimishwa) robbery Marriage.
Wazazi wanaamua kumlazimisha binti au kijana kuolewa au kuoa mtu ambaye hampendi.
Inaweza kufikia kiwango hata cha kupingwa na kuwekewa vikwazo ili uolewe au uoe huyo ambaye ni Chaguo lao na Siyo wewe. Kwahiyo mtu anajikuta ameingia kwenye ndoa Akiwa amesukumiwa.

3⃣ Fixed Marriage(Ndoa yenye Masharti ya Vifungo)

Hii ni ndoa ambayo watu wanahimizwa na Ndugu au Wazazi kuwa.

_Unatakiwa uolewe na kabila lako.

_Unatakiwa uoe kabila lako.

_Unatakiwa uoe Ukoo fulani.

_Unatakiwa uolewe na Ukoo fulani.

Na Ukienda kinyume nao Watakuinukia Ndugu wote kukupingana na Unachotaka kufanya na badala yake Unalegea na Kuamua Kuoa au Kuolewa kama Wanavyotaka wao.
Na Ukiwakatalia watatamka laana.
Mfano:
_Ukiolewa hutazaa
Au Ukiolewa Mume wako atakuwa Mto.
_Watoto wako watakuwa Bata.

Wako watu waliingia ndoa za namna hii kuogopa Vita ya Ndugu kuwainukia.

4 ⃣ CATERPILLAR MARRIAGE(Ndoa ya Tingatinga)

Hii ni ndoa ya watu ambao baada ya tu ya Kifunga ndoa wataanza kukabiliana na matatizo. Vifo vya watu wao wa karibu,biashara kuanza kudorola,miradi kuanza kuharibika,Kama ni Mifugo itapata magonjwa na kufa,Kama ni Biashara haiendi tena. Milango yao yotee ya mafanikio imeharibika. Hapo ujue Spirit of CATAPILLAR..

Inatokana na Baadhi yao Hawakuwa wamepata muda wa kuvunja roho za Ufilisi.

Ndio maana semina ya vijana na mafundisho kabla ya ndoa Ni ya muhimu sana. Ili isije kuchelewa mmeingia kwenye ndoa hayo yakawapata mkashangaa nini kimetokea.

PREVENTION IS BETTER THAN CURE.


Tumia somo hili Kujikinga kama bado hujaingia kwenye ndoa na Kama umeshaingia Usijute MTAFUTE MFINYANZI WA AJABU MWAMBIE FINYANGA NDOA HII IKAE VIZURI NA YEYE NI MWAMINIFU ATAIFINYANGA.
5

5⃣ Ndoa ya MTUMBA(Second hand Marriage)

Ndoa ya kuoa au kuolewa na Mtu ambaye tayari alishakuwa ameoa au Ameolewa.

Kuvaa Mtumba lazima uamue Kukubaliana na harufu ya Mtumba.

Ukubaliane na Kiatu cha Mtumba vingine vinakuwa vimeangalia upande.

Ukubaliane nyingine zimeshaunguzwa na Pasi.

Hivyo kuingia kwenye ndoa ya Mtumba Uwe tayati kukubaliana na Jinsi ilivyo.

Ndoa hii huwa ni Kama kulalia Kitanda kikuukuu au Cha Zamani.

Ukubaliane na Kutu na Kunguni wake.

Itabidi ukikungute sana sana mpaka kunguni wote wawe wametoka.

Anyway Hii nayo ni Ndoa na watu wengi wameingia na Kama hawakupata mwongozo bora wataishia Kushangaana na Kuangaliana bila majibu.ingawa si zote za aina hii huwa mbovu. Kikubwa ni kumtanguliza mwanzilishi wa ndoa aikarabati nae ni Muumba.

6⃣ Triangle Marriage.(Ndoa ya Pembetatu)

Hii ni Ndoa yenye Uanzishwaji Na Mungu mwenyewe kuweka Upendo wa kweli Ndani ya wawili. Na wakaamua Kupendana Bila Masharti na Mungu mwenyewe akaandaa Mpango wa Kuwakutanisha na Wakishakutana Huwa kuna Hisia Za Upendo wa Kimungu na siyo Tamaa ndani yao.

Upendo huu sio tamaa kwani utawafanya Kuwa na Nidhamu ya Kumhofu Mungu na Kusubiri wakati wake.

Upendo wenye tamaa nyuma yake huwa una madhara ya Watu Kushirki tendo la ndoa kabla ya Harusi au Siku ha Ndoa.
Ni upendo wa Kiwizi wizi. Na wote ambao Walighafirika kabla ya siki ya Ndoa kuna maombi na Kazi yq Kufanya bila Kupuuzia.
Upendo huu wa Kimungu utawafanya wapendao hao kuruhusu Mungu kuwa Msemaji Mkuu katika Mwanzo wa Uhisiano wao,Mwendelezo wa Uhusiano wao na Mwisho wa Uhisiano wao Hadi Kuingia kwenye Ndoa.

Nidhamu na Hofu mbele za Mungu huwatawala wote wawili kwasababu Yuko dereva Makini aitwaye Jehova anawaongoza. Kundi hili la Wanandoa ni wachache sana Na wengi ndoa zao Zinadumu hata kama kutakuwa na Kolugesheni na Ups and Downs.G.O.D huwa anawasaidia Kuvuka salama.

NI MAOMBI YANGU KUWA SOTE TUINGIE KWENYE KUNDI HILI LILILOJAA BARAKA NA FURAHA TELE

7⃣ Suggestion Marriage( Ndoa za Ushauri)

Hii ni ndoa ambayo Mtu anashauriwa na Mchungaji,anashauriwa na Wazazi au Anashauriwa na Baadhi ya ndugu kwamba fulani atakufaa.


USHAURI WA MCHUNGAJI AU MTU YEYOTE UTAKUBALIKA PALE TU -JEHOVA AKIWEKA APPROVAL YAKE.

Kataa ushauri wa Mchungaji hata wa Askofu kama Jehova Umwabuduye Amelikataa.

Samwel Alimuombea Saul Rehema.
Mungu akasema Nimemkataa.

Samwel aliwaona Kaka zake Daudi wanafaa.

Lakino Mungu alipingana na Ushauri wa Samwel Nabii.

Hivyo Ushauri wa Mchungajo siyo Mwisho wa Maelezo.

Take your step to ask GOD for Approval.

8⃣ MRS HUSBAND AND MR.WIFE marriage. (BI.BWANA na Bw.MKE)

Hiyo ni ndoa ambayo msemaji Mkuu katika Uchumba hadi Ndoa ni Mwanamke.
Kichwa cha Mwanamke kinakuwa juu ya kila mtu ndani ya Nyumba.

Mke huwezi kumkaripia Mumewe na Kumwamulia baadhi ya Matukio Mfano.

1. Wewe chukua nguo hizi ukafue.
2. Wewe kwanini hujatandika kitanda.
3. Wewe nini Wewe na Kwanini ni maneno yanatumika sana kwa upande wa mke kwa mumewe.

Kwa ambao bado hawajaingia Ukipata rafiko ambaye akikwambia kitu usipofanya ananuna ujue ana Roho Ya MRS.HUSBAND.

Atataka akukalie kwenye Mabega.

Si ajabu ukute Baba Anaosha vyombo na Mke kakunja Miguu sebuleni anaangalia Filamu.

Si vibaya ukute Mume anaogesha watoto na Mke Kanyoosha Miguu sebuleni.

Ujue hii Ndoa Inasumbuliwa na Roho ya MRS.HUSBAND.

Son of Alpha & Omega
Prophet Dericdady
0712412170

Saturday, June 23, 2018

_*NEVER AGAIN*_👇🏽

🍂 _Never again will I say *"I CAN'T"* because I can do all things through Christ Jesus._
📖 *Philippians 4:13*

🍂 _Never again will I say *"I DON'T HAVE"* because my God shall supply all my needs according to His riches._
📖 *Philippians 4:19*                                

🍂 _Never again will I say *"I AM AFRAID"* because God has not given me a spirit of cowardice but a spirit of power._
📖 *2 Timothy 1:7*

🍂 _Never again will I say *"I LACK FAITH"* because God has given to every man a measure of faith._
📖 *Romans 12:3*                                                                        

🍂 _Never again will I say *"I AM WEAK"* because the Lord is the strength of my life._
📖 *Psalm 27:1*                  

🍂 _Never again will I say *"SATAN IS POWERFUL"* because greater is the God that is in me than the evil in the world._
📖 *1 John 4:4*                

🍂 _Never again will I say *"I AM DEFEATED"* because we are more than conquerors through Christ Jesus._
📖 *Romans 8:37*                

🍂 _Never again will I say *"I LACK WISDOM"* because Christ has become for us the wisdom of God._
📖 *1Corinthians 1:30*    

🍂 _Never again will I say *"I AM SICK"* because through His stripes we are healed._
📖 *Isaiah 53:5*                  

🍂 _Never again will I say *"I AM BURDENED"* because I cast all my burdens upon Jesus who cares for me._
📖 *1 Peter 5:7*            

🍂 _Never again will I say *"I AM IN BONDAGE"* because where the spirit of the Lord is there is freedom._
📖 *2Corithians 3:17*        

🍂 _Never again will I say *"I AM CONDEMNED"* because there is no condemnation for those who are in Christ Jesus._
📖 *Romans 8:1*

*May God bless you Today Tomorrow and Always*

Saturday, June 16, 2018

DALILI ZA KUJIJUA KAMA UNA JINI MAHABA.
NA:MAJOR PROPHET DERICDADY
EMAIL:dericglory@gmail.com
0712412170 au 0679008354

1. Kuota unafanya MAPENZI na MTU unayomjua au usiyemjua kwa sura tofauti.
2. Kuota unafanya mapenzi na mnyama.
3. Kuota unanyonyesha au kujifungua mtoto.
4. Kutokudumu kwnye mahusiano kama ndoa au mchumba.
5. Kuwa na hasira za haraka.
6. Kukwama kwa mipango yako.
7. Kupoteza pesa au vitu vya thamani, unaweza ukaweka pesa kwenye walet au mahali salama kabisa kisha ukakuta zimepungua.
8. Kutokuwa na hamu ya mapenz kwa wanawake na wanaume kutokuwa na nguvu za kiume.
9. Kuota umefunga ndoa.
10. Maumivu ya kichwa,mgongo,kiuno na tumbo haswa chini ya kitovu.
11. Kuvulugika siku au kuharibika kwa mimba au kutoshika mimba kabisa.
12. Kuumwa U.T.I isiyoisha inayojirudia.
13. Kutokupenda kabisa mahusiano.
14. Matiti kujaa au kutoa maziwa na hauko mjamzito au unanyonyesha.

