Udhihirisho wa Roho Mtakatifu.
Roho
Mtakatifu katika asili ya kihebrania.:RUAH ( hutamkwa kama RUACH )
kumaanisha,hewa inayotembea, pumsi ama pumsi ya UZIMA. RUAH ni sawa na jina la
Kiyunani: PHNEUMA.
Roho Mtakatifu ni kama baba na mwana:wa milele, haina
kipimo, haikuumbwa, ni Mungu wa kweli na ni bwana, ametoka kwa baba na kutumwa
na mwana.
Yaliyomo:
1.
Usawa wa Roho mtakatifu. Majina ya Roho Mtakatifu.
2.
Roho
Mtakatifu kama Mungu, utatu wa Mungu.
3.
Roho
Mtakatifu kama Mtu.
4.
Roho
Mtakatifu, Jukumu na kazi ya Roho Mtakatifu.
5.
Roho
Mtakatifu kama mfariji na mwalimu wetu.
6.
Roho
Mtakatifu na vipawa tisa vya Roho.
7.
Roho
Mtakatifu na makao yake.
8.
Roho
Mtakatifu na pingamizi za Roho Mtakatifu.Kuhusunisha Roho mtakatifu.
9.
Ubatizo
katika Roho Mtakatifu.
10.
Roho
mtakatifu na kanisa.
11.
Roho
Mtakatifu na Nguvu,uweza wa kiungu, nguvu za kiungu,afya na msaada wa kiungu,
usafirishaji wa kiungu.
12.
Roho
mtakatifu na dhambi siyosameheka.
13.
Roho
mtakatifu kama mwalimu na mfariji.
14.Roho mtakatifu na kukubali dhambi zako
15.Roho Mtakatifu na huduma.
16.Upako wa Roho Mtakatifu.
17.Ujazo wa Roho Mtakatifu.Kujazwa kwa Roho
mtakatifu
18.Roho Mtakatifu na Roho ya uombezi.
19.Roho Mtakatifu na Ufufuo.
20.Roho Mtakatifu na utukufu wa Mungu.(
Shekina, Kabod, Gloria).
21.Roho Mtakatifu na matunda ya Roho.
22.Roho Mtakatifu na uhisho kwa mahubiri,
Nyimbo na Kuabudu na uimbaji.
23. Roho Mtakatifu na miujiza(mysticism). Ukweli na uongo.
24.Roho Mtakatifu na uongozi.( Njia saba ya
uongozi )
25.Roho Mtakatifu na huisho wa neno la Mungu.
26.Roho mtakatifu na Yesu kama msaliwa wa
kwanza na wa pekee wa Mungu Yahweh, baba.
27.Roho Mtakatifu na manabii wa agano la kale.
28.Roho Mtakatifu na hekalu.
29.Roho mtakatifu na ubatizo
katika Roho na moto.
30.Roho Mtakatifu na kuubiri
injili.
31.Roho Mtakatifu na mwanzo.(Genesis)
32.Roho Mtakatifu na silaha kamili za Mungu.
33.Roho Mtakatifu waweza kukasirishwa.
34.Roho Mtakatifu na Nguvu za Kiungu.
35.Roho Mtakatifu na kuzaliwa mara ya
pili.(wokovu)
36.Roho Mtakatifu na roho ya mwanadamu(ki utu)
37.Roho Mtakatifu na umoja wa kweli.
38.Roho mtakatifu na Roho ya maombi.
39.Roho mtakatifu na kuabudu.
1.
USAWA WA ROHO MTAKATIFU. MAJINA YA ROHO MTAKATIFU.
Roho wa Mungu, wa baba, ya mwokozi, ya Kristu, ya mwana,
wa ukweli, ya uzima, ya utukufu, ya nguvu, wa ushuhuda, wa maarifa, ya ufunuo,
wakili, mfariji, mwalimu, njiwa, moto, nguvu, maji, mafuta, mhuri.
2.
ROHO MTAKATIFU KAMA MUNGU WA KWELI, UTATU WA MUNGU.
a)Tuna batizwa katika JINA la Baba, la Mwana na la
Roho Mtakatifu. Mathayo 28:19.Tuna batiswa katika jina la UTATU wa Mungu.
Maandiko
yatuonyesha kwamba utu utatu wa Mungu ni MUNGU MMOJA.
b)
Mwanzo 1:26, Na tumfanye mtu kwa mfano WETU…….
Katika
andiko la kiebrania, hali ya uwingi umetumika.Wote utatu wa Mungu walikuweko
katika uumbaji. Yahweh baba, Yeshua Messia na Mungu Roho Mtakatifu.
3.
ROHO MTAKATIFU KAMA MTU:
Tazama
pia: Wakili, hunena, Hushuhudia, Anasauti, huzuni, hufu, hushawishi, huongoza,
tabia, hufunza,hukumbusha, hufariji. Haya yote ni majina ambayo tunamwuta Roho
Mtakatifu kama Mtu.
Katika
Yohana 16. Hapa Roho Mtakatifu ametajwa mara nyingi kama YEYE, Mtu wa kiume (
He).
4.
ROHO MTAKATIFU, JUKUMU NA KAZI YA ROHO MTAKATIFU
Jukumu
lake ni ku…shawishi, zalisha,fundisha, elekeza, , wito, shuhudia, boresha tabia, kumbusha, fariji,
leta maarifa, takaza, paka, angaza, fanya upya, huisha, batiza, jaza..
Warumi
5:5…
Roho
Mtakatifu humwaga upendo wake wa kiungu katika mioyo zetu. Anaumba, anaponya,
na anatenda miujiza. Yeye ndiye nguvu utokanao kwa Mungu Yahweh.
Yeye,
Roho Mtakatifu, huomba NDANI yetu na
KUPITIA kwetu, HADI kwa Mungu baba.
5.
ROHO MTAKATIFU KAMA MFARIJI NA MWALIMU.
Tazama pia, Kuadhibisha, fundisha, Kumbusha, elekeza,
elimisha, Shuhudia, Sadikisha, Huzunishwa, Mfuasi.
Matendo
ya mitume 9:31,… na
kuongezeka likitiwa moyo na Roho Mtakatifu.
Luka Mtakatifu 12:12,.. Roho Mtakatifu atawafundisheni…..
Yohana 14:26,… lakini Msaidizi, Roho Mtakatifu, ambaye Baba atamtuma
kwa jina langu, atawafundisheni kila kitu na kuwakumbusheni yote
niliyowaambieni.
ROHO MTAKATIFU NA VIPAWA .
- Kunena na ndimi
- Kutafsiri ndimi
- Kipawa cha unabii ( Njia 6 za kuamua unabii )
- Neno la Maarifa
- Neno la hekima
- Kubambanua miroho
- Vipawa vya uponyaji
- Kipawa cha miujiza
- Kipawa cha imani.
Kubatizwa katika Roho Mtakatifu ni mwanzo ya
kuhudumu katika vipawa 9 vya Roho Mtakatifu.
Ni : Vipawa 3 vya
-
Kunena kwa Lugha
-
Kipawa
cha unabii
-
Kutafsiri
ndimi
Vipawa 3 Ufunuo,
-
Neno
la hekima
-
Neno
la Maarifa
-
Kubambanua
ndimi
Vipawa 3 vya Nguvu,
-
Kipawa
cha uponyaji
-
Kipawa
cha miujiza
-
Kipawa
cha Imani.
1. Kunena katika ndimi. Matendo ya Mitume 2:
Wakati mtu anaponena kwa lugha, akili na ufahamu
hupumzika.
Roho Mtakatifu anatumia kinywa cha mtu tu, sio bongo au
akili ya mtu.
Usemi ni ya kiroho
Kuna aina nyingi za kunena kwa lugha. ( Lugha mbali mbali )
Kusudi ya
kunena kwa lugha:
1.
Ni
dhihirisho ya kiroho ya kubatizwa katika Roho Mtakatifu ( Matendo ya Mitume
10:46)
- Ili mwanadamu aweze kuwasiliana na Mungu Kiroho. ( 1 Wakorintho 14: 2 )
- Ili waumini wamtukuze Mungu. ( Matendo ya Mitume 10:46)
- Ili itubariki sisi wenye. ( 1 Wakorintho 14:39)
- Ili itubariki katika nyimbo katika Roho. ( Wakolosai 3:16)
- Ili roho zetu, mbali na mawaso yetu, iweze kuomba. ( 1 Wakorintho 14:14)
- Kwamba pamoja na kutafsiriwa kwa lugha, kanisa iweze kuinuliwa. ( 1 Wakorintho 14:12,13,5,26.)
- Ndimi ni kama ishara kwa wale wasio amini. ( 1 Wakorintho 14:22)
2. Kutafsiri ndimi ( Lugha )
Kutafsiri lugha ni katika hali ya kiroho, usemi wa
kiajabu.
Inahusika hasa na kunena kwa lugha.
Kuna
mashauri machache kuhusu maswali ambayo mara kwa mara inaulizwa:
- Kutafsiri ndimi sio sawa na kutafsiri lugha moja hadi lingine. Kutafsiri lugha fulani ni kutafsiri neno kwa neno bali kutafsiri ndimi ni kutoa maana.
Kutafsiri ndimi yaweza kuwa kupitia picha, maelezo ama kinaganaga.
2.
Asili,
vipawa vya kiasili, na elimu na pia utaifa wa mwenye kutafsiri ita adhiri
utafsiri bali kipawa sio kwa ajili hiyo ila kwa miujiza.
- Wale ambao hunena kwa ndimi ni bora waombe kwa ajili ya kipawa hiki cha kutafsiri. ( 1 Wakorinto 14:13)
- Mtu asitafsiri. ( 1 Wakorinto 14:27)
- Kutoa ujumbe kwa lugha mengine na kujitafsiria yaweza kujizoeza.
- Andiko yatueleza tusitoe zaidi ya ujumbe tatu katika mkutano moja. ( 1 Wakorinto 14:27 )
3. Unabii.
Kiyunani:
profemi=kunena, kutabiri, kubashiri.
Kiyunani:profetes=Mnabii.
Kutoa unabii:Kunena kwa ajili ya mwingine, kuwa msemaji
wa Mungu.
Unabii kwa urahisi inatokana na msingi wa kiungu na msemo
uliopakwa mafuta.
Kuna tofauti kati ya kipawa cha unabii na huduma ya
mnabii.
Mnabii kama afisi hunena kwa miji, mataifa ama dunia
nzima. Kipawa cha
unabii sana sana hutumika kuhudumia watu na umati.
Kusudi la Unabii.
1.
Unabii ni kunenea
watu katika hali ya kiroho. ( 1 Wakorinto 14:3)
- Kujenga kanisa – mwili wa waumini. ( 1 Wakorinto 14:4)
- Kuinua kanisa ( 1 Wakorinto 14:3) Kuinua haimaanishi kukemea.
