Sheria za Mungu za rohoni na mafanikio
Yaliyomo
Utangulizi
1. Je, mkristo anapaswa kufanikiwa?
2. Yesu Krsito- Je, maskini au tajiri?
3. Maagizo ya
Mungu ya mafanikio.
4. Njia ya mungu
ama njia ya ulimwengu?
5. Mungu anataka tupadilishe nia yetu kwa
pesa!
6. Tunawezaje kupadilisha na kuweka upya
mawazo yetu?
7. Tazamo la mungu kwa kazi na nidhamu.
8. Tunafuna tunachopanda.
9. Baraka kwa kulipa fungu la kumi.
10. Hatuwezi tukapeana mpaka ikawa mingi
mbele za Mungu.
11. Kutoa kwa njia ya kiungu.
12. Sheria za Mungu juu ya kupokea.
13. Sheria za Mungu ya kuweka hazina na
rasilimali.
14. Kutumia sheria za Mungu ya mafanikio.
15. Chanzo cha umaskini, umaskini na
mataifa yasiyoendelea, kila maskini.
16. Yale bibilia inasema kuhusu pesa.
17. Pesa huathiri tabia na ubinafsi.
18. Maandiko juu ya pesa.
19. Hatua muhimu katika barabara ya
umaskini kuingia kwa utele.
Utangulizi
Yote yanaanza ndani ya moyo na akili.
Mawazo yako juu ya pesa lazima yabadilike kwanza. Tamaa ya kibinafsi juu ya
pesa ambayo unatumia kwa manufaa yako pekee yako itabadilishwa kuwa kupeana na
furaha kwa watu wengine-kupeana kwa familia, kwa maskini, kwa kueneza neno kwa
njia yeyote ile, fungu la kumi na kupeana kwa nyumba ya Mungu kwa furaha.
Tumia pesa kwa mapendeleo ya Mungu. Wacha
Roho Mtakatifu akuongoze lini na wapi utumie pesa zako. Usiweka hazina katika
mambo yanayoisha bali weka katika mambo ya milele.
Epuka kununua vitu visivyofaa.
Usitumie pesa kwa kujinufaisha wewe peke
yako bali kwa mahitaji.
Tumia pesa kidogo kuliko unachopokea kwa
mshahara wako.
Epuka deni.
Ufanisi inahusu sehemu nyingi ya maisha,
kifedha, kiroho, kimwili, kiakili, kihisia.
1. Je, wakristo wanapaswa kufanikiwa?
Mungu aliumba mali
yote ya ulimwengu. je, aliwaumbia wasioamini, kwa walio na mioyo migumu,
watenda dhambi wa kike na wa kiume wanaomlaani yeye, kumkataa na kupinga sheria
zake? je, anataka kweli wafanikiwe na
watoto wake wakae bila? la sivyo. Mungu
baba yetu anataka kilichobora kwa wana wake, waumini walozaliwa mara ya bili,
wakristo.
Kama baba yetu wa
mbinguni alitupatia mwana wake wa pekee. Tayari ametupatia iliyo bora kabisa na sasa ako tayari kutupatia
hiyo yote nyingine. Warumi.8:32 Yeye asiymwachilia mwana wake mwenyewe,
bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote
pamojanaye?
2. Yesu kristo -maskini
au tajiri?
Yesu alikuwa maskini?
Hapana!-kwa yeye na kwake
vitu vyote vikaumbwa. wakolosai.1:16... vitu vyote vimeumbwa naye kwa
ajili yake.
Anamiliki dunia
yote na angali anamiliki
2.Wakorintho.8.9. hata ingawa alikuwa tajiri, hata akafanywa
maskini ili kupitia kwa umaskini wake
tukafanywa kuwa tajiri.
3. Maelezo ya Mungu kuhusu pesa.
Wengi wetu tumepokea Yesu kama mwokozi
lakini hatujakubali awe Bwana wa kila sehemu ya maisha yetu.
Baba yetu anataka
tusalimishe maisha yetu yote kwake. hataki tuweke familia, pesa raha zetu
au kitu
chochote zaidi yake. Kutoka 20:3. Usiwe na miungu mingine ila mimi.
Sheria ya mungu
ya kufanikiwa itatenda kazi kulingana na jinsi tumemweka wa kwanza katika masha yetu
Mungu hataki
tuangamizwe na tamaa mbaya. ndio sababu anaamrisha apewe nafasi ya kwanza. Kila wakati umweke Mungu wa kwanza. Mathayo 6:33 Tafuteni
kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine mtasidishiwa.
4.Njia ya
Mungu-au njia ya ulimwengu?
Njia ya
ulimwengu- au njia ya Mungu?
Mungu anataka
tutubu na kuweka upya mawazo yetu iweze kufikiri njia za Mungu juu ya
mafanikio.
Wakristo
wanaotaka ufanisi kwa njia ya ulimwengu, mwishowe watamalizia katika
''theologia ya mafanikio.''
Wakristo
wanaotaka mafanikio kwa njia ya kimungu wataheshimu Mungu kwa mali zao.