UKIJIJUA UNADALILI HIZI JUA JINI MAHABA AU ANZURA ANAKAA NDANI YAKO.MAANA WADADA WENGI HAWAOLEWI KWA SABABU HII,AMA KUVURUGA NDOA.PIGA NAMBA ZILE KWA MSAADA WA MAOMBEZI YA HARAKA.

  UBARIKIWE NA YESU.

Thursday, June 7, 2018

WHERE TO FIND HELP IN THE BIBLE

*SALVATION*
_____________
Acts 16:31
Acts 4:12
Revelation 7:10
Psalm 27:1
Isaiah 12:2
Philipians 2:12
Romans 10:9
Titus       3:5
1 John 3:14
Ephesians 1:7



*FORNICATION*
_______________
Colosians 3:5
1Thesalonians 4:3-4
1 Corinthians 16:13-18
Revelation 22:15



*LAZINESS*
___________
Proverbs 6:6-10
Proverbs  13:4
Proverbs  20:13
Proverbs   10:4
Proverbs  20:4



*HOW TO PRAY*
_______________
Matthew 6:5-6
Mark 11:24
Job 8:5
Isaiah 51:1-4
1 Samuel 1:12-13
John 15:7



*TEMPTATION*
_______________
James 1:2
2 peter 2:9
Matthew 4:3
1 Corinthians 10:13
Ephisians 6:13
Hebrews 2:18
Genesis 3:6



*IDOLATRY*
____________
Exodus 20:1-3
1 Corinthians 10:14
Leviticus 19:31
Deutronomy 27:15



*THE LOVE OF MONEY*
________________________
1 Timothy 6:6-10
Hebrews 13:5
Leviticus 19:35
Hezekial 18:13
Proverbs 20:17



*BAD COMPANY*
_________________
1 Corinthians 15:33
1 Corinthians 5:9
 2 Corinthians 6:14-16
Exodus 23:1-2



*HUMILITY*
___________
James 4:10
Matthew 18:10
Luke 14:10
1 Peter 5:5-10



*MIND YOUR DRESSING*
_________________________
1 Peter 3:3-5
Deutronomy 22:5
1 Timothy 2:9-10
Isaiah  3:16-17
1 Corinthians 6:19-20



*MARRIAGE*
____________
Genesis 2:24
Romans  7:2
1 Timothy 3:12
Mark     10:9
Proverbs 18:22
Hebrews  13:4-6
Ephesians 5:22-31
1 Peter:3:7-8



*JESUS'S SECOND COMING*
____________________________
Luke 12:40
James 5:8-9
1 John 2:28
2 Corinthians 7:1
John 14:3
Revelation 3:11
Revelation 22:12
Revelation 16:15
Matthew 24:30
Matthew 16:27
Mark 8:38
1 John 3:23



*FAITH*
________
Ephesians 2:8-9
Ephesians 6:16
Luke  17:5
1 peter 1:7
Romans 10:7
Galatians 5:6
Hebrews 11:1
James 1:3-6



*REPENTANCE*
________________
Proverbs 28:13
Proverbs 1:23
2 Chronicles 30:6
Ezekiel 18:31
Acts 17:30
Luke 18:13-14
Luke 13:3
Joel 2:12
Acts 2:38
Zephaniah 2:3


Dericglory@gmail.com
0712412170

Monday, June 4, 2018


 JIFUNZE KOZI HII YA UCHUNGAJI.
MASOMO HAYA YOTE UKIMALIZA UMEPIGA HATUA KUBWA KATIKA UTUMISHI.



SOMO LA 1
MUNGU


1.1  Uwepo wa Mungu

“Mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kuwa yeye yupo  na
kwamba huwapa dhawabu wale  wamtafutao” ( Ebr 11:6). Lengo la
masomo haya ni kuwasaidia wale wanomwendea Mungu, wakiisha
mwamini “Kwamba yupo”; kwa sababu hii hatutajitia  kwenye
ushahidi usiothibitisha  imani ya kuwa Mungu hayuko.katika
kupima muundo wa miili yetu (Zab 139:14)  Ushahidi wa kielelezo
katika ua, Kukazia macho juu kwenye anga pana wakati wa usiku
kukiwa wazi  bila mawingu, haya na mengine yasiyohesabika,
Mawazo ya kangaliifu juu ya maisha,  hakika yanafanya imani ya
kutosadiki kuwa Mungu hayupo iwe ni ya kushangaza. Kusadiki
kuwa Mungu hayuko  hakika inahitajika imani zaidi  kuliko
kuamini yupo,pasipokuwepo Mungu mpangilio haupo, Kusudi au
kutoa maelezo ya asili  ya Ulimwenguni  basi hii itafikiriwa katika
maisha ya mtu asiyeamini kuwa Mungu yupo. Tukikumbuka hili,
siyo ajabu kuwa watu wengi  wanakiri kwa kiwango fulani  cha
kumwamini kuwa Mungu yupo hata katika jamii ambayo vitu vya
mwili  ni Mungu  anayeshinda maisha ya  watu.
   11


Lakini ipo tofauti pana kati ya kuwa na fikra isiyodhahiri ya
kwamba ipo nguvu ya juu, na hasa kweli kuwa na uhakika kwa kile
ambacho Mungu anampa mtu anayemtumikia kwa Uaminifu.
Waebrania 11:6  jambo hili tunasoma;

 “Yatupasa tuamini kuwa (Mungu )yupo na
 Kwamba huwapa thawabu  wale wamtafutao kwa bidii”

Maelezo mengi ya biblia ni historia ya watu wa  Mungu
Israeli; mara kwa mara neno limetolewa kwamba kukubali kwao
kuwa Mungu yupo hakukulingana  na imani zao kwa ahadi
zake.Waliambiwa na mkubwa kiongozi wao Musa'Kwa hiyo
ujue…….Ukaweke moyoni mwako, ya kuwa BWANA ndiye
Mungu  katika mbingu juu, na katika nchi chini,  hapana mwingine.
Basi, zishike sheria zake,  na amri zake  (Kum. 4:39:40).
Neno hili hili limetolewa  - ufahamu wetu katikati yetu ya
kuwa  Mungu yupo hakumaanishi kwamba tunakubalika mbele za
Mungu bila kufikiri.Ikiwa bila mchezo  tunakubali kwamba kwa
kweli tunaye  Muumba,'Kwa sababu hiyo tuzishike sheria na amri
zake’ Ni shabaha ya  mfululizo huu wa masomo kuelezea  amri hizi
jinsi zilivyo na namna ya kuzishika. Tunapochungunza maandiko
kwa kufanya hivi, tutakuta kwamba imani yetu kuwa Mungu  yupo
inatiwa nguvu.

‘Imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la
Mungu’ (Rum 10:17). Vile vile,(Isaya 43:9-12) yaonyesha namna
ya kufahamu unabii wa  Mungu kuhusu wakati ujao - Unabii
unatufanya tujue'kuwa mimi ndiye’ (Isa. 43:13)- yaani  hilo jina la
Mungu, 'Mimi niko ambaye NIKO’ kwa ukamilifu ni kweli (Kut.
3:14.)  Mtume Paulo alifika kwenye mji unaoitwa Beroya, eneo hili
kwa sasa liko kaskazini mwa Uyunani ( Ugiriki) kama kawaida,
12

akahubiri injili (Habari njema) ya Mungu; lakini badala ya watu
kusikia neno la Paulo alilokuwa anasema, tunasoma kwamba, “
Walilipokea kwa kusikia neno (la Mungu, sio la Paulo) kwa
uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone
kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo. Basi watu wengi miongoni
mwao wakaamini  ( mdo 17:11,12)

Imani yao ilikuja kwa kuwa mioyo yao ilikuwa wazi, sawa
sawa (‘ Kila siku’)  na kwa utaratibu wa (‘mambo hayo’)
waliyachunguza katika Biblia, Basi  kupata imani ya kweli haikuwa
Mungu aliwafanya wawe nayo ghafla kwa aina fulani ya upasuaji
wa moyo wa kiroho,  pasipo kujihusisha na neno la Mungu. Ni jinsi
gani basi watu wa Ulimwengu  wanaweza kufuata kwa moyo
pigano juu ya  maovu  la Bill Graham au  uamsho wa mikutano ya
wapentekoste kisha wanahama  tena  kama'Waamini’ ? Ni muda
gani wameendelea katika masuala haya  wakiwa wanachunguza
maandiko kila siku ?  Kwa kweli kukosekana huku kwa imani
ambayo msingi wake upo kwenye Biblia bila shaka kunaonyesha
utupu wa'Waongofu’  hawa na kujikuta  baadae kwa wanayopata
Wakristo,  na ni kwa sababu gani wengi wanaondoka  kutoka
kwenye Ushirika  wa Madhehebu ya wa-Injilisti.
 
Masomo haya  lengo lake ni kukupa mjengo wa  utaratibu
wako mwenyewe  kuchunguza maandiko, ili kwamba nawe pia
uweze  basi kuamini muunganiko kati ya kusikia  Injili ya kweli na
kuwa na imani  ya kweli mara  nyingi kumejitokeza wazi  katika
taarifa ya kuhubiri injili.