- Kufariji Kanisa ( 1 Wakorintho 14:3,31)
- Iliwaumini wafundishike. ( 1 Wakorintho 14:31)
- Kushawishi asiyeamini na kudhiirisha siri za moyo wake. ( 1 Wakorintho 14:24,25)
Maswali zaidi kuhusu matumizi na udhabiti.
A: Tunaamuriwa tutamani hasa kipawa hiki. ( 1
Wakorintho 14:1)
B:
Unabii ni kuu kuliko ndimi wakati haijaambatanishwa na utafsiri – ikiwa ujumbe
utatafsiriwa,basi zatakuwa vya karama sawa.
C:
Ingawa unabii ni wasi kwa kuelewa, sio kunena na ufahamu. Ni Roho wa mungu
ananena kupitia mwanadamu.
D:
Muumini aweza kupata kipawa cha unabii ( ama yeyote ile) katika ujazo/ ubatizo
wa Roho Mtakatifu pamoja na kunena kwa lugha ( Matendo ya Mitume 19:6)
E:
Unabii haichukui nafasi ya neno lililoandikwa,
F: Neno
la Mungu ni msaada ulioimara, Kila unabii ambao unapinga neno la Mungu twaweza
kana, kataa bila hofu.
G: Aliye
na kipawa hicho anawajibika kwa utumizi, kutotumia jinsi inavyoitajika,
Kufinyilia chini au udhabiti.
H: Roho
wa unabii hutii mnabii. ( 1 Wakorintho14:32)
I: Paulo
pia alisema; ” Wasizidi watatu wenye kutoa unabii katika mkutano moja. (1
Wakorintho 14:29) na wengine waamue.
J: Ujumbe wa unabii wakati mwingine haiwezi
kubainika na kueleweka vizuri. (Mafuta unaotiririka Mwambao ya magharibi ya
Norwe)
__________________________________________________________________________
Unabii:
Mzee mmoja, Martin Anderson, kutoka kanisa la
kipentekote kule Moss, Norwe, alishuhudia unabii huu kule Moss:
Wakati mafuta itatoka
bahari za kaskazini na kutoka pwani ya Norwe, mambo yataanza kutendeka na
kurudi kwake Yesu Kristu inakaribia.
Wakati haya maneno yalinenwa, watu walisimama
kwenye miguu yao na mtu huyo aketi na aache kuongea maneno haya ya upusi,
kwamba mafuta inapitishawa juu kwenye pwani ya Norwe. Kwa wakati huo, Ujumbe
ulikuwa mgumu kuaminika, hata hivyo, sasa hivi kampuni nyingi za mafuta
zinapampu mafuta kupitia pwani ya Norwe na nchi ya Norwe sasa inaongoza kwa
kusafirisha mafuta duniani baada ya Saudi arabia
K: Inahitaji
imani kutabiri.(.... Mwenye
kipaji cha unabii na akitumie kadiri ya imani yake. Warumi 12:6)
Usitafute
habari kuhusu maisha yako ya baadaye kwenye yafuatayo:
-
Horoscopes,
Mpigaramli, Mwaguzi, Vyeti, Vyeti vya Tarot nk.
4. Neno la
maarifa.
Neno la maarifa ni ufunuo wa Roho Mtakatifu kuhusu manbo
fulani katika akili ya Mungu.
Sio kipawa vokal, ni kipawa cha ufunuo. Inakuwa vokal
wakati inashirikishwa kwa wengine.
Ni kipande cha maarifa ya kiungu. Neno la maarifa inahusu
yaliyopita ama wakati huu, haihusiki na wakati ujao/ usoni kama vile neno la
hekima hufanya.
Kusudi la Kiungu:
1.
Kukanya
mfalme kuhusu mpango wa adui ya kuharibu.
- Kuangaza na kutia moyo mtumishi wa Mungu aliyevunjika moyo.(1Wafalme 19:14-18)
- Kufichua mnafiki. ( 2 Wafalme 5:20-27)
- Kushawishi mwenye dhambi kuhusu haja ya mwokozi. ( Yohana 6:18,19,29.)
- Kutambua mtu aliyejificha. ( 1 Samwel 10:22)
- Kuonyesha mtu aliye na hitaji. ( Matendo ya mitume 9:11)
- Kubukua ufisadi kanisani.
- Kuonyesha mahali panapo stahili pa kukutania watu wa Mungu. ( Mariko 14:34-37)
- Kujua mawazo ya wanadamu.( Yohana 2:24) ( 1 Samuel 9:19).
- Neno la maarifa inaweza kusaidia sana katika maombi kamili kwa aidha mtumishi wa Mungu aliye katika dhiki ama wale ambao wanahitaji usaidizi wa Kiroho. ( Mmishinari anayekufa katika kijiji cha Afrika).
- Kupfidia watu waliopotea au rasilimali.
- Kutambua chanzo cha magonjwa a kupagawa.
5.
Neno la Hekima
Ni hekima
ya Mungu sio la Mwanadamu.
Neno la
hekima laweza kuwasilishwa kupitia sauti ya kiungu. Inaweza pia wasilisha kwa
mwaliko wa malaika, kupitia ndoto na maono, au kupitia kipawa cha unabii cha
kiungu,ama ndimi na utafsiri wake.
Hekima inahusu
siku zijazo.
Baadhi
ya maandiko katika bililia ni kama yafuatayo:
- Kuonya na kuelekeza watu kuhusu ukumu ijayo na maafa. ( Mwanzo 6:13-22, na Mungu akamwambia Nuhu......)
- Kudhihirisha mpango wa Mungu kwa wale ambao atawatumia. ( Mwanzo 41:16, 28-41, Pharaoh – Joseph)
- Kuhakikishia mtumishi wa Mungu jukumu lake la kiungu. ( Kutoka 3:10, Musa alipotumwa kwa Pharaoh.)
- Kudhihirisha maagizo sahihi na jinsi ya kuabudu kiungu. ( Kutoka 25, Onyesho la jinsi hekalu litakavyo kuwa ladhihirishwa kwa Musa).
- Uchanuzi wa pendelevu wa mungu kuhusu neema kuu inayotolewa bure kwa wote. ( Matendo ya mitume 10:9-16)
- Kuhakikisha ukombozi unayokuja katikati ya dhiki. ( Matendo ya mitume 27:24,
Paulo usiogope! Ni lazima
utasimama mbele ya Kaisari…)
7.
Kutoa hakikisho ya baraka zijazo. ( Mwanzo 23: 10-15 )
Katika nyakati
hizi:
A. Neno la hekima huonya kuhusu hatari
inayokaribia.
Ushuhuda:
Binti mmoja aruhusu jambazi kwenye gari lake.
Ilifanyika katika magharibi mwa Denmark. Dada huyu Mkristo,
alikuwa njiani kuelekea mahali pake pa kazi, akambeba mtu aliyesimama kando ya
barara. Punde tu, mtu huyo alipoingia kwenye gari, dada alihisi moyoni mwake
onyo kwamba kuna hatari inakaribia. Mwishowe aliuliza yule mtu atoke ili
ampanguzie kioo cha nyuma ya gari lake, Kisha dada huyo akaonda na kumwacha mtu
yule. Alipofika kazini, akapata mfuko chini ya gari lake na ndani yake kulikuwa
na bunduki lililotiwa risasi. Hapo ndipo alipogundua mungu amemuepusha kutokana
na hatari kubwa ambayo hangeweza fikiria nini kingetokea. Basi alikabidhi
polisi bunduki hilo. Mungu huonya wanawe wakati mwingine kupitia neno la hekima.
B. Kutambulisha
au kudhibitisha wito wa umishionari.
Ushuhuda:
Wito wa umishionari kwa Axel Jensen katika Zion
Oelgod, Denmark:
Mmoja wa wazee Asimulia kuhusu tukio lilitokea hapa kanisani
kwetu katika siku za kale. Katika jumapili moja asubuhi, Mbaba mmoja na mwanawe
( kijana mdogo ) walikuwa wanasafafiri kwenye gari la moshi. Walipofika kituo
cha oelgod, ilikuwa masaa za ibada, waliamua kutua kidogo wahudhurie ibada
kasha baadaye waendelee na safari yao. Mhubiri wa jumapili hii akatoa unabii.
Ujumbe ulikuwa mwito kwa kijana huyo mdogo, mwito wa kufanyika mmishionari.
Jina lake ni Axel Jensen. Miaka mingi baada ya tukio hili akawa mmishionari
aliyejulikana sana Afrika na baadaye China.
Roho mtakatifu anajua moyo wa mwanadamu, hata kwa kijana mdogo
kama huyu. Katika kipawa cha unabii na neno la hekima kupitia kwa roho
mtakatifu ukatoa maagizo na kudhihirisha mpango wa Mungu katika siku zijaso kwa kijana mdogo.
C.
Kudhihirisha siku za usoni.
D. Kutoa maelekezo kwa mtu binafsi.
6.Kupambanua
miroho.
Utumizi wa
vipawa vya roho katika nyakati hizi ni sawa na vile ilivyo kwenye bibilia:
1. Kusaidia katika ukombozi kwa walio teseka, gandamizwa
na kuadhibiwa. ( Mariko 5:5, ”Mchana na usiku alikaa makaburini na milimani
akipaaza sauti na kujikatakata kwa mawe.”
Miroho
michafu yaweza kusabisha uasimu, udhaifu na maelfu ya magonjwa mbali mbali.
2.
Kutambua mtumishi wa shatani. ( Matendo ya mitume 13:9-10,
“Basi, Saulo ambaye
aliitwa pia Paulo, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alimkodolea macho huyo
mchawi, akasema, "Mdanganyifu wa kupindukia na mlaghai wewe! Wewe ni mtoto wa Ibilisi! Wewe ni adui wa chochote kile kilicho cha
kweli; hukomi hata mara moja kujaribu kuzipotosha njia za Bwana zilizonyoka“
|
3. Kusaidia
katika kuangalia mipango ya mwaribivu.( Matendo ay Mitume 16:16) Paulo atambua roho ya
uaguzi.)
4.
Kuweka wazi makosa. ( mafundisho ya mapepo na laana zake.( 1 Tim 6:1, 2 Pet
2:1)
5. Kuweko wazi watenda-miujiza
za kipepo.( 2 Tesalonike 2:9, “Huyo Mwovu atakuja na nguvu za Shetani na
kufanya kila namna ya miujiza na maajabu ya uongo,”
7.(Vi)pawa vya uponyaji.
Huu ni uponyaji wa kipekee
kupitia kwa Roho mtakatifu, bila matibabu wala ujuzi wowote ule wa kisayansi.
Baadhi ya wakristo hupenda kusema:, ”Mungu pia hutumia madaktari.” Kwa hakika
ndivyo, lakini SIYO kuhusu vipawa vya uponyaji, Roho mtakatifu PEKEE hufanya
kazi hapa. Madaktari bado ni njia ya kiasili ya uponyaji.