Ni muhimu sana
tuelewe wazo hili, ya kwamba fedha, na dhahabu katika ulimwengu huu ni ya Mungu, na sisi hatuna chochote chetu, Mungu
ameturuhusu tuzitumie.
Hagai. 2:8 fedha ni yangu na dhahabu ni yngu asema
bwana wa majeshi
Usiseme: mali
yangu ni yangu, nizipata mwenyewe.”kwa sababu mungu anasema katika kumbu la
torati.8:17-18 na unasema katika moyo wako: nguvu yangu na na uwezo wa
mikono yangu imenipatia hii mali. v18: lakini utamkumbuka baba mungu wako, kwa
sababu ni yeye akupaye nguvu ya kutafuta mali. ili atimize ahadi yake kwa
mababu wanu.
Njia ya ulimwengu
ya kupata utajiri ni kwa kutegemea nguvu zangu mwenyewe. njia ya mungu ni
kumtumainia.
Marko.10:24 vile ilvyongumu kwa wanao amini kwa mali
zao kuingia katika.
Neno la muhimu
hapa ni uamini katika mali”badala ya kuamini katika bwana. yule kijana tajiri
alipenda (amini) sana pesa zake kuliko kumpenda(amini) mungu.
Sheria ya mungu
kuhusu mafanikio inatuhitaji tumtumainie yeye badala ya kumtumainia utajiri.
Nji za mungu ziko
kinyume na njia za kiduni. badala ya kuamini katika mali ya kidunia baba yetu
anatsks tumwamini yeye na ktumia kile
tunacho na watu wengine.
Timotheo.
6:17-18 wahukumu wale
walio na mali katika dunia, wasijiwazie kuwa juu na wala wasiamini katika mali
isiyoeleweka, lakini kumwamini mungu aiishiye na kupeana kila kitu kwa wingi
ili mpate kuzifurahia ili zitende mema na pia watende kazi nzuri tayari
kupeana....
Muhubiri 5:13 kuna roho chafu mbaya nimeona chini ya
jua, kwa majina mali inayowekwa na wenyewe ili kuwadhuru wenyewe.
Kusanya pesa ni mbaya na mwishowe
itatudhuru
Pia kuiba ni mbaya, kuiba chakula, mafuta,
pesa na kadhalika. hii inaonyesha uoga wetu na ya kwmba hatmwani mungu.
Sheria ya mungu ya kufanikiwa itatunyesha
wazi jinsi ya kufaidika wakati wa shida ya kiuchumi.
Isaya 48:17
mimi ni mungu baba yenu nikufundishaye kufaidika....
Sasa ni wakati wa kuacha njia zakitambo za
kuamini katika mabenki, akiba za kufaidika, mashamba, pesa za uzeeni, mipango
za kufaidika, akiba za wakati wa shida, na kadhalika. na aanza kufanya hivyo
kwa njia ya kimungu na kufwata maagizo zake za kufwata ili uendele.
Utajiri unaopatikana kwa njia ya
kiulimwengu haitoshelezi zaidi zaidi tunavyopata ndio zaidi tunahitaji.
Muhubiri 5:10
yule apendaye dheluji hawezi akatosheka na dheluji,
pia yule apendaye kwa wingi na kuongezeka, hii yote haina maana.
Mungu anataka tupadilishe nia yetu juu ya
pesa na kuweka upya mawazo yetu.
Mungu anataka tuwaze katika njia zake kwa
mambo yanayo husu pesa.
Tunawezaje kubadilisha na kuweka upya
mawazo yetu
Sheria ya Mungu ya upya: soma bibilia,
fikiri na kuomba, kuwa na imani, kutubu dhambi na kufuata maagizo ya Roho
Mtakatifu na neno la Mungu.
Mtazamo wa Mungu kwa kazi na nidhamu.
Mungu anataka tufanye kazi na kutenda
vizuri.
Mojawapo ya matunda ya roho mtakatifu ni
nidhanu. mtu lazima ajifunze kuwa na nidhamu katika kutumia pesa. si
lazimatuishi kaika maisha ya kuharibu ati kwa sababu sisi ni wakristo na tuko
na baba tajiri kabisa.
Tunavuna tunachopanda.
Ufanisi kuhusiana na kupanda na kuvuna-
mbegu ya kawaida-upenda-imani-pesa-wema.
Urafiki-elimu-hekima. sheria ya kupanda
nakuvuna inafanya kazi katika kila sehemu ya maisha yetu.
Panda mbegu yako nzuri ya pesa kwa udongo
nzuri, ndiyo katika kazi ya umishnari kwa walio maskini.
Wagalatia 6:7.... chochote apandacho mtu ndicho atakachovuna.
Mshangao, watu wanatarajia kuvuna pes mingi
bila hata kupanda mbegu kidogo. wanafikiria maombi inatosha, lakini hii ni
kuvunja sheria ya Mungu. ukitaka kuvuna pesa ni lazima upande pesa, sio maombi
katika hali hii. ukitaka kuvuna pesa nyingi ni lazima upande pesanyingi, sio
kuomba sana pesa. tunastahili
kuombea sana waliopotea kiroho na
wanaohitaji. hii ni njia rahisi sana
ya kutengeneza pesa, peana pesa na furaha, vile Roho Mtakatifu inakuongoza.
tafuta mwelekeo wake na utvuna mbegu yako ya pesa mahali pafaayo na wakati
ufaayo, na kiwango kifaacho.