• “Wakorintho wengi waliposikia waliamini wakabatizwa”
(mdo 18:8)
• Watu wasikie neno la Injili, waamini ( mdo 15:7)
• Ndivyo tuhubirivyo, na ndivyo mlivyoamini'(1 Kor. 15:11)
   13

• ‘Mbegu’  Kwenye mfano wa mpanzi  ni neno la Mungu
(Luka 8:11) wakati katika huo wa mti wa haradali  ni imani ( Luka
17:6) kwa kuona kwamba imani huja  kutokana na kupokea'Neno
kwa imani’ ( Rum 10:8) “Maneno ya imani,  na mafundisho
mazuri” ( 1Tim 4:6), katika moyo ambao upo  wazi kumwamini
Mungu  na neno lake  (Gal 2:2, Ebr 4:2)

• Mtume Yohana anaisema taarifa  iliyoandikwa ya maisha
ya Bwana  kuwa anasema' kweli ( Yaani ukweli) ili nanyi mpate
kusadiki’ ( Yohana 19:35).Basi neno la Mungu  limeitwa
‘Kweli’(Yoh:17:17) ili mpate  kuamini.

1.2 Nafsi yake Mungu

Ni mwenye enzi, Mungu aliyeandikwa katika Biblia  na
kwamba ni kweli, mtu wa kugusika, naye yupo katika umbo.
Vilevile ni mafunzo ya kwanza  ya Ukristo  kuwa Yesu ni mwana
wa Mungu. Ikiwa Mungu hana umbo , basi  haiwezekani yeye
kuwa na mwana  ambaye alikuwa ni 'Chapa ya nafsi yake' (Ebr 1:3)
Tena  inakuwa vigumu kuendeleza  maisha ya uhusiano wake na
mungu  ikiwa Mungu  ni wazo lililo kwenye akili zetu,
Mkusanyiko wa roho  mahali popote juu katika  anga lisilo na kitu.
Ni huzuni  kusikia kwamba dini za watu wengi  zina wazo lisilo la
kweli  lisilotambulika kuhusu Mungu. Yeye akiwa mkubwa mno
kuliko sisi,  inaeleweka ya kwamba imani  ya watu wengi imeweka
kikwazo kwenye ahadi  dhahiri  kuwa mwishowe tutamwona
Mungu. Israeli  walikosa imani ya kumwona Mungu  alivyo  (Yoh.
5:37) ni dhahiri ana umbo halisi, Imani hii huja kutokana na
kumjua Mungu kwa kuamini neno lake

14

 Heri walio safi wa moyo, Maana watamwona Mungu (Math
5:8)
Na watumwa wake (Mungu) watamtumikia, nao watamwona
uso wake, na jina   lake(Jina la Mungu ) litakuwa katika vipaji vya
nyuso zao (Uf 22:3-4)

Tumaini hili la ajabu kama kweli tunaliamini litaonyesha
matokeo ya matendo  kwenye maisha yetu:

• Tafuteni kwa  bidii kuwa na amani  na watu wote  na huo
utakatifu, ambao hakuna mtu atakaye mwona  Bwana asipokuwa
nao (Ebr 12:14)
• Tusiape, kwa kuwa  aapaye kwa mbingu,  Huapa kwa kiti
cha  Mungu na kwa yeye  na kwa yeye aketiye juu yake  ( Math
23:22) hii itakuwa haina maana ikiwa Mungu  sio mtu mwenye
mwili.
• Tutamwona kama alivyo (akidhihirika katika kristo ) na kila
mwenye matumaini  haya katika yeye  hujitakasa, kama yeye
alivyo mtakatifu (1 Yoh 3:2,3)

Katika maisha yetu haya kumfahamu Mungu wetu wa
mbinguni,  hakujakamilika sana. Tunaweza kutazama mbele,
kupitia giza linalotatanisha la maisha haya hadi mwisho wa
kukutana naye. Kumwona kwa macho yetu hapana shaka kutakuwa
sawa na kumfahamu kwa akili  zaidi. Kutoka vina vya masumbufu
ya mwanadamu. Ayubu aliweza kufurahia  uhusiano wake wote na
Mungu  ambao utimilifu wake  atauona mwisho wa siku.

Na  baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi (Yaani katika
mauti),Lakini pasipokuwana mwili wangu  (Yaani pasipo mwili
unaoharibika ) nitamwona Mungu;Nami nitamwona mimi nafsi
yangu,na macho yangu yatamtazama, wala si mwingine (Ayubu
   15

19:26,27). Mtume Paulo aliyatazamia maisha mengine  yasiyo
machungu  yasiyo na msukosuko: “Maana wakati wa sasa tunaona
kwa kioo kwa jinsi  ya fumbo; Wakati ule tutaona uso kwa  uso” (
1Kor 13:12)

USHAHIDI WA  AGANO  LA  KALE
Ahadi hizi  zilizo katika Agano Jipya  zimejengwa juu kwenye
ushahidi wa mambo yake makubwa  ya  Agano la kale, Kuwa ni
Mungu aliye na mwili. Ushahidi hauwezi kukaza zaidi  lakini ni
mwanzo wa kukubali  hali ya Mungu kama tunataka kuwa  na
ufahamu wa kweli  yoyote  kuhusu dini ambayo msingi wake  upo
kwenye Biblia. Agano la Kale lina mazungumuzo ya Mungu kuwa
ni mtu na mtu uhusiano wa mtu na mtu pamoja  Mungu, ambao
Agano la Kale na Jipya linausema  ni wa pekee kwa  tumaini la
Ukristo  wa kweli. Yafuatayo ni majadiliano ya nguvu  kwa ajili
yake, Mungu aliye na mwili.

“Mungu akasema, Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura
yetu” (Mwa. 1:26) Hivyo mtu amefanywa kwa mfano  na sura ya
Mungu, Kama ilivyodhihirika kupitia Malaika. Yakobo 3:9
anasema … Wanadamu waliofanywa kwa mfano  wa Mungu.
Maneno haya hayatumiki kutaja  mfano wa akili ya mwanadamu,
kwa kuwa hali ya fikra zetu  zipo mbali kabisa toka zake Mungu na
katika njia nyingi  kwa kikubwa  zimepingana na haki
yake.”Maana  mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si
njia zangu, asema Bwana. Kwa maana kama vile mbingu  zilivyo
juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu  zi juu sana  kuliko njia
zenu, na mawazo yangu  kuliko mawazo yenu” ( Isa 55:8 - 9 ).
Kwa hiyo mfano na sura, tunavyoshirikiana naye Mungu, inabidi
uwe ni mfano wa mwili- Lakini yeye hana wa dhambi.
 
16

Popote Malaika  walipoonekana duniani wamesemwa kuwa
wana umbo la watu, kwa mfano, Abrahamu aliwakaribisha malaika
bila kujua, akizania kuwa walikuwa watu wa kawaida. Sisi jinsi
tulivyoumbwa kwa mfano wa Mungu kwa kweli maana yake ni
kwamba tunaweza kufahamu  jambo lingine kuhusu mtu halisi,
ndivyo tulivyo, lakini tunafanana. Basi,  Mungu tunaye mshabihi
siyo mtu mwingine asiyedhahiri ambaye hatuwezi kumfikiria.

“Wao wenyewe Malaika wanafanana na Mungu. Hivyo
Mungu aliweza kumsema Musa, “Kwake nitanena mdomo kwa
mdomo, maana wazi wazi wala si kwa mafumbo. Na umbo la
Bwana yeye ataliona” (Hesabu 12:8) Haya yalikuwa yanamtaja
Musa, akifunzwa na Malaika  aliye kuwa na jina la Bwana (Kut.
23:20:21) Ikiwa Malaika alikuwa na umbo la Bwana, Inaonyesha
kuwa Mungu amefanana na Malaika  Yaani - Kimwili  ana umbo la
Mwanadamu. “BWANA alisema na Musa uso kwa uso  kama vile
mtu asemavyo na rafiki yake. (Kut. 33:11: Kum. 34:10 ). Bwana
alijidhihirisha katika Malaika wake, ambaye uso na kinywa
alifanana na Bwana mwenyewe.

 “Kwa maana yeye anatujua umbo letu,  (Zab. 103:14).Ana
tutaka yeye,  tumfikirie kuwa ni mtu, Baba ambaye tunaweza
kuunganishwa naye.Huyu ataelezwa kwa ushahidi mwingi  wa
mikono ya Mungu, Viganja,Macho  n.k. Ikiwa Mungu alikuwa ni
furushi la Nafsi mahali fulani katika mbingu, ambazo inabidi ziwe
Mungu, ni wazo letu kama tukitaka utu wake;  basi ushahidi huu
unatupotosha kukuza  kusudi lolote.

 “Maelezo ya sehemu ya makao ya Mungu, Wazi wazi
yanaonyesha kwamba “Mungu” ana mahali pake; “Mungu yuko
Mbinguni”( Mhubiri 5:2);Maana ametazama toka patakatifu pake
pa juu, toka mbinguni BWANA ameiangalia nchi (Zab 102:19,20);
   17

“Usikie huko mbinguni, Makao yako” (1Fal. 8:39). Lakini kwa
kupambanua zaidi kuliko hivi tunasoma kwamba Mungu ana “Kiti
cha Enzi” (2 Nya. 9:8, Zab 11:4; Isa. 6:1,66:1).Lugha kama hii ni
ngumu  kuitumia nafsi isiyo wazi  kabisa, inayokaa katika milki ya
Kimbingu. Mungu amesemwa kuwa “Ameshuka kuja chini”
wakati mwenyewe anapojidhihirisha. Hapa panadokeza  makao ya
Mungu yaliyo mbinguni. Inakuwa vigumu kueleza wazo  la
udhihirisho wa Mungu  bila kukubali hali ya umbo la Mungu. Isaya
45 ina ushahidi tele wa Mungu  kujihusisha kwake  katika mambo
ya watu  wake: “Mimi ni BWANA, wala hapana mwingine …..,
mimi ni  BWANA anayetenda haya yote …., Mimi, BWANA
nimeiumba Ole  wake ashindanaye na Muumba wake … Mimi,
naam, mikono yangu mimi,  imezitanda mbingu …, niangalieni
mimi mkaokolewe, enyi ncha zote  za  dunia. mstari hasa kweli huu
wa mwisho  unaonyesha uwepo wake Mungu - Anawataka watu
wamwangalie yeye, Kuwaza uwepo wake  halisi pamoja na jicho la
imani.