Vipawa vya uponyaji hufaya
kazi kwa imani na kwa kuwekea mikono kichani kwa muumini ama tu kwa kuamini
maombi.
Imani:dhambi ya kutoamini
haihusu kusindikana kwa uponyaji – bali inahusu dhambi ya kutoamini katika Yesu
kristu mwana wa Mungu.
Vipawa vya uponyaji
imeandikwa katika uwingi katika maandiko asili.
Ni kama ifuatavyo:
1.
Uponyaji wa magonjwa katika mwili.
2.
Uponyaji wa ulemavu.
3.
Uponyaji wa hisia, na kumbukumbu.
4.
Uponyaji wa akili, ukichaa na kadhalika
5.
Uponyaji kwa uweza wa miujiza.
6.
Uponyaji kwa kupakwa kwa mafuta.
7.
Uponyaji kupitia nguo uliopakwa mafuta.
8.
Uponyaji kupitia punguo.
Kwa
kuongezea:
9.
Uponyaji wa kiasili kupitia nguvu za mwilini.
10. Uponyaji kupitia kufunga.
11. Uponyaji kupitia Mungu anapotuma neno lake la uponyaji, kama jibu kwa
maombi. ( Zaburi 107:20 )
Uponyaji
kupitia matibabu na upasuaji ni njia ya kiasili sio njia ya uponyaji wa kiungu.
Uponyaji
kupitia kufunga sio uponyaji kutokana na vipawa vya uponyaji, bali ni kutumia
njia ya uweza wa kiasili ya mwili kujitawasha na kujirejesha na hivyo uponyaji
unafanyika.
Mifano
katoka bibilia kwa ajili ya kufafanua zaidi:
a)
Kwanza kabisa, vipawa vya uponyaji unaleta ukombozi kutokana na magonjwa
na kuharibu kazi za ibilisi mwilini mwa mwanadamu.
Matayo
8:2-4 ( Luka 5:12-16 ) Yesu aponya ukoma.
Matayo
9:1-8 ( Luka 5:17-26 ) Yesu aponya mtu kiwete ugonjwa wa mifupa.
Matayo
9:27-31. Vipovu wawili waponywa?
Matayo
14:34-36, Yesu akiponya wengi.
Matayo
9:18-26,( Mariko 5:21-43 ) Mwanamke aponywa ugonjwa wa damu.
b)
Uponyaji wa kiungu sio sawa na ukombozi kutokana na nguvu za giza.
Mifano
ya uponyaji baada ya ukombozi kwa sababu nguvu za giza mara kwa mara
husababisha aina nyingi ya magonjwa:
Matayo
9:32-34, bubu na aliyepagawa aponywa.
Matayo
15:21-28, Yes aponya mtoto mdogo msiria kutokana na nguvu za giza.
Matayo
17:14-21, kijana mwenye kichaa aponywa.
Luke
13:10-17, Mwanamke aliyefungwa na nguvu za giza awekwa huru.
c)
Kudhibitisha madai ya kushangaza za Yesu:
Yohana
10:37-38, Kama sifanyi kazi za Baba yangu msiniamini, Lakini ikiwa ninazifanya,
hata kama hamniamini, walau ziaminini hizo kazi mpate kujua na kutambua
kwamba Baba yuko ndani yangu, nami niko ndani yake."
d)
Kumamlakisha ujumbe wa habari njema ihubiriwayo na watumishi wa Mungu.
Wakati
viwete wanatembea, vibovu wanaona, wagonjwa wanaponywa, mapepo yafukuzwa, yote
katika jina la Yesu, kila mtu atajua kwamba Yesu hakika yu HAI, na alifufuka
kutoka kwa wavu.
e)
Kuvuta watu waje kwa kristo, waje wasikie habari njema.
Kila
mmoja ameona umati kubwa wakingoja mlangoni mwa mkutanoni wakingojea zamu yao ya kupokea uponyaji, je, sio nguvu hizi
za vipawa vya uponyaji inayo wa vutia kuja kuudhuria mkutano na wengi pamoja na
wao?
f)
Kuresha watu kwa Mungu:
Peter
akiwa Lydda. Matendo ya mitume 9:33-35, Huko alimkuta mtu mmoja aitwaye Enea
ambaye kwa muda wa miaka minane alikuwa amelala kitandani kwa sababu alikuwa
amepooza, v34Basi, Petro akamwambia, "Enea, Yesu Kristo anakuponya. Amka
utandike kitanda chako." Enea akaamka mara.v35Wakazi wote wa Luda na
Saroni walimwona Enea, na wote wakamgeukia Bwana.
g)
Kushawishi wasiomini kuhusu ukweli wa neon la Mungu.
Hakuna
lililo la nguvu la kuvutia asiyeamini zaidi ya uponyaji wa kimiujiza, ambalo
hauwezi kuikataa wala kuipuuza.
h)
Kuleta utukufu kwa Mungu, Halleluyah:
Na watu
wakashangilia kwa ajili ya matendo matakatifu yalifanywa naye. Mariko 2:12,
Luke 13-17.
i)
Kuinua imani na ushujaa katika
watu wa Mungu:
Wakati
mwinjilisti anapoombea wagonjwa kisha wakapona, wote tunainuliwa hadi kiwango
kingine cha imani na tunahisi kutiwa ujasiri kufanya hivyo.
Upako
wa mafuta ( Yakobo 5:14 ) sio kupitia kazi ya vipawa vya uponyaji kwa roho bali
ni jawabu kutokana na kutii na pia kwa majibu ya kuamini katika maombi.
Wazee
na wahudumu ndio wanajukumu la kutekeleza upako wa mafuta.
Mchungaji
ndiye mkuu wa viongozi.
Kuwekelewa
mikono sio tu kwa walio na vipawa vya Roho, bali nikitendo cha imani ya kila
mmoja na kwa kila mmoja.
Ilhali
upako wa mafuta ni kwa wale wagonjwa waaminio.
Kwanini
sio wote huponywa?
Kulikuwa
na watu wengi wagonjwa katika kizima cha Betsaida – ni mmoja tu aliponywa- na
hiyo kwa mshindi wetu Yesu Kristo. Tunaweza waza kwamba Yesu ataponya wote
lakini hakufanya hivyo, kwa ajili ya sababu isiyojulikani.
Imeandikwa:
kwa sababu ya kutoamini kwao katika mji huo, yesu hakufanya muujiza yeyote ile
ama kuponya. Matayo 13:58, “Kwa hiyo, hakutenda miujiza mingi pale kwa sababu
ya kutoamini kwao.”
Wakati
mwingine kutosamehe ni sababu ya mtu kutopona ijapo maombi mengi yamefanywa.
Wakati
mwingine kazi za miungu mingine (occult ) ina zuia uponyaji.
Wakati
mwingine nadhiri iliyovunjwa ni kisuizi.
Wakati
mwingine kutoamini maishani mwetu ndio sababu.
Wakati
mwingine ibada ya sanamu (miungu mengine) imeharibu uhusiano wetu na Mungu.
Pengine
wakati mwingi kutoamini tu ndio sababu, kupuuza neno la Mungu kama neno
lililoandikwa.
Mahali
ambapo haustahili kutafuta uponyaji:
(Zonetherapi
– Acupunture – Hypnosis – Pendulum – Homeopathic – copper arm rings – means of
protection against radiation from the underground – mesmerism – Wanaoponya bila
kutumia jina la Yesu – uchawi – uganguzi mweupe na mweuzi – n. k ( samahani,
maneno mengi hayaelezeki kwa kiswahili. )
MIUJIZA:
Maana:
Muujiza ni njia ya kiungu inayodhihirishwa katika hali ya kawaida ya kiasili.
Muujiza ni tendo la Roho wa Mungu. Ni kitanguo cha sheria za kawaida.
Haiwezi
kuelezeka pasipo nguvu za Mungu. Kipawa cha muujiza ni kipawa cha nguvu.
Uponyaji
wote mwilini mwa mwanadamu, ulemavu na kivunjo – hata uponyaji wa kitaalamu,
unatokana na kipawa cha uponyaji, kwa sababu inatendeka ndani ya mwili. Hii
haitakuwa utendaji wa miujiza.
Tofauti
kati ya kipawa cha imani na kipawa cha miujiza ni : Miujiza hutendeka papo hapo
na kwa njia ya kustaajabu ilhali, kipawa cha imanihufanya kazi kwa muda mrefu
na sana sana sio la kustajabisha bali bado ni kipawa chenye nguvu kwa vipawa
vyote.
Baadhi
ya maandiko ya kipawa kinavyotumika:
Kipawa
kilitumika kwa ukombozi wa kimuujiza kwa wana wa Mungu kutoka mkono ya adui.
Kutoka
14:16, Nawe inua fimbo yako, ukanyoshe mkono wako juu ya bahari, na kuigawanya;
nao wana wa Israeli watapita kati ya bahari katika nchi kavu. Nao majeshi ya
wamisri pia litaingia bahari mtakapopita nitasababisha maji yarudi pamoja na
Jeshi la Farao lote litaangamia. Miujiza mengi yalitendeka hapa.
Kuzaidia walio na hitaji.
Kutoka
14: Musa mara tena kainua fimbo na kugonga mwamba, na maji yakatiririka, mengi
inayotosha kunywesha wanawaisreli milioni 1.5 jangwani. Hii ni ukumbusho kwetu
kwamba Yesu ndiye mwamba wetu.
Mariko 6:36-37, Yesu afanya muujiza wa kulisha umati kubwa, kwa hakika
ni muujiza.
Ushuhuda:
Ilitendeka kule China, Watoto waliokuwa na njaa walikuwa kwa maombi,
biwi la ngano liliangushwa papo hapo kwenye watoto walikuwa wakiomba kwa
Yehovah Jireh, kwa hakika ni jibu la kiajabu la maombi.
Kufanya
uamuzi wa kiungu na nidhamu:
Tauni
kumi za mizri zilikuwa miujiza kumi kutoa nidhamu, kumpa Farao nafasi ya mwisho
ya kutubu na kuwapa watu wa Mungu uhuru wao wa kuondoka, lakini hakukubali,
ilhali alipata nafasi ya mwisho.
Kudhibitisha
neno lililo hubiriwa.
Matendo
ya mitume 13:11-12, ni mafundisho ya nani yalikuwa kweli, Elymas ama Paulo,
Muujiza ulifanya Elymas muofu, katika giza, kipofu kwa muda na maneno ya Paulo
yakakubalika na kuaminika.
Kutuliza hali siziso epukika katika hali ya
hatari.
Matayo 13:23, Yesu atuliza mawimbi katika bahari la
Galilaya.
Kufufua
walio kufa.
Kijana
wa njane, Lazaro, Tabitha.
Kudhihirisha
nguvu za Mungu na ukuu wake.
Fununu
kuhusu Yesu akitenda miujiza ilifanya watu wamtukuze na wamheshimu Mungu.