Kumbuka pia kupanda: upndo-uzuri-pia neno
la Mungu-mbegu zote nzuri.
Panda mbegu yako ya pesa kwa umishonari,
katika kanisa, kwamaskini, kwa famili yako na kadhalika.
Baraka ya kutoa fungu la kumi.
Hakuna amri wazi katika agano. jipya juu ya
fungu la kumi.
Mungu anakubali tumjaribu anaahidi baraka
tele tukifanya hivyo.
Malaki 3:10 leteni zaka ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu,
mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama
sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo
nafasi ya kutosha.
Mungu anatujaribu tumhakikishe. hapo ndio
mahali papekee katika bibilia ampabo anatujaribu tumhakikishe.
Tunamheshimu Mungu kwa kutoa asilia kumi ya
mapato yetu.
Ni vigumu Mungu kubariki watoto wake ikiwa
tutamwibia fungu la kumi bibilia intuambia sehemu kumi ni yake.
Unachopeana kama zawadi kwa ajili ya kusudi
spesheli sio fungu la kumi lakini hupeana kando na fungu la kumi.
Nyumbani mwangu inaamrisha kuleta fungu
lako la kumi katika kanisa lako la nyumbani.
Ushuhuda.: wakati ule nilikuwanina hubiri
katika kanisa, rafiki wangu mwema
alikuja na agizo la pesa,35,000dkr. hii pesa nyingi ambayo alitaka
kupatia kanisa kama mbegu la kupanda. saa hiyo alikuwa hakika
katika shida ya kifedha. mwagizaji wake alikuwa amemuhatarisha asifanye hivyo. kama
mtu asiyeokoka alidhania pesa hiyo itapotea, na hakuamini katika kutoa kupanda mbegu ya kiroho na kuvuna biashara.
bibila inasema: ünavuna unavyopanda
Hatuwezi tukapeana Mungu zaidi
Matendo ya mitume10:14....na yeye (malaika) akamwambia(cornelio)¨maombi yako na sadaka
amemkujia Bwana kama ukumbusho.
Marko 9:41
kwa hiyo yeyote atakayekupa hata maji ya kunywa
kwajina langu, kwa sababu wewe ni mali
ya kristo, ama kweli nawambieni, hatapoteza kamwe zawadi yake.
Kutoa- njia ya kiungu.
Peana nawe utapewa, kipimokizuri, imefinywa
na kutingishwa pamoja, na kupitishwa juu, watu watakupatia kwa maendeleo yako.
kwa sababu kipimo ukitumiacho ndio itatumiwa kukupimia. luka 6:38
Sheria ya Mungu juu ya kupokea.
Mungu hupeana kwa njia ambayo haitadhuru
nafsi zetu.
James 4:3 hata mwaomba wala hampati kwa sababu
mwaomba vibaya ili mvitumie kwa tamaa zenu.
sheria za Mungu juu ya kuweka hazina na
rasilimali.
Matayo. 6:20 Bali jiweekeni hazina binguni,,
kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wavi hawavunji wala hawaibi.
Mithali19:17. amhurumia maskini humkopesha bwana: naye atamlipa kwa tendo
lake
jema.
Kutumia sheria za Mungu juu ya mafanikio
Tafuta maandiko katika biblia juu ya
mafanikio- tendo la imani.
Sababu ya umaskini,
kutokuendelea na taifa maskini, na watu maskini.
Elimu ya upotovu
Nyumba zilizochafuliwa
Kuabudu miungu aina zote
kati utamaduni ya mashariki- utamaduni ya kaskazini
Kuunguzwa na pepo ya
tamaa, ulevi, madawa ya kulevya.
Uzembe.
Kuongezeka kwa asilimia
ya wakristo wanaotoa ushuhuda ndivyo mali inavyoongezeka na pia
utaratibu katika nchi hiyo. kuongezeka
kwa dini na kuabudu miungu ndivyo umaskini na kutokuwa na utaratibu na ufisadi
katika nchi hiyo.
Tumaini kwa ajili ya pesa
zako.
Uwe na tumaini kwa sheria
za Mungu juu ya kupanda na kufuna
Bibilia husema nini
kuhusu pesa.
Pesa- na mafunzo ya
kikristo, je, wakristo wanastahili kuendelea? soma 2.wakoritntho8:9
Pesa- na kufunga na
kuomba na kutoa misaada.(matendo ya mitume 10:4,30) kornelio
Pesa- na imani 2.wakorintho9:10
mbegu ya kupana iongezeke maradufu.