Mungu amejifunua  kwetu akiwa ni mwenye kusamehe
anayesema, maneno kwa watu. Hata hivyo msamaha  na usemi
unaweza  tu kutoka kwa mtu: ni matendo ya akili, Hivyo Daudi
alikuwa ni mtu  aliyeupendeza moyo wa Mungu  (1 Sam 13: 14),
inaonyesha kwamba Mungu ana moyo, unaoweza kunakiliwa kwa
kiwango kidogo na mtu, ingawa mwanadamu wa mwili
haupendezi moyo wa Mungu. Mafungu ya maneno kama  BWANA
akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu  duniani akahuzunika
moyo (Mwa. 6:6), hufunua hisia ya Mungu, mwenye ufahamu
kuliko kuwa kishindo cha roho  ya kuwazika katika hewa. Hapa
tunasaidiwa tukubali  jinsi  kwa kweli tunaweza pande zote mbili
kumpendeza na kutokumpendeza,  Kama mtoto anavyoweza  kwa
baba wa mwili.

18

IKIWA MUNGU SI MTU MMOJA
Kama  Mungu si wa kweli, mmoja mwenye kuwepo, Basi
wazo la kupenda  mambo ya roho ni vigumu  kushikana nayo.
ikiwa Mungu ni mwenye haki kabisa  lakini si mtu mwenye umbo,
basi kwa kweli hatuwezi kuiwazia  haki yake ilivyodhihirika kwa
watu. Pande zote mbili, Ukristo uliokenguka na wayahudi  wana
wazo la kwamba haki ya Mungu  inaingia katika maisha ya watu
kwa njia ya
‘Roho Mtakatifu’  Asiyedhahiri  ambaye kwa namna
isiyoeleweka tunafanywa  mfano kwenye akili ya  Mungu, na
kukubalika kwake. Kwa maneno mengine, mara tukitambua ya kwa
mba yupo  mtu mwenyewe aitwaye Mungu, basi tunaweza
kurekebisha tabia  yetu kufuata atakavyo, Kwa msaada wake
utokao  kwenye ushawishi wa neno lake  na kwa kuleta  sifa
inayoonyesha tabia ya  Mungu katika utu wetu.

Lengo la Mungu ni kujidhihirisha mwenyewe  katika mkutano
wa watu waliotukuzwa. Jina la kumbukumbu yake, YEHOVA
ELOI, linamaanisha hivi ( Atakaye kuwa kwa wenye nguvu ni
tafsiri  iliyo karibu sahihi.)  ikiwa Mungu si mtu mwenye umbo,
basi thawabu ya waaminifu  katika ufalme wa Mungu  ujao duniani
inaonyesha ya kwamba  watakuwa nayo wazi tena dhahiri
wakiwepo  katika mwili, Ingawa hawatakuwa katika udhaifu  wa
mwili wa Mwanadamu tena. Ayubu alitamani' Siku ya mwisho’
atakapofunguliwa na mwili wake ( Ayubu 19:25:27); Abrahamu
itabidi awe mmojawapo  wa wale wengi wa hao  walalao katika
mavumbi ya nchi ambao wataamka…… Kwa uzima wa Milele wa
nchi ya Kanani (Dan. 12:2) hivyo basi  ataweza kupata ahadi ya
urithi wa milele  wa nchi ya kanaani, Sehemu inayoonekana katika
dunia hii
(Mwa. 17:8.)  “ Na wataua wake watashangilia….. waimbe
kwa sauti  kuu  vitandani mwao….. ili  kufanya kisasi juu ya
   19

mataifa  (Zab 132: 16; 149: 5,7) Kushindwa kwa watu wote wa
pande mbili, Wayahudi na watu wa mataifa,

Kutambua mafungu ya maneno kama haya  vyema, kwa
ukubwa wa maneno  yenyewe Kuletwa ahadi za kuonekana kwa
Abrahamu, kumeongoza watu kwenye imani potovu la' Nafsi haifi’
ya kwamba Mwanadamu halisi anakuwepo  hai akifa. Wazo hili
halina msaada wa Biblia kabisa. Mungu  hapatikani na mauti, Mtu
mwenye utukufu, analifanya lengo lake, ili kwamba wanaume na
wanawake waweze kuitwa na kuishi katika ufalme wake  ujao
kwenye dunia hii, Kushiriki sifa, zilizoelezwa katika umbo la
mwili.

Waaminifu  wameahidi wa kwamba watarithi mwili wa
Mungu  (2 Pet. 1:4) Ikiwa Mungu si mtu mmoja, basi hii ina maana
tutaishi  milele kwa roho zisizo na mwili. Lakini hili si fundisho la
Biblia. Tutapewa mwili kama ule wa Yesu. (Flp. 3:21), Nasi
tunajua kwamba tutakuwa na  mwili halisi kwenye ufalme  mwili
utakaokuwa na mikono  macho na masikio  (Zek. 13:6, Isa. 11:3 ),
mafunzo ya Mungu  kuwa ni  Mmoja, kwa sababu  hii yanasimulia
Injili ya Ufalme.

Itakuwa  wazi kwamba  hakutaweza kuwa na wazo la kujua
Ibada,  dini au uhusiano  mmoja na Mungu  mpaka itambulike
kuwa Mungu  ni mtu mmoja, na kwamba kwa mwili sisi ni mfano
wake. Ingawa ni mfano usio kamili sana unahitajika kuukuza
kufuata  mfano wa akili yake, Hivyo basi, tutaweza kupata
utimilifu wa mfano wake unaoonekana katika ufalme wa Mungu.
Maana nyingi zaidi  na faraja tunaweza kupata kutoka  mafunzo ya
maneno ambayo yanamtaja Mungu kuwa ni Baba aliye na upendo,
akiturudi kama Baba afanyavyo kwa mwanae (mfano. Kum. 8:5).
Katika maneno yenyewe  ya mateso ya Kristo  tunasoma
20

kwamba,'Lakini BWANA aliriidhika kumchubua’  (Isa. 53:10
),Ingawa  “Alimlilia Mungu” aliisikia sauti yangu…….. Kilio
changu kikaingia masikioni mwake (Zab.18:6). Ahadi ya Mungu
kwa Daudi kuhusu mzao atakaye kuwa ni mwana wa Mungu
ilitakiwa azaliwe kwa Muujiza kwa Mwanadamu; Ikiwa Mungu
hakuwa ni mtu mmoja, asingekuwa na mwana huyo.

Kumfahamu Mungu kwa usahihi ni ufunguo unaofungua
maneno  mengi mengine ya muhimu katika mafundisho ya Biblia.
Lakini kama uongo mmoja  huongoza kwenye uongo mwingine,
Hivyo dhana potovu juu ya mungu inaficha utaratibu  wa kweli
ambao maandiko yanatoa. Kama umepata kuona  kuwa hii sehemu
inadhibitisha, au hata ikiwa ni ndogo, basi, swali linakuja. Je?
Unamjua Mungu kweli?. Sasa  tutachunguza maandiko ya Biblia
zaidi kuhusu  yeye.

1.3 Jina La Mungu Na Tabia Ya Sifa Yake

Ikiwa Mungu yupo, inafaa kufikiri kuwa atakuwa  amevumbua
njia nyingine ya kutuambia habari zinazo mhusu yeye mwenyewe.
Tunaamini ya kwamba Biblia ni ufunuo wa Mungu kumjulisha
Mwanadamu,  na humo ndani ya kitabu tunaona kudhihirika tabia
ya sifa ya Mungu. Hii ndio sababu Neno la Mungu linasemwa
kuwa ni'Mbegu’ yake (1 Petro 1:23) Kwa kuwa kama likigeuza hali
ya mioyo yetu, kiumbe mpya anaumbwa ndani yetu ambaye ana
sifa za Mungu  (Yakobo. 1:18,  2Kor. 5:17). Kwa hiyo sisi
wenyewe tunapotumia  zaidi neno la Mungu na kuchukua masomo
sisi wenyewe, ndivyo zaidi tutafanana  mfano wa mwana wake (
Rum, 8:29) ambaye kwa tabia ya sifa alikuwa mfano kamili  wa
Mungu (Kol. 1:15).Kwa hii imelala thamani ya kusoma sehemu  za
historia ya Biblia, Zimejaa kadhia ya  masomo jinsi Mungu
   21

alivyojishughulisha na watu pamoja na matifa, Daima  akionyesha
msingi ule ule wa sifa.

Katika Kiebrania jina la mtu mara nyingi  lilileta tabia ya sifa
zao  au  taarifa zinazowahusu. Mifano mingine iliyowazi:

• ‘Yesu’'Mwokozi’  Kwa kuwa atawaokoa watu wake kutoka
dhambi zao’ (Math. 1:21)
• ‘Abrahamu’'Baba wa mkutano mkubwa’  Maana
nimekufanya kuwa baba wa mataifa mengi’(Mwa. 17:5)
• ‘Hawa (Eva)'Uhai’ Kwa kuwa alikuwa mama wa wenye
uhai wote (Mwa. 3:20)
• ‘Simeoni’'Kusikia’ Kwa kuwa bwana amesikia kwamba
nalichukiwa, kwa sababu amenipa mwana  huyu (Mwa. 29: 33).
Katika Yeremia 48:17, kuwajua watu wa Moabu ni sawa sawa
na kufahamu jina la moabu.Mara nyingi zaburi  zinamlinganisha
Mungu mwenyewe na jina lake, neno lake na matendo (Zab. 103:1,
105:1, 106:1,2,12,13.) Kwa sababu hii itegemewe kwamba majina
ya Mungu  na heshima vitatupatia  habari nyingi kuhusu yeye
mwenyewe, kwa kuwa  yapo maelekeo mengi  ya tabia ya sifa  na
kusudi  kwa kweli  ana jina zaidi ya moja.Somo lenye kueleza
jambo moja moja  la jina Mungu  linafaa baada ya Ubatizo;
kufahamu zaidi sifa na tabia ya Mungu  kumeelezwa katika jina
lake, ni jambo lingine ambalo  liendelee wakati wa maisha yetu
yote katika Bwana. Linalofuata sana kwa hilo, mengi ni Utangulizi.