John 4:48,
Yesu akamwambia, "Msipoona ishara na maajabu hamtaamini!"
Luka
1:5, ububu wa Zachariah, Vs 64, Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu
Mungu.
Katika
maandiko kumejaa mifano mengi ya miujiza ya kiungu, hata leo waumini,
wamishonari, mitume, wainjilisti waweza kushuhudia miujiza mengi yanayofanyika
kwa - utukufu wa Mungu.
Mahali
ambapo haustahili kutafuta miujiza!
Uaguzi
wa maji – Voodoo – Uchawi n.k.
KIPAWA CHA IMANI.
Kipawa
cha imani ndio bado kipawa chenye nguvu kati ya vipawa zote tatu vya nguvu –
kipawa cha uponyaji – kipawa cha muujiza – kipawa cha imani.
Kuna
aina tofauti vya imani.
1)
Imani ya kuokoa. Aina hii hufanya kazi kabla ya mtu kuoka.
2)
Kuna pia imani asili; tunaamini kile ambacho tunasimuliwa kilitendeka
katika kihistoria. Mkulima huamini kuna mavuno baada ya kupanda mbegu.
3)
Pia kuna imani kama tunda la Roho. Wagalatia 5:22, Imani ni tunda huleta
tabia. Kipawa cha imani ni ya nguvu.
Imani
kama tunda la Roho hukua, ( imani kama mbegu ya haradari ), Imani kama kipawa ni kiwango fulani cha
imani ambacho mtu hupewa mara moja. Iko tayari siku zote kutumika. Imani kama
tunda hukua katika muumini, sio vile kwa kipawa cha imani, lakini inavyotumika
zaidi ndivyo zaidi hupokelewa.
Imani
cha kuokoa huja kabla ya mtu kuokoka.
Imani
kama tunda huja baada ya mtu kuokoka.
Imani
kama kipawa huja baa ya ubatizo katika Roho mtakatifu.
4)
Imani kama kipawa cha Roho mtakatifu, ni kiwango spesheli cha imani inayo
pokekelewa kutoka kwa Mungu moja kwa moja. Ni imani ya Mungu.
Kipawa cha imani ni tofauti na kipawa cha muujiza
kwa sababu; kipawa cha miujiuzi inaonekana ila haijatulia bali kipawa cha imani
kimetulia na kinafanya kazi kwa mda mrefu, hata hivyo huwa cha nguvu zaidi
mwishoni.
Kipawa cha imani ni chombo cha kiroho cha mhumini
na mhuduma na ina,; baraka na laana, uumbaji na pia katika kubamoa, kuondoa ama
kubadilisha hali, na mengine mengi.
Kipawa cha imani sana sana ni kitendo cha papo
hapo, wakati mwingine cha kushangaza. Kipawa cha imani ni hatua inayoweza
kufanyika kwa muda fulani lakini matokeo yake ni ya nguvu hata ingawa sio cha
kuonekana.
Mwanzo 17:27, Isaka akibariki Yakobo ( Waebrania
11:20 )
Vipawa vyote tisa vya Roho vyafanya kazi kwa imani
( imani kama tunda la Roho ) hata kipawa cha imani inafanya kazi kwa imani(
tunda la imani ), kama vile meli yote kubwa inaendeshwa kwa kutumia mafuta,
sawa na malori.
Tunda la imani ndilo la muhimu machoni pa Mungu,
ndio aina ya imani inayo heshimu Mungu na kufurahisha moyoni mwake. Kipawa cha
imani haizai matunda kwa sababu ni imani ya Mungu mwenyewe inafanya kazi
kupitia mtumishi wake.
Kipawa cha imani ni sehemu ya imani
tunayokabidhiwa na Mungu, sehemu ya imani yake mwenyewe.Haikui kama tunda la
imani bali inatiwa nguvu nalo.
Mifano kutoka maandiko:
Baraka za Miujiza
Baraka za Isaka kwa Yakobo. Mwanzo 17:28,
Waebrania 11:20.
Baraka za Yakobo kwa Ephraim na Manasseh
Unabii wa Nuhu kwa Cam ( laana pia inafanya kazi
kwa imani )
Ulinzi katika nyakati za hatari
Danieli katika tundu la simba. Dan 6:17-23,
Wahebrania 11:33
Paulo na nyoka. Matendo ya Mitume 18:5, Mariko
16:18.
Kuhifadhiwa kimujiza katika
njaa na kwa kufunga.
Eliya katika kijito cha cherith. Kunguru walimletea
nyama. 1 Wafalme 17:3-6
Mjane katika Zareptha. Unga na mafuta ilitosha
hadi wakati mvua ilipoanza. 1 Wafalme 17:14-16.
Kupokea ahadi za Mungu za
kustaajabisha.
Abrahamu hakuwa na shaka bali alikuwa na imani ya
nguvu. Mwanzo 21:5, Warumi 4:20.
Kuadhibisha nidhamu ya kiroho
kwa wanao kosa.
1 Wakorinto 5:1-5. Mtu aliyezini na mke wa babaye.
Mwili wake ulikabidhiwa ibilisi na adhabu ya kiroho ukobadilisha maisha yake.
Elisha akiwazuia watoto
wadhihaki. 2 Wafalme 11:2-3, 24.
Kwa ushindi wa kimujiza
vitani.
Haruni na Hur wakishikilia
mkono wa Musa. Kutoka 17:11
Kusaidia
katika shida za kinyumbani na pia shinda kubwa kubwa.
Mwanamke
mmaskini alipiwa deni zake kupitia kwa kipawa cha imani.2 Wafalme 4:1-7.
Kufufua
wafu.
Hapa,
vipawa zaidi ya moja inafanya kazi. Vipawa vya Roho wakati mwingine vinahusika
pamoja. Kipawa cha uponyaji na kipawa cha kutenda miujiza vyaweza kuhusika pia
katika kufufua wafu. Lazaro alikuwa mgonjwa na alipofufuliwa akawa mzima.
Pia
imani ni kipawa kinacho tumika katika kutoa mapepo.
Imani
kama kipawa na kubambanua miroho huweza kufanya kazi pamoja hapa.
Kuna
mifano nyingi katika bibilia na hata sasa hii inatendeka kwa wahuduma wengi na
wahumini pia.
Shetani
na miroho ya kufisidi huiga vipawa zote tisa vya Roho mtakatifu. Kuna roho mchafu
nyuma ya kila ibada isiyo ya kiungu.
Baadhi
ya mapepo huiga vipawa vya Roho mtakatifu ni kama yafuatayo;
(
Clairvoyance, familiar spirits, crystal ball, fortune telling, horoscopes,
black magic, voodoo, witchcraft, water divination, spell, hypnosis, n.k )
Samahani kiswahili hakitafsiri sawasawa hapa ).
7.Roho Mtakatifu na makao yake:
Tazama
pia, Wana wa Mungu, kanisa,( mwili wa Kristo ) na moyo.
Miili yetu ni hekalu ya Roho Mtakatifu. 1 Wakorinto
3:16, Je, hamjui kuwa, miili yenu ni hekalu…
Roho mtakatifu anaishi ndani
yetu. Warumi 8:11, Ikiwa Roho wa Mungu aliyemfufua Kristo kutoka wafu anaishi ndani yenu,
basi huyo aliyemfufua Kristo kutoka wafu ataipa uzima miili yenu yenye hali ya
kufa; atafanya hivyo kwa njia ya Roho wake AKKYE NDANI YENU.
MUNGU yuaishi ndani yetu
kupitia kwa Roho. Waefeso 8:11, Katika kuungana naye,
ninyi pia mnajengwa pamoja na wote wengine, muwe makao ya Mungu kwa njia ya
Roho wake.
8.
Roho Mtakatifu na pingamizi za Roho Mtakatifu. Kukufuru Roho Mtakatifu:
Tazama pia: Ulimwengu, shetani,
uofu, kutoamini, uongo, utu, Kuvunjika moyo
a).Pingamizi kwa Roho
Mtakatifu:
Matendo ya Mitume 7:51,Enyi wakaidi wakuu! Mioyo na masikio yenu ni kama ya watu wa mataifa.
Ninyi ni kama baba zenu. Siku zote mnampinga Roho Mtakatifu.
b).Kuhuzunisha Roho
mtakatifu.
Waefeso 4:30, Msimhuzunishe Roho Mtakatifu wa Mungu maana Roho huyo ni alama ya Mungu
kwenu kwamba ninyi ni watu wake, na thibitisho kwamba siku itakuja ambapo Mungu
atawakomboeni.
9. Ubatizo katika Roho
Mtakatifu.
Luke 3:16,….Yeye atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
Matendo ya mitume 1:5,…. Kwani
Yohane alibatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache, ninyi mtabatizwa kwa
Roho Mtakatifu."
Matendo ya mitume 2:4,.. Wote
wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema LUGHA MBALIMBALI kadiri Roho
alivyowawezesha.
Matendo ya mitume 2:38,.. Tubuni
na kila mmoja wenu abatizwe kwa jina la Yesu Kristo ili mpate kuondolewa dhambi
zenu na kupokea ile zawadi ya Roho Mtakatifu.
10.Roho mtakatifu na kanisa.
Matendo ya mitume 4:31,Walipomaliza
kusali, pale mahali walipokuwa wamekutanika pakatikiswa, nao wote wakajazwa
Roho Mtakatifu. Wote wakaanza kuhubiri neno la Mungu bila uoga.
Matendo ya Mitume 9:31, Wakati huo kanisa likawa na
amani popote katika Yudea, Galilaya, na Samaria. Lilijengwa na kukua katika
kumcha Bwana, na kuongezeka likitiwa moyo na Roho Mtakatifu.
M. ya mitume 15:28, Watume
walitii Roho mtakatifu.
Warumi 8:9,…. Yeyote
asiye na Roho wa Kristo, huyo si wake Kristo.
M. ya mitume 10:47, "Watu
hawa wamempokea Roho Mtakatifu kama sisi wenyewe tulivyompokea. Je, kuna yeyote
atakayeweza kuwazuia wasibatizwe kwa maji?"
11.Roho mtakatifu na vipawa,
utawala wa kiungu juu ya sheria za kiasili, uweza, afya, egemio na uchukuzi.
a). Utawala wa kiajabu juu
ya sheria za asili. 2 Wafalme 6:6.
b). Nguvu za kiajabu.
Waamuzi 14:6, 16:3.
c). Afya na egemeo la
kiajabu. Kumbu
kumbu la torati 8:4.
d). Uchukuzi isiyo ya kawaida. M. ya mitume
8:39-40.