Pesa- na ukweli, luka
16:10-13 hasa v 12
Pesa- na nidhamu mithali
6:9-10
Pesa- na wakati muhubiri11:4
na 6
Pesa- na kupanda na kuvuna wagalatia
6:7, wakorintho wa pili 9:6
Pesa- na mtindo wa ulimwengu kulinganishwa
na mtindo wa mbinguni. luka 6:38, mathayo 6:19-20
Pesa- na rasilimali ya benki ya dunia luka
12:21
Pesa na rasilimali katika benki ya dunia mathayo
6:19-20 na mathayo 19:21
Pesa- na faida. mithali 28:8,kutoka
22:25 na kumbukumbu la torati
23:19 (dhambi ya kuchukua faida
nyingi)
Pesa- na kupeana ulinzi, hakikisho, ya
kufunguliwa. mithali 22:26 na
11:15 na 20:16
Pesa- na fungu la kumi malaki 3:10, luka
11:42, mithali 3:9
Pesa- na sadaka matendo ya mitume 10:4.
Pesa- na kupeanamithali 28:27, wafilipi
4:17-19, luka 6:38.
Pesa- na kumwibia
Mungu malaki 3:10
Pesa- na watoto wakorintho zaburi 37:25
Pesa na ulafi zaburi 127:2
Pesa- na kuiba Yohana 12:6 na
1wakorintho 6:10
Pesa- na karata mithali16:33
Pesa- na mwenye haki mithali 15:6
Pesa- na ukweli mithali 21:6
Pesa- na nia nzuri luka 6:35
na luka 6:38 pana na wewe
utapewa
Pesa- na hasara ya milele( Judas) mathayo
27:3-5 na Yohana 17:12
Pesa- dhambi kinyume na Roho Mtakatifu
matendo ya mitume 5:1-5
Pesa- na waanzilishi (Abrahamu, Yakobo, Ayubu,
Daudi na Suleimani)
Pesa- na kubadilika kwa uchumi Mathayo
6:19-21
Pesa- na kazi Mithali
28:19
Pesa- na uzembe Mithali
6:6,9 Mithali24:33-34
Pesa- na kulala
sana asubuhi Mithali 6:10, MIthali 24:33-34
Pesa- na deni Mithali 22:7
Pesa- na kupenda sana
pesa 1 thimoteo 6:10 na waebrania
13:5
pesa- na utajiri uliofichwa Isaya 45:3
Pesa- na kuirithi. Mithali 13:22, 19:14,
14:18.
Pesa- na mataifa wanaojiita maskini na
matajiri. Ibada ya miungu licha ya asilimia kubwa ya wakristo katika taifa. Kumbukumbu
la torati 31:16
Pesa- na yesu alifanywa maskini ili sisi
tuwe matajiri. anamiliki ulimwengu mzima- aliziumba pesa zote. wakolosai
1:16
Pesa- na Mungu Yahweh. Hagai 2:8
fedha ni yangu na dhahabu ni yangu...
Pesa- na kusanya kidogo kidogo Mithali
13:11
Pesa- na maafisaa (kodi) Mathayo 22:21,
Mariko 12:17, Luka 20:25, Warumi 13:7
Pesa- na
kuchochea; kutia moyo. Proverbs 4:4
Pesa- na wivu
(kutajirika haraka haraka) Mithali13:11, Mithali 28:22
Pesa na baraka za
Mungu. Mithali 10:22
Pesa- na laana za
kifamilia.Kutoka 20:5
Pesa- na ahadi
zilizovunjwa. Zaburi 15:4. (Anayeapa kwa moyo
wake na abadiliki)
Pesa- na mambo ya kwanza. Luka 12:31
tafuteni kwanza ufalme wa Mungu
Pesa na tabia yako. (tabia nzuri
inayozalisha inaweza kupokea baraka za mali
bila kuadhiri nafsi)
Pesa- na kuridhika (utauwa pamoja na
kuridhika ni faida kubwa) 1,thimoteo 6:6.
Pesa- na kanisa mwanzo 18:
26 fungo la kumi.
Pesa- na wahudumu 1. timateo 3:3 na tito
1:7
Pesa na mpangilio
Pesa- na ndoa mithali 31:10.
Pesa na kunywa na kulala zaidi mithali 23:20
walevi ............
Pesa- na hakikisho mithali 6:1, 11:15,
17:18, 20:16, 27: 13.
Pesa- na adui wako mithali 25: 21
Pesa na kazi mithali 18: 9, 1.timateo 5;18,
mithali 14:23, zaburi 127:2.
Pesa na jinsi ya kuomba Mungu yahweh mithali
19:17.
Pesa na kupokea neno la mungu mathayo 13:23
Pesa na mambo ya kwanza Muhubiri 11:4, na
mithali 24:27
Pesa- na mali
chini ya laana na chini ya lahana na chini ya baraka.kutoka 28.
Pesa- na viongozi wa kanisa; kuweka pesa za
kanisa, na pesa za kibinafsi kuganywa vizuri.yahana 12:6 ............
yuda mweka hazina alikuwa mwizi.
Pesa- na kuanguka kwake shetani Ezekiel
28:4-5.
Pesa- kupenda pesa 1Thimoty 6:10.
......ni chanzo cha maovu yote...
Pesa- visababisho kwa tabia
na ubinafsi utu.
Mkarimu.
Atoaye kwa furaha.