Musa alipotaka aelimishwe kwa undani  kuhusu  Mungu ili
imani yake  iimalike wakati wa kipindi kisicho sahaulika sana  cha
maisha yake. Malaika,'Alitangaza
jina
la BWANA:
BWANA,BWANA Mungu, Mwingi wa huruma, Mwenye fadhili,
Si mwepesi wa hasira, Mwingi wa rehema na kweli, Mwenye
kuwaonea huruma watu elfu elfu, Mwenye kusamehe uovu na
22

makosa na dhambi; Wala si mwenye kumhesabia mtu  mwovu
kuwa hana hatia,’ (Kut. 34:5-7)

Huu ni ushahidi ulio  wazi wa kwamba  majina ya Mungu
yanaweka sifa zake.Tendo la kuwa nazo ni uhakika  kuwa ni mtu
mmoja, si busara  kufikiri ya kwamba  fungu la roho laweza kuwa
na dalili na sifa ya tabia  hizi  ambazo vile vile  zaweza
kuendelezwa  ndani yetu wanadamu.

Mungu amechagua hasa jina moja  ambalo amependa ajulikane
na kukumbukwa na watu wake, ni kwa  ufupi, maelezo mafupi, ya
kusudi lake kwa watu.

Israeli walikuwa watumwa Misri, Walihitajika kukumbushwa
lengo  la Mungu kwao. Musa aliambiwa awaambie  Jina la Mungu,
ili kwamba  hili liwasaidie  kuwaletea kusudi la kuondoka Misri na
kuanza safari kuelekea nchi ya Ahadi (1Kor. 10:1) Nasi pia
tunahitajika  kuelewa mambo ya msingi yahusuyo jina la Mungu
kabla ya kubatizwa na kuanza  safari yetu ya kuelekea Ufalme wa
Mungu. Mungu aliwaambia  Israeli  kuwa Jina lake alikuwa
YAHWEH-YAHU (Zab 89:8 uv); Maana yake“Mimi niko ambaye
NIKO” au limetafsiriwa kwa usahihi zaidi,'Nitakuwa ambaye
Nitakuwa’(Kut 3:13-15) Jina hili, kidogo likapanuka wakati ule:”
Tena  Mungu akamwambia  ( Ikiwa ni nyongeza) Musa, Hivi
ndivyo utawaambia wana wa Israel, BWANA (Yahweh) Mungu
wa Babu zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, Mungu wa
Yakobo, ….Hili ni Jina  langu Milele, la kumbukumbu yangu kwa
vizazi vyote. (Kut. 3:15). Kwa sababu hiyo jina kamili la Mungu ni
“BWANA Mungu”
Zaidi Agano la kale liliandikwa kwa Kiebrania  na tafsiri ya
Kiswahili ni lazima kutukia visivyo sawa sawa  wakati ujapo wa
kutafsiri maneno ya Kiebrania  hasa neno “Mungu”  mengi ya
   23

maelezo moja moja  yakosekana  - Tafsiri yetu ya Kiswahili
imetoka kwenye  Kiingereza. Moja ya maneno yanayotumiwa  na
Kiebrania  limetafsiriwa'Mungu’ ni Elohim (ELOI) maana
yake'Wenye Nguvu’ Kumbukumbu ya jina la Mungu, jina ambalo
anatutaka  tumkumbuke, kwa sababu hiyo.

YAHWEH  ELOHIM  -  YAHU  ELOI
 Maana yake
ATAKAYEDHIHIRIKA KATIKA KUNDI LA WENYE
NGUVU.

Kwa hiyo ni kusudi la Mungu kuidhihirisha tabia ya sifa yake,
Umuhimu wake katika kundi kubwa  la watu. Kwa kulitii neno lake
tunaweza  kukuza sifa zingine za Mungu  ndani yetu wenyewe
sasa, hivyo basi kadri ya busara  sana. Mungu alijifunua
mwenyewe  kwa waamini wa kweli katika maisha haya.lakini jina
lake Mungu ni la Unabii wa wakati ujao  hapo dunia itakapo jaa
watu  watakao kuwa sawa naye, pande mbili kwa tabia na mwili
(2Petr 1:4). Ikiwa tunataka kuungana na lengo la shabaha  ya
Mungu na kuwa kama Mungu bila hata kufa tena, kuishi milele
katika uadilifu  wote uliokamilika, basi yatupasa  sisi wenyewe
tujiunge na jina lake.

Namna ya kufanya hivi ni kubatizwa katika jina, yaani la
Yahweh Elohim (Math. 28:19). Hili linatufanya tuwe watoto
(‘Uzao’) wa Abrahamu (Gal,. 3:27-29) uliohaidiwa kurithi milele
nchi (Mwa. 17:8; Rum. 4:13) Kundi la wenye nguvu  (Elohim Eloi)

ambao unabii wa jina la Mungu  utatimilika. Limeelezwa
zaidi kwa habari katika  somo la  3.4. 
24

1.4  Malaika
Yote ambayo  tumeyapima sana katika somo hili yanaletwa
pamoja kwenye tafakari ya Malaika:

• Viumbe walio na mwili
• Huchukua jina la Mungu
• Wao ni njia ambayo roho wa Mungu  anatenda kazi ya
kutimiza mapenzi yake
• Wanapatana tabia na kusudi lake
• Na kwa hiyo wanamdhihirisha yeye.

Tumetaja kwenye somo la 1.3  ya kwamba moja kati ya
maneno  yanayotumika zaidi katika  Kiebrania lililotafsiriwa
“Mungu” ni' Eloi’ ambalo hasa maana yake ' Wenye nguvu’
hawa,'Wenye nguvu’  ambao huchukua jina la Mungu
wanapotokea wana weza  kuitwa 'Mungu’  kwakushirikiana kwao
pamoja na naye karibu. Hawa viumbe wanaitwa Malaika.

Taarifa ya uumbaji wa ulimwengu katika mwanzo  1
inatuambia ya kwamba Mungu  alitamka amri halisi kuhusu
Uumbaji'Ikiwa hivyo’ walikuwa ni Malaika waliotimiza amri hizo:

“Enyi Malaika zake, mliohodari mtendao neno lake,
mkiisikiliza sauti ya neno lake (Zab. 103:20).

Kwa sababu hii  busara husadiki kuwa tunaposoma 'Mungu’
akiumba ulimwengu, kazi hii kweli ilifanywa na Malaika. (Ayubu
38:4-7) anadokeza vile vile namna hii. Sasa ni wakati mzuri
kuelezea kwa kifupi  matukio ya uumbaji kama yalivyoandikwa
Mwanzo 1:

   25

Siku ya Kwanza‘   Mungu  akasema, Na iwe nuru, Ikawa’
(Mstari  3)

Siku ya Pili
'Mungu  akasema, Na iwe anga katikati ya
maji, likayatenga  maji na maji.Mungu akalifanya anga ,akayatenga
yale maji   yaliyo juu ya anga na yale yaliyo chini ya anga: Ikawa
hivyo’  (Mstari 6,7)

Siku ya Tatu ‘Mungu  akasema, Maji yaliyo chini ya
mbingu na yakusanyike  mahali pamoja, (akifanya Bahari na
Bahari kuu)  ili pakavu paonekane; Ikawa hivyo’ (Mstari wa 9)

Siku ya Nne   ‘Mungu akasema, Na iwe  mianga katika
anga la mbingu… Ikawa hivyo’ (Mstari 14:15)

Siku ya Tano ‘Mungu akasema,  Maji na yajae kwawingi
na kitu kiendacho chenye uhai …. ndege waruke juu ya nchi …..
Mungu akaumba kila kiumbe  chenye uhai (Mstari wa 20:21),
Ikawa hivyo.

Siku ya Sita ‘Mungu akasema, Nchi na izae kiumbe
haikwa jinsi  zake…. Mnyama wa kufugwa,nacho kitaambaacho
…. Ikawa hivyo (Mstari 24)

Siku hiyo hiyo ya sita mtu aliumbwa. Mungu akasema, na
tufanye  mtu  kwa mfano wetu, na kwa sura yetu  (Mwa 1:26).
Tuliwahi kutoa maelezo  juu ya mstari  huu katika somo la 1.2.
Kwa muda uliopo, tunataka kujua hapa ya kwamba.'Mungu’ sio tu
anatajwa Mungumwenyewe katika utu'Na tufanye mtu’ inaonyesha
kuwa Mungu anatajwa  mtu zaidi ya mmojaNeno  la Kiebrania
linalotafsiriwa hapa'Mungu’ ni Elohim (Eloi), Maana yake'Wenye
nguvu’ Ukiwa ni ushahidi unaotaja Malaika. Ukweli ni kwamba
26

Malaika  walituumba sisi kwa mfano wao  maana yake ni kuwa
wana sura ya mwili ule ule kama tulio nao. Kwa sababu hiyo ni wa
kweli, wa kugusika, viumbe wenye mwili, wakishiriki mwili ule
ule kama wa Mungu.

‘Mwili’ Kwa maana  hii unatajwa kwa msingi jinsi mtu
mwingine alivyo kwa sababu ya muundo wa mwili wao. Katika
Biblia ipo “Miili” ya  aina mbili  katika  maana halisi ya neno
haiwezekani kwa wakati huo huo kuwa miili hii ya aina mbili.