12.Roho mtakatifu na dhambi
isiyosameheka:
a).Ukufuru wa Roho
mtakatifu. Matayo 12:31, Kwa sababu hiyo,
nawaambieni, watu watasamehewa dhambi na kufuru zao zote, lakini hawatasamehewa
dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu.
b).Kudanganya Roho
mtakatifu. M. ya mitume 5:3,9,10. Ms 3, …mbona Shetani ameuingia
moyo wako na kukufanya umdanganye Roho Mtakatifu…..Ms 5, Anania aliposikia
hayo, akaanguka chini, akafa……
13.Roho mtakatifu kama mwalimu
na muombolezaji:
a). Roho mtakatifu hufundisha. 1. Wakorinto 2:13, Basi sisi twafundisha,
si kwa maneno tuliyofundishwa kwa hekima ya binadamu, bali kwa maneno
tuliyofundishwa na Roho, tukifafanua mambo ya kiroho kwa walio na huyo Roho.
b). Hufundisha wanafunzi
kila kitu. Yohana 14:26, lakini Msaidizi, Roho
Mtakatifu, ambaye Baba atamtuma kwa jina langu, atawafundisheni kila kitu na
kuwakumbusheni yote niliyowaambieni
14.Roho mtakatifu dhamira ya
dhambi:
a).Dhibitisho la dhambi.
Yohana 16:8, Naye atakapokuja atawathibitishia walimwengu
kwamba wamekosea kuhusu dhambi, uadilifu na hukumu ya Mungu.
Roho mtakatifu ndiyo tu
pekee awezawe kushawishi mtu kutoka dhambini. Dhamira ya mtu ni sehemu ya roho
ya mtu. Roho mtakatifu hushawishi mtu kupitia DHAMIRA yake. Hatua ya kushawishi
kutoka dhambini ni hakika kupitia Roho mtakatifu – kwa neema ya Mungu.
15.Roho mtakatifu na huduma.
Huduma inahusika pia na –
uadimishaji wa vipawa vya Roho mtakatifu.
Huduma zatiwa upako wa Roho
mtakatifu.
Roho mtakatifu huongoza kila
huduma iliyo ya haki.
Mhuduma ndani yake ni makao
ya Roho mtakatifu.
1 Cor 12:28 Mungu ameweka katika kanisa: kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu;
kisha ameweka wale wenye kipaji cha kufanya miujiza, kuponya, kusaidia;
viongozi na wenye kusema lugha ngeni.
A). Mtume. Kigiriki:
apostolos=”kutumwa” ( na Kristo ) pia ya maanisha kumamlakishwa na Kristo.
B). Nabii. Kigiriki:
prophetes, inamaanisha “wito ama kutangaza mapenzi ya Kiungu.”.Hivyo ndivyo
Yahweh asema”.Kwa ujumla, twaweza kusema wanabii ni waume na wanawake
wanaopokea maono ama ndoto za kiungu ( kupitia uwezo wa Roho mtakatifu) ambayo
wanapitisha kwa umati kwa usemi ama kwa vitendo.
C). Muinjilisti. Kigiriki: Euaggelistes=anaye tangaza habari njema.
D). Mchungaji. Kwa kigiriki maneno 3 ya viongozi
wa kanisa imetajwa: Episkopos=Askovu, Poimen=Mchungaji( anayeshughulikia
kondoo), Prebyteros=Wazee( katika uwingi kwa agano jibya).
E). Mwalimu. Kigiriki:Didaskalos=mwalimu.
F). Huduma ya usaidizi. ( Kipawa katika
kuadimisha).
G). Huduma ya utawala. ( Kipawa katika upangaji ).
H). Shemasi. Kigiriki: Diakonos=Yule ambaye
aliyepewa jukumu ya kuhuduma kwenye meza, karamu ya upendo.
I). Wazee. Kigiriki=elders, sio huduma bali ni
ofisi maalum kanisani, pia aweza kusimamia huduma yeyote.
Tazama pia: Mafunzo katika huduma. (
The fivefold ministries).
16.Upako wa Roho Mtakatifu:
Luka 4:18-19, "Roho
wa Bwana yu juu yangu, kwani amenipaka mafuta niwahubirie maskini Habari Njema.
Amenituma niwatangazie mateka watapata uhuru, vipofu watapata kuona tena;
amenituma niwakomboe wanaoonewa, Ms 19,na kutangaza mwaka wa neema ya Bwana."
Yesu kristu alitiwa mafuta katika njia spesheli kuhubiri. Upoka ni Roho
mtakatifu JUU yake. Kila mhuduma wa bwana ametiwa mafuta kwa kiwango Fulani –
Zaidi au kidogo. Yesu ndiye mpakwa mafuta kuliko wote. Upako utaonekana katika
maisha ya mhuduma. Mhuduma anavyojihuzisha katika huduma ndivyo anavyokuwa na
upako zaidi.
17.Ujazo wa Roho Mtakatifu:kujazwa na Roho mtakatifu:
Mbali na kubatizwa katika Roho mtakatifu, ujazo wa Roho mtakatifu ni
HATUA. Vile ubatizo katika Roho mtakatifu hufanyika mara moja katika maisha ya
mtu, ujazo yaweza kuwa mara kwa mara.Ni hatua. Kama vile Paulo amesema katika
waefeso 5:18-19,… bali mjazwe katika Roho mtakatifu. Ms 19,Zungumzeni kwa maneno ya Zaburi, nyimbo na
tenzi za kiroho; mwimbieni Bwana nyimbo na zaburi kwa shukrani mioyoni mwenu.
Njia moja ya kujazwa na Roho mtakatifu ni KUABUDU katika nyimbo na
maombi ya kuabudu na shukrani.
Waweza kuomba kujazwa zaidi na zaidi na Roho mtakatifu.
Dhihirisho ya kwamba umejazwa na Roho mtakatifu ni matunda ya roho
inaanza kuonekana maishani mwako.
Tazama pia Ujazo wa Roho
mtakatifu na (the 4 temperaments).
18.Roho mtakatifu na maombi
ya uombezi:
Hutupa nguvu katika maombi. Warumi 8:26-27,Hali kadhalika, naye Roho anatusaidia katika udhaifu wetu. Maana hatujui
inavyotupasa kuomba; lakini Roho mwenyewe anatuombea kwa Mungu kwa mlio wa
huzuni usioelezeka.Ms 27, Naye Mungu aonaye mpaka ndani ya mioyo ya watu, anajua
fikira ya huyo Roho; kwani huyo Roho huwaombea watu wa Mungu kufuatana na
mapenzi ya Mungu.
19.Roho mtakatifu na ufufuo.
Toba itokanayo na kushawishiwa na Roho mtakatifu
ndiyo njia ya kweli na ya kibibilia ya kuleta ufufuo, haijalishi iwe ni ufufuo
kwa taifa ama kwa mtu binafsi. Kila ufufuo ulio halali hutokana na uweza wa
Roho mtakatifu ndani ya Mtu. Ufufuo utokanayo na bidii ama uwezo wa mwanadamu
haudumu mda mrefu na baadaye huleta mwanguko mkubwa wakati moto huo umepoa.
Kitabu cha Yoel pia ni cha ufufuo.
Yoeli 2:23,….kwa kuwa yeye huwapa ninyi mvua ya
masika,…na mvua ya vuli, kama kwanza.
Yoeli 2:28-29, Hata itakuwa, baada ya hayo,ya kwamba nitamimina Roho yangu juu ya wote
wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto,
na vijana wenu wataona maono; Ms 29,tena juu ya watumishi wenu waume kwa
wanawake, katika siku zile, nitamimina roho yangu.
Mstari kuu ya ufufuo, ahadi
ya Mungu ya UFUFUO kwa watu WAKE: 2 Mambo ya nyakati 7:14,…ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na
kuomba, na kunitafuta uso wangu, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia
toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.
Matendo ya mitume 1:5, Kwani
Yohane alibatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache, ninyi mtabatizwa kwa
Roho Mtakatifu."
Matendo ya mitume 1:8, Lakini
wakati Roho Mtakatifu atakapowashukieni ninyi, mtajazwa nguvu na mtakuwa
mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika nchi yote ya Yudea na Samaria, na
hata miisho ya dunia."
Kanisa la kwanza na ufufuo
wa kwanza, msingi wake ulikuwa:
1)Ujazo wa roho mtakatifu,
2)Ubatizo wa roho mtakatifu
na moto,
3)Kupokea nguvu za roho
mtakatifu.
Huo ndio ulikuwa kielelezo
ya mvua ya KWANZA.
Pendekezo ya Mungu kuhusu
ufufuo haija badilika. Kielelezo ya mvua wa sasa(masika) ya ufufuo na kujengwa
kwa kanisa, bado inatekelezwa katika roho mtakatifu kwa njia ile ile sawa na
kielelezo ya “mvua ya kwanza” ufufuo, ile tu mvua wa ufufuo wa sasa, umwagikaji
wa roho mtakatifu na moto na nguvu utakuwa ya kiwango cha juu kisicho onekana
katika historia. Wakati mvua ya kwanza ulitolewa kwa kiasi, mvua ya sasa
unamwagika kama mto. Yoeli 2:23-24.
Ufufuo hauji tu kwa kipindi
fulani wala kutoka hewani. Pendekezo ya Mungu kuhusu matayarisho ya ufufuo
haija badilika. Kitabu cha Yoeli, mnabii wa ufufuo, anakili: Yoeli 2:12-13, lakini hata sasa, asema BWANA, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, na
kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuombolea; Ms 13, rarueni mioyo yenu, wala si
mavasi yenu, mkamrudie BWANA, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema,
amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi mabaya.
Kufunga na kuomba na kutubu
umekuwa usioepukika na chanzo cha matayarisho ya Ufufuo wa halali wa roho
mtakatifu.
Tazama pia mafunzo kuhusu
Kufunga: Kijitabu cha kufunga na kuomba.
Tazama pia: mafunzo kuhusu
masharti za ufufuo, matayarisho ya ufufuo.
Tazama pia: mafunzo kanuni
za ufufuo.
20.Roho mtakatifu na utukufu
wa Mungu, ( Shekinah, Kabod, Gloria.)
Utukufu Wa Mungu Yahweh.
Yohana 17:22, Mimi nimewapa utukufu uleule
ulionipa mimi, ili wawe kitu kimoja kama nasi tulivyo mmoja;
Yesu atawapa utukufu wake waliokombolewa.
Matendo ya mitume 7:55, Lakini
Stefano akiwa amejawa na Roho Mtakatifu, akatazama juu mbinguni, akauona
utukufu wa Mungu na Yesu amekaa upande wa kulia wa Mungu.
Stefano, katika dakika zake za mwisho, kabla
hajauwawa na wayahudi, aliona utukufu wa Mungu JUU mbinguni.
Musa pamoja na wana wa israeli, pia waliona
utukufu wa Mungu na macho yao.
Kutoka 16:7, 10.
Ms. 7, na asubuhi ndipo
mtakapoona utukufu wa BWANA; na sisi tu nani, hata mkatunung´unikia?......
Ms. 10, Ilikuwa Haruni aliponena
na huo mkutano wote wa wana wa Israeli, wakaangalia upande wa bara, na tazama,
utukufu wa BWANA ukaonekana katika hilo wingu.