Mgumu kwa kupeana.
Mchoyo
Anayejua kutumia pesa vizuri
Mpole na asiyeitisha kwa nguvu.
Mcheza kamari
Mpotevu na mharibivu.
Mwaribivu.
Mwingiliaji
Mwizi
Tamaa ya mwili
Muuzaji
Mweka hazina
Mkweli
Mpangilio katika mambo yanayohusu pesa.
Mwerevu kwa mambo yanayohusu pesa.
Mpumbavu, kwa mambo ya fedha, asiyejifunzi
kwa kukosea.
Anayetamani nguvu
Mpenda nguvu
Kuweka hazina
Kuweka kwa lazima
Akusanyaye vitu
Aliye na nidhamu kwa mambo yanayohusu pesa.
Wewe ni wa aina gani? Uwe mwaminifu kwako
mwenyewe. unataka mabadiliko? Jambo nzuri kuihusu: ni kwamba kuna uwezekano wa
mabadiliko. hatua zinazofaa kuchukua ni
: kutubu, kuamua mabadiliko na kuifanyia kazi. Maendeleo ama kukuwa nayo, yote
inategemea nia. uamuzi wa mwanadamu ni muhimu.
Maandiko juu ya fedha
Kanuni za biashara katika biblia
Jinsi Mkristo anapaswa kuvitumia pesa.
Mithali 22:7 -Tajiri humtawala maskini, naye akopaye ni mtumwa wake akopeshaye.
Mithali 23:4 -Usijitaabishe ili kupata utajiri;
acha kuzitegemea hekima akili mwenyewe.
Mithali 23:21
-kwa maana mlevi na mlafi huingia umaskini, na
utepetevu humvika mtu nguo tambara.
Mithali 24:27 -Tengeneza kazi yako bila ( nje), na ufanye ikufaye shambani,
ukiisha, na badaye ujenge nyumba yako.
Mithali 24:30-31 -Nalipita karibu na shamba la mvivu, na shamba la mizabibu la mtu asiye
na akili. v31 kumbe ! lote pia limemea miiba: uso wake ulifunikwa kwa viwawi;
na ukuta wake wa mawe umebomoka.
Mithali 24:33-34 -Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono upate usingizi! hivyo umaskini wako huja kama mnyang'anyi,
na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha.
Mithali 27:23-24 -Fanya bidii kuijua hali ya makundi yako; na kuwaangalia sana
ng'ombe zako. v24 kwa maana mali
haziwi za milele; na taji je! yadumu tangu kizazi hata kizazi?
Mithali 28:8 -Yeye azidishaye mali
yake kwa riba na faida; humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.
Mithali 28:19 -Alimaye shamba lake
atakuwa
na chakula tele; bali afuataye mambo ya upuzi atapata umaskini wa kumtosha.
Mithali 28 : 22 - Mwenye husuda afanya haraka kuwa tajiri ;Wala haufikiri uhitaji
utakaomjilia.
Mithali 28:27 -Mwenye kuwagawia maskini hatahitaji kitu ;Bali
afichaye macho yake atakuwa na laana nyingi.
Mithali 30: 8-Uniondolee ubatili na uongo;Usinipe umaskini wala
utajiri;Usinilishe chakula kilicho kadiri yangu.
Mithali 31:10-Mke mwema ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima
cha majirani.
Mhubiri 4:4 -Tena nikafikiri amali zote,na kila kazi ya ustadi ,ya kwamba inatoka
katika mtu kupingana na mwenzake .Hayo nayo ni ubatili na kujilisha upepo.
Mhubiri 11:4-Mwenye
kuuangalia upepo hatapanda; Naye ayatazamaye mawingu hatavuna.
Mhubiri 11:6-Asubuhi panda mbegu zako,Wala jioni usiuzuie mkono wako.
Kwa
maana wewe hujui ni zipi zitakazofanikiwa ,kama ni hii
au ni hii .au kama zote zinafaa sawasawa
Mithali 11:24 Kuna atawanyaye ,lakini huongezewa zaidi; Kuna azuiaye isivyo haki,
lakini huelekea uhitaji.
Malaki 3:10 Leteni zaka kamili ghalani, ili
kiwemo chakula katika nyumba yangu,mkanijaribu kwa njia hiyo ,asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia
madirisha ya mbinguni ,na kuwamwagieni
baraka , hata isiwepo nafasi ya kutosha ,au la
Warumi 13:7 Wapeni
wote haki zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahihiye hofu, hofu;
astahiliye heshima, heshima.
Luka 6:38 Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa ;kipimo cha kujaa na kushindiliwa
,na kusukwa-sukwa hata kumwagika ,ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa
kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa.
Luka 6: 35
Bali wapendeni adui zenu,
tendeni mema, na kukopesha msitumaini kupata malipo na thawabu yenu itakuwa
nyingi; nanyi mtakuwa wana wa Aliye juu kwa kuwa yeye ni mwema kwa
wasiomshukuru, na waovu.
Mathayo 6:33-Bali
utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.