 Mwili wa Mungu (‘Mwili wa Uungu’)
 Hauwezi kutenda dhambi (Mkamilifu)  Rum 9:14,6:23;
Zab. 90:2, Math 5:48,Yak 1:13)Haupatikani na Mauti ( 1Timotheo
6:16)
 Una nguvu tele na uweza ( Isaya 40:28)

Huu  ndio mwili wa Mungu na Malaika na ambao alipewa
Yesu  baada ya kufufuliwa (Matendo 13:34; Ufunuo  1:18; Ebr.
1:3) Huu ndio mwili  ambao  tumeahaidiwa kupewa  (Luka
20:35,36; Isa. 40:28,31)

 Mwili wa mwanadamu
Hujaribiwa na kutenda dhambi ( Yak 1:13-15 )kwa nia mbaya
ya asili (Yer 17:9; Marko 7:21-23) Huangamia mautini, Yaani
unapatwa na kifo ( Rum. 5:12,17; 1Kor  15:22)  Una kikomo cha
nguvu, sehemu mbili,  kwa mwili (Isa. 40:30) na kwa akili ( Yer
10:23)

Huu ni mwili ambao watu wote, wema na wabaya, kwa sasa
wanao mwisho  wa mwili huo ni kifo (Rum 6:23). Ulikuwa ni
mwili ambao  Yesu alikuwa nao  wakati wa maisha yake  ya  mwili
   27

unaokufa  hapa duniani (Ebr. 2:14-18,Rum. 8:3 Yoh 2:25, Marko
10:18)

MATENDO YA KUONEKANA  NA  MALAIKA
Malaika wakiwa na mwili wa Uungu, inabidi wawe hawana
dhambi na kwa sababu hiyo hawawezi kufa  kwa kuona kwamba
dhambi  huleta mauti (Rum. 6:23). Inapasa wawe na umbo halisi na
mwili wa kuwepo mauti  “Na yaletwe basi maji kidogo  ukanawe
miguu, mkapumzike chini ya mti huu”(Mwanzo 18:4)

Wawili kati ya hao Malaika wakati ule  walikwenda kwa lutu
katika mji wa Sodoma. Tena, walitambuliwa kuwa ni watu  na lutu
pamoja na watu wa  Sodoma.'Basi,  wale malaika Wawili wakaja
Sodomaa jioni aliowakaribisha wakae kwake usiku. Lakini watu
wa Sodoma wakaja kwenye nyumba yake, wakiuliza kwa namna ya
kutisha,'Wawapi wale watu waliokuja  kwako usiku huu ?’ Lutu
akawasihi,' Watu hawa msiwatende neno’  Taarifa ya maandiko ya
Mungu  pia inawaita ni'Watu’, Wale watu ( Malaika )
wakanyoosha mikono yao, wakamwokoa Lutu,  Basi wale  watu
wakamwambia Lutu … BWANA ametutuma tuuharibu  Sodoma
(Mwanzo 19: 1,5,8,10,12,13).

Ufafanuzi wa  Agano jipya  juu ya matukio haya
yanadhibitisha kwamba Malaika wanafanana na umbile la watu.
“Msisahau kuwafadhili wageni; Maana kwa njia hii wengine (Kwa
mfano Lutu na Abrahamu ) waliwakaribisha Malaika pasipo kujua
(Ebr 13:2)

Yakobo alishindana usiku kucha na mtu mmoja ( Mwa 32:24)
ambaye baadae tumeambiwa kuwa  alikuwa Malaika (Hosea 12:4)

28

Watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe
walikuwepo kwenye  ufufuo (Luka 24:4) na wakati wa kupaa (Mat.
1:10) Yesu, kwa  uhakika hawa walikuwa ni Malaika. Ona
vidokezo vya'Kipimo cha Kibinadamu, maana yake cha Malaika’
(Uf 21:17).

MALAIKA   HAWATENDI    DHAMBI
Malaika wakiwa na mwili wa Uungu, hawawezi  kufa, kwa
sababu dhambi huleta mauti, Basi wao hawawezi  kutenda dhambi.
Maneno ya asili katika lugha ya Kiyunani na Kiebrania
yaliyotafsiriwa'Malaika’  maana yake ni mjumbe;  Malaika ni
wajumbe au watumishi wa Mungu, Watiifu kwake, Kwa hiyo
hawafikiriwi wao kuwa ni wenye dhambi. Kwa hivyo neno la
Kiyunani’Agelos’
lililotafsiriwa'Malaika’

vile vile
limetafsiriwa'Wajumbe’ Wanaposemwa wanadamu kwa mfano
Yohana mbatizaji, (Math 11:10) na  wajumbe wake (Luk. 7:25)
wajumbe wa Yesu (Luk. 9:52) na watu walioupeleleza mji wa
Yeriko (Yak. 2:25). Kwa kweli  inawezekana kwamba'Malaika’
katika maana ya wajumbe  wanadamu wanaweza kutenda dhambi.

Mafungu ya maneno yafuatayo ni wazi kwamba  Malaika wote
( Sio tu baadhi yao) kwa umbile ni watiifu kwa Mungu, na hivyo
hawawezi kutenda dhambi.

‘BWANA  ameweka kiti chake cha Enzi mbinguni Na Ufalme
wake unavitawala vitu  vyote (Yaani  haiwezekani kuwepo uasi juu
ya Mungu mbinguni)Mhimidini BWANA, Enyi  Malaika zake,
Ninyi mlio hodari, mtendao neno lake, Mkisikiliza sauti ya  neno
lake Mhimidini BWANA, enyi majeshi yake Yote;  Ninyi
watumishi wake  mfanyao mapenzi yake (Zab. 103:19-21)

   29

“Msifuni, enyi Malaika wake wote …. Majeshi yake yote (
Zab 148: 2 )  Je ! hao wote si roho (Malaika ) watumikao,
wakitumwa kuwahudumia wale watakaourithi wokovu ? ( Ebra. 1:
13,14 )

Kurudiwa kwa neno'Wote’ linaonyesha ya kwamba Malaika
hawajagawanyika katika makundi mawili, kundi moja zuri na
jingine lenye dhambi. umuhimu wa kufahamu vema  umbile la
malaika ni kwamba  thawabu ya waaminifu ni kushiriki mwili wao.
“Wale  wahesabiwao kuwa wamestahili…. Hawaoi  wala
hawaolewi … wala hawawezi kufa tena. kwa sababu huwa sawa
sawa na Malaika (Luk 20:35, 36).

Hili ni neno la muhimu  kulishika. Malaika hawawezi
kufa'Maana hatwai asili ya Malaika (Kwa kuwa tangu asili
hawajatenda dhambi). Ila atwaa asili ya mzao wa Abrahamu ,sababu

ya dhambi’ (Ebr 2:16) Ikiwa Malaika waweza kufanya
dhambi, Basi wale ambao  watakuwa wamestahili thawabu  ya
Kristo atakapo kuja bado  wataweza kutenda dhambi pia, Na kwa
kuwa dhambi huleta mauti  (Rum 6:23)  kwa sababu hiyo
hawataweza kuwa na uzima wa milele, kama tukiwa na uwezekano
wa kutenda dhambi  ni kufanya ahadi ya Mungu  ya uzima wa
milele  haina maana, kwa kufahamu kuwa thawabu yetu ni
kushiriki  mwili ule wa Malaika.  Ushuhuda wa'Malaika (Luk.
20:35,36) unaonyesha kwamba hakuna aina ya Malaika wema na
wenye dhambi; ipo aina moja ya Malaika tu.

Ikiwa  Malaika waweza kutenda dhambi, Basi Mungu
ameachwa  hana  nguvu  za kutenda  tendo la haki  katika maisha
yetu  na mambo ya ulimwengu, kwa kufahamu kuwa ameeleza
kwamba anafanya matendo yake kwa njia ya Malaika zake( Zab
103:19-21) Wamefanywa kwa'Roho wa Mungu  katika  maana  ya
30

kwamba anatimiza  yote kwa nguvu zake. Akitenda kazi katika
Malaika  (Zab 104:4). Kwamba wanamwasi Mungu  haiwezekani.
Mkristo amwombe  kila siku, Mungu ili ufalme  uje duniani, ili
mapenzi yake yafanyike  kama sasa yanavyofanyika mbinguni
(Math 6:10) Ikiwa Malaika wa Mungu iliwapasa washindane na
Malaika wenye dhambi  huko mbinguni, basi,  kwa utimilifu
mapenzi yake  hayakuweza kufanyika huko,  na kwa sababu hiyo
hali hiyo hiyo itapatikana kwenye ufalme wa Mungu  ujao.
Kutumia maisha ya milele kwenye ulimwengu  ambao utakuwa ni
uwanja wa vita  kati ya dhambi na utii, kwa shida hayo sio
matazamio  ya kutia moyo, lakini hilo, kwa kweli, sio ndiyo suala
lenyewe.

MALAIKA  NA  WATU  WANAOAMINI
Ipo sababu nzuri ya kuamini kuwa kila mwamini wa kweli ana
Malaika pengine mmoja maalumu-wa kuwasaidia katika maisha
yao:-

 ‘Malaika wa BWANA hufanya kituo, akiwazungukia na
kuwaokoa  wamchao’  (Zab 34:7)
Mmojawapo wa wadogo hawa  waniaminio  (Yaani wafuasi
dhaifu- Zek, 13:7  Mat 26:31)…Malaika wao mbinguni siku zote
huutazama uso wa  Baba yangu’ (Mat.
18:6,10)
 Wakristo wa kwanza ni wazi waliamini kwamba Petro
alikuwa na  Malaika mlinzi  (Matendo 12:14,15).
Watu  wa Israeli  walipita katika bahari ya Shamu,
waliongozwa na malaika  kwenye jangwa  kuelekea nchi ya Ahadi.
Kutembea kupitia katika bahari ya shamu maana yake ni Ubatizo
wetu katika maji  (1Kor 10:1), Hivyo nasi  vile vile  ina maana
tusadiki  kuwa baadae tunaongozwa  na kusaidiwa na Malaika
   31

tunaposafiri katika jangwa la maisha  kuel;ekea nchi ya ufalme wa
Mungu.
Ikiwa  Malaika wana weza kuwa waovu  katika maana ya
kuwa wenye dhambi, basi Ahadi hizi za Malaika kuongoza  na
kushawishi katika maisha  yetu zinakuwa laana badala ya Baraka.

• Basi tufahamu ya kuwa Malaika ni Viumbe………
• Wenye  mwili ulio sawa na Mungu na huonekana kwa mwili
• Ambao  hawawezi kutenda dhambi
• Daima hufuata amri za Mungu
• Wao ni njia ambayo Mungu katika Roho  nguvu hunena na
• kutenda kazi (Zab. 104:4)

 LAKINI..?
Makanisa mengi ya'Kikiristo’ yana wazo la kwamba  Malaika
wanaweza kutenda dhambi, na kwamba Malaika wenye dhambi
sasa hivi wapo na  wao  wanahusika na dhambi pamoja na matatizo
yaliyopo hapa Duniani. Tutajadili zaidi vya kutosha juu ya
kutofahamu vema jambo hili  kwenye somo la  6. Kwa sasa
tutatengeneza vipengele vifuatavyo:-

Inawezekana kwamba uumbaji ulikuwepo  uliotutangulia sisi
wa kweli,  yaani huo ulioandikwa katika  Mwanzo 1. Pia inaweza
kusadikika ya kwamba  Malaika waliopo walikuja kuwa na
fahamu  za'Wema na Ubaya’ (Mwa. 3:5) walipo kuwa katika hali
kama hii  tuliyonayo katika maisha haya.