Kutoka 40:34-35:
Ms. 34, Ndipo lile wingu
likaifunikiza hema ya kukutania, na huo utukufu wa BWANA ukaijaza maskani.
Ms. 35, Wala Musa hakuweza
kuliingia hema la kukutania, kwa sababu lile wingu lilikaa juu yake, na huo
utukufu wa BWANA ukaijaza maskani.
Tazama pia, Kutoka 29:43.
Mambo ya walawi 9:4,6,23. Hesabu 14:10, 16. Hesabu 16:19,42.
Hesabu 20:6.
1 Wafalme 8:10-11.
Ms.10, Ikawa, makuhani
walipotoka katika patakatifu, nyumba ya BWANA ikajaa wingu.
Ms.11, hata makuhani hawakuweza
kusimama ili kufanya huduma yao, kwa sababu ya wingu lile; kwa kuwa nyumba ya
BWANA ilikuwa imejaa utukufu wa BWANA.
2 Mambo ya nyakati 5:11-14:
Ms.11, Ikawa, makuhani
walipotoka katika patakatifu,.......
Ms.12, tena walawi waimbaji,
wote pia, yaani Asafu, na Hemani, na Yeduthuni, na wana wao,na ndugu zao, hali
wamevaa kitani safi, wenye matoaazi na vinanda na vinubi......
Ms.13, hata ikawa, wenye panda
na waimbaji walipokuwa kama mmoja, wakisikizisha sauti moja ya kumsifu na
kumshukuru BWANA nao wakipasa sauti pamoja na panda na matoazi na vinanda,
wakimsifu BWANA, wakisema, kwa kuwa ni mwema; kwa maana fadhili zake ni za
milele; ndipo nyumba ikajawa na wingu, naam, nyumba ya BWANA.
Ms.14, hata makuhani hawakuweza
kusimama ili kufanya huduma yao, kwa sababu ya wingu lile; kwa kuwa nyumba ya
BWANA ilikuwa imejaa utukufu wa BWANA.
2 Mambo ya nyakati 7:1-2:
Ms. 1, Basi Suleimani
alipokwisha maombi hayo, moto ukashuka kutoka mbinguni, ukateketeza sadaka ya
kuteketezwa na dhabihu; utukufu wa BWANA ukajaza nyumba.
Ms. 2, wala makuhani
hawakuweza kuingia nyumbani mwa BWANA, kwa sababu kwa kuwa utukufu wa BWANA
umeijaza nyumba ya BWANA.
Isaya 58:8:
Ms. 8, Ndipo nuru yako
itakapopambazuka kama asubuhi, na afya yako itatokea mara; na haki yako
itakutangulia; utukufu wa BWANA utakufuata nyuma ukulinde.
Isaya 59:19:
Ms. 19, Basi, wataliogopa jina
la BWANA toka magharibi, na utukufu wake toka maawio ya jua; maana yeye atakuja
kama mkondo wa mto ufurikao, uendeshwao kwa pumzi ya BWANA.
Utukufu wa BWANA ni – Roho wa BWANA!
Isaya 60:1-3:
Ms. 1,Ondoka, uangaze; kwa
kuwa nuru yako imekuja, Na utukufu wa BWANA umekuzukia.
Ms. 2, Maana, tazama, giza
litafunika dunia, na giza kuu litazifunika kabila za watu; Bali BWANA
atakuzukia wewe, Na utukufu wake utaonekana juu yako.
Ms. 3, Na mataifa wataijilia
nuru yako, na wafalme kkjia mwanga wa kuzuka kwako.
Ezekiel 3:23, Basi,
nikaondoka, nikaenda uwandani, na tazama, utukufu wa BWANA ulisimama huko, kama
utukufu ule niliouona karibu na mto Kebari; nami nikaanguka kifudifudi.
Ezekieli aliuona utukufu wa Bwana:
Ezekieli 1:28, Kama
kuonekana kwa upinde wa mvua, ulio katika mawingu siku ya mvua, ndivyo
kulivyokuwa kuonekana kwa mwangaza ule pande zote. Ndivyo kulivyokuwa kuonekana
kwake mfano huo wa utukufu wa BWANA.
Ezekieli 8:4, Na
tazama, huo utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwapo hapo, sawasawa na maono yale
niliyoyaona katika uwanda.
Ezekieli 10:4,
Utukufu wa BWANA ukapaa kutoka kwa kerubi yule, ukasimama juu ya kizingiti cha
nyumba; nayo nyumba ikajazwa na lile wingu, na ua ulikuwa umejaa mwangaza wa
utukufu wa BWANA.
Ezekieli 43:2, 4,5
Ms 2, na tazama, huo utukufu
wa Mungu wa Israeli ulitokea kwa njia ya mashariki; na sauti yake ilikuwa kama
mshindo wa maji mengi, nayo nchi iling,aakwa utukufu wake.
Ms.4, Na huo utukufu wa
BWANA ukaingia ndani ya nyumba, kwa njia ya lango lile lielekealo upande wa mashariki.
Ms. 5, Kisha Roho ikaniinua,
ikanichukua mpaka ua wa ndani; na tazama, utukufu wa BWANA uliijaza nyumba.
Ezekieli 44:4, Kisha
akanileta, kwa njia ya lango la upande wa kaskazini, mbele ya nyumba;
nikaangalia, na tazama, huo utukufu wa BWANA uliijaza nyumba ya BWANA,
nikaanguka kifudifudi.
Maandiko katika agano jipya kuhusu utukufu wa
Mungu:
Matayo 17:1-6, Ms.1,Baada
ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohane nduguye, akaenda nao
peke yao juu ya mlima mrefu.Ms.2,Huko, wakiwa wanamtazama, akageuka
sura, uso wake ukang`aa kama jua na mavazi yake yakawa meupe kama nuru. Ms.3,
Mose na Eliya wakawatokea, wakawa wanazungumza naye. Ms.4, Hapo Petro
akamwambia Yesu, "Bwana, ni vizuri sana kwamba tupo hapa! Ukipenda
nitajenga vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha
Eliya." Ms.5, Alipokuwa bado anasema hivyo, wingu jeupe
likawafunika, na sauti ikasikika kutoka katika hilo wingu: "Huyu ni
Mwanangu mpendwa, ninayependezwa naye, msikilizeni." Ms.6,Wanafunzi
waliposikia hivyo wakaanguka kifudifudi, wakaogopa sana.
Katika kitabu cha Luka tunasoma kwa wafuasi
waliingia katika mawingu. Lk 9:34.
Luka 2:8-9,Katika
sehemu hizo, walikuwako wachungaji wakikesha usiku mbugani kulinda mifugo yao.Ms.9,
Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, na utukufu wa Bwana ukawaangazia pande
zote. Wakaogopa sana.
Utukufu ulingáa, na wakaweza kuiona na macho yao.
Stefano ahubiria wayahudi:
Matendo ya Mitume 7:2, Naye
Stefano akasema, "Ndugu zangu na akina baba, nisikilizeni! Mungu alimtokea
baba yetu Abrahamu alipokuwa kule Mesopotamia kabla hajaenda kukaa kule Harani.
Stefano aliuona utukufu wa
Mungu!
Matendo ya Mitume 7:55, Lakini Stefano akiwa amejawa na Roho Mtakatifu, akatazama juu mbinguni,
akauona utukufu wa Mungu na Yesu amekaa upande wa kulia wa Mungu.
Matendo ya Mitume 9:3-4, Lakini alipokuwa njiani karibu kufika Damasko, ghafla mwanga kutoka
angani ulimwangazia pande zote.Ms.4, Akaanguka chini na kusikia
sauti ikimwambia: "Saulo, Saulo! Kwa nini unanitesa?"
Tazama jinsi Saulo
alivyoielezea wakati alipoilinganisha tukio hili na hali zingi mbili baadaye:
Matendo ya mitume 22:6,
11,…Ms. 6,.. Basi, nilipokuwa njiani karibu kufika Damasko, yapata saa sita mchana,
mwangu mkubwa kutoka mbinguni ulitokea ghafla ukaniangazia pande zote. Ms. 11,..
Kutokana na ule mwanga mkali sikuweza kuona na hivyo iliwabidi wale wenzangu
kuniongoza kwa kunishika mkono mpaka nikafika Damasko
Matendo ya Mitume 26:13-14, Mheshimiwa, wakati nilipokuwa njiani, saa sita mchana, niliona mwanga
mkubwa kuliko wa jua ukiangaza kutoka mbinguni, ukanizunguka mimi na wale
wasafiri wenzangu.Ms.14,..Sisi sote tulianguka chini, nami nikasikia
sauti ikiniambia kwa Kiebrania: `Saulo, Saulo! Kwa nini unanitesa? Unajiumiza
bure kama punda anayepiga teke fimbo ya bwana wake.`
Utukufu wa bwana ni Roho wa
Bwana:
Warumi 6:4, Tulipobatizwa tuliungana na kifo chake, tukazikwa pamoja naye, ili kama
vile Kristo alivyofufuliwa kutoka wafu kwa kitendo kitukufu cha Baba, sisi pia
tuweze kuishi maisha mapya.
“Utukufu wa baba” ni nini?.
Warumi 8:11, Ikiwa Roho wa Mungu aliyemfufua Kristo kutoka wafu anaishi ndani yenu,
basi huyo aliyemfufua Kristo kutoka wafu ataipa uzima miili yenu yenye hali ya
kufa; atafanya hivyo kwa njia ya Roho wake akaaye ndani yenu.
Ufunuo 15:8, Hekalu likajaa moshi uliosababishwa na utukufu na nguvu ya Mungu, na
hakuna mtu aliyeweza kuingia Hekaluni mpaka mwisho wa mabaa makubwa saba ya
wale malaika saba.
Ufunuo 21:23, Mji huo hauhitaji jua wala mwezi kuangazia, maana utukufu wa Mungu
huuangazia, na taa yake ni yule Mwanakondoo.
Tazama vile neno la Mungu
linaelezea Neno la Mungu kama: wingu, mwangaza, mwanga, ng,aa, moshi na Roho wa
Mungu, ijapokuwa utukufu wa Mungu kwa hakika haielezeki.
Daudi alisema kwamba
mwishowe Mungu atampokea katika utukufu:
Zaburi 73:24, Utaniongoza
kwa shauri lako, Na baadaye utanikaribisha kwa utukufu.
Tunafahamu nakala ya Petero
kuhusu unabii wa Yoeli wakati wa pentekote:
Matendo ya mitume 2:17-18, `Katika siku zile za mwisho, asema Bwana, nitawamiminia binadamu wote
Roho wangu. Watoto wenu, wanaume kwa wanawake, watautangaza ujumbe wangu;
vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.Ms.18, Naam, hata
watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, nitawamiminia Roho wangu, siku zile, nao
watautangaza ujumbe wangu.