Wakorintho wa pili 9:6 Lakini nasema neno hili, Apandaye haba atavuna haba ;Apandaye kwa
ukarimu atavuna kwa ukarimu.
Wagalatia 6:7 Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa chochote apandacho mtu,
ndicho atakacho vuna.
Mithali 3: 9 -10 Mheshimu Bwana kwa mali
yako.Na kwa malimbuko ya mazao yako yote .Ndipo ghala zako zitakapojazwa kwa
wingi,Na mashinikizo yako yatafurika divai mpya.
Mithali 6:6 Ewe
mvivu, mwendee chungu, Zitafakari njia zake ukapate hekima.
Mithali 6:9
Ewe mvivu utalala mpaka lini? Utaondoka lini katika usingizi wako?
Mithali 8:18 Utajiri na heshima ziko kwangu,Naam, utajiri udumuo ,na haki pia.
Mithali 10:22
Baraka ya Bwana hutajirisha Wala hachanganyi uzuni
nayo.
Mithali 13:
11 Mali
inayopatikana kwa haraka itapunguka; Bali yeye achumaye
kidogo kidogo atazidishiwa.
Mithali 14:23 Katika kila kazi mna faida; Bali maneno ya
midomo tu huleta hasara tu.
Mithali 15:6 Katika nyumba ya mwenye haki mna akiba nyingi; Bali
mabato ya mtu mbaya huwa taabu tu.
Mithali 16:33 Kura kutupwa katika mikunjo ya nguo; Lakini
hakumu zake zote ni za Bwana.
Mithali 17:18 Aliyepungukiwa na ukali
hupana mkono wa mtu ;Na kuawa mdhamini mbele ya mwenzake.
Mthali 18: 9
Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake, Ni ndugu yake aliye mharabu.
Mithali 19:
17 Amhurumiaye maskini humkopesha BWANA
Naye atamlipa kwa tendo lake
njema.
Mithali 20:
16 Twaa
nguo yake amudhaminiye mgeni; Mtoze rehema aliye mdhamini wa mgeni.
Mithali 21: 6 Kupata akiba ya mali
kwa ulimi wa uongo Ni moshi upeperushwao; ni kutafuta mauti.
Mithali 3:27
Usiwanyime
watu mema yaliyo haki yao,
Ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda.
Waebrania 13:5 Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo ;
kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, sitakupungia kabisa ,wala sitakuacha kabisa.
1Timotheo 6:10 Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha ; ambayo
wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu
mengi.
2Wakirintho 9:7 Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni
mwake, wala si kwa lazima ;maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa
ukunjufu.
Mithali 25: 21 Adui yako akiwa ana njaa, mpe chakula;Tena akiwa ana kiu ,mpe maji
ya kunywa.
Mathayo 6:24
Hakuna mtu
awezaye kutumikia mambwana
wawili;kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu,
na kumdharahu huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.
Zaburi
127:2 Ndipo kinywa chetu kilipojaa kicheko ,Na ulimi wetu kelele za furaha.
Ndipo waliposema katika mataifa,Bwana amewatendea mambo makuu.
Mwanzo 3:
19 Kwa jasho la uso wako utakula
chakula,hata utakapoirudia ardhi,ambayo katika hiyo ulitaliwa ;kwa maana u
mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.
Timotheo wa kwanza .....kwa maana mfanyi
kazi anastahili ujira wake.
Matendo ya mitume 10:4 Kornelio .... sala zako na sadaka zako zimefika juu na kuwa
ukumbusho mbele za Mungu.
Timotheo wa kwanza 6:6 Walakini utauwa pamoja na kuridhika ni faida kubwa .
Kugharamia deni
Mithali 27:13 Twaa nguo yake amdhaminiye mgeni;Mtoza rehani aliye mdhamini wa
malaya.
Mithali 6:1 -2 Mwanangu,kama umekuwa mdhamini wa rafiki yako,Ikiwa wewe na mgeni
mmepana mikono,Basi umetegwa kwa maneno ya kinywa chako,Umekamatwa kaw maneno
ya kinywa chako.
Mithali 11:15
Amudhaminiye mgeni hakosi ataumia; Achukiaye mambo
ya dhamana yu salama.
Mithali 17:18 Aliyepungukiwa na akili hupana mkono wa mtu; Na kuwa mdhamini mbele
ya mwenzake.
Jiwekeni katika umilele.
Mathayo 6:19-20 Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo,na wevi huvunja
na kuiba; bali jivukeni hazina
mbinguni, kusikoharibika kitu kwa nondo wala kutu, wala wevi hawavunji wala
hawaibi.
Marko
10:29:30 Yesu akasema, Amin, nawaambiyeni, Hakuna mtu aliye acha nyumba, au
ndugu waume ,au ndugu wake, ua mama ,au baba, au watoto, au mashamba kwa ajili
yangu, na kwa ajili ya injili ila atapewamara mia sasa wakati huu, nyumba,na
ndugu waume,na nduguwake,na mama, na watoto,na mashamba,pamoja na udhia; na
katika ulimwengu ujao uzima wa milele.
Luka 14:33 Basi, kadhlika kila mmoja wenu asiye acha vyote alivyo navyo,hawezi
kuwa mwanafunzi wangu.