Ya kwamba  viumbe wengine walioishi kwa kipindi kile
walitenda dhambi hatujakatazwa kufikiri;  lakini yote haya ni
mawazo  ambayo mioyo ya watu  hupenda kujishughulisha. Biblia
yatuambia kile ambacho tunakihitaji  kujua kuhusiana na hali
iliyopo,  ambayo ni kwamba hawapo Malaika  watenda dhambi,
Malaika wote ni watiifu kwa Mungu kabisa.
32

Hawawezi kuwepo viumbe wenye dhambi mbinguni, kwa
kufahamu kuwa Mungu'ana macho safi na hawezi  kuangalia
uovu’ (Ab. 1:3) katika maelezo haya,  Zaburi 5:4,5  yatuambia:-

‘Mtu mwovu  hatakaa kwako.  wajivunao hawatasimama
mbele za macho yako’ yaani makao ya mbinguni. Jambo la
kwamba ulikuwepo  Uasi juu ya Mungu mbinguni na Malaika
watenda dhambi  ni wazo linalopingana kabisa  na maneno
yaliyotolewa.
       
 Neno
la kiyunani
lililotafsiriwa'Malaika’ maana
yake'Mjumbe’
linataja
wanadamu,
kama
tulivyoonyeshwa'Wajumbe’  wanadamu hawa wanaweza  kwa
kweli kufanya dhambi.

Ya kwamba upo uovu, viumbe wenye dhambi ambao juu yao
mwelekeo wa maisha yote yasiyofaa  wanaweza kutupiwa lawama
kwa kawaida ni moja ya  Imani zaidi iliyoshikiliwa  katika
Upagani.Kwa njia hiyo hiyo mambo yanayohusu Krismas
yameingia kwenye  kile kinachodhaniwa ni'Ukristo’ Basi, vile vile
Ukristo una fikra hizo za Kipagani

Yapo mafungu ya maneno  ya Bibilia yaliyojaa tele ambayo
yanaweza kutoeleweka kusaidia wazo hili la Malaika wenye
dhambi kwa sasa wapo. Haya yamepimwa katika 'Kumsaka
Shetani’  yanapatikana kwa  wachapishaji - Mafungu haya ya
maneno  hayawezi kuruhusiwa kupingana na mafunzo tele ya
Biblia  kwa kutofautiana na haya yaliyokwisha tolewa.


   33

Tumeacha  Kitambo sehemu ya 1:'Mungu ni roho’
(Yohana 4:24)

Katika somo la pili  tunafafanua  kwa  utaratibu zaidi  jinsi
Roho wa Mungu  alivyo. Tunaweza kutoa maelezo kwa ufupi
sababu zilizoonyeshwa  hapo kwa kusema kwamba  roho wa /ya
Mungu ni nguvu au pumzi yake ambayo kwa hiyo nafsi yake
mwenyewe,  Utu wake na tabia,  vimedhihirika kwa mwanadamu
kwa njia ya matendo yake ambavyo Roho huyo
anatimiza.Hivyo'Mungu ni Roho’ kama katika Yohana 4:24
atafsiriwe vema kwa kuwa Roho yake  ndiyo inafanya utu wake.

Mungu amesemwa kuwa yumo katika vitu vingi, kwa mfano:-

 ‘Mungu wetu ni moto ulao’   (Ebr. 12:29)
 ‘Mungu ni Nuru’

   (1 Yoh. 1:5)
 ‘Mungu ni Pendo

   (1 Yoh.4:8)
 ‘Neno (Kiyunani'Lagos’ - Mpango, Lengo,Kusudi, wazo)
  alikuwa Mungu’  (Yoh 1:1)

Hivyo,'Mungu’ ni sifa yake.  Ni kosa lililo wazi kuleta  sababu
za kupinga kwamba  sifa za upendo wa Mungu ni za kuwazika,
kwa kuwa tunasoma  kwamba 'Mungu ni pendo’  tunaweza
kumwita mtu mwingine  Mwema  wenyewe; lakini hii haina maana
kwamba  haupo bila mwili ni namna ya kuwepo yeye ndiko
kunatudhihirishia wema kwetu.

Roho ikiwa ni nguvu ya Mungu, mara nyingi tunasoma Mungu
akiituma au akiiongoza roho yake  kutimiliza mabo yake kwa
kupatana na mapenzi yake  na tabia ya sifa yake. Hata ameelezewa
kuwa anaumba roho  (Yaani Upepo UV). Kusema kwamba  Mungu
34

na roho yake katika maana safi iliyo halisi ni msemo ule ule kwa
namna nyingine - katika maana inakuwa  Uwepo wa Mungu.

Mifano ya  Mungu  akiiongoza Roho yake ni mingi,
inaonyesha mtengano wa Mungu na Roho yake:-

 ‘Yeye (Mungu)  aliyetia kati yao Roho yake mtakatifu’(Is. 63:11)
 ‘Nitatia Roho yangu  (Mungu)  juu yake  (Yesu )’ ( Math.12:18)
 ‘Baba huwapa  Roho mtakatifu’     (Luk. 11:13)
 ‘Roho akishuka kama  hua  toka Mbinguni’ (Yoh. 1:32)
 ‘Nitawamwagia watu wote Roho yangu’   (Matendo. 2:17).

Kwa kweli ushahidi  juu ya 'Roho wa Mungu’ ni uhakika wa
kutosha  kuwa Roho sio Mungu mwenyewe. Tofauti hizi kati ya
Mungu na Roho ni shida nyingine  ilio kwa wale wanao amini
kuwa Mungu ana  Nafsi'Tatu’ ambazo Mungu amelingana na Yesu
na Roho Mtakatifu. Jambo hili kama lingekuwa la  kweli, na kama
Mungu amedhaniwa kuwa sio mtu, basi halikadharika hata Yesu
naye sio mtu halisi.

Kwa umuhimu sana, Mungu asiye mtu hata sala  kuelekea
kwake inakuwa haina maana, kwenye alama  ambayo sala ni
mazungumuzo kati ya fahamu  zetu  na wazo la Mungu ambalo lipo
katika akili  zetu. Daima tunakumbushwa kwamba  tunamwomba
Mungu ambaye ana Umbo makao yake  yapo  Mbinguni (Mhu. 5:2;
Math. 6:9,5:16, 1Fal. 8:30) na kwamba Yesu sasa yuko  mkono wa
kuume huko ili kutoa maombi yetu mbele zake  (1Pet. 3:21, Ebr.
9:24).

Ikiwa Mungu si mtu binafsi, maneno haya yametolewa  bila
kuwa na maana. Bali, Mungu akieleweka kuwa ni wa kweli, Baba
mwenye upendo, Sala ya kumwomba inakuwa ya kweli, Jambo
   35

lililowazi na dhahiri - hasa  tukizungumza na mtu mwingine
ambaye tunamwamini ana mapenzi sana na anaweza kujibu.

Tumeacha  Kitambo sehemu ya 2:'Matumizi ya jina la
Mungu’

Tumefahamu kwamba Jina la Mungu na hilo la mwanae Yesu
yana maana  ya kina sana. Tunaposema 'Mungu’ tunagusa juu ya
kila mwelekeo  wa kusudi lake la Ajabu la upendo na kweli. Ya
kwamba Jina la Mungu  litumike bure kama upole  usio na maana
au kwa maelezo ya kukasirisha, ni moja ya mambo ambayo mtu
hufanya na kumnena  vibaya zaidi Muumba wake.  Kwa sababu hii
kila mtu anayetaka  kumpendeza Mungu na kumheshimu atafanya
kila jitihada  kutotumia vibaya Jina la Mungu  kirahisi- rahisi.
Katika jamii  ulimwenguni pote kufuru  hii  imekuwa sehemu ya
kawaida kwa Lugha za siku hizi;  Kukatisha ile iliyokuwa ni tabia
ya mazoea haita kuwa kazi rahisi. Sala ya kweli ya kuomba msaada
wa Mungu  hakika itasikika. Wale ambao  wapo ndani ya shughuli
yetu  ya kuwaongoza na kuwavuta,  Mf. Watoto,  pia
watakumbushwa
 hatari ya kukufuru:”Maana BWANA
hatamhesabia kuwa hana hatia alitajaye jina lake bure (Kum. 5:11)

Kwa upande mwingine  wapo wale wanaosisitiza kwamba
tusipotumia maneno ya Kiebrania Yahweh  au Yehova (Njia tofauti
ya kutamka  neno lile lile) Tunapozungumuza kuhusu Mungu,
wakati huo tunakuwa tumepotea sana. Miongoni mwao zaidi ya
hawa ni  Chama cha mlinzi, wanasisitiza kuwa  Mkristo asipojiita
mwenyewe ni'Shahidi wa  Yehova’  Basi hana uhusiano na Mungu.

Kwa kufanya hivi, watu hawa  wanatumia jina  takatifu  la
Mungu na  la ajabu kuchochea aina fulani ya mfumo wa Imani wa
36

kuelimisha kiroho, ambapo wanawadharau  watu wengine tu kwa
matamshi au matumizi ya neno moja. Hii sio kusema kuwa ni
vibaya  kutumia Jina la Mungu; Hasa kweli linafaa kutumika
kwenye Sala zetu wenyewe mara tukibatizwa kwa usahihi katika
Jina lake. Ingawa hivyo, Agano Jipya  halitupatii ishara yoyote
kuwa  hili ni lazima au  inatakiwa na Mungu. Aliongoza kuandika
Agano Jipya hivyo basi liliandikwa kwa Kiyunani (Kigriki)
likitumika neno moja la'Mungu’ -‘theos’  likiwa na maana  “Mtu
mkubwa”.