Lakini tazama kile aliendelea kusema:
Matendo ya mitume 2:19, Nitatenda miujiza juu angani, na ishara chini
duniani; kutakuwa na damu, moto na moshi mzito;
Wengine wanatafsiri hii kama bomu zinazoanguka duniani, lakini siyo
hivi bwana aongea juu yake, Anatangaza UMWAGIKAJI wa ROHO WAKE na UTUKUFU.
Damu! – Damu ya Yesu.
Moto! – Moto wa Roho
mtakatifu! Ndimi za moto zikashuka na kukaa juu ya kila mmoja wao.
Yesu alipaa mawinguni,
ambayo ni wingu wa utukufu.
Matendo ya mitume 1:9, Baada ya kusema hayo, wote wakiwa wanamtazama, alichukuliwa mbinguni;
WINGU LIKAMFICHA wasimwone tena.
Yesu atarudi duniani
akishuka kutoka wingu wa utukufu.
Matendo ya mitume 1:11,…. wakasema,
"Enyi wananchi wa Galilaya! Mbona mnasimama mkitazama angani? Yesu huyu
ambaye amechukuliwa kutoka kwenu kwenda mbinguni atakuja tena namna hiyohiyo
mliivyomwona akienda mbinguni."
Mungu mwenyewe, utukufu wake
unangáa ndani ya mioyo yetu.
2 Wakorintho 4:6-7, Mungu
ambaye alisema, "Mwanga na uangaze kutoka gizani," ndiye mwenye
kuiangaza mioyo yetu, na kutupatia mwanga wa ujuzi wa utukufu wa Mungu uangazao
katika uso wa Kristo. Ms.7, Basi, sisi tulio na hazina hii tuko tu kama
vyombo vya udongo, ili ionekane wazi kwamba nguvu hiyo kuu yatoka kwa Mungu
wala si kwetu sisi wenyewe.
Mambo mengine makuu yalikuwa
ya kuvutia kama nuru ya ajabu ndani ya mioyo zao.
21.Roho Mtakatifu na matunda
ya Roho mtakatifu:
·
Wagalatia 5:22-23, matunda ya Roho mtakatifu.
·
Wagalatia 5:19-21, matendo ya mwili.
·
Tabia – aina 4, ( the 4 temperaments )
A).Wagalatia 5:22-23, Lakini matokeo ya kuongozwa na Roho ni mapendo, furaha, amani,
uvumilivu, wema, fadhili, uaminifu, Ms 23,upole na kuwa na kiasi.
Hakuna Sheria inayoweza kupinga mambo hayo.
Matunda ya Roho ndio hakika
inayojalisha machoni pa Mungu. Matunda haya ndani ya maisha yako hujenga tabia
ya kweli, inakupa kibali cha mbinguni, na kukufanya kuwa kama Kristu.
Upendo – (Upendo wa kiungu
unaotiririka ndani ya mioyo yetu kupitia kwa Roho )
Furaha – ( Raha ya bwana
ndiyo nguvu yetu.)
Amani – ( Amani ya Mungu
siyo ya ulimwengu )
Uvumilivu
Wema
Fadhili – ( Mungu ni fadhili)
Uaminifu – ( Uaminivu kama tunda la Roho )
Upole
Kiasi – ( adabu na kiasi kwa mtu binafsi)
B).Matunda na matendo ya
mwili:
Wagalatia 5:19-21, Basi, matendo ya kidunia yanajulikana: uzinzi, uasherati, ufisadi; Ms.
20, kuabudu sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, choyo, mabishano,
mafarakano; Ms.21,husuda, ulevi, ulafi na mambo mengine kama hayo.
Kinyume cha matunda ya Roho
ni:
Upendo: Kinyume cha upendo ni chuki, ubinafsi,
majisifu. Kwa kawaida, kuna aina mbili
za nguvu au mvutu. UPENDO na KUJI-PENDA. Mungu NI upendo. Shetani ni
mpinzani, Upenda wa kujipenda. Hiza ndizo nguvu zinazopingana mbinguni na hapa
duniani. Mungu Yahweh ni mwenye enzi, NSHINDI, kwa sababu: Yohana 3:16, Maana Mungu aliupenda ulimwengu hivi hata akamtoa Mwana wake wa pekee,
ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
Furaha: Kinyume cha furaha kama tunda la Roho
ni: raha ya ulimwengu, tamaa ya ulimwengu, usherati, ulevi, madawa za kulevya
nk.
Amani: Kinyume cha amani ya Mungu ni: hofu,
wasiwasi, walimwengu hawana amani, asema bwana. Isaya 48:22.
Uvumilifu: Kinyume ni: Hasira, uasi, chuki.
Wema: Kinyume ni: Moyo mgumu, hukumu,
ubinafsi.
Fadhili: Kinyume
ni: uchoyo, mgumu( Mkono gamu),
Uaminifu: Kinyume
ni: kutoamini, uoga(hofu). Uoga ni kuamini shetani kuliko ahadi za Mungu katika
bibilia.
Upole: Kinyume
ni: kiburi, ujeuri.
Kiasi: Kinyume
ni: ulafi, kukosa kiasi, kutowajibika kifedha, upungufu wa pesa wakati wote.
Tabia
– ( The four temperaments )
a)
The phlegmatic
b)
The choleric
c)
The melancholy- ( usununo – kusononeka )
d)
The sanguine
(
Samahani maneno mengine hayana utafsiri kwa kiswahili. )
Tazama pia funzo kuhusu:
Temperaments na Roho Mtakatifu.
22. Roho Mtakatifu na
ushawishi. Musiki, kuabudu katika Roho. Maandiko itokanayo kwa Roho mtakatifu:
a)Usanifu ( Inspired art )
Kutoka 31:3-5, nami nimemjaza roho ya Mungu, katika hekima, na maarifa, na ujuzi, na
mambo ya KAZI YA KILA AINA. Ms. 4, ili abuni kazi ya ustadi,kuwa fundi wa
dhahabu, na wa fedha, na wa shaba, Ms. 5, na kukata vito kwa kutiwa mahali, na
kuchora miti, na kufanya kazi ya ustadi iwayo yote.
Kutoka 28:3, Nawe utawambia watu wote wenye moyo wa hekima, niliowajaza na roho ya
hekima wamfanyie Haruni mavazi ili kumtakasa anitumikie…….
b) Nyimbo zilizohuishwa na
Roho mtakatifu:
1 Mambo ya nyakati 25:1-3, Tena Daudi na maakida wa jeshi wakatenga kwa utumishi baadhi ya wana wa
Asafu, na wa Hemani, na wa Yeduthuni, watakaotabiri kwa vinubi na vinanda, na
matoazi; …Ms 3, …walioamuriwa na baba yao Yeduthuni mwenye kinubi,aliyetabiri
katika kumshukuru na kumsifu BWANA.
Waefeso 5:18-19, Acheni kulewa divai maana hiyo itawaangamiza, bali mjazwe Roho
Mtakatifu. Ms 19,Zungumzeni kwa maneno ya Zaburi, nyimbo na tenzi za
kiroho; mwimbieni Bwana nyimbo na zaburi kwa shukrani mioyoni mwenu.
c) Ibada katika Roho:
Yohana 4:23-24, Lakini wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo
wanaoabudu kweli, watamwabudu Baba kwa nguvu ya Roho; watu wanaomwabudu hivyo
ndio Baba anaotaka. Ms 24, Mungu ni Roho, na watu wataweza tu kumwabudu
kweli kwa nguvu ya Roho wake."
D)Maandiko kupitia Roho mtakatifu:
2 Timoteo 3:16. Maandiko yote Matakatifu
yameandikwa kwa uongozi wa Mungu, na yanafaa katika kufundishia ukweli, kuonya,
kusahihisha makosa, na kuwaongoza watu waishi maisha adili,
23.Roho mtakatifu na miujiza(
Mysticism), ukweli na za uongo(false)
2 Wakorinto 4:6-7, Mungu
ambaye alisema, "Mwanga na uangaze kutoka gizani," ndiye mwenye
kuiangaza mioyo yetu, na kutupatia mwanga wa ujuzi wa utukufu wa Mungu uangazao
katika uso wa Kristo.Ms 7,Basi, sisi tulio na hazina hii tuko tu kama vyombo vya
udongo.....
Mysticism za uongo
Matendo yote ya ajabu ajabu, mwangaza inayoangaza
isiyo ya kawaida inayohusika na dini zisizo za kikristo ni za uongo (FALSE)
2 Wakorinto 11:14,.....Wala
si ajabu, maana hata Shetani mwenyewe hujisingizia kuwa malaika wa mwanga!
24. Njia saba za uongozo wa
Roho Mtakatifu:
A.
Kupitia utu wa ndani (the innerman)
Utu wa ndani = mwili – nafsi – roho yako
iliyookoka – Roho mtakatifu aishiye ndani
Tunatumia siku zetu za maisha katika kiwango cha
mawazo yetu, hali ya kiasili, na muda mchache tu katika hali ya kiroho. Lazima
tujizoeshe kukaa katika roho. Inachukua muda na pia mazoezi kusikiliza sauti ya
ndani ya roho, shahidi wa ndani.
1.
Uongozo kupitia utu wa ndani, roho yako.
-Kupitia hisia ( sauti ya ROHO):-(Intuition) –( uongozo wa dio au la, kama Urim na Tummim katika kikundi cha wakuhani wakuu.
-Uongozo wa ndani(Taa ndogo inayoangaza ndani yako)
-Ushahidi wa ndani( kuhisi vizuri na amani moyoni – ama kusumbuka, unyonge ama kuhatarika moyoni.
2.
Uongozo kupitia maono na pia ndoto kutokana na Roho Mtakatifu.
3.
Uongozo kupitia unabii.
4.
Uongozo kupitia sauti ya kiungu.
Pointi
hizo tatu za mwisho zote ni kwa vipawa vya Roho Mtakatifu.
5.
Uongozo kupitia neno la Mungu, ikiangazwa na Roho Mtakatifu.
6.
Uongozo kupitia hali ya maisha. ( Yona
katika dhoruba )
7.
Uongozo kupitia matendo ya unabii, (Agabus mnabii, Ezekieli mnabii)
Matayo 18:16, ....Asipokusikia,
chukua mtu mmoja au wawili pamoja nawe, ili kwa mawaidha ya mashahidi wawili au
watatu, kila tatizo litatuliwe.Dhibitisho la hakika ni kwa uongozo, wakati inakuja mara mbili ama tatu kuhusu jambo fulani.
Tena, kwa kawaida kuna muongozo kupitia hekima ya kiasili, hisia za kawaida. Inadhihirisha waziwazi nini la kufanya katika tukio fulani.
Usidhubutu kutafuta ushauri kupitia yafuatayo:
·
Kwenye miroho ndani ya glass.