Kutoa fungu la kumi katika bibilia.
Mathayo 23:23
Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! kwa
kuwa mnalipa zaka za mnanaa na bizari najira, lakini mmeacha mambo makuu ya
sheria, yani adili na rehema, na imani; hayo inawapasa kuyafanya wala yale
mengine msiyaache.
Malaki 3: 10 Leteni zaka kamili ghalani,ili kiwemo chakula katika nyumba
yangu,mkanijaribu kwa njia hiyo, asema BWANA wa majeshi ;mjue kama
sitawafungulia madirisha ya mbinguni , na kuawmwagieni baraka, hata
isiweponafasi ya kutosha ,au la.
Wabrania 7:2
Ambaye Ibrahimu alimgawia sehemu ya kumi na vitu vyote; (tafsiri ya jina lake
kwanza ni mfalme wa haki ,tena, mfalme wa Salemu, maana yake, mfalme wa amani;
Hesabu 18:26
Tena utanena na Walawi, na kuwaambia, Hapo
mtakapoitwaa zaka mkononi mwa wana wa Israeli, niliyowapa ninyi kutoka kwao
kuwa urithi wenu, ndipo mtakaposongeza sadaka ya kuinuliwa kwa BWANA katika
hiyo, iwe zaka katika hiyo zaka.
Nehemiah 10
..... Walawi, watwaapo zaka Walawi .nao Walawi wataipandisha zaka ya hizo zaka
nyumbani kwa Mungu wetu, katika nyumba ya hazina.
Fungu
la kumi ya Walawi. Fungu la kumi la Haruni.
Kabila ya walawi walichaguliwa na Mungu
wahudumu katika hekalu . Walikuwa makuhani .
Swali: Je huduma yako ya kanisa hutoa fungu
la kumi?
Jibu liko katika Hesabu 18:26-29
Makuhani Walawi waliamurishwa walipe fungu la kumi kutokana na fungu la kumi
ambao watu waliwatolea.
Himizo: Mchungaji na wahuduma na wote ambao
kanisa linawalipa mshahara nao wanapaswa walipe fungu la kumi kutoka kwa
mshahara wao.
Luka 18:12
Mimi nafunga mara mbili kwa juma;hutoa zaka katika
mapato yangu yote.
(Mfarasayo
alilipa fungu la kumi ,mtoza ushuru hakulipa,lakini akahesabiwa haki.)
Luka 12:32-34 Msiogope ,enyi kundi ndogo;kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule
ufalme. Viuzeni mlivyo navyo, mtoe sadaka . Jifanyieni mifuko isiyochakaa,akiba
asiopungua katika mbingu ,mahali pasipokaribia mwivi, wala nondo haharibu. Kwa
kuwa hazina yenu ilipo, ndipo itakapo waponya mioyo yenu.
Matendo ya mitume 20:35 Katika mambo yote nimewaonyesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi
imewapasa kuwasaidia wanyonge,na kuyakumbuka maneno ya bwana Yesu jinsi
alivyosema mwenyewe ,heri kutoa kuliko kupokea.
Wefeso
4:28 Mwibaji asiibe tena; bali
afadhali afanye juhudi, akitenda kazi ilyo nzuri kwa nikono yake mwenyewe,apate
kuwa na kitu cha kumgawia mhitaji.
Wafilipi 4:19 Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachohitaji kwa kadri ya utajiri
wake, katika utukufu, ndani ya Kristo.
Mathayo 6:3 Amin,
nawaambieni, Wamekwisha kupata thawabu yao.
Bali wewe utoapo sadaka, hata mkono wako wa kushoto
usijue ufanyalo mkono wa kuume;
Mathayo 6:1
Angalieni msifanye wemw wenu machoni pa watu, kama wanafiki
wafanyavyo katika masinagogi na njiani ,ili watukuzwe na watu.
Mathayo 5:42 Akuombaye, mpe;naye atakaye kukopa kwako, usimpe kisogo.
Kuiba pesa za kanisa na mwisho kuingia
jehenamu kwa sababu ya pesa.
Yuda Iskariote alipotezwa milele kwa sababu
ya kupewa pesa na akawa mwizi na msaliti kwa fedha thelathini.
KUHUSU KUCHUKUA FAIDA
Zaburi 15:5 Hakutoa
fedha zake apate kula riba,Hakutwaa rushwa amwangamize asiye na hatia.
Mtu atandaye mambo hayo Hataondoshwa
milele.
Kutoka22;25
Usikopeshe mtu aliye maskini, katika watu wangu waliopamoja nawe, usiwe kwake
mfano wa mwenye kumdai;wala hutamwandikia faida.
Mithali28;8`
Yeye azidishaye mali
yake kwa riba na faida, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.
Hazina zilizofichika.
Isaya 45: 3
Nami nitakupa hazina za giza, na mali
zilizofichwa za mahali pa siri, upate kujua ya kuwa mimi ni BWANA, nikuitaye
kwa jina lako, naam, Mungu wa Isreali.