Hakuna tofauti  iliyofanywa  ndani yake  kati ya'Mungu’ na
'Yahweh’ wala haipo amri yoyote dhahiri  inayohusiana kwa
waamini wakiwa ni jumuiya wajiiteje.Petro anamsema mwamini
kuwa ni “ Mkristo” kuliko kumwita ni'Mtu wa Yehova’  au jambo
lingine kama hili (1 Petro 4:16)  kutilia mkazo zaidi  katika
matumizi ya Jina la 'Yehova’  kunapelekea kupunguza thamani ya
kazi  na  Nafsi ya BWANA'Yesu’  kwa njia hii ambayo  wakristo
wengi wa kiinjili wanatia msukumo zaidi kwenye jina  na kazi ya
Yesu huku wakiacha kuangalia  nafsi ya nguvu zaidi iliyo ya
Mungu.

Majina  mengine ambayo jumuia  ya waaminiao ya wakristo
wa kwanza  waliyojiita wenyewe,  hayatii ndani jina la Yehova:-
 
‘Jamii ya Israeli’ (Ef. 2:12)
‘Mkutano mkuu  na kanisa la wazaliwa wa kwanza’ (Ebr. 12:23)
‘Kanisa lake Mungu’ (Matendo 20:28)
‘Kanisa la Mungu aliye hai, Nguzo na Msingi  wa kweli’ (1
Timotheo 3:15)
‘Nyumba  ya Mungu’ ( 1 Timotheo 3:15)

   37

Tunapopita, ujue kuwa waamini
 hawakujiita
wenyewe'Wakristo’. Neno hili maana yake  lilikuwa la kuvunja
heshima, hawa watu wa Kristo walibezwa na maadui zao.

Tumeacha  Kitambo sehemu ya 3: 'Ufunuo wa Mungu’

Kinachufuata sio rahisi  kukishika chote wakati  tunaposoma
kwanza,lakini umuhimu wa jambo  tunalolizungumzia litakuwa
dhahiri kadri masomo yake yanavyosonga mbele. Tunajumuisha
kwenye maana hii ili  uliache somo hili lote  Msingi wa Biblia
ukisha pimwa wenye ufunuo kuhusu Mungu mwenyewe.

Jina la Mungu laweza kuchukuliwa na yeyote  ambaye
amemchagua kujifunua  au kujidhihirisha yeye mwenyewe. Hivyo
watu na Malaika  sawa sawa  na  Yesu huweza kuchukua jina la
Mungu. Hili ni jambo la muhimu ambalo  linatufunulia mengi ya
Biblia. Hata mwana anaweza kuchukua jina la Baba; ana mambo
mamoja na Baba yake,  anaweza kuwa na jina lile lile la kwanza-
lakini si mmoja na kuwa mtu yeye yule kama Baba.  Kwa njia hiyo
hiyo mwakilishi wa kundi  anaweza kusema kwa niaba ya kundi,
anaweza kumpigia mtu wa kwenye shughuli na kusema, Haloo !
hapa ni  wakulima, Si  Bw. Wakulima,  bali anachukua jina lao kwa
kuwa anafanya kazi kwa niaba yao. Basi hiyo hata kwa Yesu
ilikuwa hivyo.

MALAIKA HUCHUKUA JINA LA MUNGU
Tumeambiwa katika Kutoka 23:20,21 ya kwamba  Mungu
aliwaambia watu wa  Israeli kuwa Malaika atawatangulia mbele
yao;'Jina langu limo ndani yake’, waliambiwa. Jina lake Mungu
ni'Yahweh’. Basi,  Malaika huchukua jina la Yahweh,  na hivi
38

anaweza kuitwa Yahweh, au BWANA  kwa herufi kubwa neno
BWANA linatokana na Yahweh, katika Biblia UV ya Kiswahili ni
sehemu moja tu Zaburi  89:8 utakuta neno
YAHU = YAHWEH. Tumeambiwa  kuwa katika  kutoka
33:20 Mtu hataniona uso akaishi;  lakini katika Kutoka  33:11
tunasoma kwamba “BWANA”(Yahweh) alinena na Musa  uso kwa
uso, kama mtu anaposema na rafiki yake - Yaani  kirafiki. Hakuwa
ni BWANA, Yahweh  mwenyewe alikuwepo,  aliyenena na Musa
uso kwa uso,  Kwa kuwa hakuna mtu anayeweza kumwona Mungu
yeye mwenyewe. Alikuwa ni Malaika  aliyechukua jina la Mungu
ndiye aliye fanya hivyo, na tunasoma  habari  za BWANA  akisema
uso kwa uso na Musa  wakati hasa ni Malaika aliyefanya hivyo
(Mdo. 7:30-33).

Ipo mifano mingine mingi ya maneno' Mungu' na BWANA
ikitaja  Malaika  wakiwa Mungu mwenyewe. Mfano mmoja ulio
wazi ni Mwa. 1: 26 “Mungu (Malaika) akisema, na tufanye mtu
kwa mfano wetu”

WATU  NA  JINA  LA  MUNGU
Moja ya maneno  ambayo yanayosaidia  sana katika kuelezea
yote haya  ni katika Yohana 10:34-36. Hapa Wayahudi walifanya
kosa  ambalo wengi wanaoitwa'Wakristo’ wanafanya leo.
Walidhani kuwa Yesu alikuwa anasema kuwa yeye ni Mungu
mwenyewe. Yesu alisahihisha kwa kusema “Haija andikwa katika
sheria yenu,  nimesema Ninyi ni Mungu ? Ikiwa aliwaita Miungu
….. inakuwaje mimi ….” Mnaniambia ninakufuru, kwa sababu
nalisema,  Mimi ni mwana wa Mungu  ? Yesu kwa kweli alikuwa
anasema 'Katika Agano la Kale watu waliitwa Miungu;  mimi
nasema ni mwana wa Mungu, basi imekuwaje mnaudhika  sana?
   39

Yesu kwa kweli alikuwa ananukuu toka  Zab 82 mahali ambapo
waamuzi wa Israeli  waliitwa'Miungu’.

Kama ilivyoonekana, Jina kamili la Mungu katika Kiebrania ni
'Yahweh Elohim’  likiwa na maana, Nitadhihirika katika kundi la
wenye nguvu. Waamini wa kweli ni wale wengi  wenye nguvu
katika maana ndogo ya maisha  haya  nao watakuwa na nguvu tele
kwenye Ufalme. Kwa mlinganisho huu wote umeonyeshwa kwa
Isa. 64:4 na 1 Kor.2:9.

“Watu  hawakusikia,  wala kufahamu kwa masikio, wala jicho
halikumwona Mungu, ila wewe, atendaye mambo kwa ajili yake
amngojaye” Paulo ananukuu mstari huu katika  1 Kor.2:9-10:
Imeandikwa, Jicho halikuyaona, wala sikio halikuyasikia wala
hayakuingia katika moyo wa mwanadamu, mambo ambayo Mungu
amewaandalia wampendao. Lakini  Mungu ametufunulia sisi kwa
Roho. Fungu la maneno katika Isa. 64:4  linasema hakuna hata
mmoja isipokuwa  Mungu anaweza kufahamu mambo
aliyowaandalia waamini; Lakini 1Kor. 2:10 mstari unasema
kwamba  mambo hayo yamefunuliwa kwetu, hivyo katika maana
sisi ni  “Mungu”: sio Mungu mwenyewe katika utu, bali ufunuo wa
Mungu kwa matokeo kuwa tumebatizwa katika jina lake na kujua
Ukweli.

YESU  NA  JINA  LA  MUNGU
Sio jambo la kushangaza kwamba Yesu,  Ikiwa ni mwana wa
Mungu na ufunuo wake mkuu kwa watu, Pia naye atachukua jina la
Mungu. Aliweza kusema “Nimekuja katika jina la Baba yangu”
(Yoh.5:43). Kwa utii  wake, Yesu alipaa kwenda mbinguni, naye
Mungu akampa jina lipitalo majina - Jina la Yahweh, la Mungu
mwenyewe
40

(Fil. 2:9).basi hii ndiyo sababu tunasoma  Yesu anasema katika
Uf 3:12  “Nami nitaandika juu yake  (Mwamini) Jina la Mungu
wangu……na jina langu mwenyewe, lile jpya”Kumbuka Yesu
alitoa kitabu cha Ufunuo miaka mingi baada ya kupaa  kwenda
mbinguni na akiisha kupewa jina la Mungu,  kama ilivyoelezwa
katika  Wafilipi 2:9.

Hivyo anaweza kuliita jina la Mungu “Jina langu Jipya”; Jina
ambalo hivi karibuni alipewa. Sasa tunaweza kuelewa vema  Isaya
9:6,  mahali ambapo kuhusu yeye tumeambiwa “Jina  lake (Ujue
kuwa) utaitwa, Mshauri wa Ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba
wa milele, ….” Huu ni Unabii wa kwamba Yesu  atachukua majina
yote ya Mungu ya kwamba atakuwa ni ufunuo  wote wa Mungu
kwetu.Na ndivyo kwa maana hii aliitwa  “Emmanueli” maana yake
'Mungu  ni pamoja nasi’ ingawa yeye hakuwa Mungu.

Somo  La Kwanza :  Maswali

1.Ni nini  kitakachotusaidia zaidi  kuamini Mungu ?
a)  Kwenda  Kanisani
b)  Maombi na Kusoma  Biblia
c)  Kuzungumuza na  Wakristo
d)  Kutazama maumbile.

2.  Yapi ya haya yafuatayo ni ufafanuzi  sahihi  zaidi wa
Mungu ?
a)  Ni wazo tu katika mioyo yetu
b)  Kipande cha Roho katika Hewa
c)  Mungu Hayupo
d)  Mtu halisi wa Umbo

   41

3.  Je ? Mungu ni
a)  Ummoja
b)  Utatu
c)  Miungu wengi katika mmoja
d)   Haiwezekani kufafanua kwa njia ya  yoyote

4.  Jina la Mungu' Yahweh  Elohim’  lina maana gani ?
a)  Yeye atakaye  kuwa
b)  Atakayedhihirika katika kundi la wenye nguvu
c)  Mkuu
d)  Nguvu

5.  neno'Malaika lina maana gani ?
a)  Kama mtu
b)  Aliyefunikwa na Mabawa
c)   Mjumbe
d)   Msaidizi

6.  Je ?  Malaika  anaweza  kutenda Dhambi ?

7. Ni kitu gani  kinacho kudhihirishia kuwa Mungu  yupo ?
42