·
Uenyemali (fortune telling)
·
Bilauri(crystal ball)
·
Horoscopes
·
Usoaji wa kadi
·
Mizani(pendulums)
·
Mwaaguzi(water diviner)
·
(Seances)
·
(Occult practice)
·
Ushirikina(superstition)
Yote haya ni mashauri kupitia roho mchafu ambalo kwa
hakika litakupotosha.Wapsykologia na mapsychiatrists hawawezi kutoa ushauri wa kiroho kwa sababu hawana imani kwamba roho mtokatikatifu yuaishi ndani ya mtu wala hawaamini kwamba roho ya mauofu iko.
Ndoto zina huishwa kwa njia tatu;
1)
Kupitia kwa roho mtakatifu
2)
Kupitia kwa roho mchafu wa
ibilisi
3)
Kupitia tukio la siku kwa siku,
mara nyingi huja kwa njia tofauti zizizo eleweka.
Utabiri wa ndoto wa kweli hufanyika kupitia uweza
wa roho mtakatifu. Ni halali kutumia akili za werevu ama ujuzi wa mwanadamu ni
limuko na mwishowe mtu anaweze kuwa na roho ya uongo.
Danieli
alitabiri ndoto kwa sababu roho mtakatifu alikuwa NDANI yake. Danieli 4:8-9.
Usiwaendee wasiomcha Mungu kwa mashauri kuhusu
mambo ya kiroho wala ushauri kuhusu maisha yako na siku zako za usoni.
25.
Roho Mtakatifu na huisho wa neno la Mungu.
2 Tim 3:16, Maandiko yote Matakatifu
yameandikwa kwa uongozi wa Mungu, ( naye
ni roho mtakatifu)….
Bibilia, ambayo ni neno
la Mungu kupiti uweza wa roho mtakatifu, haibadiliki, kamilifu na ina dumu
milele. Yesu ndiye nembo(muhuri) ya neno la Mungu.Yehovah Yahweh „ MIMI
NDIYE“ mwenye enzi na ni wa milele.
26.Roho mtakatifu na Yesu Kristu kama
mzaliwa wa pekee wa Mungu baba.
Mathayo 12:40,Jinsi Yona alivyokaa siku
tatu kutwa kucha tumboni mwa nyangumi, ndivyo naye Mwana wa Mtu atakavyokaa
ndani ya ardhi siku tatu kutwa kucha. (Hades-ufalme wa giza)
Jukumu ya roho mtakatifu
kati ya msalaba na kiti cha enzi:
Yesu alipokelewa katika
wafu na Roho mtakatifu, kafufuka,akapaa
juu enzini mwa mungu na akatukuka.
1 Petero 3:18:19, Kwa maana Kristo mwenyewe alikufa kwa ajili ya
dhambi zenu; alikufa mara moja tu na ikatosha, mtu mwema kwa ajili ya waovu,
ili awapeleke ninyi kwa Mungu. Aliuawa kimwili lakini akafanywa hai
kiroho;Ms.19,na kwa maisha yake ya kiroho alikwenda kuwahubiria wale roho
waliokuwa kifungoni.(kaburini)
Katika nguvu za roho
mtakatifu, Yesu alihuishwa baada ya kubeba dhambi ya wengi. Isayah 53:10-12
Katika nguvu za roho
mtakatifuYesu alihubiri ujumbe wa wokovu kwa wote walioishi duniani na tokea
mwanzo hadi wakati wa kifo chake kwa miaka 4000, hakika ndio mkutano wa ufifio
mkubwa katika historia.
Warumi 8:29, …Maana hao aliowachagua
tangu mwanzo, ndio aliowateua wapate kufanana na Mwanae, ili Mwana awe wa
kwanza miongoni mwa ndugu wengi.
Soma pia Zekariah 12:10.
Tazama pia somo kuhusu.
Atonement.
27. Roho mtakatifu na manabii wa agano
jibya:
Wanabii wote wa Agano
jibya walifanya kazi katika uwezo na imizo ya roho mtakatifu.
Hannah pekee alitabiri
kupitia roho ya uongo.Jeremiah 28:10,12,15.
28. Roho mtakatifu na hekalu.
Kinara cha mshumaa chenye
sehemu saba katika hekula ni ishara ya roho mtakatifu na dhihisho zake.
29. Roho mtakatifu na ubatizo wa wa Roho
mtakatifu na moto.
Luka 3:16,…..Yeye atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
Matendo ya mitume 2:3-4, Kisha, vikatokea vitu vilivyoonekana kama ndimi za
moto, vikagawanyika na kutua juu ya kila mmoja wao.,Ms 4, Wote wakajazwa Roho
Mtakatifu, wakaanza kusema lugha mbalimbali kadiri Roho alivyowawezesha.
Waebrania 1:7 (Zaburi
104:4)…. na watumishi wake
kuwa ndimi za moto."
Yaonekana kwamba
sehemu ya pili, za moto, wa uatizo katika roho na moto, mara nyingi huachwa
nje.
30. Roho
mtakatifu na kuhubiri injili.
a) Injili yahubiriwa kupitia Roho mtakatifu.1 Petero
1:12, …ambayo ninyi mmekwisha sikia
sasa kutoka kwa wale wajumbe waliowatangazieni Habari Njema KWA nguvu ya ROHO
MTAKATIFU aliyetumwa kutoka mbinguni, hiyo kazi yao haikuwa kwa faida yao
wenyewe, bali kwa ajili yenu. Hayo ndiyo mambo ambayo hata malaika wangependa
kuyafahamu.
b) Roho mtakatifu huubiri.Yohana 16:13-14,Lakini atakapokuja huyo
Roho wa kweli atawaongoza kwenye ukweli wote; maana hatasema kwa mamlaka yake
mwenyewe, bali atawaambieni yote atakayosikia, na atasema mambo yatakayokuwa
yanakuja.Ms.14, Yeye atanitukuza
mimi kwa kuwa atawaambieni yale atakayopata kutoka kwangu.31. Roho Mtakatifu na Mwanzo.
Mwanzo 1:2,….na Roho wa Mungu Yahweh ikatembea kwenye maji.
Mwanzo 1:26,kisha Mungu akasema,” NASI tumuumbe mwanadamu kwa sura YETU wenye…..
NASI na YETU ni utatu wa Mungu baba.
Mungu baba, Mwana na Roho Mtakatifu walikuwa na walihusuka katika umbaji wa ulimwengu.
32.Roho Mtakatifu na silaha kamili, zilaha za kuangamiza na zilaha za
Silaha
kamilifu ya Mungu. Waefeso 6:11-18,
Vaeni silaha anazowapeni Mungu mpate kuzipinga mbinu mbaya za Ibilisi.Ms,12.
Maana vita vyenu si vita kati yetu na binadamu, bali ni vita dhidi ya jeshi ovu
la ulimwengu wa roho; tunapigana na watawala, wakuu na wenye nguvu wanaomiliki
ulimwengu huu wa giza.ms.13, Kwa sababu hiyo, vaeni silaha za Mungu ili siku
ile itakapofika muweze kuyapinga mashambulio ya adui; na mkisha pigana mpaka
mwisho, muwe bado thabiti.Ms.14, Basi, simameni imara! Ukweli uwe kama ukanda
kiunoni mwenu, uadilifu uwe kama vazi la kujikinga kifuani,Ms.15, na hamu ya
kutangaza Habari Njema ya amani iwe kama viatu miguuni mwenu.Ms.16, na hamu ya
kutangaza Habari Njema ya amani iwe kama viatu miguuni mwenu.Ms.17, Upokeeni
wokovu kama kofia yenu ya chuma, na neno la Mungu kama upanga mnaopewa na Roho
Mtakatifu.Ms.18, Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu. Salini kila wakati kwa
nguvu ya Roho. Kesheni bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.
33. Roho Mtakatifu haweza kuzimwa(kukasirishwa).
1 Thesalonike 5:19, Msimpinge Roho Mtakatifu;
34. Roho Mtakatifu na nguvu za kiungu.
Samsoni. Waamuzi 14:5-6,….Simba akamghurumia, Ms.6, na Roho wa Mungu hukashuka kwa nguvu juu yake, akamrarua zimba simba kama vile angerarua mtoto na hakuwa na chochote mkononi…..
35.Roho Mtakatifu na kuzaliwa mara ya pili. (wokovu).
Yohana 3:5-6,…. Yesu akamjibu, "Kweli nakwambia, mtu asipozaliwa kwa maji na Roho, hawezi kamwe kuingia katika ufalme wa Mungu.Ms.6, Mtu huzaliwa kimwili kwa baba na mama, lakini huzaliwa kiroho kwa Roho.
Wokovu sio kwa kubatizwa kwa maji bali ni kwa kuzaliwa mara ya pili kwa roho.
36. Roho Mtakatifu na r oho ya mwanadamu.
Warumi 8:16, Naye Roho mwenyewe anajiunga na ROHO ZETU na
kuthibitisha kwamba sisi ni watoto wa Mungu.
Kuna
tofauti kati ya Roho Mtakatifu na Roho ya mwanadamu.37.Roho Mtakatifu na umoja wa kweli.
Yohana 17:22, Mimi nimewapa utukufu uleule ulionipa mimi, ili wawe
kitu kimoja kama nasi tulivyo mmoja;
Umoja kanisani, umoja katika ya waumini,
haipatikani kwa nguvu za mwanadamu, wala katika vyama na mtandao, haiwezi
kuonekana katika hakili za mwanadamu lakini umoja wa kweli unatokana na Roho
Mtakatifu katika mioyo ya waumini.
38.Roho Mtakatifu na Roho ya maombi.
Zakariah 12:10.Na nitamwaga juu ya
nyumba ya Daudi, na wakaaji wa Yerusalemu, ROHO YA NEEMA NA MAOMBEZI; na
watanitazamia mimi, ambaye walinichoma na watahuzunika.
Kumetolewa Kiwango specieli cha Roho ya
neema na uombezi utakaomwa juu ya kanisa. Unabii inahusu wakati Yesu Kristo
alisulubishwa na kuchomwa pavuni.
Yesu kristu, mwana wa pekee akafanyika
mzaliwa wa kwanza kwa wandugu wote. Tazama pia 8:29.
Tazama pia mazama: Maombi ya muumini.
39.Roho
Mtakatifu na kuabudu.
Yohana 4:23 Lakini
wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wanaoabudu kweli, watamwabudu Baba
kwa nguvu ya ROHO; watu wanaomwabudu hivyo ndio Baba anaotaka.
Ibada ya kweli katika Roho Mtakatifu ni njia
ya kweli ya kuonyesha upendo na utukufu kwa Mungu baba na mwana.Wakati umati
wanaimba katika Roho, huimbaji wa zaburi hizo kwa Mungu, katika hivyo
anamwabudu Mungu katika umoja. Tazama pia 1 Korinto 14:15. Nifanye nini, basi? Nitasali kwa roho yangu, nitasali
pia kwa akili yangu; nitaimba kwa roho yangu, nitaimba pia kwa akili yangu.
No comments:
Post a Comment