2 Wakorintho 9:10 Na yeye ampaye mbegu mwenye kupanda, na mkate uwe chakula, atawapa
mbegu za kupanda na kuzizidisha, naye atayaongeza mazao ya haki yenu;
Isaya 33:6 Nyakati zako zitakua
nyakati za kukaa imara ;za wokovu tele na hekima na maarifa ;kumcha BWANA ni hazina yake ya akiba.
Zaburi 119: 127 Ndiyo maana nimeyapenda maagizo yako, Kuliko dhahabu, naam, dhahabu
iliyo safi.
Mhubir 5:10
Apandaye fedha atavuna fedha, Wala apandaye wingi
hatashiba maongeo. Hayo pia ni ubatili.
Mhubiri 5:
12 Usingizi wakekibarua ni mtamu, kwamba
amekula kingi ;lakini kushiba kwake tajiri hakumwachi kulala usingizi.
Mhubiri 5:13
Kuna na balaa mbaya sana
niliyoiona chini ya jua, nayo ni hii, mali
alizoziweka mwenyewe kwa kujinyima.
Mhubiri 5:19
Tena, kwa habari za kila mwanadamu,ambaye Mungu
amempa mali na ukwasi,
akamwezesha kula katika hizo, na kuipokea sehemu yake na kuhifurahia mali
yake ;hiyo ndiyo karama ya Mungu.
Mathayo 6:25 Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au
mnywe nini,wala miili yenu, mvae nini. Maisha je? si zaidi ya chakula, na mwili
zaidi ya mavazi?
Mithali 23:4 Usijitaabishe ili kupata utajiri Acha kuzitegemea akili zako
mwenyewe.
Mathayo 6:24 Haku mtu awezaye kutumikia mabwana wawili ;kwa maana atamchukia
huyu na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu na kumdharahu huyu .Huwezi
kumtumikia Mungu na mali.
1Timotheo 6:10
Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenad
fedha, amabayo wengine hali wakiitamani
hiyo wamefarakana na Imani,na kujichoma kwa maumivu mengi.
Kuhusu kulipa ushuru.
Mathayo 22;21na Marko 12;17 na Luka 20:25
Akawaambia ,Basi vya Kaisari mpeni Kaisari, na vya Mungu mpeni Mungu.
Warumi 13:7
Wapeni wote haki zao mtu wa kodi, kodi, mtu wa ushuru, astahili hofu hofu,
astahili heshima,heshima.
Luka 16:10-13 Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana
huwa mwaminifu lililo kubwa pia . 11, Basi kama ninyi hamkuwa waaminifu
katika mali ya
udhalimu ni nani atakaye wapa amana mali
ya kweli.12, Na kama hamkuwa waaminifu katika mali
ya mtu mwingine, ni nani atakayewapa iliyo yenu wenyewe? 13, Hakuna mtumishi
awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana ama atamchukia huyu na kumpenda
huyu, ama atashikamana na huyu na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.
Maandiko zaidi kuhusiana na pesa.
Mithali 22:1
Heri kuchagua jina jema kuliko mali
nyingi;na nehema kuliko mali
na fedha.
Mhubiri 5:10 Apendaye fedha atashiba fedha wala apendaye wingi hatashiba
maongeo.
Mhubiri 5:12 Usingizi wake kibarua ni mtamu, kwamba amekula kidogo, au ;au
kwamba amekula kingi; lakini kushiba kwake tajiri hakumachi kulala usingizi.
Zaburi 119:127 Ndiyo maana nimeyapenda maagizo yako, kuloko dhahabu, naam, dhahabu
iliyo safi.
Mithali 23 :4 Usijitaabishe ili kupata
utajiri Achakuzitegemea akkilil zako mwenyewe.
Mathayo 6:24 Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili;kwa maana atmchukia
huyu na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu na kumchukia huyu,huwezi
kumtumikia Mungu na mali.
19. Hatua muhimu katika Barabara ya kutoka
kwa umasikini kuingia utele.
Kuwaza kama
mtu aliye na mali.
Badilisha hali
yako ya kufikiria juu ya mambo yahusuyo pesa.
Weka upya mawazo
yako kwa kusoma neno la Mungu Kujifunza bibilia.
Fanya mabadiliko
katika mtindo wa ulimwengu ingie njia za Mungu.
Elewa kanuni za
kiungu ya kupanda na kuvuna.
Lipa fungu la
kumi kwanza si mwishowe.
Lipa fungu la
kumi kwa kanisa lako la nyumbani.
Mpende Yesu zaidi
ya pesa zako Yule tajiri mdogo hakupenda Luka 18:23.
Anza kupanda -kwa
wingi ama kidogo- haijalishi, lakini panda kila wakati , fanya iwe sehemu ya
maisha yako.
Anza kuweka
katika hazina ya soko la mbinguni na ufanye kwa furaha.
Jifunze nafasi
iliyo sawa juu ya kutoa na kutumia pesa.
Tumia mpango wa mda mrefu. Hakikisha
umejiokoa kutokana na laana.
Jifunze jinsi ya kupokea pesa kiutaraji
bila kuadhiri nafsi yako.
No comments:
Post a Comment